...Utakuta wabongo huku Marekani ambao wakiulizwa na mtu hususan Mmarekani kuwa wanatoka wapi (where are you from?) wanasema eti wanatoka Jamaica? Kwa nini wanadanganya? Je ni kwa sababu wanaona aibu kusema wanatoka Tanzania ambayo iko katika bara la Afrika au wanadhani kutoka Jamaica ni "cool"? Mimi sielewei kabisa kwa nini baadhi ya watu hudanganya namna hii.
Sasa mtu unadanganya unakotoka ili iweje? Is coming from Jamaica supposed to impress somebody or what? Yaani mtu mzima una umri wa miaka thelathini na kitu halafu bado unaona noma kusema unatokea wapi. Na ikitokea siku umeulizwa na Mjamaica aliyeishi hapa Marekani kwa muda mrefu ambaye hana lafudhi ya Kijamaica na wewe ukasema unatokea Jamaica huoni kama utakuwa unajiadhirisha kwa kuongopa? Maana jamaa atakustukia tu kwa sababu Wajamaica wana lafudhi yao iliyo tofauti kabisa la lafudhi za sisi tunaotokea Afrika.
Nyinyi wabongo mnaoishi majimbo ya New York, New Jersey, Georgia, na Florida kuweni waangalifu sana maana Jamaican massive katika hayo majimbo inawakilishwa vizuri. Watu wanaoishi majimbo kama ya Nebraska, Minnesota, North Dakota, na mengine kama hayo wanaweza ku get away na uongo wao lakini huko kwingine nilikokutaja ipo siku uongo wao utawatokea puani.
Halafu nikisema Miafrika Ndivyo...........mnakasirika.