Wana-jf nimefiwa na mke wangu!!

Wana-jf nimefiwa na mke wangu!!

tuelekeze home tuje kuhani au weka namba yako hapa wasamaria wanaweza kukutumia hata M-PESA.
...Mkuu msiba uko makongo juu mwisho zinapoishia dala dala eneo husika linaitwa kizota. Kama unatokea ubungo unapanda dala dala za changanyikeni kupitia chuo kikuu unashuka kituo cha bondeni karibu na chuo cha takwimu unauliza eneo la kizota. Na kwa taarifa leo saa 10 alasiri tunahitimisha msiba nawakaribisha tujumuike sote. Namba yangu ya simu 0765 068886.
 
...Mkuu msiba uko makongo juu mwisho zinapoishia dala dala eneo husika linaitwa kizota. Kama unatokea ubungo unapanda dala dala za changanyikeni kupitia chuo kikuu unashuka kituo cha bondeni karibu na chuo cha takwimu unauliza eneo la kizota. Na kwa taarifa leo saa 10 alasiri tunahitimisha msiba nawakaribisha tujumuike sote. Namba yangu ya simu 0765 068886.
Mkuu, pole tena!
Kama vipi fanya editing ya original thread yako ili iwe na namba hiyo ya simu!
Wengine huwa hawasomi thread nzima!...just advice!

 
Sajenti pole sana. Unapitia wakati mgumu sana...tunakuombea upate faraja. Mungu awashikilie watoto pia.
 
pole sana kwa yaliyokukuta ndugu yetu.Mungu akupe nguvu na faraja katika kipindi hiki.
mimi ni mgeni kidogo hapa jamvini,sijajua utaratibu wa hapa mtu akifiwa mnafanyaje.but hatuwezi kuwa na something like kapu ya pole au ubani kwa mfiwa??naona kama hatutimizi ule utaratibu wetu wa ujirani mwema.wengine tumezoea huku uswahili kwetu mtu akifikwa na mambo kama haya basi tunatembeza bakuli la ubani.sijui viongozi wa jamvi hili wanalionaje hili,kama ikibidi watengeneze utaratibu wa mambo kama haya.ni wazo tu jamani,nawakilisha
 
Aisee, pole sana mkuu, Mungu akupe faraja ya pekee pamoja na watoto na wote kwa ujumla
 
Pole na kuondokewa na umpendaye...na uwe na uvumilivu ktk kipindi hiki kigumu
 
Mkuu, pole sana kwa msiba, najua umeumia sana, lkn nimapenzi ya Mungu wengine watangulie na ss kuwafuata baada yao, ni vigumu sana kusema wapi roho ya mkeo itakuwa lkn Mungu wa kweli na Yesu mwanawe mpendwa wanajua atakuwa wapi, chamsingi vumilia uchungu huo huku tukijiuliza na sisi tupo kwenye foleni yakufuata tutakuwa wapi this time of our death?
Mungu wangu akutie nguvu na amani yakutosha ili uwasaidie wanao wapate elimu yakuwasaidia mbele ya safari ukijua wazi kuwa mama ndiye alikuwa waziri wa elimu na mabo ya ndani ss unachua nafasi zote, usikubali kuutii mwli mpaka nao wamejiweka sawa kwa kujitegemea.
Jipe moyo mkuu Mungu yupo nawe na ss ndugu zako tupo nawe.
Regards
JF member.
 
Pole sanaaaa mwenzetu, ni mipango ya Mungu na ana sababu zake....tunakuombea Mungu akutie nguvu ktk kipindi hiki kigumu. Wape pole sana watoto jamani.

RIP Mama Sajenti
 
pole sana brother, Mungu akupe nguvu na hekima katika matatizo yaliyokupata. My condolence
 
Pole sana Mkuu. Tunakuombea kwa Mungu akupe nguvu za kukupitisha katika wakati huu mgumu. Fadhila zake ni za milelel na hakika atakuvusha.
 
Pople sana Mkuu Sajent....what a tragic loss....! Mungu amrehemu....
 
Pole sana mkuu, mwenyezi mungu akupe subira katika wakati huu mgumu. R.I.P
 
Pole sana Sajent. Tunatambua ni kiasi gani unaumia kwa kupoteza mke lakini jipe moyo - Utashinda
 
Inna lillahi wainna ilayhi rajiuun. We will miss shemeji so much. The angels are always near to those who are grieving, to whisper to them that their loved ones are safe in the hands of God. May God give you strength to overcome the pain!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom