Wa mwisho ndiyo mshindi

Wa mwisho ndiyo mshindi

Mrima ndugu Mtebetini kabla sijaiona kamusi nilifikiri Ni Bara Kumbe Ni pwani.Asante Kwa Elimu
Elimu hana mwisho kila siku twajifunza na wala haina mipaka kusema kwamba mwisho hapa,ahsante nawe kwa shukuran
 
Sinema za sasa tunaangalia kwenye sebule zetu,miaka ya nyuma ilikuwa mpaka tuende kwenye majumba ya sinema hasa mijini

Mijini ilikuwa Tabu kupata tiketi za sinema mpya.Miaka hiyo Dar kulikuwa Na Empress,Empire,Drive in,Cameo zamani ilikuwa Raha Na starehe
 
Starehe mnazipenda ila maskini wa kutupa, hamna hata buku harafu kutwa mnajadili na kufikiri mambo yasiyowasaidia kuinua uchumi wa taifa.haaa, haa,haaa
 
Haaa kicheko cha kejeli ila tafadhali asiyejuwa maana hambiwa maana japo fani yako ni uandishi hapo kwenye bandiko lako kuna neno rekebisha
Harafu= Halafu
Halafu huyu ajiitae "jiwelawaashi" hatorudi tena hapa!! Ustaarabu ni kuingia jukwaani kwa heshima ndiyo utafaidi na kujifunza elimu ya dunia na mema ya kuishi kijamii....
 
Halafu huyu ajiitae "jiwelawaashi" hatorudi tena hapa!! Ustaarabu ni kuingia jukwaani kwa heshima ndiyo utafaidi na kujifunza elimu ya dunia na mema ya kuishi kijamii....
Kijamii tumekwisha mbaini hilo Jiwe la waashi ni kuku mgeni ndiyo kwanza kaingia humu jamvini na hilo bandiko lake ni la nne toka ajiunge na JF, tumsamehe kwa utovu wake nidhamu
 
Kijamii tumekwisha mbaini hilo Jiwe la waashi ni kuku mgeni ndiyo kwanza kaingia humu jamvini na hilo bandiko lake ni la nne toka ajiunge na JF, tumsamehe kwa utovu wake nidhamu

Nidhamu Ni bure ila adimu.Raha ya jukwa hili Ni kuelimisha,kustahamiliana Na kupendana
 
Back
Top Bottom