Wamekataa mahari ya binti yao, tufanyeje?

Wamekataa mahari ya binti yao, tufanyeje?

hata mimi kama ungefanya hivyo nyumbani kwetu, tusingekuruhusu umchukue dada yetu.
Bila kupepesa macho wala kuumauma maneno, mlifanya dharau sana.
 
Acha kutisha watu wewe, inamaana hakuna MBENA aliyewahi kutiwa mimba? Restriction zingine zilikuwa zinafanya kazi zamani tu si katika dunia ya sasa ya utandawazi! Siku hizi kila kitu kimeshabadilika mkuu pingu mkoka!
Umtie mimba!!!unawajua WABENA wewee?au unawasikia?
 
Last edited by a moderator:
Hivi huko Songea hakuna simu?
Ilitakiwa mpige simu mapema sana ukweni kwako Iringa, mara baada ya ninyi kufiwa na ndugu yenu wa karibu. Biashara ya kutuma mtu Iringa ndio hio inakukosesha mke.

Ujue hata mimi hilo swali lipo kichwani mwangu. Kwa issue sensitive kama hiyo, muoaji ulipaswa wewe mwenyewe uhangaike kufanya mawasiliano ili wakwe zako wajue. Halafu mlipanga tarehe mbadala peke yenu tu bila kuwajulisha ukweni! Hata mimi nasema hiyo ni dharau. Ushauri wangu, tuma washenga wako tena wakawatake radhi hao wanyalukolo maana wana hasira wanaweza hata kujinyonga kwa hasira(joke)
 
Kwa haraka haraka naweza kusema ile hamasa kutoka wa upande wa mume haikuwepo kivile na walichukulia ni jambo la kawaida kutokana na uwepo wa muda mrefu katika mahusiano yenu ya kimapenzi maana miaka kumi na tano sio haba ni kama mke tu.

Kitu cha pili niuzembe, hasara zitokanazo na uzembe ni nyingi kuliko faida nandio matokeo yake yamekuwa haya tunayo yashuhudia hapa.Taarifa ilikuwa muhimu sana kwa hatua iliyokuwepo.

Inamaana ukoo wa huyu binti hauna hata wazee wenye busara ambao wanaweza kulichulia hili swala la msiba kwa uzito kiasi fulani?? Hapa panahitaji busara zitumike zaidi kuliko jaziba.

Chakufanya ni kujadiliana nahuyo mchumba wako lenu liwe moja, kimsingi hata nyie pia mnahaki yenu katika maamuzi juu ya swala hili, kwa wazazi huwa ni kama kufuata baraka, na kuwapelekea shukrani, maana baada ya hapo hakuna kinachoendelea zaidi ya wewe kuchukua mke na kaanzisha familia yako.

acha kumlisha maneno! yeyey kasema miezi 15 wewe umeitoa wapi miaka 15?
 
dont force marrage mkuu

Hiyo pia ni point ya kuzingatia. Hakuna kitu kibaya kama kuoa kwa kulazimisha. Siku ndoa ikibuma mtaenda wapi kwa usuluhishi endapo mmeoana bila ridhaa. Ikishindikana jua siyo riziki yako, tafuta kwingine Mungu kakuwekea
 
Mkuu uko Mwanza? sasa wasukuma kibaao wanyantuzu unapata shida na hilo,kidding

Back to the issue: Mkuu hapo kwa kweli inabidi ujipe mda tu labda hasira zitapungua ama kuna mtu ameweza kuunganisha terminal kati ya familia yako na ya mchuchu kakusemea mabaya ila hao wakwe wameona hawana excuse ya kukutosa. Lakini la mwisho, msikilize zaid mkeo mtarajiwa mana yeye ndio anawafahamu zaidi hao ndugu zake. Ukiona tu anaegemea kwao we chukua zako, kwa sababu kwa stage hii mchumba ndio steering wa fate yenu. Akionesha kutobalance mambo basi hatari chukua zako fasta
 
Hiyo pia ni point ya kuzingatia. Hakuna kitu kibaya kama kuoa kwa kulazimisha. Siku ndoa ikibuma mtaenda wapi kwa usuluhishi endapo mmeoana bila ridhaa. Ikishindikana jua siyo riziki yako, tafuta kwingine Mungu kakuwekea
real marrage ni mambo mengi sana
 
kwa means zote za mawasiliano zilizopo duniani umeshindwa fikisha ujumbe hapana sikubali kabisa na hoja ya jamaa something not okey. tell me the alll relative walikuwa wanajua kuwa wanaenda kutoa mahari do u think walikuwa wote wamezimia kwa ajili ya kilio wakasahau hilo hapana that family is careless... mbona walikumbuka kuomba ruhusa kazini na kuja kwenye msiba? mbona walikumbuka kuombea ruhusa wanafunzi kwa ajili ya msiba ?... mbona walikumbuka kutoa taarfa za msiba kwa ndugu na marafiki? kwa nini wasahau familia ambayo their about to be a family? think twice...ni kweli wanadharau anataka kutuambia huo msiba ulikuwa amuhsu binti no nono

Kimsingi dharau wanayo, hawana jinsi ya kukwepa hilo. Ina maana hata bwn muoaji mwenyewe hana mawasiliano na mchumbake amweleze kuwa kafiwa home??? Hapa kuna kitu, wenye mtoto wana haki ya kufura.

Ila wangerudisha roho nyuma, kama sababu ni hii tu, otherwise iwe kuna mengine yamejificha
 
Kimsingi dharau wanayo, hawana jinsi ya kukwepa hilo. Ina maana hata bwn muoaji mwenyewe hana mawasiliano na mchumbake amweleze kuwa kafiwa home??? Hapa kuna kitu, wenye mtoto wana haki ya kufura.

Ila wangerudisha roho nyuma, kama sababu ni hii tu, otherwise iwe kuna mengine yamejificha
yah ni kweli mambo ya ndoa yaendeleee
 
Back
Top Bottom