VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Halikuwa jambo la kiungwana. Wahusika mnisikie na kunielewa. Jana, pale Ikulu Chamwino kwenye utiaji saini mikataba mitatu ya uwekezaji katika Bandari ya Dar es Salaam kati ya Serikali/TPA na DP World vilirushwa vijembe kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).

Tuliofuatilia tunajua kuwa pale ukumbini alikuwepo Askofu Liberatus Sangu kama mwakilishi wa TEC. Wahusika mkaanza kumtumia Mrisho Mpoto kurusha vijembe. Badala ya kughani au kuimba kama ilivyotarajiwa, Mpoto alitoa hotuba na kutamba alivyotaka.

Akadai kuwa kwakuwa mikataba sasa iko vizuri 'hata waliokuwa wanapinga wamehudhuria pale na watakula nao chakula'. Kila mmoja anajua kuwa waliotoa Tamko ni TEC. Na jana walikuwepo pale. Kwanini uwepo wao uonekane ni kuunga mkono mikataba iliyosainiwa jana?

Kiukweli, vijembe vya Mpoto na wengineo vilimkosesha amani na utulivu Askofu Sangu. Akajiweka 'busy' na kuchukua 'notes' huku akishindwa hata kuwatazama wazungumzaji au majirani zake. Askofu Sangu alikuwa kwenye wakati mgumu. Hakukuwa na haja ya mambo yale.

Kama maoni ya watanzania yamezingatiwa, tuonesheni mikataba iliyosainiwa jana!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Mpwapwa, Dodoma)
 
Ukiwa huhimili joto la jikoni usiingie jikoni. Kwani uongo kuna waliokuwa wakipinga kwa nia njema na waliokuwa wakipinga kwa maslahi yao binafsi. Hivyo kama ulipinga kwa nia njema na ukasikilizwa huna sababu ya kuwa uncomfortable.
 
Halikuwa jambo la kiungwana. Wahusika mnisikie na kunielewa. Jana, pale Ikulu Chamwino kwenye utiaji saini mikataba mitatu ya uwekezaji katika Bandari ya Dar es Salaam kati ya Serikali/TPA na DP World vilirushwa vijembe kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).

Tuliofuatilia tunajua kuwa pale ukumbini alikuwepo Askofu Liberatus Sangu kama mwakilishi wa TEC. Wahusika mkaanza kumtumia Mrisho Mpoto kurusha vijembe. Badala ya kughani au kuimba kama ilivyotarajiwa, Mpoto alitoa hotuba na kutamba alivyotaka.

Akadai kuwa kwakuwa mikataba sasa iko vizuri 'hata waliokuwa wanapinga wamehudhuria pale na watakula nao chakula'. Kila mmoja anajua kuwa waliotoa Tamko ni TEC. Na jana walikuwepo pale. Kwanini uwepo wao uonekane ni kuunga mkono mikataba iliyosainiwa jana?

Kiukweli, vijembe vya Mpoto na wengineo vilimkosesha amani na utulivu Askofu Sangu. Akajiweka 'busy' na kuchukua 'notes' huku akishindwa hata kuwatazama wazungumzaji au majirani zake. Askofu Sangu alikuwa kwenye wakati mgumu. Hakukuwa na haja ya mambo yale.

Kama maoni ya watanzania yamezingatiwa, tuonesheni mikataba iliyosainiwa jana!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Mpwapwa, Dodoma)
Jiwe lilirushwa gizani ajabu lilikupata wewe uliyekuwa nje ya ukumbi tena nyumbani kwako ukiangalia tv!
 
Waarabu wametumia pesa ya mafuta na TEC wakatumia ushawishi wa kanisa kutokea vatican.

Pesa ikaelea juu ya maji na ushawishi wa kukomboa mateka ukazama chini ya maji.

Maana yake ni moja kuu, masikini hana hiari linapokuja suala la uhitaji wa mlo.

Hajui kama kesho yake utapatikana mlo hivyo hula kilafi leo hata kama ameshiba. Hii ni kukaba penalty ambayo kikanuni ni kosa.

Hivi ndivyo watanzania tumeiuza haki yetu ya uzaliwa wa kwanza katika ardhi yetu kwa Waarabu.
 
Back
Top Bottom