majam19
JF-Expert Member
- Nov 13, 2024
- 1,667
- 1,911
Habarini wakubwa,
Poleni na majukumu. Nianze kwa kuomba radhi kwa nitakaowakwaza.
Mimi ni kijana wa miaka 27. Baada ya majaribio ya muda mrefu ya kutafuta mke kushindikana, nilikata tamaa ya kuoa kabisa na nikaamua kubaki single.
Baada ya muda, dada yangu alinipatia binti mwenye miaka 17 na kunitambulisha naye. Kwa upande wangu sikuwa na jibu la moja kwa moja, ingawa familia yangu ilikuwa inaweka msukumo mkubwa ili nimuoe. Mimi bado sikuwa tayari.
Baada ya kuonana, alikuwa binti mzuri sana kwa muonekano, mashaallah, mtoto wa Kiislamu.
Baadaye dada yangu alinieleza nimpatie zawadi. Nikanunua mavazi ya Kiislamu kwa ajili yake pamoja na fedha, nikatoa zaidi ya laki mbili na nusu na pia nikawapatia nauli ya kurudi kwao.
Baada ya hapo niliendelea kuwaza kuchukua hatua gani, lakini moyo bado haukuwa tayari kwa sababu muonekano siyo kipaumbele changu, na pia nilikuwa sijajiridhisha kuhusu tabia yake na mambo mengine.
Binti aliporudi kwao, wazazi wake walimuuliza kuhusu mimi. Akawajibu kuwa ameridhika na mimi na yuko tayari kuolewa.
Changamoto ikaibuka upande wangu nilipoulizwa na dada yangu. Nilimwambia anipe muda zaidi nijifikirie kwa sababu hii ni hatma ya maisha yangu, na sikujihisi tayari.
Nilikaa zaidi ya wiki mbili, ndipo nikatoa majibu kuwa nakubali, lakini siwezi kuoa kwa wakati huo mwaka jana kwa sababu sikuwa vizuri kiuchumi na akili yangu haikuwa na utulivu wa kutosha. Wakakubali.
Baada ya hapo wazazi wa binti wakawa wanamuuliza dada yangu kuhusu hatua ya ndoa. Dada yangu aliwajibu kuwa nimekubali, lakini tunaomba ndoa iwe mwaka unaofuata.
Wazazi wa binti wakasema sawa, lakini kama ni hivyo nipelekewe barua ya posa ili binti atambulike rasmi kama mchumba.
Nilipata taarifa hiyo nikachukua muda kufanya maamuzi kwa sababu bado sikuwa na imani ya moja kwa moja na binti huyo.
Baada ya miezi miwili kupita, nikaandaa barua ya posa kupitia mshenga na nikatoa kiasi cha pesa akaipeleka kwa wazazi wa binti na wakapokea.
Baada ya hapo nikawa mchumba rasmi.
Sasa mwaka umeisha na sasa ni mwezi wa sita, wazazi wa binti wanaona bado nipo kimya, ingawa naendelea kumhudumia kwa fedha na mavazi japo si kwa kiwango kikubwa sana.
Kwa sasa wanataka nipeleke mahali ili hatua zifuate, lakini moyoni bado nahisi hofu. Natamani nimwambie mshenga tuachane kabisa, lakini bado nina wasiwasi. Ingawa yule binti anaonekana kunijali na kunitafuta, mimi bado sijajipa utulivu.
Najiuliza maswali mengi na majibu yake siyapati.
Naombeni ushauri, kaka zangu, dada, wajomba, bibi na babu zangu.
Asante sana.
Poleni na majukumu. Nianze kwa kuomba radhi kwa nitakaowakwaza.
Mimi ni kijana wa miaka 27. Baada ya majaribio ya muda mrefu ya kutafuta mke kushindikana, nilikata tamaa ya kuoa kabisa na nikaamua kubaki single.
Baada ya muda, dada yangu alinipatia binti mwenye miaka 17 na kunitambulisha naye. Kwa upande wangu sikuwa na jibu la moja kwa moja, ingawa familia yangu ilikuwa inaweka msukumo mkubwa ili nimuoe. Mimi bado sikuwa tayari.
Baada ya kuonana, alikuwa binti mzuri sana kwa muonekano, mashaallah, mtoto wa Kiislamu.
Baadaye dada yangu alinieleza nimpatie zawadi. Nikanunua mavazi ya Kiislamu kwa ajili yake pamoja na fedha, nikatoa zaidi ya laki mbili na nusu na pia nikawapatia nauli ya kurudi kwao.
Baada ya hapo niliendelea kuwaza kuchukua hatua gani, lakini moyo bado haukuwa tayari kwa sababu muonekano siyo kipaumbele changu, na pia nilikuwa sijajiridhisha kuhusu tabia yake na mambo mengine.
Binti aliporudi kwao, wazazi wake walimuuliza kuhusu mimi. Akawajibu kuwa ameridhika na mimi na yuko tayari kuolewa.
Changamoto ikaibuka upande wangu nilipoulizwa na dada yangu. Nilimwambia anipe muda zaidi nijifikirie kwa sababu hii ni hatma ya maisha yangu, na sikujihisi tayari.
Nilikaa zaidi ya wiki mbili, ndipo nikatoa majibu kuwa nakubali, lakini siwezi kuoa kwa wakati huo mwaka jana kwa sababu sikuwa vizuri kiuchumi na akili yangu haikuwa na utulivu wa kutosha. Wakakubali.
Baada ya hapo wazazi wa binti wakawa wanamuuliza dada yangu kuhusu hatua ya ndoa. Dada yangu aliwajibu kuwa nimekubali, lakini tunaomba ndoa iwe mwaka unaofuata.
Wazazi wa binti wakasema sawa, lakini kama ni hivyo nipelekewe barua ya posa ili binti atambulike rasmi kama mchumba.
Nilipata taarifa hiyo nikachukua muda kufanya maamuzi kwa sababu bado sikuwa na imani ya moja kwa moja na binti huyo.
Baada ya miezi miwili kupita, nikaandaa barua ya posa kupitia mshenga na nikatoa kiasi cha pesa akaipeleka kwa wazazi wa binti na wakapokea.
Baada ya hapo nikawa mchumba rasmi.
Sasa mwaka umeisha na sasa ni mwezi wa sita, wazazi wa binti wanaona bado nipo kimya, ingawa naendelea kumhudumia kwa fedha na mavazi japo si kwa kiwango kikubwa sana.
Kwa sasa wanataka nipeleke mahali ili hatua zifuate, lakini moyoni bado nahisi hofu. Natamani nimwambie mshenga tuachane kabisa, lakini bado nina wasiwasi. Ingawa yule binti anaonekana kunijali na kunitafuta, mimi bado sijajipa utulivu.
Najiuliza maswali mengi na majibu yake siyapati.
Naombeni ushauri, kaka zangu, dada, wajomba, bibi na babu zangu.
Asante sana.