Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,498
- 113,597
Wanabodi,
Kama kawaida yangu, kila nikipata fursa, huja na makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa". Dunia nzima, issues za Afya, Elimu, Maji, Umeme, Gesi, Usafiri na Usafirishaji ni issues zenye maslahi makubwa sana kwa taifa, hivyo leo tunaendelea na ile issue ya mabehewa yetu yaliyowasili hivi karibuni kama ni mapya au ni used, mitumba, yaliyotumika, yakafanyiwa ukarabati na kutiwa nakshi nakshi, tukaletewa tukiambiwa ni mapya, brand new kutoka kiwandani, ndio maana yameshushwa na nailoni zake tuya 'b' sisi wenyewe!.
Hii ni story mwendelezo, anzia hapa Hongera TRL kwa Mabehewa Mapya. SGR ni Reli Mpya ya Kisasa; Je, Mabehewa Haya ni Mapya ya Kisasa? Hakuna Ubaya Kutumia Mitumba, Ila Tuambiwe Ukweli!
Huu utata kuhusu haya mabehewa 'mapya' ya SGR yaliyowasili nchini hivi karibuni kutokea nchini Korea Kusini, yakiwa mapya kwenye manailoni kabisa, huku yakiwa na muundo wa kizamani, hali iliyopelekea watu kujiuliza, je, ni mapya kweli au ni used yaliyofanyiwa ukarabati na kuwekewa nakshi nakshi, kumbe ulishamalizwa kitambo sana na Rais mwenyewe, Mama Samia Suluhu Hassan, hali iliyopelekea sisi baadhi yenu kuhoji kama tumepigwa tena kama kwenye Rada! Hivyo msiwe na wasiwasi wala msiwe na mashaka kabisa, harujapigwa!
Hebu msikilize mwenyewe Rais Mama Samia,
Kama Mhe. Rais, aliisha zungumza haya, kigugumizi cha nini kwa hawa viongozi wetu wengine kuubainisha ukweli huu kama Rais wetu, Mama Samia?.
Kati ya vitu vitakavyomfanya Samia anarikiwe sana na Tanzania ya Samia kupata ustawi, ni kitendo cha huyu Mama kuwa mkweli toka ndani ya nafsi yake!. Ubarikiwe sana Mama Samia, tell the truth, and the truth will set you free!.
Hii maana yake ni mambo mawili;
1. Kuna vichwa na mabehewa mapya ambayo tumeagiza na tunatengezewa, kwa sababu it will take time, tumeagiza pia vichwa na mabehewa used kwa kuanzia ambayo tumenunua. Hivyo vichwa na mabehewa used ni kutoka nchini Ujerumani.
2. Rais amesema mzigo utakao anza kuwasili ni used. Kwa vile haya yaliyowasili kutoka Korea ya Kusini ni mabehewa 'mapya' kutoka kiwandani, na unapoagiza, unaagiza according to specifications zako, hizo box bodies mnazoziona ndiyo specifications zetu tulizoagiza, hivyo haya ni mabehewa mapya kutoka kiwandani, japo muundo wake ni wa kizamani sana.
3. Ina maana zile vichwa viwili na mabehewa 30 used kutoka Eurowagons ya Uturuki, iliyonunua Ujerumani nao utafika.
4. Kama ni kweli haya mabehewa ni mapya, Tanzania inaweza kuingia kwenye Guiness Book of Record kuwa ni nchi ya kwanza Duniani kuundiwa mabehewa kwa muda mfupi ajabu. Hivyo hiki kiwanda cha Korea, sasa ndiyo kiwanda kinachounda mabehewa kwa haraka zaidi kuliko viwanda vyote duniani.
5. Waziri Mkuu. Mhe. Kasim Majaliwa Majaliwa, alipotembelea nchini Korea Kusini kukagua kazi ya uundaji mabehewa yetu 'mapya' toka kampuni ya Sung Shin Rolling Stock Technology Company (SSRST) na hiki ndicho Waziri Mkuu alichokisema
Hii maana yake, mabehewa haya ni mapya kabisa kutoka kiwandani!.
6. Shirika la Reli Tanzania (TRC) na kampuni ya EUROWAGON ya kutoka Turkey ziliingia makubaliano Oktoba 2020 kwa ajili ya ujenzi (ukarabati na utiaji nakshi) wa vichwa viwili vya treni ya umeme na mabehewa 30 ya abiria ambao ulitegemewa kukamilika ifikapo Novemba 2021. ( mkataba huu ulikuwa ni wa vichwa na mabehewa used!)
7. TRC ilisitisha mkataba huo Februari 25, 2022 kwa madai kwamba EUROWAGON wamechelewesha kazi na
baada ya kuvunja mkataba huo Februari 25, 2022 na EUROWAGON, TRC wakaingia mkataba mpya na kampuni nyingine kwa ajili ya ukarabati wa mabehewa na kutia nakshi. Kampuni hizo ni Zeller KG Engineer (Austria), Baltic Port Service GmbH na Lueckemeir Transport Logistics GmbH (Germany)
8. TRC hawakununua vichwa na mabehewa mapya kwa ajili ya SGR, isipokuwa, EUROWAGON waliopewa zabuni walinunua vichwa 2 na mabehewa 30 used kutoka kampuni ya Reli inayomilikiwa na serikali ya Germany, DB Regio, ili kuvikarabati na kuvitia nakshi nakshi, kisha vilisajiliwa kuwa mali ya TRC.
9. TRC ilisitisha mkataba na kuwataarifu kwa barua Februari 25, 2022 na kuendelea na kazi ya kukamilisha ukarabati unaotarajiwa kukamilika Agosti mwaka 2022,” ambayo ilikamika.
10. Kwa mujibu wa Tanzania Railways Corporation, taarifa waliyoeleza kwa waandishi wa habari June 15, 2022, walisema Mkataba kati yao na EUROWAGON unaipa TRC haki ya kuchukua jukumu la kukamilisha ukarabati iwapo mzabuni atashindwa kuzingatia masharti ya mkataba, hivyo vichwa hivyo 2 na mabehewa 30 used kutoka Ujerumani tayari ni mali ya TRC!.
11. Hivyo kitendo cha kisitisha mkataba mmoja na huku tayari mzigo ni wako, halafu ukaingia mkataba mwingine na mzigo kuwasili nchini ni ndani ya miezi 5 tuu!, this goes without saying, mzigo wa mabehewa uliotua nchini!, ama ni mzigo ule ule wa used za Uerowagons ama kweli haya ni mabehewa mapya kabisa ya dukani, yaliyokuwa yakisubiri mnunuzi, baada ya kununuliwa kiwandani kabisa South Korea's Sung Shin Rolling Stock Technology Company (SSRST) na yametiwa nakshi nakshi na kuletwa nchini!, ama haya ni yale yale mabehewa mitumba ya EUROWAGON, hivyo hoja za jee mabehewa haya ni mapya ama used, bado zinaendelea hadi TRC waseme yalipo mabehewa used ya Ujerumani!
12. Japo ule mkataba wa EUROWAGON uliovunjwa ulikuwa ni vichwa na mabehewa used, by the time mkataba unavunjwa, hao EUROWAGONS waliisha lipwa malipo ya awali na kuvununua hivyo vichwa na mabehewa 30, ambayo tayari ni mali ya TRC, Watanzania tuna haki ya kuelezwa, hivyo vichwa na mabehewa ya EUROWAGONS, vilinunuliwa wapi, viliundwa lini, wapi?, vimetumika wapi na kwa muda gani kabla TRC hatujauziwa?
13. Watanzania tuelezwe ukweli gharama halisi za manunuzi ya hayo mabehewa mtumba ya Euroeagons kule Ujerumani, kuyasafirisha mpaka Korea Kusini, gharama za ukarabati na naksh naksh na gharama za usafirishaji mpaka yamepokelewa nchini, ili tufanyiwe a comparative analysis, kama tungenunua vichwa na mabehewa mapya, tungetumia gharama kiasi gani, compared na kununua vichwa na mabehewa used ili tujue tumeokoa fedha kiasi gani kwa kununua hii mitumba used?
14. Japo gharama za kununua vitu vipya ni juu ila gharama za maintenance ni ndogo, unaweza kununua kitu used kwa bei poa kumbe ni kitu chakavu sana choka mbaya, hivyo gharama ya maintenance ikawa juu kuliko hata ungenunua kipya!.
15. Ukiingia mkataba wa manunuzi, kwa matengenezo, mzigo ukanunuliwa, delivery ndio ikachelewa, huwezi kuvunja mkataba huo ukabaki salama, hivyo kesi ikifunguliwa, Tanzania tunashindwa hata kabla kesi haijaanza!.
16. Tulivunja mkataba wa Dowans, wanasheria wetu wakatuhakikishia hatutashitakiwa!, tukashitakiwa!, wanasheria wetu wakatuhakikishia tutashinda!, tukashindwa na tukadaiwa tozo ya Dowans, wanasheria wetu wakatuhakikishia hatutalipa na hawatatufanya lolote!, tena kuna wakajiapisha "over my dead body", hatulipi!.
ukweli ni kwa tumelipa every cent kisiri siri bila Watanzania kuelezwa, bila Bunge kujulishwa na kuidhinisha, bila CAG kudhibiti na kukagua!. Kwanini hatuambiwi ukweli?.
17. Tulipo vunja mkataba wa Dowans, Zitto akashauri tuitaifishe ile mitambo, waheshimiwa Wabunge wetu wakagoma kuwa Tanzania hatununui mitambo chakavu, mitambo mitumba, na kweli kwa wakati huo hatukuwa na sheria ya kununua mitambo chakavu.
18. Tulivunja mkataba ule wa Dowans kwasababu ya gharama kubwa cha capacity charges na umeme wenyewe!, Mitambo ile Dowans ikanunuliwa na Simbion, tukaingia nao mkataba ule ule wa Dowans!, kwa capacity charge ile ile!, watu wale wale walio ikataa dowams, ndio hao hao danced to the tune na Hilary Clinton kuzindua Simbion!, kwa mkataba ule ule tuliovunja!, kwa gharama zile zile!, na capacity charge ile ile!, na tukawalipa!.
19. JPM alipoingia tukavunja tena na mkataba wa Simbion, tukashitakiwa, tukashindwa, tukadaiwa, JPM akagoma kulipa!, ila baada tuu ya JPM kuitwa kule alipoitwa huku nyuma, sisi hao hao, sio tuu tumelipa!, bali pia tumeinunua ile mitambo ya Simbion kwa bei ya ajabu!, sasa mitambo ile tuliosema ni chakavu, mtumba, na serikali yetu hatununui, mitambo chakavu, sasa ndio tumeinunua!, sasa mitambo ile ya Simbion ni mitambo yetu, ni mali yetu! na malipo yote yaliisha fanyika chap chap fasta fasta!, bila bajeti yake kuombwa popote!, bila Bunge letu kuijadili, kuipitisha na kuidhinisha, bila CAG kuidhinisha malipo hayo!, na haya yote yamefanyika bila sisi Watanzania kuambiwa!, kwanini vitu vikubwa kama hivi hatuambiwi?.
20. Kichwa chetu kipya cha ukweli na mabehewa yake ni hiki.
Kitawasili kutoka Hyundai mwaka 2024.
Hitimisho
Namalizia kwa msisitizo, hakuna ubaya wowote kununua vifaa used na kutumia vitu used!, tena vingine ni vizuri, imara, bora, na madhubuti kuliko hata vipya!, na Watanzania walio wengi, kutokana na low purchasing power due to umasikini uliotopea, wengi wetu affordability yetu ni mitumba kuanzia magari, nguo hadi mitambo, hivyo tumezoea, tunachohitaji ni kuambiwa ukweli tuu!,
Tunacho demand ni kuelezwa ukweli tuu, tusiletewe mitumba hapa tukaelezwa ni mpya!, tukawa tumenunua mitumba kwa bei ya mpya!.
NB. Makala hizi ni free kutumiwa na gazeti, jarida, mtandao wowote, hazina copyright, ila source na mwandishi
Wasalaam
Paskali
Kama kawaida yangu, kila nikipata fursa, huja na makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa". Dunia nzima, issues za Afya, Elimu, Maji, Umeme, Gesi, Usafiri na Usafirishaji ni issues zenye maslahi makubwa sana kwa taifa, hivyo leo tunaendelea na ile issue ya mabehewa yetu yaliyowasili hivi karibuni kama ni mapya au ni used, mitumba, yaliyotumika, yakafanyiwa ukarabati na kutiwa nakshi nakshi, tukaletewa tukiambiwa ni mapya, brand new kutoka kiwandani, ndio maana yameshushwa na nailoni zake tuya 'b' sisi wenyewe!.
Hii ni story mwendelezo, anzia hapa Hongera TRL kwa Mabehewa Mapya. SGR ni Reli Mpya ya Kisasa; Je, Mabehewa Haya ni Mapya ya Kisasa? Hakuna Ubaya Kutumia Mitumba, Ila Tuambiwe Ukweli!
Huu utata kuhusu haya mabehewa 'mapya' ya SGR yaliyowasili nchini hivi karibuni kutokea nchini Korea Kusini, yakiwa mapya kwenye manailoni kabisa, huku yakiwa na muundo wa kizamani, hali iliyopelekea watu kujiuliza, je, ni mapya kweli au ni used yaliyofanyiwa ukarabati na kuwekewa nakshi nakshi, kumbe ulishamalizwa kitambo sana na Rais mwenyewe, Mama Samia Suluhu Hassan, hali iliyopelekea sisi baadhi yenu kuhoji kama tumepigwa tena kama kwenye Rada! Hivyo msiwe na wasiwasi wala msiwe na mashaka kabisa, harujapigwa!
Hebu msikilize mwenyewe Rais Mama Samia,
Kama Mhe. Rais, aliisha zungumza haya, kigugumizi cha nini kwa hawa viongozi wetu wengine kuubainisha ukweli huu kama Rais wetu, Mama Samia?.
Kati ya vitu vitakavyomfanya Samia anarikiwe sana na Tanzania ya Samia kupata ustawi, ni kitendo cha huyu Mama kuwa mkweli toka ndani ya nafsi yake!. Ubarikiwe sana Mama Samia, tell the truth, and the truth will set you free!.
Hii maana yake ni mambo mawili;
1. Kuna vichwa na mabehewa mapya ambayo tumeagiza na tunatengezewa, kwa sababu it will take time, tumeagiza pia vichwa na mabehewa used kwa kuanzia ambayo tumenunua. Hivyo vichwa na mabehewa used ni kutoka nchini Ujerumani.
2. Rais amesema mzigo utakao anza kuwasili ni used. Kwa vile haya yaliyowasili kutoka Korea ya Kusini ni mabehewa 'mapya' kutoka kiwandani, na unapoagiza, unaagiza according to specifications zako, hizo box bodies mnazoziona ndiyo specifications zetu tulizoagiza, hivyo haya ni mabehewa mapya kutoka kiwandani, japo muundo wake ni wa kizamani sana.
3. Ina maana zile vichwa viwili na mabehewa 30 used kutoka Eurowagons ya Uturuki, iliyonunua Ujerumani nao utafika.
4. Kama ni kweli haya mabehewa ni mapya, Tanzania inaweza kuingia kwenye Guiness Book of Record kuwa ni nchi ya kwanza Duniani kuundiwa mabehewa kwa muda mfupi ajabu. Hivyo hiki kiwanda cha Korea, sasa ndiyo kiwanda kinachounda mabehewa kwa haraka zaidi kuliko viwanda vyote duniani.
5. Waziri Mkuu. Mhe. Kasim Majaliwa Majaliwa, alipotembelea nchini Korea Kusini kukagua kazi ya uundaji mabehewa yetu 'mapya' toka kampuni ya Sung Shin Rolling Stock Technology Company (SSRST) na hiki ndicho Waziri Mkuu alichokisema
Hii maana yake, mabehewa haya ni mapya kabisa kutoka kiwandani!.
6. Shirika la Reli Tanzania (TRC) na kampuni ya EUROWAGON ya kutoka Turkey ziliingia makubaliano Oktoba 2020 kwa ajili ya ujenzi (ukarabati na utiaji nakshi) wa vichwa viwili vya treni ya umeme na mabehewa 30 ya abiria ambao ulitegemewa kukamilika ifikapo Novemba 2021. ( mkataba huu ulikuwa ni wa vichwa na mabehewa used!)
7. TRC ilisitisha mkataba huo Februari 25, 2022 kwa madai kwamba EUROWAGON wamechelewesha kazi na
baada ya kuvunja mkataba huo Februari 25, 2022 na EUROWAGON, TRC wakaingia mkataba mpya na kampuni nyingine kwa ajili ya ukarabati wa mabehewa na kutia nakshi. Kampuni hizo ni Zeller KG Engineer (Austria), Baltic Port Service GmbH na Lueckemeir Transport Logistics GmbH (Germany)
8. TRC hawakununua vichwa na mabehewa mapya kwa ajili ya SGR, isipokuwa, EUROWAGON waliopewa zabuni walinunua vichwa 2 na mabehewa 30 used kutoka kampuni ya Reli inayomilikiwa na serikali ya Germany, DB Regio, ili kuvikarabati na kuvitia nakshi nakshi, kisha vilisajiliwa kuwa mali ya TRC.
9. TRC ilisitisha mkataba na kuwataarifu kwa barua Februari 25, 2022 na kuendelea na kazi ya kukamilisha ukarabati unaotarajiwa kukamilika Agosti mwaka 2022,” ambayo ilikamika.
10. Kwa mujibu wa Tanzania Railways Corporation, taarifa waliyoeleza kwa waandishi wa habari June 15, 2022, walisema Mkataba kati yao na EUROWAGON unaipa TRC haki ya kuchukua jukumu la kukamilisha ukarabati iwapo mzabuni atashindwa kuzingatia masharti ya mkataba, hivyo vichwa hivyo 2 na mabehewa 30 used kutoka Ujerumani tayari ni mali ya TRC!.
11. Hivyo kitendo cha kisitisha mkataba mmoja na huku tayari mzigo ni wako, halafu ukaingia mkataba mwingine na mzigo kuwasili nchini ni ndani ya miezi 5 tuu!, this goes without saying, mzigo wa mabehewa uliotua nchini!, ama ni mzigo ule ule wa used za Uerowagons ama kweli haya ni mabehewa mapya kabisa ya dukani, yaliyokuwa yakisubiri mnunuzi, baada ya kununuliwa kiwandani kabisa South Korea's Sung Shin Rolling Stock Technology Company (SSRST) na yametiwa nakshi nakshi na kuletwa nchini!, ama haya ni yale yale mabehewa mitumba ya EUROWAGON, hivyo hoja za jee mabehewa haya ni mapya ama used, bado zinaendelea hadi TRC waseme yalipo mabehewa used ya Ujerumani!
12. Japo ule mkataba wa EUROWAGON uliovunjwa ulikuwa ni vichwa na mabehewa used, by the time mkataba unavunjwa, hao EUROWAGONS waliisha lipwa malipo ya awali na kuvununua hivyo vichwa na mabehewa 30, ambayo tayari ni mali ya TRC, Watanzania tuna haki ya kuelezwa, hivyo vichwa na mabehewa ya EUROWAGONS, vilinunuliwa wapi, viliundwa lini, wapi?, vimetumika wapi na kwa muda gani kabla TRC hatujauziwa?
13. Watanzania tuelezwe ukweli gharama halisi za manunuzi ya hayo mabehewa mtumba ya Euroeagons kule Ujerumani, kuyasafirisha mpaka Korea Kusini, gharama za ukarabati na naksh naksh na gharama za usafirishaji mpaka yamepokelewa nchini, ili tufanyiwe a comparative analysis, kama tungenunua vichwa na mabehewa mapya, tungetumia gharama kiasi gani, compared na kununua vichwa na mabehewa used ili tujue tumeokoa fedha kiasi gani kwa kununua hii mitumba used?
14. Japo gharama za kununua vitu vipya ni juu ila gharama za maintenance ni ndogo, unaweza kununua kitu used kwa bei poa kumbe ni kitu chakavu sana choka mbaya, hivyo gharama ya maintenance ikawa juu kuliko hata ungenunua kipya!.
15. Ukiingia mkataba wa manunuzi, kwa matengenezo, mzigo ukanunuliwa, delivery ndio ikachelewa, huwezi kuvunja mkataba huo ukabaki salama, hivyo kesi ikifunguliwa, Tanzania tunashindwa hata kabla kesi haijaanza!.
16. Tulivunja mkataba wa Dowans, wanasheria wetu wakatuhakikishia hatutashitakiwa!, tukashitakiwa!, wanasheria wetu wakatuhakikishia tutashinda!, tukashindwa na tukadaiwa tozo ya Dowans, wanasheria wetu wakatuhakikishia hatutalipa na hawatatufanya lolote!, tena kuna wakajiapisha "over my dead body", hatulipi!.
ukweli ni kwa tumelipa every cent kisiri siri bila Watanzania kuelezwa, bila Bunge kujulishwa na kuidhinisha, bila CAG kudhibiti na kukagua!. Kwanini hatuambiwi ukweli?.
17. Tulipo vunja mkataba wa Dowans, Zitto akashauri tuitaifishe ile mitambo, waheshimiwa Wabunge wetu wakagoma kuwa Tanzania hatununui mitambo chakavu, mitambo mitumba, na kweli kwa wakati huo hatukuwa na sheria ya kununua mitambo chakavu.
18. Tulivunja mkataba ule wa Dowans kwasababu ya gharama kubwa cha capacity charges na umeme wenyewe!, Mitambo ile Dowans ikanunuliwa na Simbion, tukaingia nao mkataba ule ule wa Dowans!, kwa capacity charge ile ile!, watu wale wale walio ikataa dowams, ndio hao hao danced to the tune na Hilary Clinton kuzindua Simbion!, kwa mkataba ule ule tuliovunja!, kwa gharama zile zile!, na capacity charge ile ile!, na tukawalipa!.
19. JPM alipoingia tukavunja tena na mkataba wa Simbion, tukashitakiwa, tukashindwa, tukadaiwa, JPM akagoma kulipa!, ila baada tuu ya JPM kuitwa kule alipoitwa huku nyuma, sisi hao hao, sio tuu tumelipa!, bali pia tumeinunua ile mitambo ya Simbion kwa bei ya ajabu!, sasa mitambo ile tuliosema ni chakavu, mtumba, na serikali yetu hatununui, mitambo chakavu, sasa ndio tumeinunua!, sasa mitambo ile ya Simbion ni mitambo yetu, ni mali yetu! na malipo yote yaliisha fanyika chap chap fasta fasta!, bila bajeti yake kuombwa popote!, bila Bunge letu kuijadili, kuipitisha na kuidhinisha, bila CAG kuidhinisha malipo hayo!, na haya yote yamefanyika bila sisi Watanzania kuambiwa!, kwanini vitu vikubwa kama hivi hatuambiwi?.
20. Kichwa chetu kipya cha ukweli na mabehewa yake ni hiki.
Kitawasili kutoka Hyundai mwaka 2024.
Hitimisho
Namalizia kwa msisitizo, hakuna ubaya wowote kununua vifaa used na kutumia vitu used!, tena vingine ni vizuri, imara, bora, na madhubuti kuliko hata vipya!, na Watanzania walio wengi, kutokana na low purchasing power due to umasikini uliotopea, wengi wetu affordability yetu ni mitumba kuanzia magari, nguo hadi mitambo, hivyo tumezoea, tunachohitaji ni kuambiwa ukweli tuu!,
Tunacho demand ni kuelezwa ukweli tuu, tusiletewe mitumba hapa tukaelezwa ni mpya!, tukawa tumenunua mitumba kwa bei ya mpya!.
NB. Makala hizi ni free kutumiwa na gazeti, jarida, mtandao wowote, hazina copyright, ila source na mwandishi
Wasalaam
Paskali