Habari wana jf?
Nina mchumba wangu kwa takribani,miezi kumi na tano sasa.
Wote tumeajiriwa katika wizara flani nchini.
Yeye kwao Iringa na mimi kwetu Songea,kipindi chote cha mahusiano yetu hatujawahi kwenda kwa wazazi wa pande zote mbili,isipokuwa taarifa zilipelekwa upande wa mwanamke na waliopeleka taarifa ni wazazi wangu wakitokea songea,taarifa ilipokelewa vizuri na wazazi wa mwanamke.
Mahali ilijadiliwa na kukubaliwa na pande zote mbili na tarehe ya kupeleka mahali ilipangwa na wazazi wa mwanamke na kuafikiwa na wazazi wangu.
Tazizo limekuja baada ya tarehe ya mahali kupangwa ambayo ilikuwa tarehe 13/03/2014.Tarehe hiyo ilikuja na matatizo nyumbani tulifiwa na ndugu wa damu hivyo wakatuma mtu akahairishe ,tatizo mtu aliyetumwa bahati mbaya akafika Iringa na kusahau kupitisha taarifa ukweni ,maana yeye ni mtu wa huko iringa.
Tarehe iliyopendekezwa kupeleka mahari baada ya kuhairishwa ni tarehe 3 April mwaka huu.
Kweli tarehe hiyo ilizingatiwa kwa upande wa wazazi wangu waka fika mpaka Iringa na mshenga akiwa mkuu wa msafara,bahati mbaya ukweni hawa kupata taarifa hivyo wakang'aka kupokea ile mahali ambayo kilikuwa kiasi flani cha pesa wakidai kuwa kimila tumewadharau sana na tumejiamulia tu.
Wakaitana wanaukoo na kushauriana wasiipokee licha ya kuwaomba msamaha na kuwaeleza yaliyotusibu wamekataa katakata wanadai KAMA KUOLEWA BINTI YAO ATAOLEWA TUU.
Yaani wamekataa katakata na hawataki kuona nyayo zetu pale.
Juzi mchumba wangu akanishauri tuchukue likizo ya dharura twende kwao.Tukafanya hivyo baada ya kwenda wanaukoo waliitana na kututamkia kuwa kuanzia siku hiyo hatuna mamlaka ya kuishi pamoja na kunambia hivi
Nanukuu, "wewe kijana hauna nafasi ya kuishi na binti yetu tena ,ukoo wenu mmejaa dharau na kiburi,binti yetu ataolewa tu sehemu stahiki".
Kiukweli baada ya kutamkiwa hivyo niliwaeleza wazazi wangu wakaniambia kama ipo ipo tu.
Niliaga nikaondoka lakini walimzuia binti yao kuondoka siku hiyo,yeye aliondoka siku iliyofuata,alipowasili hapa Mwanza alinieleza kuwa wazazi wake wanamsihi aachane na mimi endapo atataka kuendelea kuwa miongoni mwa wanafamilia yao.
Nikamuuliza aumuzi wake kaniambia,hayupo tayari kuwakosea wazazi wake hivyo tufanye kila tuliwezalo kupatanisha ama sivyo itifaki itazingatiwa.
NAOMBENI WASAA WENU JAMANI NIFANYEJE HAPO?
Kuna jamaa mmoja alinambia hapo wanataka fidia nusu mahari kulingana na mila zao Wabena na sie hali ngumu.
Au wana mpango wa kuninyima mke?
Ni habari ya ukweli kabisa.