Utajiri wa matajiri wanne Kenya unazidi Wakenya milioni 22 wakiunganishwa kwa pamoja. Tanzania vipi?

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,447
7,832
Oxfam imesema matajiri wanne nchini Kenya, utajiri wao unazidi karibu nusu ya wakenya wote(40%) wakichanganywa kwa pamoja. Matajiri hao wana utajiri unaofikia Ksh. bilioni 333( Tsh. trilioni 6.26).

Utafiti unaonesha ukuaji wa tofauti kati ya walio nacho na wasio nacho ambapo wakenya 130 matajiri zaidi wanamiliki mali sawa na 70% bajeti ya Kenya kwa mwaka. Matajiri watano zaidi nchini Kenya ni Merali, Shah, Bedi, Kenyatta na Mahendra wakiwa na utajiri wa jumla ya dola za kimarekani 3.2.

Duniani, watu walijizalishia mifukoni $ trilioni 42 miaka miwili iliyopita, asilimia moja ya watu duniani wamechukua 2/3 ya utajiri huo huku 99% ya watu wakigombania 1/3 iliyobaki. Kwa mara ya kwanza katika miaka 25 utajiri wa kutisha na umasikini wa kutisha vimeongezeka kwa pamoja.

Hali ya watanzania ikoje kwenye dunia hii ya kibepari!

Pia, jisomee HAPA

Oxfam.jpg
 
1. Manu Chandaria yupo wapi? Moi family wamefilisika? Ongeza upcoming Ruto & Associates,

2. Uzuri Wanasiasa wa Kenya hawaibi Kwa kificho na wanawekeza Kenya, Uganda na kununua Benki DRC, tofauti na TZ wanaenda kuficha Uswisi.

3. Kesi za Anne Waiguru, Sonko na Kidero ziliishia wapi?

RIP Dr Mengi
 
Hii iko hivi kote nchi za dunia ya pili na tatu, wenye nacho ni 0.1% huku makapuku wakiwa 99.9%
The top 1% of households in the United States held 32.3% of the country's wealth, while the bottom 50% held 2.6%.
 
sijajua kosa lake hasa ni lipi!

kununua kitu kibichi mbona sio kosa?
Wivu tu na ujinga unawasumbua!
Mie nikajua kayaiba shambani hayo maparachichi kumbe kauziwa na wakulima kwa hiari yao wenyewe.

Basi kama ni kosa polisi ikawakamate na hao wakulima kwa kuuza maparachichi mabichi.
 
This world is not fair
Ndio maana Nyerere alitaka leta equality kwenye keki ya taifa ila capitalism inaleta fairness.. Unachoweza kung'ata ndio utaweza kula ONLY.
 
Oxfam imesema matajiri wanne nchini Kenya, utajiri wao unazidi karibu nusu ya wakenya wote(40%) wakichanganywa kwa pamoja. Matajiri hao wana utajiri unaofikia Ksh. bilioni 333( Tsh. trilioni 6.26)...
When you convert that money in dollars it means that there is no any dollar billionaire in Kenya .
 
When you convert that money in dollars it means that there is no any dollar billionaire in Kenya .
Hii inamaanisha Tanzania gap ni kubwa zaidi maana tunae/tunaona wanaofika dola bilioni huku uchumi wa jumla ukiwa mdogo kuliko Kenya!
 
Sijajua kosa lake hasa ni lipi!

Kununua kitu kibichi mbona sio kosa?
Ni kosa kubwa hasa kwenye medani za ushindani kibiashara. Tanzania tunaonekana products yetu haipo vizuri kumbe kuna jinga mmoja anataka kutuharibia.

Mfano waziri amesema kwa kuuzwa parachichi hizo kutoka Tanzania na huyo mkenya zisizokomaa nje ya nchi wizara inaletewa notification za warning za kutosha..hii maana yake tunaharibiwa vibaya sana.

Mbona Kenya hawafanyi hivyo.
 
Oxfam imesema matajiri wanne nchini Kenya, utajiri wao unazidi karibu nusu ya wakenya wote(40%) wakichanganywa kwa pamoja. Matajiri hao wana utajiri unaofikia Ksh. bilioni 333( Tsh. trilioni 6.26)...
Naona hapo Uhuru Kenyatta anayo a modest sh60 bilion.
 
Back
Top Bottom