Utata kifo cha Nusura, Ndugu wahoji uharaka wa mazishi bila uchunguzi

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
1683796107364.png

Picha: Nusura Abdala enzi za uhai wake​

Vumbi la kifo cha mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Nusura Abdalah bado linazidi kutimka baada ya ndugu kutilia mashaka uharaka wa mazishi yake huku baba mkubwa wa marehemu akija na maswali matano.

Wakati umma ukiendelea kupaza sauti ukitaka majibu juu ya kifo cha mwanafunzi huyo, mwanamume anayedaiwa kuwa mpenzi wake, Salim Kundyah (47) na ndiye aliyempeleka Hospitali ya Faraja iliyopo Himo, ameruka viunzi kulizungumzia.

Kwa nyakati tofauti jana, Rais wa Jumuiya ya Wanafunzi Elimu ya Juu (Tahliso), Maria John alisema wanasubiri taarifa ya uchunguzi huo huku Rais wa Serikali ya wanafunzi UDOM (UDOSO), Tryphone Mwinuka akisema hawezi kulizungumzia.

Taarifa kutoka hospitali hiyo zilizomkariri daktari aliyemhudumia, Peter Minja zilieleza mwanafunzi huyo alifikishwa hospitalini hapo Mei 1, mwaka huu kati ya saa 2 na 3 usiku na mpenzi wake huyo, wakati huo akiwa ni mgonjwa mahututi.

Kwa mujibu wa daktari huyo, vipimo vya awali vilionyesha sukari ilikuwa juu katika kiwango kisicho cha kawaida huku akiwa na upungufu wa damu na kwamba alifariki dunia wakati madaktari wakiendelea na jitihada za kukokoa maisha yake.

Hata hivyo, pamoja na maelezo hayo, mitandao ya kijamii imekuwa ikihusisha kifo hicho na ajali ya Naibu Waziri Tamisemi, Dk Festo Dugange iliyotokea usiku wa Aprili 26, mwaka huu jijini Dodoma huku wengine wakikihusisha na kipigo.

Tayari Jeshi la Polisi nchini kupitia kwa msemaji wake, David Misime wametangaza kuanza uchunguzi kutokana na utata huo, uchunguzi utakaoshirikisha Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) na Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali.

Misime alipotafutwa tena jana ili kufahamu maendeleo ya uchunguzi huo, aliwataka wananchi kuendelea kuwa na subira katika kipindi hiki ambacho uchunguzi unaendelea na uchunguzi ukikamilika umma utajulishwa matokeo.

Juzi, Ofisi ya Rais Tamisemi ilitoa taarifa kwa umma kukanusha Dk Dugange kuwa amejizulu wadhifa wake ili kupisha uchunguzi.

“Taarifa hiyo ni uzushi na wananchi wanaombwa kuipuuza kwani Dk Dugange hajajiuzulu wadhifa wake huo. Bado ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais-Tamisemi na Mbunge wa Wang’ingombe mkoani Njombe anaendelea na matibabu Hospitali ya Benjamin Mkapa,” ilieleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Nteghenjwa Hosseah, Msemaji wa Ofisi hiyo

Msingi wa madai hayo ya kujizulu ni baada ya baadhi ya watu mitandaoni kumtaka naibu waziri huyo ajiuzulu ili kupisha uchunguzi wa sakata hilo analotuhumiwa nalo la ajali hiyo na Nusura ambayo hata hivyo imekwisha kanushwa na Polisi.

Maswali 5 ya baba mkubwa
Baba mkubwa wa marehemu aliyejitambulisha kama Ali Seleman alisema kifo hicho kina utata na yeye ana maswali matano yanayomuumiza kichwa na kueleza siku ya mazishi yalikuja magari matano yakiwa na mwili na waombolezaji.

“Mmmm, kuna utata. Ukiniuliza naweza kusema kifupi hapa ndipo alipozikwa, lakini maswali mengi nitashindwa kuyajibu. Baba wa huyu mtoto ni mdogo wangu tumbo moja, lakini msiba ulivyofika hadi tunazika bado sielewi,” alisema Ali.

Ali (67) anayeishi Kitongoji cha Mtakuja kijijini hapo kwenye eneo la familia huku mdogo wake (Baba wa Nusura) yeye akiishi Mtaa wa Kiwanja cha ndege Singida mjini ambako msafara wa kusindikiza mwili wa Nusura ndiko ulikoanzia.

Mzee Ali anaeleza yapo maswali matano ambayo angetamani kuyajua kuhusu msiba wa binti wa mdogo wake lakini kwa namna ilivyo ameshindwa na amekosa mtu wa kumjibu kwani yeye na mdogo wake walikaa muda usiozidi saa moja walipofika hapo kuzika kisha wakaondoka na msafara wote.

Miongozi mwa maswali yanayomtatiza ni je, Nusura alikuwa na mchumba? Alitokaje Dodoma ghafla kwenda Kilimanjaro? Kwanini hawakusachi nguo zake wapate tiketi aliyosafiria? Kwanini ahusishwe na ajari nyingine Dodoma? Kwa nini mdogo wake alikubali kumzika bila kufanya uchunguzi?

“Hili la kufanya uchunguzi wa mwili lilikuwa muhimu, lakini hadi tunamzika mimi sikuwa najua kuhusu utata baadae ndiyo wanakijiji nasikia wanasema,mwanzo nilipokea taarifa kwamba Nusura amefariki ghafla na baadae mdogo wangu akasema tuandae malalo wanakuja kuzika huku,” anasema.

“Lakini siku ya kumsitiri ulikuja msafara wa magari kama matano hivi, walifikia eneo la kaburi kama unavyojua mdogo wangu hana mji hapa, ile wamemaliza kuzika akasema hakuna arobaini na msiba ndiyo umekwisha hapo, mimi sina simu nizungumze naye kwa hiyo hadi nitafute nauli nikamhani huko mjini,”alisema.

Hata hivyo anasema taarifa za msiba aliambiwa kuwa ulitokea Moshi ambako anakiri kuwa wapo ndugu wachache huko lakini kwamba mdogo wake (baba mzazi wa marehemu) alifanya kazi kwa miaka mingi kiwanda cha sukari TPC.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mtakuja, Omari Said ambaye anaishi jirani na lilipo kaburi la binti huyo, alisema mazingira ya msiba tangu awali yalishaonyesha utata na hata mazishi yake kwa wenyeji bado yaliwaacha na sintofahamu.

Said anasema mara baada ya kupokea taarifa za msiba, hakukuwa na maelezo zaidi wala mtu aliyetoka mjini ambaye angeweza kuwasimulia mkasa mzima isipokuwa waliombwa kutafuta vijana wachimbe kaburi kwa ajili ya maziko.

“Basi niliita vijana na Mzee Ali akatuonyesha mahali pa kuchimba, wale wenzetu walikuja na magari kama matano au sita hivi wakazika na muda huo huo wakaondoka wote tukabaki sisi ambao tangu mwanzo hatukuwa tunajua kitu,”

Hata hivyo anakiri kumfahamu binti huyo katika kipindi cha uhai wake kwani amewahi kufika hapo mara kadhaa kwa shangazi yake ambayo ni nyumba ya tatu kutoka anapoishi Mwenyekiti huyo na kwamba alikuwa na taarifa kuwa anasoma Dodoma ingawa hakujua anasoma chuo gani na fani gani.

Kiongozi huyo anakiri kuna mkanganyiko wa taarifa kwani awali waliambiwa alifikwana mauti akiwa Dodoma lakini ghafla wakapata taarifa alikuwa Moshi kwa hiyo hawajafahamu mazingira halisi ukizingatia kuwa wahusika wote wapo mjini.

Mpenzi wa Nusura apiga chenga
Gazeti hili lilifanya jitihada za kumtafuta Salim Kundyah (47) anayetajwa na uongozi wa hospitali kuwa ndiye mpenzi wa Nusura na ndiye aliyempeleka hospitali ya Faraja ziligonga mwamba baada ya kutoa ahadi zisizotekelezeka.

Mei 7, mwaka huu mwanaume huyo aliahidi kuonana na Mwandishi wa Gazeti hili Mjini Moshi lakini alipotafutwa siku hiyo alisema amebanwa kikazi hivyo hawataweza kuonana naye licha ya kusisitiza hataki kuzungumzia suala hilo kwenye simu.

Hata hivyo alimuahidi mwandishi hiyo kuwa atatoka Arusha na kwenda Moshi ili kuonana naye ana kwa ana kwa kile alichodai kuwa hawezi kumpa taarifa kwa njia ya simu kwa kuwa hana uhakika kwamba ni mwandishi kweli au la.

Mei 8, 2023 alipotafutwa tena kwa njia ya simu kujua alipo ili wakutane kama alivyoahidi, napo ilishindikana kwa kuwa alidai amebanwa na kazi na hawezi kutoka na kumuahidi wataonana siku inayofuata ambayo ni jana Jijini Arusha.

Mwandishi hakukata tamaa alimfuata hadi Arusha na alipofika alimpigia simu kujua alipo ili amfuate kwa ajili ya mahojiano lakini alipofika Arusha alimweleza kuwa hayupo Arusha anaelekea Singida kupeleka ndugu wa waliofiwa.

Tahliso, UDOSO wafunguka
Gazeti hili lilipomtafuta Rais wa Tahliso, Maria John Thomas kuhusu sakata hilo na ukimya wao katika suala hilo alisema kwa kifupi “Tunasubiri uchunguzi (wa Polisi, DPP na mkemia mkuu wa Serikali) na hatuwezi kutoa kauli yoyote kwa sasa”

Rais wa UDOSO, Mwinuka alipoulizwa jana kuhusu kutoa tamko kuhusiana na kifo cha mwanafunzi Nusura Abdallah alisema hawawezi kutoa tamko tofauti na lililotolewa na Makamu mkuu wa Chuo UDOM, Profesa Lughano Kusiluka.

Mwinuka alisema Chuo kina idara maalum ya kutoa taarifa nje ya Chuo na hana mamlaka ya kutoa tamko kwa mujibu wa taratibu wa Chuo chao.

“Taarifa zozote zinazohusiana na masuala ya uhusiano na matangazo kuna idara maalum ambazo zinatoa taarifa kwa umma lakini msemaji mkuu ni Mkamu mkuu wa Chuo na tamko lake lilishaonekana kupitia barua ya Afisa uhusiano, hata taarifa zetu sisi wanafunzi nazipeleka kwa Makamu,”alisema Mwinuka.

Simulizi ya mwandishi kutoka kijijini
Ni umbali wa kurusha jiwe kutoka katika nyumba ndogo iliyojengwa kwa matofari ya udongo upande wa Magharibu, kuna kitu mfano wa tuta pembeni kukiwa na miti minne iliyochomekwa kila kona.

Haihitaji kuambiwa lakini kwa mila za Kiafrika hili ni kaburi, tena ni la muda usiozidi wiki moja tangu shughuli za mazishi zilipofanyika katika eneo hilo ambalo lina kaburi moja pekee chini ya mti unaojulikana kwa lugha ya wenyeji ‘msugala’.

Safari ya kufika hapo ilikuwa ni kushuhudia mahali ulipolala mwili Nusura, watu wawili wamenifika hapa ambao ni Baba mkubwa wa Marehemu na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mtakuja kijiji cha Kikonge wilaya ya Iramba mkoani Singida.

“Ni hapa hapa ndipo tulipomsitiri binti yetu, inaumiza mioyo lakini kwenye ukoo bado kuna maswali makubwa matano hayana majibu, hata hivyo mtoaji ni Mungu na anayetwaa ni yeye kwa wakati wake, acha iwe hivyo,” anasema mmojawao.

Siyo rahisi kumaliza utata wa maswali ya namna kifo kilivyotokea na mazingira yake, kwani fumbo hilo ameondoka nalo binti huyo aliyekuwa anasubiriwa na familia na Taifa kutumika miongoni mwa wasomi.

Miongoni mwa utata wa maswali kwenye msiba huo ambayo hata Polisi wameona kuna haja ya kufanya uchunguzi ni hatua ndefu za kutoka Dodoma kwenda mkoani Kilimanjaro na hata mauti kumfika akiwa Hospitali ya Faraja, Kilimanjaro.

Ugumu kumpata Baba
Gazeti hili lilifanya jitihada za kumpata Mzee Hassan Abdallah, baba mzazi wa marehemu au mama yake kwa nyakati tofauti ikiwemo kufika nyumbani kwake, mjini kati eneo maarufu la stendi ya zamani, mkoani Singida bila mafanikio.

Kabla ya kwenda, mwandishi alipata taarifa kwa siku mbili mfululizo baadhi ya watu walikwenda na kukutana naye lakini hakuwa tayari kuzungumza jambo ambalo hakuliamini.

Nilipofika hapo nilipokewa na mtu ambaye alikuwa anaingia ndani ya nyumba aliyeomba nikaribie wakati anakwenda kuwaita wenyeji ambao hata hivyo alitoka msichana anayekadiriwa kuwa na miaka kati ya 19 hadi 20 aliyenidadisi kwa maswali mengi.

Msichana huyo alikwepa kujibu yale niliyomuuliza ndipo akasema,"sasa kama si ndugu huwezi kumuona mzee kwani anatakiwa kutosema jambo lolote kuhusu msiba,". Licha ya kugoma kuingia ndani kumuita baba mwenye nyumba, lakini alieleza marehemu ni dada yake.

Kuhusu watu waliofika kwenye mazishi hayo, anasema Shekh aliyeongoza mazishi hayo ni Athuman Hussein (Shekh Ulaya) alitoa shukrani akiwatambua wageni kutoka Moshi waliosindikiza mwili na wengine aliwataja kutoka Dodoma licha ya kuwa hakuna waliosimama kusema neno bali walitajwa hivyo hajui walikuwa akina nani.

Nyumbani kwao singida
Katika Mtaa wa Kiwanja cha Ndege kwenye nyumba ya kawaida, masufuria yamejaa nje kuashiria kulikuwa na pilika za chakula cha kusanyiko,hata hivyo inakuwa vigumu kuwapata wazazi wa Nusura kwani sharti la hapo ni kutokusema kitu kwa sasa kwa madai kuna vyombo vinachunguza.

Hata hivyo mdogo wake anayeitwa Ummukulthum anatoka nje na kuzungumza kwa ufupi “Tumempoteza mtu muhimu ambaye tulimtarajia kuwa msaada kwa siku za usoni, ni dada yangu tumezaliwa pamoja yeye akiwa mtoto wa tatu, baba hawezi kusema hadi hapo vyombo vya uchunguzi vitakapomaliza kazi yao.”

Binamu wa marehemu Seleman Segu ambaye ni mtoto wa shangazi ya marehemu Nusura, anasema kuwa kilichoficha ukweli wa msiba wa dada yake siyo aliyefariki bali uharaka wa kumzika.

Seleman anaeleza kuwa taarifa za msiba zilitolewa kwa haraka wakati huo naye alikuwa Moshi, lakini alipokwenda kufuatilia kwa ndugu wakasema tayari wamesafirisha na siku ya pili anafunga safari kurudi nyumbani akaambiwa wamezika mchana huo.

“Muulize mtu yeyote, mimi nilianza kulala toka siku hiyo nikamwambia mjomba kwamba tulichofanya si chema, hili jambo tungejua ukweli wake kama pangefanyika uchunguzi kidogo wa mwili kabla ya kuzika, haya maswali tusingeulizwa lakini mjomba wangu dini imemkaa sana ndiyo maana kila kitu kwake ni ndiyo tu,” anasema.

Seleman anasema taarifa zilimkuta akiwa TPC Moshi akifuatilia haki zake baada ya kupunguzwa kazini, lakini anasema mbali na mahusiano mazuri yaliyokuwepo baina yake na dada yake huyo, hakuwahi kusikia kama alikuwa na mchumba.

Safari ya kufika Kikonge
Ili uweze kufika katika kijiji hiki ambacho ni kikubwa, yakupasa kujifunga mkanda na hasa ukiwa mgeni na mazingira ya usafiri wa eneo husika.

Anzia Singida mjini, popote ulipo waulize wenyeji wakupeleke stendi ya Mkombozi, imeitwa hivyo kwa sababu ukuta wake unapakana na shule kongwe ya msingi ya Ukombozi. Usafiri wa hapa ni gari ndogo aina ya Noha.

Kwa hakika jifunge mkanda, ni mateso na adhabu kwa mgeni, lakini ni wanaishi sawa na msemo wa wahenga hiyari yashinda utumwa kwani burudani ya muziki inatosha kuwaburudisha na kuwariwaza.

Watu wazima ndani ya Noah tulikuwa 17, watoto wawili,juu mizigo usipime, safari inaanzia Mkombozi tunazunguka kupitia Sekondari ya Senge kisha kutokeza Uhasibu. Kumbuka njia hiyo inatusaidia kuwakwepa Polisi wa usalama barabarani.

Mbele kidogo anapanda anaongezeka abiria ambaye anakwenda kukaa juu ya mizigo kukamilisha idadi ya watu 20 kwenye gari hiyo yenye uwezo wa kubeba watu 8 wanaomjumlisha dereva.

Sikiliza, tunakaa hivi, dereva mbele amekaa na watu wazima wawili na mtoto mmoja ambayo jumla yao ni wanne, yeye akiendesha kwa kukaa upande,sehemu ya pili wamekaa wanne, sehemu ya tatu wanne wakimpaka kijana wa darasa la nne au tano lakini viti vyao vimelazwa ili kupisha watu wanne kukaa nyuma sehemu ya mizigo, mtu mmoja amejikunja akisimama sehemu ya kati ya kulalia mwegemeo wa viti vya nyumba ndipo mwingine anakaa juu ya gari kulinda mizigo.

Ni kweli kuwa barabara si ya lami lakini haina mashimo kama maeneo mengine, lakini mwendo wa gari hiyo unaweza kuomba maji. Tunatumia dakika 87 kufika kituoni na anayeshuka ni mimi peke yangu gari ikielekea Ndola ambako ndiko mwisho wa safari.

Ili usijazane hivyo, yakupasa kupanda pikipiki hadi Kaselya (mahali alipozikwa Dk Sima aliyeuawa kwa mapanga wiklayani Tarime) ambako Noha zinabeba watu 10 tu lakini gharama yake ukijumlisha na usafiri wa pikipiki ni sawa na nauli ya basi kutoka Singida kwenda Mwanza.

MWANANCHI
 
Mshahara wa dhambi ni mauti!

Kililichosikitisha ni kutoa taarifa ya kishezi eti binti kafia Moshi badala ya ukweli wa ajali ya Dodoma!

Aibu sana sana na ni dhambi mbaya kabisa!
 
Vumbi la kifo cha mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Nusura Abdalah bado linazidi kutimka baada ya ndugu kutilia mashaka uharaka wa mazishi yake huku baba mkubwa wa marehemu akija na maswali matano...
Mwananchi nawapa heko kwa kujua kuchimba habari hafi kutufikia
 
Mwananchi nalo linaandika Kama kiu
Mwananchi wapo vizuri baadhi ya magazeti yapo kimya hawa jamaa wamejaribu kuichimba hii habari na kuwaachia wachunguzi mwanzo walitupakia rangi na taarifa ya uongo ya Chuo hata aliesambaza ile taarifa hajakamatwa ukitaka ujue hii ni Bongo...
 
Mikono yao imejaa damu za wananchi waliowapigia kura , inasikitisha sana kwa uhuni huu... mpaka kesho naendelea kuamini TRump was right, Africa countries are shiit holes.
 
Naibu waziri aseme tu alikula hiyo mafuta.Famchezo na V8 nn,hata Mimi ningetembeza sana vijiko Kwa totozi.Solusheni mawaziri wanunuliwe bajaji
 
Iramba. Vumbi linazidi kutimka kwenye sakata la kifo cha mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Nusura Abdallah baada ya ndugu kutilia shaka uharaka wa mazishi yake na kuibua maswali matano.

Wakati umma ukiendelea kupaza sauti ukitaka majibu ya uchunguzi wa kifo hicho, mwanamume anayedaiwa kuwa mpenzi wa mwanafunzi huyo na aliyempeleka Hospitali ya Faraja iliyopo Himo, ameruka viunzi kulizungumzia.

Vilevile, kwa nyakati tofauti jana viongozi wa taasisi za wanafunzi walisita kuzungumzia sakata hilo linaloendelea na uchungzi.

Wakati hayo yakiendelea, Ofisi ya Rais Tamisemi imetoa taarifa kwa umma ikikanusha taarifa za mitandaoni kuwa Naibu Waziri Dk Festo Dugange amejiuzulu wadhifa wake ili kupisha uchunguzi wa sakati hilo.

“Taarifa hiyo ni uzushi na wananchi wanaombwa kuipuuza, kwani Dk Dugange hajajiuzulu wadhifa wake huo. Bado ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais-Tamisemi na Mbunge wa Wang’ingombe mkoani Njombe anaendelea na matibabu Hospitali ya Benjamin Mkapa,” ilieleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Nteghenjwa Hosseah, msemaji wa ofisi hiyo.

Msingi wa madai hayo ni taarifa za mitandaoni zilizohusisha kifo cha Nusura na ajali aliyopata Dk Dugange, taarifa ambazo tayari zinachunguzwa na Polisi, Ofisi ya Mashtaka, Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali na vyombo vingine vya haki jinai.

Uchunguzi huo unafanyika, licha ya awali jeshi hilo mkoani Dodoma kukanusha taarifa zilizokuwa zinasambaa kuwa katika ajali hiyo Dk Dugange alikuwa na mwanamke ambaye alifariki dunia.

Maswali matano
Mbali na uchungizi huo, Mwananchi limezungumza na baba mkubwa wa marehemu aliyejitambulisha kama Ali Seleman, alidai kifo hicho kina utata na yeye ana maswali matano yanayomuumiza kichwa.

Alidai siku ya mazishi yalifika magari matano yakiwa na mwili wa marehemu na waombolezaji na baada ya mazishi wakaondoka.

“Mmmm, kuna utata. Ukiniuliza naweza kusema kifupi hapa ndipo alipozikwa, lakini maswali mengi nitashindwa kuyajibu. Baba wa huyu mtoto ni mdogo wangu tumbo moja, lakini msiba ulivyofika hadi tunazika bado sielewi,” alidai Ali.

Ali (67) anaishi Kitongoji cha Mtakuja kijijini Kikonge, kwenye eneo la familia huku mdogo wake (baba wa Nusura) yeye akiishi Mtaa wa Kiwanja cha Ndege, mjini Singida ambako msafara wa kusindikiza mwili wa Nusura ulianzia.

Mzee Ali anadai yapo maswali matano ambayo angetamani kuyajua kuhusu msiba wa binti huyo, lakini kwa namna ilivyo ameshindwa na amekosa mtu wa kumjibu, kwani yeye na mdogo wake walikaa muda usiozidi saa moja walipofika hapo kuzika, kisha wakaondoka na msafara wote.

Miongozi mwa maswali hayo ni je, Nusura alikuwa na mchumba? Alitokaje Dodoma ghafla kwenda Kilimanjaro? Kwa nini hawakusachi nguo zake wapate tiketi aliyosafiria? Kwa nini ahusishwe na ajali nyingine Dodoma? Kwa nini mdogo wake alikubali kumzika bila kufanya uchunguzi?

“Hili la kufanya uchunguzi wa mwili lilikuwa muhimu, lakini hadi tunamzika mimi sikuwa najua kuhusu utata, baadaye ndiyo wanakijiji nasikia wanasema. Mwanzo nilipokea taarifa kwamba Nusura amefariki ghafla na baadaye mdogo wangu akasema tuandae malalo wanakuja kuzika huku,” anadai.

“Lakini siku ya kumsitiri ulikuja msafara wa magari kama matano hivi, walifikia eneo la kaburi kama unavyojua mdogo wangu hana mji hapa, ile wamemaliza kuzika akasema hakuna arobaini na msiba ndio umekwisha hapo. Mimi sina simu nizungumze naye, kwa hiyo hadi nitafute nauli nikamhani huko mjini,” alidai

Hata hivyo, anadai aliambiwa msiba ulitokea Moshi ambako anasema wapo ndugu wachache huko na kwamba mdogo wake (baba mzazi wa marehemu) alifanya kazi kwa miaka mingi katika Kiwanda cha Sukari TPC.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mtakuja, Omari Said ambaye anaishi jirani na lilipo kaburi la binti huyo, alidai mazingira ya msiba tangu awali yalishaonyesha utata na hata mazishi yenyewe yaliwaacha wenyeji na sintofahamu.

Said anadai mara baada ya kupokea taarifa za msiba, hakukuwa na maelezo zaidi wala mtu aliyetoka mjini ambaye angeweza kuwasimulia mkasa mzima isipokuwa waliombwa kutafuta vijana wachimbe kaburi kwa ajili ya maziko.

“Basi niliita vijana na Mzee Ali akatuonyesha mahali pa kuchimba, wale wenzetu walikuja na magari kama matano au sita hivi wakazika na muda huo huo wakaondoka wote, tukabaki sisi ambao tangu mwanzo hatukuwa tunajua kitu,” alisema.

Hata hivyo anasema alimfahamu binti huyo wakati wa uhai wake, kwani amewahi kufika hapo mara kadhaa kwa shangazi yake ambayo ni nyumba ya tatu kutoka anapoishi mwenyekiti huyo na kwamba alikuwa na taarifa kuwa anasoma Dodoma.

Kiongozi huyo anasema kuna mkanganyiko wa taarifa kwa kuwa awali waliambiwa Nusura alifikwa na mauti akiwa Dodoma, lakini ghafla wakapata taarifa alikuwa Moshi, hivyo hawajafahamu mazingira halisi.

Mpenzi wa Nusura aingia mitini
Jitihada za Mwananchi kumtafuta mwanamume anayetajwa kama mpenzi wa Nusura (jina tunalo), anayetajwa na uongozi wa Hospitali ya Faraja kuwa ndiye aliyempeleka hapo ziligonga mwamba baada ya kutoa miadi isiyotekelezeka.

Mei 7, mwaka huu, mwanamume huyo, aliyetajwa kuwa na umri wa miaka 47 aliahidi kuonana na mwandishi wa gazeti hili mjini Moshi, akitokea Arusha lakini alipotafutwa muda aliotaja alisema amebanwa kikazi hivyo, hataweza na kusisitiza kuwa hataki kuzungumzia suala hilo kwenye simu.

Alisisitiza anataka kuonana na mwandishi kwa ana kwa ana kwa kuwa hakuwa na uhakika kwamba kweli ni mwandishi

Mei 8, 2023 alipotafutwa tena kama alivyoahidi, pia ilishindikana na kuahidi tena siku iliyofuata (jana) jijini Arusha.

Mwandishi alipomfuata Arusha na kumpigia simu kujua alipo ili amfuate kwa mahojiano, alimweleza kuwa hayupo tena Arusha, bali yuko njiani anaelekea Singida kuwapeleka ndugu wa waliofiwa.

Nyumbani Singida
Katika Mtaa wa Kiwanja cha Ndege kwenye nyumba ya kawaida, masufuria yamejaa nje kuashiria kulikuwa na pilika za chakula cha kusanyiko. Hata hivyo inakuwa vigumu kuwapata wazazi wa Nusura, kwani sharti la hapo ni kutokusema kitu kwa sasa kwa madai kuna vyombo vinachunguza.

Hata hivyo mdogo wake anayeitwa Ummukulthum anatoka nje na kuzungumza kwa ufupi: “Tumempoteza mtu muhimu ambaye tulimtarajia kuwa msaada kwa siku za usoni, ni dada yangu tumezaliwa pamoja yeye akiwa mtoto wa tatu, baba hawezi kusema hadi hapo vyombo vya uchunguzi vitakapomaliza kazi yao.”

Binamu wa marehemu, Seleman Segu ambaye ni mtoto wa shangazi ya marehemu Nusura, anasema kuwa kilichoficha ukweli wa msiba wa dada yake si aliyefariki, bali uharaka wa kumzika.

Seleman anaeleza kuwa taarifa za msiba zilitolewa kwa haraka wakati huo naye alikuwa Moshi, lakini alipokwenda kufuatilia kwa ndugu wakasema tayari wamesafirisha na siku ya pili anafunga safari kurudi nyumbani akaambiwa wamezika mchana huo.

“Muulize mtu yeyote, mimi nilimwambia mjomba kwamba tulichofanya si chema, hili jambo tungejua ukweli wake kama pangefanyika uchunguzi kidogo wa mwili kabla ya kuzika, haya maswali tusingeulizwa lakini mjomba wangu dini imemkaa sana, ndiyo maana kila kitu kwake ni ndiyo tu,” anasema.

Seleman anasema taarifa zilimkuta akiwa TPC Moshi akifuatilia haki zake baada ya kupunguzwa kazini, lakini anasema mbali na mahusiano mazuri yaliyokuwepo baina yake na dada yake huyo, hakuwahi kusikia kama alikuwa na mchumba.

Gazeti hili lilifanya jitihada za kumpata Hassan Abdallah, baba mzazi wa marehemu, ikiwemo kufika nyumbani kwake, mjini kati eneo maarufu la Stendi ya Zamani, mkoani Singida bila mafanikio.

Kabla ya kwenda, mwandishi alipata taarifa kuwa hakuwa tayari kuzungumza jambo hilo, ambalo hakuliamini.
“Nilipofika hapo nilipokewa na mtu aliyeomba nikaribie ndani wakati anakwenda kuwaita wenyeji. Ndipo alifika msichana anayekadiriwa kuwa na miaka kati ya 19 hadi 20 aliyenidadisi kwa maswali mengi, kisha akasema haitawezekana kuwaona wenyeji.

Sasa wewe kama si ndugu huwezi kumuona mzee, kwani anatakiwa kutosema jambo lolote kuhusu msiba,” alisema binti huyo aliyeeleza kuwa marehemu ni dada yake.

Safari ya kijijini
Umbali wa kurusha jiwe kutoka katika nyumba ndogo ya matofali ya udongo upande wa magharibi, kuna tuta ambalo pembeni kuna miti minne iliyochomekwa katika kila kona.

Haihitaji kuambiwa lakini kwa mila za Kiafrika hili ni kaburi, tena ni la muda usiozidi wiki moja katika eneo ambalo lina kaburi moja pekee, chini ya mti unaojulikana kwa lugha ya wenyeji ‘msugala’.

Safari ya kufika hapo ilikuwa ni kushuhudia mahali ulipolala mwili wa Nusura. Watu wawili wamefika hapo – Baba mkubwa wa marehemu na mwenyekiti wa Kitongoji cha Mtakuja kijiji cha Kikonge wilaya ya Iramba mkoani Singida.

“Ni hapa hapa ndipo tulipomsitiri binti yetu, inaumiza mioyo lakini kwenye ukoo bado kuna maswali makubwa matano hayana majibu, hata hivyo mtoaji ni Mungu na anayetwaa ni yeye kwa wakati wake, acha iwe hivyo,” anasema mmoja wao.

Safari hadi Kikonge
Ili kufika katika kijiji cha Kikonge ambacho ni kikubwa, yakupasa kujifunga mkanda na hasa ukiwa mgeni na mazingira ya usafiri wa eneo husika.

Anzia Singida mjini, popote ulipo waulize wenyeji wakupeleke stendi ya Mkombozi, imeitwa hivyo kwa sababu ukuta wake unapakana na Shule kongwe ya Msingi Ukombozi. Usafiri wa hapa ni gari ndogo aina ya Noah.

Kwa hakika jifunge mkanda, ni mateso na adhabu kwa mgeni, lakini ni wanaishi sawa na msemo wa wahenga hiari yashinda utumwa, kwani burudani ya muziki inatosha kuwaburudisha na kuwaliwaza.

Watu wazima ndani ya Noah tulikuwa 17, watoto wawili, juu mizigo usipime. Safari inaanzia Mkombozi tunazunguka kupitia Sekondari ya Senge kisha kutokeza Uhasibu. Kumbuka njia hiyo inatusaidia kuwakwepa askari wa usalama barabarani.

Mbele kidogo anaongezeka abiria ambaye anakwenda kukaa juu ya mizigo kukamilisha idadi ya watu 20 kwenye gari hilo lenye uwezo wa kubeba watu wanane wanaomjumlisha dereva.

Sikiliza, tunakaa hivi, dereva mbele amekaa na watu wazima wawili na mtoto mmoja ambayo jumla yao ni wanne, yeye akiendesha kwa kukaa upande, sehemu ya pili wamekaa wanne, sehemu ya tatu wanne wakimpakata kijana wa darasa la nne au tano lakini viti vyao vimelazwa ili kupisha watu wanne kukaa nyuma sehemu ya mizigo.

Mtu mmoja amejikunja akisimama sehemu ya kati na kulalia mwegemeo wa viti vya nyuma huku mwingine akikaa juu ya gari kulinda mizigo.

Ni kweli kuwa barabara si ya lami lakini haina mashimo kama maeneo mengine, lakini mwendo wa gari hiyo unaweza kuomba maji. Tunatumia dakika 87 kufika kituoni na anayeshuka ni mimi peke yangu, gari likielekea Ndola ambako ndiko mwisho wa safari.

Ili usijazane hivyo, yakupasa kupanda pikipiki hadi Kaselya (mahali alipozikwa Isack Sima, daktari aliyeuawa kwa mapanga wilayani Tarime wiki iliyopita)

Katika eneo hilo, Noah zinabeba watu 10 tu lakini gharama yake ukijumlisha na usafiri wa pikipiki ni sawa na nauli ya basi kutoka Singida kwenda Mwanza.

Subira Tahliso, Udoso
Gazeti hili lilipomtafuta Rais wa Shirikisho la Vyama vya wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu Tanzania (Tahliso), Maria Thomas kuhusu sakata hilo na ukimya wao, alisema kwa kifupi “tunasubiri uchunguzi (wa Polisi, DPP na mkemia mkuu wa Serikali) na hatuwezi kutoa kauli yoyote kwa sasa.”

Naye Rais wa Chama cha Wanafunzi Udom, Udoso, Tryphone Mwinuka alipoulizwa kuhusiana na kifo cha mwanafunzi mwenzao, alisema hawawezi kutoa tamko tofauti na lililotolewa na Makamu Mkuu wa Chuo Udom, Profesa Lughano Kusiluka.

“Taarifa zozote zinazohusiana na masuala ya uhusiano na matangazo kuna idara maalumu ambazo zinatoa taarifa kwa umma, lakini msemaji mkuu ni Makamu Mkuu wa Chuo na tamko lake lilishaonekana kupitia barua ya ofisa uhusiano, hata taarifa zetu sisi wanafunzi nazipeleka kwa makamu,” alisema Mwinuka.

Ilivyokuwa hospitali
Taarifa kutoka hospitali hiyo zilizomnukuu daktari aliyemhudumia, Peter Minja zilieleza mwanafunzi huyo alifikishwa hospitalini hapo Mei 1, mwaka huu kati ya saa 2 na 3 usiku na mpenzi wake akiwa mahututi.

Kwa mujibu wa daktari huyo, vipimo vya awali vilionyesha sukari ilikuwa juu katika kiwango kisicho cha kawaida, huku akiwa na upungufu wa damu na kwamba alifariki dunia wakati madaktari wakiendelea na jitihada za kukokoa maisha yake.

Hata hivyo, pamoja na maelezo hayo, mitandao ya kijamii imekuwa ikihusisha kifo hicho na ajali iliyotokea usiku wa Aprili 26, mwaka huu jijini Dodoma, huku wengine wakikihusisha na kipigo, masuala ambayo yanachunguzwa.

Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime alipotafutwa tena jana ili kufahamu maendeleo ya uchunguzi huo, aliwataka wananchi kuendelea kuwa na subira katika kipindi hiki ambacho uchunguzi unaendelea na uchunguzi ukikamilika umma utajulishwa matokeo.

MWANANCHI
 
Hii ngoma watu waliipika kiujinga sana, inavyoonekana wende kunamakubwa zaidi nyuma ya pazia, mfano wenda akawa aliuwawa baada ya ajali.
 
Aisee umaskini mbaya sana watu wamenyamazishwa shwaaa 🤐.lakini wakumbuke karma is a bitch. hivi angekuwa alie kufa ni mtoto wa kigogo ingekuwaje
 
Singida/Dodoma. Wakati Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) ikitia mguu katika uchunguzi wa kifo cha Nusura Hassan Abdallah, wazazi wake wameibuka pia kukizungumzia huku wakiibua maswali zaidi.

nusura-pic.jpg
Nusura, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) alifariki dunia Mei mosi katika Hospitali ya Faraja iliyopo Himo mkoani Kilimanjaro, huku mazingira ya kifo hicho yakizua utata baada ya kuhusishwa na ajali iliyotokea Dodoma, ikimhusisha pia Naibu Waziri wa Tamisemi, Dk Festo Dugange.

Wakati tukio zima likiendelea kugubikwa na sintofahamu, wazazi wa binti huyo hawakuwa wamezungumza chochote, achilia mbali baba yake mkubwa, Ali Selemani aliyeibua maswali matano.

Jana, baba na mama mzazi wakiambatana na binti yao (dadake Nusura) walijitokeza mbele ya waandishi wa habari mjini Singida kuzungumzia kifo hicho kinachodaiwa kutokea Aprili 29 mwaka huu.

Tofauti na maswali yaliyoibuliwa na baba mkubwa wa marehemu, wazazi hao pia wameibua mengine juu ya kifo hicho ambacho kimeendelea kuzua mjadala.

Katikati ya sintofahamu hiyo, THBUB imesema itafanya uchunguzi huru katika mikoa ya Singida, Kilimanjaro na Dodoma kwa madhamuni ya kujua ukweli wa tukio hilo.

Kauli ya wazazi
Hassan Abdallah, baba mzazi wa marehemu akiambatana na mkewe, Amina Shaban na binti yao Kuruthumu Hassan walikutana na waandishi wa habari nyumbani kwao Uwanja wa Ndege, eneo la Sabasaba mkoani Singida, wakieleza kushangazwa baada ya kukuta “mwili wa binti huyo umevalishwa kanzu.”

Nusura alikuwa anasoma Shahada ya kwanza ya Sanaa katika Elimu, katika Ndaki ya Jinsia na Sayansi ya Jamii.

Walieleza pia kushangazwa jinsi wanavyoendelea kusikia mchumba wa marehemu ambaye wanakiri kumtambua, akiendelea kuvinjari uraiani bila kuchukuliwa hatua hata kuhojiwa.

Pia, kukutwa na matapishi kwenye moja ya nguo za binti yao na namna alivyoumwa bila kupewa taarifa hadi walipopokea kifo.

Familia hiyo ilizungumza jana ikiwa ni siku moja tangu gazeti hili kufika kijiji cha Kikonge, wilayani Iramba ulipozikwa mwili wa Nusura na kuzungumza na wanafamilia wengine, akiwemo baba mkubwa wa marehemu aliyejitambulisha kama Ali Seleman ambaye alidai kifo hicho kina utata na yeye akahoji maswali matano.

Miongozi mwa maswali hayo ni je, Nusura alikuwa na mchumba? Alitokaje Dodoma ghafla kwenda Kilimanjaro? Kwa nini hawakusachi nguo zake wapate tiketi aliyosafiria? Kwa nini ahusishwe na ajali nyingine Dodoma? Kwa nini mdogo wake alikubali kumzika bila kufanya uchunguzi?

Wakati Mzee Ali akihoji hayo, jana wazazi wake Nusura walijibu maswali mbalimbali ya waandishi wa habari kuhusu kifo hicho, huku wakijitenga na ajali iliyotokea Dodoma wakidai hadi Aprili 26, mwaka huu walikuwa na mawasiliano na mtoto wao.

Baba wa marehemu Nusura, Mzee Hassan Abdallah alisema wao kama familia hawana kitu chochote cha kuhusisha kifo hicho na mtu mwingine zaidi ya kuomba aliyejitokeza kama mchumba wake ndiye ahojiwe.

“Tunachoweza kujiuliza ni jinsi gani huyo aliyekuwa na binti yetu bado yupo uraiani, hajahojiwa, hatujui kama atahojiwa, lakini hatukujua kuhusu uchumba huo, hakuja kwenye mazishi,” alisema Hassan.

Awali, mama mzazi wa mwanafunzi huyo, Amina Shaban, alisema Aprili 29 mwaka huu alimpigia simu mtoto wake Nusura, lakini iliita mara nyingi na haikupokelewa, kitendo kilichompa hofu kwani hakuwa na kawaida ya namna hiyo.

Mama huyo alisema siku iliyofuata aliendelea kumtafuta kwenye simu lakini hakupatikana, ndipo ikabidi afanye juhudi kutafuta namba ya simu ya rafiki yake ambaye pia ni mwanafunzi wa UDOM.

“Mwanafunzi huyo akaniomba nimpe nafasi amtafute halafu angenipa majibu, hakufanikiwa kumpata mwanangu, ndipo akaniomba nipokee namba ya mwanafunzi mwingine ambaye pia ni rafiki wa Nusura,” alisema Amina.

Alisema siku iliyofuata alimpigia mwanafunzi huyo ambaye alimjulisha mtoto wake hayupo alikwenda kwa mchumba wake aliyeko Marangu mkoani Kilimanjaro, ambaye kwa mujibu wa maelezo ya mama huyo alishaelezwa habari za uchumba huo.

Alisema mtoto wake, Nusura, wakati akiwa kwenye mazoezi ya vitendo (field), alipata mchumba (jina tunalihifadhi) ambaye ni Mwalimu kwenye shule ya sekondari iliyopo Marangu ambayo hata hivyo hakuitaja.

“Mwanafunzi huyo alisema, siku za hivi karibuni, Nusura alitumiwa ujumbe mfupi wa maandishi kutoka kwa mchumba wake huyo kupitia simu, kwamba anamhitaji haraka Marangu na mwanangu alimuonyesha ujumbe huo rafiki yake huyo wanayesoma naye, hata hivyo, mwenzake alihoji ni kwa nini anatumiwa meseji za aina hiyo,” alisema Amina.

Kwa mujibu wa mama huyo, licha ya rafiki yake kuhoji hayo, lakini Nusura alifunga safari kwenda Marangu, Kilimanjaro kwa ajili ya kuonana na mchumba wake huyo ambaye hata hivyo familia haimfahamu.
Alisema mbali na taarifa hiyo, kijana huyo hakuonekana hospitalini, hakuonekana msibani na wala haijajulikana hizo meseji alizomtumia zilihusu nini, lakini walishangazwa kukuta mwili umevishwa kanzu.

“Ndipo nikampigia simu huyo kijana ambaye kwa kweli hakuna mtu ambaye anamfahamu, hata kwa sura, ndipo akasema mwanafunzi alifika kwake lakini aliugua homa ya ghafla na kufariki dunia,” alisema

Mshangao wa dada
Akizungumza kwenye kusanyiko hilo, Dada yake na marehemu, Kuruthumu Hassan, alieleza kushangazwa mwili wa marehemu Nusura kupelekwa ukiwa umevalishwa kanzu wakati Nusura alikuwa ni mwanamke.

Kuruthumu alisema hadi sasa hawajashirikishwa kuhusu kifo cha ndugu yao huyo na hawajui matapishi na mabaki ya chakula waliyoyaona kwenye moja ya nguo za marehemu, ambayo wanazo taarifa yamepelekwa kwa mkemia.

“Kwa mtindo huu, tuna uhakika hatutapata sababu halisi iliyochangia kifo cha ndugu yetu kama hayo majibu ya wakemia hayajatufikia, lakini tunasikitishwa zaidi na kwa nini (anamtaja huyo mchumba wa mdogo wake), bado yupo uraiani, hajachukuliwa hatua zozote za kisheria,” alisema Kuruthumu.

Tume yajitosa
Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Tume Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu alisema takribani wiki mbili, tume imekuwa ikiona katika vyombo vya habari taarifa inayohusu ajali ya Naibu Waziri wa Tamisemi, Dk Ndugange iliyotokea Dodoma ikihusishwa na kifo cha mwanafunzi huyo.

Jaji Mwaimu alisema taarifa hizo zimenukuliwa kutoka Jeshi la Polisi, Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Hospitali ya Faraja iliyopo Himo, Mkoa wa Kilimanjaro na taarifa za wananchi kupitia mitandaoni.

Hata hivyo, alisema Tume inatambua uwepo wa vyombo vinavyoshughulikia masuala ya haki jinai, hususani Jeshi la Polisi na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na kwamba Tume inavipa heshima vyombo hivyo katika utekelezaji wa majukumu yake.

“Tume imeazimia kufanya uchunguzi huru kwa madhumuni ya kubaini ukweli kuhusu matukio hayo,” alisema mwenyekiti huyo.

Alipoulizwa watajikita katika maeneo yapi katika uchunguzi huo, alisema watafanya katika maeneo yote yaliyotajwa Dodoma, Kilimanjaro na Singida ili kupata ukweli hasa kwa kuzingatia kwamba yanasemwa mambo mengi kutoka maeneo tofauti na taarifa zinapishana.

Jaji alisema uchunguzi utaanza mara moja na mchakato unaendelea na mara watakapokamilisha watatoa majibu ili kuondoa sintofahamu katika jamii.

Chanzo:- Mwananchi
Pitia tena taarifa ya UDOM

UDOM.jpg
 
Back
Top Bottom