Wakili Peter Madeleka: Freeman Mbowe amechanganywa na wafungwa wanaosubiri kunyongwa gerezani

marine 1

Member
Jul 29, 2015
60
67
Nimeshtushwa na kusikitishwa sana, na hii taarifa kuwa mh. Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kuwekwa 'Condemn'. Yaan kuwekwa katika gerezani kwa kuchanganywa na wafungwa wanaosubiri kunyongwa.

Hii Ina leta maana kwamba wanamuandaa na kumtesa kisaikolojia kufanya ajiskie si chochote, na kwamba wanaweza hata kumnyonga.

Kwa kweli huu sio utu, kinyume cha haki za binadamu na kinyume cha katiba. Kwa katiba yetu, kila mtu anatakiwa kutafsiriwa kuwa huru mpaka atakapodhibitishwa na mahaka kuwa na kosa la kisheria.

Nchi ya Tanzania ni kwaajili ya watanzania wote.

----
Anaandika Wakili Peter Madeleka

Serikali ya SSH inafanya mambo yasiyokubalika kwa Freeman Aikael Mbowe.

Nilienda gereza la Ukonga na kwa bahati mbaya Sana nilikataliwa kumuona Mbowe Ingawa ninafahamika mimi ni wakili na nimeenda pale kwa mambo ya kisheria.

Kitu Cha ajabu imetolewa amri kutoka sehemu fulani na uongozi wa magereza umemtenga Mbowe na mahabusu wenzake na badala yake amewekwa pamoja na wafungwa wanaosubiri kunyongwa

Hii haikubaliki na ni Lazima kila mtu apige Kelele kwa anachofanyiwa Mbowe.

 
Hahaha!.

Mkuu acha kudanganyika.

Kwa ujinga wangu, ninafahamu kwamba wafungwa waliohukumiwa kunyongwa husafirishwa kwenda gereza la Isanga Dodoma. Ukishahukumiwa basi taratibu hufanyika uende huko ukasubiri adhabu yako.

Hivyo, hakuna wafungwa ambao wanasubiri kunyongwa katika magereza mengine yote hapa nchini.

Unadanganyika tu Mkuu.
 
Kinachosikitisha, wakati hayo Yakijiri kwa Muheshimiwa wetu...Watu Bado wameng'ang'ania Kuchangia mawazo nyuma Ya Keyboard .... ! Tujitokeze jamani kuonyesha kuwa tuna Uchungu tutoke huku nyuma ya Keyboard.Tujue kwamba Mwenzetu akitaka kujisaidia analetewa Ndoo...!
 
Chadema ilivyojaa magwiji wa sheria wanasemaje muelekeo wa kesi? Lisu haji kuongeza nguvu?
 
Ila uonevu huu kuna siku utaisha tu. Hivi yaliyomkuta nguli hayajawaohopesha wafuasi na wakiokuwa chini yake tu?? Ila Mungu wa kwetu sote
 
Kinachosikitisha, wakati hayo Yakijiri kwa Muheshimiwa wetu...Watu Bado wameng'ang'ania Kuchangia mawazo nyuma Ya Keyboard .... ! Tujitokeze jamani kuonyesha kuwa tuna Uchungu tutoke huku nyuma ya Keyboard.Tujue kwamba Mwenzetu akitaka kujisaidia analetewa Ndoo...!
Anza kwa mfano tupo nyuma yako. Mbona watu kibao wanasingiziwa kesi wanaosota miaka
 
Wewe ni muongo wa kupindukia kabisa. Kwanza Mhabusu hawachanganywi na wafungwa pia wafungwa waliaadhibiwa kunyongwa hawakai na wafungwa wengine kabisa. Acha uongo mkuu!!
Mkuu umekosea kuhusu mfungwa na mahabusu kutokukaa pamoja
Na wafungwa wanaosubiri hukumu za vifo wao huwa hawafanyi kazi za nje ila za ndani tu
 
Back
Top Bottom