Wana-jf nimefiwa na mke wangu!!

Wana-jf nimefiwa na mke wangu!!

Duh, Pole sana Mkuu! Wana JF wote tuko pamoja na wewe, japo wengine tuko mbali tunaungana na wewe ktk msiba huu mzito!
 
Pole sana Kaka, Mungu akutie nguvu.
Tupo pamoja katika Majonzi.
 
Aisee Kifo ni Pazia Jamani lenye siri humo Ndani yake..
Pole sana.. tupee njia yoyote tupitishie rambirambi zetu ..
 
Kamanda tunakupa pole sana kwako na kwa familia yako yote...Mungu alitoa Mungu ametwaa,jina lake lihimidiwe!

Usiwasahau wanao katika kuwapatia matunzo kama ilvyokuwa wakati wa uhai wa mama yao.
 
Pole sana. Tuko pamoja katika kipindi hiki kigumu.
 
Pole sana mkuu. Mungu akupe nguvu na azidi kukufariji. Tupo nawe katika kipindi hiki kigumu. Pole nyingi zaidi kwa watoto wako. Mungu anatuagiza "Nishukuruni kwa kila jambO." Raha ya milele umpe Eeh Bwana na mwanga wa milele umwangazie, astarehe kwa amani.
 
Wewe na wanao mlimpenda, lakini yeye aliye juu yetu kampenda zaidi. Mungu awape nguvu ktk kipindi hiki kigumu!
 
Nasikitika kuwafahamisha kuwa nimepata msiba leo alfajiri mke wangu kipenzi amenitoka. Kimsingi mazishi yamefanyika leo saa 10 kwenye makaburi ya changanyikeni...wife ameniachia watoto wawili wa kike 11 & 8.

Pole sana kaka!
 
.....Pole sana Sajenti, maisha ya mwanadamu ni mafupi sana siku hizi.......inasikitisha kwa kweli, ila yote ni mipango ya Mungu.
Bwana alitoa na ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe.
RIP mke wa Sajenti.
 
Niungane na wenzangu kukupa pole sana daah watoto wadogo sana walimuhitaji sana mama yao, Mungu awape nguvu.
 
Nasikitika kuwafahamisha kuwa nimepata msiba leo alfajiri mke wangu kipenzi amenitoka. Kimsingi mazishi yamefanyika leo saa 10 kwenye makaburi ya changanyikeni...wife ameniachia watoto wawili wa kike 11 & 8.
Kaka Sajenti, pole sana na MUNGU awafariji na machungu haya wewe, watoto na familia nzima. Mlimpenda lakini MUNGU alimpenda zaidi.
 
Pole sana Sajenti.....

Tupo pamoja nawe katika kipindi hiki kigumu kwako na watoto.....

Mungu ailaze pema roho ya marehemu shemeji yetu.....Apumzike kwa amani....Amina
 
Pole sana mkuu. Sisi sote ni waja na kwake tutarejea.
 
nasikitika kuwafahamisha kuwa nimepata msiba leo alfajiri mke wangu kipenzi amenitoka. Kimsingi mazishi yamefanyika leo saa 10 kwenye makaburi ya changanyikeni...wife ameniachia watoto wawili wa kike 11 & 8.

polee sana,
 
Pole sana Mkuu. Tuko pamoja nawe, na Mwenyezi Mungu akupe nguvu katika kipindi hiki kigumu.
 
Mkuu pole sana. Tutakuwa pamoja katika sala katika kipindi hiki kigumu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom