Wahanga hawa wako wengi-Mama, mtoto wafia mapokezi ya hospitali kwa kukataliwa huduma

swala ni kudeal na mamlaka zinazohusika ili kuliondoa hili tatizo..

The most effective of dealing with this in this age of market system is through the market, by not enrolling into nursing.

A shortage of nurses will come about and they will realize how important nurses are, they will raise wages and working conditions.

My thing is you cannot sign up knowing how deplorable conditions are and then embark on a strike that will jeopardize peoples life, after you signed up nonetheless.

I understand the problem is with the biggerheads, lakini sisi wenyewe kama wananchi (hao wanaokubali kuwa nurses bila ya kuangalia maslahi kwanza kabla ya ku sign up) tunaendekeza sana njaa na matatizo yake ndiyo haya.Watu wanataka kuajiriwa tu bila kuangalia maslahi, wakiajiriwa ndiyo wanalalamika maslahi madogo, conditions mbaya.Uswahili mtupu!

Kwangu mimi ukishakuwa nurse maana yake umechukua risk ya kufa, that is bigger than any money/ resources issue.Sasa kwa nini uchukue risk ya kufa wakati wewe uko concerned sana na mshiko kuliko hata maisha yangu?

Au ni geresha tu ili mradi upate ajira?

Kuna story moja ya Engineer aliyekuwa analalamika kuwa engineers hawapati ujiko bali kila kitu kizuri kikijengwa anayepata ujiko ni architect, engineer mwingine akamjibu akamwambia kama unataka ujiko nenda Hollywood kawe actor.

Kuna kazi nyingine zinataka moyo wa sacrifice na tusitake kuwatetea wauaji eti kwa sababu ya conditions na mishahara.I understand they gotta eat and all, but damn, do they have to kill somebody? Kama wao kinachowa motivate ni mishahara they are in the wrong profession.
 
Hao wafanyakazi hawana tofauti na viongozi wa ccm wanaonunua ndege na rada mbovu kwa bei za kuruka na kuuza nchi kwa bei za karanga huku wakiacha watz wakila nyasi (kama alivyosema Mramba).

Jamani yaani inatia huruma na hasira ... yaani acha tu.

pumba ! manesi na viongozi wa ccm wapi na wapi ? pumba tupu zinakutoka !
 
Hi mentality ya "fulani must go" haitatufikisha popote.

Tuna systemic problem, tunahitaji a systemic solution.

CCM must go is more like it.Mwakyusa as a person may not be the problem and may actually be better than many a possible replacements, but what do you do when the entire system is plagued? You start an overhaul of the entire system, you do not change nuts and bolts.

i wish wengi humu wangekuwa na mind kama yako !
 
Alitaja vifaa hivyo kuwa ni pamoja na 'glovu' (mipira ya kuvaa mikononi), pamba, sindano, dawa za maumivu na maji ya uchungu.

Kama serekali inadai kuwa huduma kwa wajawazito ni bure, sioni kwanini hivyo vitu hapo juu visiwe bure. Hawa wauguzi waliohusika na tukio hili siwezi kuwashambulia directly kwa kuwa nahisi wali act according to policies zilizowekwa na 'wakubwa'.Ninachojua ni kwamba mjazito anatakiwa atoe shilingi elfu tano akienda kujifungua na serekali ina assume kwamba kila mtu atakuwa nayo.
 
msikimbilie kusema hizi kazi ni wito wito tu,hivi kwenye pesa wapi pameandikwa wito??kila kazi ni wito mazee..
wewe unafikiri mtu atajitoaje kimasomaso kama kapesa anakopata ni ka duchu hakawezi kumtoa hata kwa wiki 2?Mbunge anapiga porojo bungeni anaondoka na lundo la fwedha,iweje watu muhimu kama hawa serikali haiwajali?Kama mpiga deki wa TRL analipwa mshahara mkubwa kuliko daktari aliyesota more than 5 years kula shule ngumu na katika mazingira magumu,huu wito utatoka wapi hapa?
Pale muhimbili kuna mpaka ma surgeon hawawezi hata ku afford ka mark 2 wanakwenda kazini kwa daladala,sasa hebu jiulize huyu mtu atakuwa na morali ya kazi kweli wakati anamuona jirani yake labba yuko tigo tu ana sukuma mashine.
msikimbilie kulaumu tu ndugu zangu

Kwani hawa unaowatetea wamelazimishwa kufanya hizo kazi? Kwa mshahara huo? Kama mambo ni pesa kwa nini hao ma surgeon wasiende kupiga deki TRL? Tusiendekeze uzembe kwa kusingizia malipo duni. Wameamua kufanya hiyo kazi basi waifanye kwa uadilifu. Wakiona hawawezi, wawapishe wenzao wao wawafuate wenzao ughaibuni au kwenye siasa. Hao ma surgeon unaowatetea wamebanana kwenye mahospitali binafsi ambako wanafanya wanachokiita konsaltansi. Hawataki kuondoka Muhimbili na hospitali za serikali kwa sababu wanazitumia kama back up(maabara, support staff n.k.) ya konsaltansiz zao. Nesi anayemwangalia mja mzito anakufa kwa sababu hana glavu hastahili kubaki kwenye ajira. Uongozi unaoruhusu mwananchi wake afe kwa sababu ya kukosa glavu haustahili kuongoza.

Amandla!
 
Mama, mtoto wafia mapokezi ya hospitali kwa kukataliwa huduma
* Ni baada wauguzi kukataa kumhudumia mjamzito

Na Jackson Odoyo


MAMA mjamzito, Teddy Kimoso amefia katika mapokezi ya Hospitali ya Mwananyamala, jijini Dar es Salaam wakati akijifungua, baada ya wahudumu waliokuwa zamu kugoma kumhudumia kwa vile hakuwa na vifaa vya huduma hiyo.


Mama huyo amekufa pamoja na mtoto wake ambaye alikuwa tayari anaanza kutoka.

Duh!!! Maskini ya mungu! Mwenyezi azipumzishe roho zao mahali pema peponi. Ndugu na jamaa wa marehemu wawafungulie mashtaka hospitali ya Mwananyamala kwa uzembe uliosababisha kifo cha mama na mtoto ili walipwe fidia.
 
Usalama wa taifa mpo hapo??? Nina uhakika ikiwa Usalama wa Taifa watafuatilia hilo wataona mengi. Nendeni Amana, Temeke, na hata Muhimbili kote huko ni hayo hayo.
 
Hawa wahudumu kweli wamekula kiapo cha Florence Nightingale au ndiyo tunaokoteza watu wanaotaka kuganga njaa na kuwaita wahudumu?

Kama habari imeripotiwa vizuri, mtu anayefahamu miiko ya uhudumu hawezi kufanya hivi.Hata huku magharibi wanakoijua hela juu chini na kila mtu anapotakiwa kuwa na bima ya afya watu wanaelewa kuwa kwa mambo ya emergency (or will some argue that this is not?) huwa mtu anatibiwa kwanza halafu mengine yanaangaliwa baadaye.

Hospitali haitakiwi kukosa vifaa kwa cases kama hizi.Pia hata kama hospitali imekosa vifaa kama wakunga wa wahenga waliweza kuzalisha bila vifaa hawa maaluni kilichowashinda ni nini?

Hizi kazi zina wenyewe na sio kila mtu kujitwika kazi kwa sababu ya kuganga njaa tu, kazi zinataka watu wenye kujitoa hizi.Ndiyo maana mimi nikasema siwezi kuwa daktari.

Inasikitisha sana. Sasa tunakuwa mabepari kuliko hata hao mabepari wenyewe.Hatuna hata simile.Tunajimaliza wenyewe, by default.

mzee Pundit.. viapo vingekuwa vinamaana Tanzania unajua tusingefika huku tulikofika. Nadhani kwa wengi viapo ni kama alama ya box tu ambapo unatakiwa utiki yaishe..
 
tupitishe petition Mwakyusa must Go maana sijui anafanya nini pale... madaktari wanaacha kutibu wanakimbilia researches na kutimkia nje je kweli hii serikali inajali maisha ya watu wake kweli??
nina hasira siyo kidogo

serikali yooote kimyaaaa nw iko busy na sullivan sijui nin,
may their souls rest in peace...
ndio maana jana nikauliza hivi bongo ya sasa ni sekta gani iko na amaniii??
hivi ingekua huyo mama anaishiwa na jina la ukoo kama kikwete,lowasa etc etc hii kesi ingenyamaziwa??
may b lets wait kwa vile ni mlalahoi mwenzetu serikali ikimalizana na kina chris tucker kule arusha utasikia waziri husika anakwambia tunaunda tume kuchunguza....in which ni pesa zetu tena zatumika n de report wil b kutupwad kapuni as usual!!!yan ndo itakua kimoja hivyooo
inauma sana...nikifikiria,huwaga mi nalia............................
 
''Marehemu aliletwa hapa wodini akiwa na hali mbaya na ninadhani alishafariki kwani alipoletwa akalazwa kitandani kisha akazungushiwa pazia la kijani na ndani ya pazia hilo kulikuwa na wauguzi watatu huku mmoja akiingia na kutoka. Na baada ya hapo hawakuelewa kilichoendelea,'' alisema na kuongeza:

Sitetei uoza lakini ukiangalia statement hizo juu utaona kuwa mama huyo alifika akiwa moribund patient, na alizungukwa na manesi ambao walikuwa wakiingia na kutoka (walikua wanahangaikia kitu fulani?) je hapo mtasema hakushughulikiwa? yaonekana wazi huyo mgonjwa alifika mahututi ingawa vital sign zake( BP.Pulse rate, Record ya uchungu-Partogram etc) hatuzijui hivyo kulaumu moja kwa moja kuwa kuna uzembe mara ccm nakadhalika bila ushahidi wa kitaalamu inakuwa ngumu kidogo.na pia jamani kufiwa nako inauma hivyo ni rahisi kumtupia lawama mtu mwingine ukasahau ya kwako. ni vipi ukiambiwa kuwa alicheleweshwa akiwa kwa mganga wa kienyeji na alifika hapo beyond repair? ni vipi ukiambiwa kuwa alikuwa kapewa KOMBE na likam- intoxicate???ikumbukwe kuwa katika mahospitali yetu mtu akifa huachwa kidogo mpaka apoe (sijui nani alitunga hiyo) ndipo hupelekwa Mortuary sasa yaweza kuwa ndivyo sivyo na akina Lunyungu wakadai katelekezwa
 
Sina cha kusema inasikitisha sana na matukio haya sio mara moja.Yapo yale ambayo yanatokea wahanga wanazibwa midomo wasitoe siri hadharani kwa ajili ya kibarua cha fulani. Na yapo mengine ambayo watu hutishiwa na haya machache tunayoyasikia na kwa sababu ya uerevu wa watu tu . Yale ya kichwa na miguu ya MOI nadhani bado yanakereketa masikioni mwetu.Kuna wakati mwingine watu wanafanya kazi na kutotilia umuhimu wa kazi yao hususan linapokuja suala la maslahi. Ubinafsi,professionalism,nepotism vinatuunguza kidogokidogo.
 
Kufanya research ni sawa kabisa, ila tatizo ni serikali, maana inawezekana hizo research zinafanyika nchi za watu na kuwanufaisha wengine wakati watanzania wakiendelea kufa tu

Inauma sana.

Mkuu hawa wanaofanya research huko ni katika kutafuta mahala ambapo wanathaminiwa. Sisi serikali zetu zimekalia siasa siasa tu hakuna cha kuwaangalia wataalamu, asikudanganye mtu uwezi ukaadhirika wakati una utaalamu wako na unatakiwa mahala pengine. Huwa wanasema wema usizidi uwezo.
 
''Marehemu aliletwa hapa wodini akiwa na hali mbaya na ninadhani alishafariki kwani alipoletwa akalazwa kitandani kisha akazungushiwa pazia la kijani na ndani ya pazia hilo kulikuwa na wauguzi watatu huku mmoja akiingia na kutoka. Na baada ya hapo hawakuelewa kilichoendelea,'' alisema na kuongeza:

Sitetei uoza lakini ukiangalia statement hizo juu utaona kuwa mama huyo alifika akiwa moribund patient, na alizungukwa na manesi ambao walikuwa wakiingia na kutoka (walikua wanahangaikia kitu fulani?) je hapo mtasema hakushughulikiwa? yaonekana wazi huyo mgonjwa alifika mahututi ingawa vital sign zake( BP.Pulse rate, Record ya uchungu-Partogram etc) hatuzijui hivyo kulaumu moja kwa moja kuwa kuna uzembe mara ccm nakadhalika bila ushahidi wa kitaalamu inakuwa ngumu kidogo.na pia jamani kufiwa nako inauma hivyo ni rahisi kumtupia lawama mtu mwingine ukasahau ya kwako. ni vipi ukiambiwa kuwa alicheleweshwa akiwa kwa mganga wa kienyeji na alifika hapo beyond repair? ni vipi ukiambiwa kuwa alikuwa kapewa KOMBE na likam- intoxicate???ikumbukwe kuwa katika mahospitali yetu mtu akifa huachwa kidogo mpaka apoe (sijui nani alitunga hiyo) ndipo hupelekwa Mortuary sasa yaweza kuwa ndivyo sivyo na akina Lunyungu wakadai katelekezwa


Kinte
Naomba sema tena habati hii kwa makini .Kuna 2 stories in one .Habari ya kuzungushiwa pazia imesemwa na Mama aliyeko wodini juu ya mtu mwingine aliyekufa kabla ya huyu tunaye mlalamikia hapa .Lakini mimi nawapa onyo Mungu hamfichi mnafiki kuna siku yatawafika makubwa ya aina hii kwa uzembe sijui kama mtakuja hapa na kusema haya .

Soma umetulia utaona habaro 2 ndani ya hii moja .Usikurupuke .
 
Kwa uzembe Mwananyamala Hospital ni wazembe kupindukia kuna Gynecology mmoja yupo pale ana case za uzembe kibao alihamishwa kutoka Amana Hosp kwa ajili hiyo hiyo huyo mama atakuwa amekufa kwa uzembe, inasikitisha sana pole yao waliopoteza mama na mwana.
 
habari hizi zimenitia huzuni sana ... bora nisingesoma.

Wameshatukuta na sisi

Mzazi kazidiwa tukapewa rufaa muhimbili ... mgonjwa akawa anatizamwa kama nyani kwenye cage ... tulivyoona mda unazidi kwenda na kitoto tumboni kinazidi kupigania uhai .. tukawaambia kwamba Amana tuliambiwa kwamba mtoto anaishiwa nguvu afanyiwe upasuwaji haraka mzazi ... walitujibu kwamba amana ni kichanga kwao kwani muhimbili ndiyo mama kama si bibi wao.. tukajaribu kuhonga wee .. ubaya hatukujuwa nani alikuwa kwenye zamu maana wote walochukuwa hongo waliondoka huku zamu wakiwaachia wengine wapya.

To cut the long story short , siku ya pili tena usiku mzazi kapasuliwa ... kitoto tukakikosa ...

Laana ya Mungu iwafikiye maana wanawauwa mama na dada zetu na malaika wa Mungu wasiokuwa na hatia
 
The most effective of dealing with this in this age of market system is through the market, by not enrolling into nursing.

A shortage of nurses will come about and they will realize how important nurses are, they will raise wages and working conditions.

My thing is you cannot sign up knowing how deplorable conditions are and then embark on a strike that will jeopardize peoples life, after you signed up nonetheless.

I understand the problem is with the biggerheads, lakini sisi wenyewe kama wananchi (hao wanaokubali kuwa nurses bila ya kuangalia maslahi kwanza kabla ya ku sign up) tunaendekeza sana njaa na matatizo yake ndiyo haya.Watu wanataka kuajiriwa tu bila kuangalia maslahi, wakiajiriwa ndiyo wanalalamika maslahi madogo, conditions mbaya.Uswahili mtupu!

Kwangu mimi ukishakuwa nurse maana yake umechukua risk ya kufa, that is bigger than any money/ resources issue.Sasa kwa nini uchukue risk ya kufa wakati wewe uko concerned sana na mshiko kuliko hata maisha yangu?

Au ni geresha tu ili mradi upate ajira?

Kuna story moja ya Engineer aliyekuwa analalamika kuwa engineers hawapati ujiko bali kila kitu kizuri kikijengwa anayepata ujiko ni architect, engineer mwingine akamjibu akamwambia kama unataka ujiko nenda Hollywood kawe actor.

Kuna kazi nyingine zinataka moyo wa sacrifice na tusitake kuwatetea wauaji eti kwa sababu ya conditions na mishahara.I understand they gotta eat and all, but damn, do they have to kill somebody? Kama wao kinachowa motivate ni mishahara they are in the wrong profession.



hiyo argument yako kwa tanzania bado sana.Wanafunzi wengi wa kitanzania wako vyuoni lakini hawajui focus yao ni nini.Wanachukuliwa wanapelekwa kusomea unesi lakini hakuna mwenye utafiti tayari wa kujua mazingira ya unesi yakoje na nesi wa tanzania analipwa nini.
Kifupi mwanafunzi ana enroll kozi ama kwa kufuata mkumbo ama kwa vile taasisi ile imekuja kumchagua tu afanye ile kozi.
Kwahiyo mimi sioni mantiki ya kusema eti walaumie kwa vile wamekwenda wenyewe kufanya hospitali.
Hivi wewe unafikiri hizi hospitali zetu tayari zina manesi wa kutosha?
Kama tunataka maendeleo ya kweli basi ni lazima tukubali kuheshimu professions za watu,tukubali kuwa kwa kufanya kazi yoyote(si unesi,udaktari tu)yakupasa kuchukua risk kwa lolote ambalo litapelekea kuleta maslahi kwa jamii kubwa ya watu.Tuache kuwa wabinafsi na wanafiki.
 
kilichobaki wajimini mkiwa mwaenda hospitali kama hizo hata ka jina lako ni mwaimuna kikaragosi,badilisha jina jiite mwaimuna kikwete,raheli lowasa,fatuma shein,rose tibaigana,asha mwema..hata ukipenda ngozi nyeusi we jiite tu mwantumu rostam aziz...wakiona majina kama hayo huwa kusema kweli wanajitahidi mnoo otherwise waoneshe hela!
its a shame as if na wao siku moja hawatakuja zaa au pata shida yeyote wanasahau mganga hajigangi hata siku moja!
 
''Marehemu aliletwa hapa wodini akiwa na hali mbaya na ninadhani alishafariki kwani alipoletwa akalazwa kitandani kisha akazungushiwa pazia la kijani na ndani ya pazia hilo kulikuwa na wauguzi watatu huku mmoja akiingia na kutoka. Na baada ya hapo hawakuelewa kilichoendelea,'' alisema na kuongeza:

Sitetei uoza lakini ukiangalia statement hizo juu utaona kuwa mama huyo alifika akiwa moribund patient, na alizungukwa na manesi ambao walikuwa wakiingia na kutoka (walikua wanahangaikia kitu fulani?) je hapo mtasema hakushughulikiwa? yaonekana wazi huyo mgonjwa alifika mahututi ingawa vital sign zake( BP.Pulse rate, Record ya uchungu-Partogram etc) hatuzijui hivyo kulaumu moja kwa moja kuwa kuna uzembe mara ccm nakadhalika bila ushahidi wa kitaalamu inakuwa ngumu kidogo.na pia jamani kufiwa nako inauma hivyo ni rahisi kumtupia lawama mtu mwingine ukasahau ya kwako. ni vipi ukiambiwa kuwa alicheleweshwa akiwa kwa mganga wa kienyeji na alifika hapo beyond repair? ni vipi ukiambiwa kuwa alikuwa kapewa KOMBE na likam- intoxicate???ikumbukwe kuwa katika mahospitali yetu mtu akifa huachwa kidogo mpaka apoe (sijui nani alitunga hiyo) ndipo hupelekwa Mortuary sasa yaweza kuwa ndivyo sivyo na akina Lunyungu wakadai katelekezwa

mkuu usiwe mvivu wa kusoma hebu jifarague na hii au rudi mwanzo wa thread kisha upost tena maana inaonesha hautetei uozo bali unaushabikia...

.........Alitaja vifaa hivyo kuwa ni pamoja na 'glovu' (mipira ya kuvaa mikononi), pamba, sindano, dawa za maumivu na maji ya uchungu.
Alisema baada ya vifaa hivyo kupatikana, walimchukua na kumpeleka katika wodi ya Karume, lakini wahudumu hao waliendelea kuwa wazito kumpatia mgonjwa wao huduma kwa wakati unaohitajika.
Alifafanua hata walipoamua kwenda kwa hiyari yao, walikuwa wakitoa maneno ya kejeli kwamba anawapigia kelele wakati anafahamu utaratibu wa hospitali ulivyo.
Alisema wakati huo mtoto alikuwa ameshaanza kutoka, huku hali ya mgonjwa ikizidi kuwa mbaya
.............Ndugu mwingine aliyezungumzia suala hilo ni Yekonia Gabrieli alisema kuwa wanatarajia kumsafirisha marehemu kwenda Morogoro kwa mazishi na baada ya mazishi wataanza kufuatilia kwa undani wa kifo cha ndugu yao.
Mazingira ya kifo cha marehemu huyo, yaliwashangaza wangonjwa wengi waliokuwa hospitalini hapo, huku wakisema kuwa mama huyo alihangaika kwa muda mrefu bila kupatiwa huduma.
Mama mmoja aliyekuwa katika wodi ya Karume, alisema marehemu alipelekwa wodini hapo akiwa hajitambui huku mtoto akiwa ameanza kutoka, lakini wauguzi hao hawakuonyesha jitihada za kumsaidia.
Akizungumza kwa masharti ya kutotajwa jina lake gazetini, mgonjwa huyo alisema yeye alipelekwa hospitalini hapo tangu juzi asubuhi na akajifungua usiku na kubainisha kwamba, katika kipindi alichokaa hospitalini hapo, amejionea uzembe mwingi unaofanywa na wahudumu wa hospitali hiyo.
Alisema mbali na kifo cha marehemu Kimoso, kuna akinamama wawili walifariki dunia hospitalini hapo wakati wa kujifungua kutokana na uzembe wa wauguzi....

jitahidi mkuu
 
Haya matukio yote yanatufikisha mahali pamoja tu. "Tulipoangukia, na si tulipojikwaa". Mfumo mzima wa malezi katika familia na jamii kwa jumla hauwatayarishi wengi kubeba majukumu kwa umakini na uadilifu.

Elimu itolewayo na matarajio tunayojiandalia hayakidhi. Elimu iko duni, lakini pia mazingira ya kazi yako duni vilevile. Ni hii Vicious circle ndio inatuacha tuzunguke hapa hapa kila siku. Na ikitokea jambo ndipo tunakumbuka. Kuonyesha hii ndio hali halisi, jaribu kukumbuka matukio ya namna hii yametokea mara ngapi na nini kimefanywa kuonyesha kwamba halistahili, halitarudia na hata ikibidi kuchukua tahadhari kabla ya tukio. Kumbukumbu zangu zinanionyesha ni tunasahau kwa urahisi na watu hawajawajibishwa ipasavyo huenda ndio maana mambo haya yanarudia.

Pamoja na kuwa ni jukumu la serikali lakini kama wananchi haya ni matukio ya kila siku katika nyanja mbalimbali. Ni mpaka pale tutakapoamua kubadili mtazamo wetu kama watu binafsi, jamii ndipo tutaweza kuishinda hii hali. Mahali tulipofikia ni pabaya kweli. Kinachoonekana kwa sana na urahisi ni kunyoosha vidole nani kakosea na kakosea wapi.

Kama kianzio sio vibaya ila tukubali ni safari ndefu na ngumu. Maadili ni muhimu. Utu ni muhimu. Elimu bora ni muhimu. Lakini ajira nzuri pia muhimu. Mazingira mazuri ya kazi pia muhimu.

Sijui Mzee wa Vijisenti anajisikia vipi kwenye hali kama hii. Hizi ni zile priorities ambazo kama sio ubinafsi au malezi mabaya ya ulafi huko tulikolelewa au tulivyojilea, ndizo zingezingatiwa.

Masheikh, Mapadre, Wachungaji, Wazazi na jamii kwa ujumla tieni shime maadili yarudi. Ubinafsi, ukatili na uzembe umezidi.

Poleni waliofikwa na shida hii.
 
Jamani bonge la aibu aibu aibu sana sana tu mama mjamzito anakataliwa kujifungua kisa vifaa hospital kubwa kama Mwananyamala mmh aibu ufisadi hadi mahospital duh!! Mwakyusa tunaomba ajiuzuru.
 
Back
Top Bottom