Uzalendo unahitajika kwenye timu za taifa

Uzalendo unahitajika kwenye timu za taifa

Hata wazazi wanatumia gharama kubwa kusomesha watoto wao ila ajira hazipo atarudishwa ambaye ashapita kwenye kitengo fulani akastaafu
 
Eti jambo lolote lazima libume!
1. Ni enzi za mh. Samia yanga kafika fainali ya shirikisho caf tangu ulimwengu wa yanga kuumbwa

2. Ni enzi za mh. Samia simba kafika fainali ya shirikisho caf

3. Tangu ulimwengu kuumbwa, ni enzi hizi za mh. Samia taifa stars imefika 16 bora afcon

4. Ni enzi ya mh. Samia ligi ya tanzania imekuwa kwenye sita bora africa.

5. Tangu ulimwengu kuumbwa, ni enzi ya samia taifa u17 wamecheza fainali afcon.

6. Tangu ulimwengu uwepo, ni enzi ya samia afcon kufanyikia tanzania.

Bado wale serengeti girls walioenda kombe la dunia india, bado CHAN.

HAYA WEWE TUONYESHE AMBAYO HAYAKUBUMA ENZI ZA BARAKA TOFAUTI NA SASA!
Vijana kwenye mafanikio wanaziba macho😂😂
 
Kumuhubiria uzalendo kijana ambaye ametengenezewa dhiki ya kimkakati hata kumfanya atamani angezaliwa mbwa Ulaya au Marekani sio Jambo jepesi.
Hapana mkuu hata ulaya wanatamani sana kuishi Africa
 
Kama taifa lazima tuzikemee hizi tabia zinazochipukia Kwa Hawa vijana wa hovyo kufurahia matokeo mabaya ya mpira .....kama mdau wa soka nakemea jambo hili

Lazima tuwe wazalendo Kwa kuwa serikali inatumia gharama kubwa ku fund timu zetu😬😬😬
mnaeenda kuimba Samia shikamoh uwanjani alafu mnataka uzalendo? uzalendo wa nini kwa uchawa?
 
Kama taifa lazima tuzikemee hizi tabia zinazochipukia Kwa Hawa vijana wa hovyo kufurahia matokeo mabaya ya mpira .....kama mdau wa soka nakemea jambo hili

Lazima tuwe wazalendo Kwa kuwa serikali inatumia gharama kubwa ku fund timu zetu😬😬😬
mnaeenda kuimba Samia shikamoh uwanjani alafu mnataka uzalendo? uzalendo wa nini kwa uchawa?
 
Uzalendo unaanzia kwenye mamlaka za juu, kama hata viongozi hawana uzalendo na upendo kwa taifa lao unategemea nini?? Chuki katika mioyo ya wananchi kwa serikali hii dhalimu na iliyojaa damu ni kubwa sana, na hii tabia ya kila kizuri anapewa sifa Rais na kibaya ni chetu wote wananchi imepelekea hata watu kushabikia timu pinzani na zetu kwa sababu wanajua zikishinda sifa zote zinaenda kwa huyo Rais na machawa wake
 
Back
Top Bottom