Quemu
JF-Expert Member
- Jun 27, 2007
- 984
- 133
Nyani,
Hao wanaongelea kitu tofauti kabisa. Labda kama wamejenga mwaka huu lakini mpaka 2007 nilipokuwa TZ hakukuwa na hizo ridges. Nafikiri kilichopo bongo ni vile vyuma ambavyo kwa kiasi fulani vinafanya kazi karibu na hiyo lakini si kwa ufanisi mkubwa.
Hizo ridges unazozisema wewe mara nyingi zinakuwa kwenye outer lanes au kwenye barabara kubwa unapokaribia roundabouts. Gari linatikisika utafikiri limepata pancha.
Mtanzania, tunaongelea hizo hizo ridges. Si zinakuwa kama bunch of stripes fulani ambazo ziko parallel? Jamani zipo. Mimi nimeziacha huko wiki tatu zilizopita. Zimejaa kibao Morogoro road.
Kama alivyosema JMushi ni kweli. Unakuta zinatangulia kabla ya tuta kubwa ili kukupunguzisha speed. Bongo bado hawajaweka pembeni ya barabara, lakini zimewekwa zikikatisha barabara.
Hata hapa Marekani, baadhi ya airport zipo za kucross barabara. Sina uhakika lakini nafikiri O'hare airport zipo.