Mhaya
JF-Expert Member
- Aug 20, 2023
- 2,563
- 7,321
Ukifanya upembuzi yakinifu utagundua viongozi wengi serikalini sio kwamba hawaoni yanayotendeka.
Shida inakuja ni kuwa wenye uwezo wa kusema hapana ni wananchi wenyewe. Hivyo viongozi wengi wanasubiri kuona nguvu ya umma ikifanya maamuzi.
Fuatilia kwa umakini tu huko maofisini utagundua wengi hawaridhishwi na utendaji kazi wa serikali ya sasa. Wanangoja tu wananchi wakinukishe hili nao watoe sapoti.
Hawa viongozi wana mengi ya kusema ila hawawezi, kuhofia maisha yao. Pia wengine wanasema watanzania ni ngumu kuwapigania kwa sababu hawajali, na wanasahau shida ndani ya siku chache. Mfano polepole katekwa, baada ya wiki chache wananchi watasahau na itakuwa kama hakuna kilichotokea. Hii inafanya viongozi wengi wafyate mkia, kwa sababu wananchi wanasahau haraka.
Ni hatari sana kwa mtu mmoja kutoka mbele ya umma na kuikemea serikali, ila ni rahisi sana na salama kama umma wote wa wananchi watakuwa na kauli moja.
Ogopa sana wananchi wakichoka na wakajitoa kupambana na ukiritimba
Shida inakuja ni kuwa wenye uwezo wa kusema hapana ni wananchi wenyewe. Hivyo viongozi wengi wanasubiri kuona nguvu ya umma ikifanya maamuzi.
Fuatilia kwa umakini tu huko maofisini utagundua wengi hawaridhishwi na utendaji kazi wa serikali ya sasa. Wanangoja tu wananchi wakinukishe hili nao watoe sapoti.
Hawa viongozi wana mengi ya kusema ila hawawezi, kuhofia maisha yao. Pia wengine wanasema watanzania ni ngumu kuwapigania kwa sababu hawajali, na wanasahau shida ndani ya siku chache. Mfano polepole katekwa, baada ya wiki chache wananchi watasahau na itakuwa kama hakuna kilichotokea. Hii inafanya viongozi wengi wafyate mkia, kwa sababu wananchi wanasahau haraka.
Ni hatari sana kwa mtu mmoja kutoka mbele ya umma na kuikemea serikali, ila ni rahisi sana na salama kama umma wote wa wananchi watakuwa na kauli moja.
Ogopa sana wananchi wakichoka na wakajitoa kupambana na ukiritimba