Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 7,220
- 12,726
Nakumbuka miaka ya 90 mwishoni kuliandikwa habari kwenye magazeti kadhaa kuwa mlima Meru unaongezwa urefu. Kulikuwa na picha za Helkopta kuwa zitabeba mchanga kupeleka juu mlimani.
Picha nyingine ilimuonyesha mtu ameshika sururu eti ni mtaalamu wa kuongeza milima urefu. Iliandikwa kwa namna ya kuaminisha sana.
Na baadaye ukiamini na kuambiwa ni siku ya wajinga, unajiona mjinga hasa. Kwamba wanaongeza mlima urefu!! Kutoa habari ya sikukuu ya wajinga kunahitaji akili sana.
Sasa siku hizi hakuna ubunifu wowote wa siku ya wajinga. Mtu badala ya kutoa kitu "Absurd" anaishia kudanganya na kudai ni siku ya wajinga.
Mmoja anasema simba imetolewa superleague sababu ya kukosa vigezo. Mtu kuamini hilo si ujinga, ni jambo linalowezekana.
Mwisho aliyetoa ndiye anaonekana mjinga. Mwingine anaweza kukuambia mzazi wako kafariki!! Sasa huo kama siyo ujinga wenyewe ni nini.
Yaani nchi imejaa wajinga hadi wanashindwa kusherekea sikukuu yao wenyewe.
Picha nyingine ilimuonyesha mtu ameshika sururu eti ni mtaalamu wa kuongeza milima urefu. Iliandikwa kwa namna ya kuaminisha sana.
Na baadaye ukiamini na kuambiwa ni siku ya wajinga, unajiona mjinga hasa. Kwamba wanaongeza mlima urefu!! Kutoa habari ya sikukuu ya wajinga kunahitaji akili sana.
Sasa siku hizi hakuna ubunifu wowote wa siku ya wajinga. Mtu badala ya kutoa kitu "Absurd" anaishia kudanganya na kudai ni siku ya wajinga.
Mmoja anasema simba imetolewa superleague sababu ya kukosa vigezo. Mtu kuamini hilo si ujinga, ni jambo linalowezekana.
Mwisho aliyetoa ndiye anaonekana mjinga. Mwingine anaweza kukuambia mzazi wako kafariki!! Sasa huo kama siyo ujinga wenyewe ni nini.
Yaani nchi imejaa wajinga hadi wanashindwa kusherekea sikukuu yao wenyewe.