Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,486
- 30,166
Wakati kampeni kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka huu zinaanza mwishoni mwa wiki hii, ni dhahiri kuwa mapambano huo utakuwa mkali sana, baina ya mgombea wa Chadema, Tundu Lissu na mgombea wa CCM John Pombe Magufuli.
Kwanza niainishe ni kwanini naona Tundu Lissu atampiku Magufuli kwenye kampeni hizo
1. Utawala huu wa awamu ya tano kupiga marufuku mikutano yote ya vyama vya siasa vya upinzani na wakati huo huo kuruhusu chama cha CCM kuwa ndiyo pekee kilichoruhusiwa kuzunguka nchi nzima, kujitangaza kwa kipindi chote cha miaka mitano mfululizo, ndiko kutakakomuongezea mgombea wa Chadema, Tundu Lissu, kwa kuwa Umma wa watanzania utakuwa na hamu kubwa kusikiliza sera za Chadema, ambazo muda mrefu sana walikuwa hawazipati.
2. Ktendo cha CCM kutegemea vyombo vyote vya dola na vyombo vyote vya habari vya Umma na vya binafsi, kuwa upande wa CCM, kutaongeza mvuto mkubwa kwa wananchi kwenda kuzisikiliza sera za Chadema.
3. Kitendo cha kuonewa kupita kiasi kwa viongozi wa Chadema, ambao wamekuwa katika mazingira magumu mno katika kipindi chote hiki cha utawala huu wa awamu ya tano chini ya Mwenyekiti wao, John Magufuli, wamekuwa wakihangaika mno kukabiliana na kesi mbalimbali, ambazo ni za kubambika, zitawaongezea Sana umaarufu, mgombea wao wa Urais Tundu Lissu na chama chake cha Chadema.
4. Lakini kitendo kikubwa kabisa ambacho kitamuongezea umarufu mno Tundu Lissu, ni kitendo cha yeye kushambuliwa kwa kupigwa risasi 16 mfululizo, akiwa ndani ya gari yake, hapo Septemba 7, mwaka 2017, mchana kweupe, tena kwenye makazi ya viongozi wakuu wa serikali hii, ambapo ni kitu ambacho siyo cha kawaida, kusikia hivi sasa takribani miaka 3, eti watu hao bado hawajajulikana!
Kwa sababu hizo Kuu, naamini kabisa mgombea wa Chadema atakuwa kama lulu, ambapo kila mwananchi atakuwa na hamu sana ya kumuona na kusikia sera zake, huku tukitarajia, CCM kama kawaida yao kutumia vyombo vya usafiri yakiwemo malori, kuwasomba wananchi sehemu mbalimbali ya nchi ili kuja kwa "kulazimishwa" kuja kumsikia mgombea wa Urais wa CCM, wakati wale watakaokwenda kumsikiliza Lissu watajitolea hata kwa kutembea kwa miguu kwa masafa marefu!
Kwanza niainishe ni kwanini naona Tundu Lissu atampiku Magufuli kwenye kampeni hizo
1. Utawala huu wa awamu ya tano kupiga marufuku mikutano yote ya vyama vya siasa vya upinzani na wakati huo huo kuruhusu chama cha CCM kuwa ndiyo pekee kilichoruhusiwa kuzunguka nchi nzima, kujitangaza kwa kipindi chote cha miaka mitano mfululizo, ndiko kutakakomuongezea mgombea wa Chadema, Tundu Lissu, kwa kuwa Umma wa watanzania utakuwa na hamu kubwa kusikiliza sera za Chadema, ambazo muda mrefu sana walikuwa hawazipati.
2. Ktendo cha CCM kutegemea vyombo vyote vya dola na vyombo vyote vya habari vya Umma na vya binafsi, kuwa upande wa CCM, kutaongeza mvuto mkubwa kwa wananchi kwenda kuzisikiliza sera za Chadema.
3. Kitendo cha kuonewa kupita kiasi kwa viongozi wa Chadema, ambao wamekuwa katika mazingira magumu mno katika kipindi chote hiki cha utawala huu wa awamu ya tano chini ya Mwenyekiti wao, John Magufuli, wamekuwa wakihangaika mno kukabiliana na kesi mbalimbali, ambazo ni za kubambika, zitawaongezea Sana umaarufu, mgombea wao wa Urais Tundu Lissu na chama chake cha Chadema.
4. Lakini kitendo kikubwa kabisa ambacho kitamuongezea umarufu mno Tundu Lissu, ni kitendo cha yeye kushambuliwa kwa kupigwa risasi 16 mfululizo, akiwa ndani ya gari yake, hapo Septemba 7, mwaka 2017, mchana kweupe, tena kwenye makazi ya viongozi wakuu wa serikali hii, ambapo ni kitu ambacho siyo cha kawaida, kusikia hivi sasa takribani miaka 3, eti watu hao bado hawajajulikana!
Kwa sababu hizo Kuu, naamini kabisa mgombea wa Chadema atakuwa kama lulu, ambapo kila mwananchi atakuwa na hamu sana ya kumuona na kusikia sera zake, huku tukitarajia, CCM kama kawaida yao kutumia vyombo vya usafiri yakiwemo malori, kuwasomba wananchi sehemu mbalimbali ya nchi ili kuja kwa "kulazimishwa" kuja kumsikia mgombea wa Urais wa CCM, wakati wale watakaokwenda kumsikiliza Lissu watajitolea hata kwa kutembea kwa miguu kwa masafa marefu!