Kenya 2022 MAHESABU YA KURA: Kumbe elimu ya Kenya ipo chini sana na upeo wa wakenya upo chini mnoo!

Kenya 2022 General Election

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,131
35,167
Kituko kikubwa cha karne kuhusu hesabu leo kimeonekana huko Kenya baada ya makamishina wanne wa tume ya uchaguzi waliotangaza kujitoa kwenye mchakato wa kutangaza matokeo ya urais kuja na hoja finyu za ukilaza wa mahesabu.

Mbali na sababu zingine walizozitoa, kubwa lilikuwa ni wao kujenga hoja kwenye mahesabu ya matokeo kwenye mambo mawili.

-Wao kushangaa hesabu ya jumla ya kura zilizovutwa (round off) kuwa 100.01% (Kitu ambacho kimahesabu kiko sahihi)

-Kudai kuwa hiyo 0.01% iliyozidi wao wanaitafsiri katika kura zote (milioni 14) ni sawa na kura 140,000. (Kitu ambacho sio sahihi, usahihi ni kura 1400)

Ajabu ni kuwa, wahusika waliojenga hoja hizo walijitamba kuwa wao ni wasomi na karibu kila mtu kwa Kenya ni msomi wa kuweza kuchambua hayo mahesabu. Na mwisho hoja zao zikachukuliwa na kupigiwa debe na mamilioni ya wakenya wanaomuunga mkono upande wa Raila Odinga.

Hizo hesabu za desimali na makadirio huwa zinazofundishwa watoto wa darasa la nne hapa Tanzania na nyingine kurejewa kwa kina kidato cha kwanza.

Ni aibu kubwa kwa taifa la Kenya, ukilaza unaposhabikiwa na kuungwa mkono.

Poleni Wakenya kwa hii aibu.
 
Kituko kikubwa cha karne kuhusu hesabu leo kimeonekana huko Kenya baada ya makamishina wanne wa tume ya uchaguzi waliotangaza kujitoa kwenye mchakato wa kutangaza matokeo ya urais kuja na hoja finyu za ukilaza wa mahesabu.

Mbali na sababu zingine walizozitoa, kubwa lilikuwa ni wao kujenga hoja kwenye mahesabu ya matokeo kwenye mambo mawili.

-Hesabu ya jumla ya kura zilizovutwa (round off) kuwa 100.01%
-0.01% ya kura zote (milioni 14) kuwa sawa na kura 140,000.

Ajabu ni kuwa, wahusika waliojenga hoja hizo walijitamba kuwa wao ni wasomi na karibu kila mtu kwa Kenya ni msomi wa kuweza kuchambua hayo mahesabu. Na mwisho hoja zao zikachukuliwa na kupigiwa debe na mamilioni ya wakenya wanaomuunga mkono upande wa Raila Odinga.

Hizo hesabu za desimali na makadirio huwa zinazofundishwa watoto wa darasa la nne hapa Tanzania na nyingine kurejewa kwa kina kidato cha kwanza.

Ni aibu kubwa kwa taifa la Kenya, ukilaza unaposhabikiwa na kuungwa mkono.

Poleni Wakenya kwa hii aibu.
Sasa mbona umewapa pole tu bila kutoa ufafanuzi?
Maana hata mimi hizi mambo za kubadili desimali kuwa asilimia, mara kuwa sehemu, hata sizijuagi!
Toa ufafanuzi wa hiyo .01
 
What is 10% ya 14 000,000
What is 1% ya 14,000,000
What is 0.1% ya 14,000,000
What is 0.01% ya 14,000,000
Compare the answers of the above to maths calculations za four commissioner's
 
What is 10% ya 14 000,000
What is 1% ya 14,000,000
What is 0.1% ya 14,000,000
What is 0.01% ya 14,000,000
Compare the answers of the above to maths calculations za four commissioner's
Ok sawa weka wazi na wewe
 
20220816_184627.jpg

Mkuu hizo kura hata kama ni desimali bado ni tatizo, huwezi kutoa ushindi kwenye makosa ya aina hiyo hata kama ni madogo!.
 
Sasa mbona umewapa pole tu bila kutoa ufafanuzi?
Maana hata mimi hizi mambo za kubadili desimali kuwa asilimia, mara kuwa sehemu, hata sizijuagi!
Toa ufafanuzi wa hiyo .01
Ni hesabu rahisi sana.
Mahesabu ya asilimia yaliyovutwa (Round off percentage) yakijumlishwa yanaweza kukupa 100+/-, na hilo sio ajabu au makosa, ndio ilivyo kimahesabu.

Sasa hizo +/- zinazopungua au kuzidi kwenye mahesabu ya majumuisho ya asilimia yalivutwa yanapaswa kupuuziwa (negligible error).

Na 0.01% kwenye milioni 14 ni sawa na 1400 (yaani 0.01/100 × 14,000,000= 1400).
 
Sasa mbona umewapa pole tu bila kutoa ufafanuzi?
Maana hata mimi hizi mambo za kubadili desimali kuwa asilimia, mara kuwa sehemu, hata sizijuagi!
Toa ufafanuzi wa hiyo .01
Ni hesabu rahisi sana.
Mahesabu ya asilimia yaliyovutwa (Round off percentage) yakijumlishwa yanaweza kukupa 100+/-, na hilo sio ajabu au makosa, ndio ilivyo kimahesabu.

Sasa hizo +/- zinazopungua au kuzidi kwenye mahesabu ya majumuisho ya asilimia yalivutwa yanapaswa kupuuziwa (negligible error).

Na 0.01% kwenye milioni 14 ni sawa na 1400 (yaani 0.01/100 × 14,000,000= 1400)
View attachment 2325745
Mkuu hizo kura hata kama ni desimali bado ni tatizo, huwezi kutoa ushindi kwenye makosa ya aina hiyo hata kama ni madogo!.
Mkuu ushindi unatolewa kwa jumla ya kura halisi zilizopigwa (na sio tafsiri ya asilimia), lakini ushindi unatafsiriwa kwa lugha rahisi ya kimahesabu kwa asilimia. Hivyo sio sahihi kuja na any argument ya kupinga ushindi kwa kutumia majumuisho ya asilimia hata kama yasingekuwa sahihi.

All ni all, hizo figure za asilimia hapo juu ziko sahihi kabisa kimahesabu na Hakuna namna nyingine yoyote bora zaidi kimahesabu inayokubalika ambayo Chebukati angeweza kuja nayo kutafsiri figure za kura zaidi ya hiyo.
 
Ni hesabu rahisi sana.
Mahesabu ya asilimia yaliyovutwa (Round off percentage) yakijumlishwa yanaweza kukupa 100+/-, na hilo sio ajabu au makosa, ndio ilivyo kimahesabu.

Sasa hizo +/- zinazopungua au kuzidi kwenye mahesabu ya majumuisho ya asilimia yalivutwa yanapaswa kupuuziwa (negligible error).

Na 0.01% kwenye milioni 14 ni sawa na 1400 (yaani 0.01/100 × 14,000,000= 1400).
Kwa maana hiyo sasa, kama walipiga kura watu 14,000,000 manaake kwenye majumuisho wanakuwa 14,001,400
Hao 1400 wametoka wapi?

Japo mwisho wa siku baba apumzike. Imetosha sasa!
Wacha Hustler Ruto aongoze Kenya kwa amani!
 
Tuko wengi tunao subiri ufafanuzi huon.

Hesabu ikiwa na decimal nyingi kuna mawili izidi au ipungue. Hapo ndio inakuja mbinu ya makadirio, tunaangalia decimal ya pili kama imevuka nusu ya 10 yaani kama imeanzia 5 na kuendelea basi itambadilisha yule wa awali ipi twende na decimal moja tu.
Mfano 6.78% itakuwa 6.8%.
Mfano 6.72% itakuwa 6.7%.

William Ruto (UDA)
50.49% (50.5%)
7,176,121 Votes
Raila Odinga (AZIMIO)
48.85% (48.9%)
6,942,930 Votes
George Wajackoyah (RPK)
0.44% (0.4%)
61,969 Votes
David Waihiga (AGANO)
0.23% (0.2%)
31,987 Votes
Mabano ni 100%
Hizo 100.01%
 
Ni hesabu rahisi sana.
Mahesabu ya asilimia yaliyovutwa (Round off percentage) yakijumlishwa yanaweza kukupa 100+/-, na hilo sio ajabu au makosa, ndio ilivyo kimahesabu.

Sasa hizo +/- zinazopungua au kuzidi kwenye mahesabu ya majumuisho ya asilimia yalivutwa yanapaswa kupuuziwa (negligible error).

Na 0.01% kwenye milioni 14 ni sawa na 1400 (yaani 0.01/100 × 14,000,000= 1400).
Wewe hujui kanuni za hesabu za darasa la 3 za decimal point
 
Kwa maana hiyo sasa, kama walipiga kura watu 14,000,000 manaake kwenye majumuisho wanakuwa 14,001,400
Hao 1400 wametoka wapi?

Japo mwisho wa siku baba apumzike. Imetosha sasa!
Wacha Hustler Ruto aongoze Kenya kwa amani!
Umechanganya vitu viwili kwa wakati mmoja. Hoja za wale makamishina wanne za hesabu ziko mbili.

Hoja yao ya kwanza ni kuwa Jumla ya asilimia ya wagombea wote wanne ni 100.01% badala ya kuwa 100%. Kuwajibu hoja yao hiyo ni kuwa hiyo 100.01% inajitokeza ikiwa umejumlisha asilimia zenye desimali zilizovutwa (Round off decimal), kimahesabu ni jambo linaweza kujitokeza, na linapojitokeza linapaswa kuupuziwa kimahesabu (Neglibible error). Hivyo haipo popote na haijajumuishwa popote kwenye kura.

Hoja yao ya pili ni kuwa hiyo 0.01% iliyozidi (ikiwa imejumuishwa katika kura) ni kubwa mnoo kiasi cha kuweza kuathiri matokeo ya jumla kumpa mgombea ushindi kwa kuwa ni sawa na kura 140,000. Kuwajibu ni kuwa hiyo 0.01 ni sawa na kura 1400, na pia haikuingizwa popote kwa majumuisho ya kura, bali ni tafsiri ya kimahesabu.
 
Kituko kikubwa cha karne kuhusu hesabu leo kimeonekana huko Kenya baada ya makamishina wanne wa tume ya uchaguzi waliotangaza kujitoa kwenye mchakato wa kutangaza matokeo ya urais kuja na hoja finyu za ukilaza wa mahesabu.

Mbali na sababu zingine walizozitoa, kubwa lilikuwa ni wao kujenga hoja kwenye mahesabu ya matokeo kwenye mambo mawili.

-Wao kushangaa hesabu ya jumla ya kura zilizovutwa (round off) kuwa 100.01% (Kitu ambacho kimahesabu kiko sahihi)

-Kudai kuwa hiyo 0.01% iliyozidi wao wanaitafsiri katika kura zote (milioni 14) ni sawa na kura 140,000. (Kitu ambacho sio sahihi, usahihi ni kura 1400)

Ajabu ni kuwa, wahusika waliojenga hoja hizo walijitamba kuwa wao ni wasomi na karibu kila mtu kwa Kenya ni msomi wa kuweza kuchambua hayo mahesabu. Na mwisho hoja zao zikachukuliwa na kupigiwa debe na mamilioni ya wakenya wanaomuunga mkono upande wa Raila Odinga.

Hizo hesabu za desimali na makadirio huwa zinazofundishwa watoto wa darasa la nne hapa Tanzania na nyingine kurejewa kwa kina kidato cha kwanza.

Ni aibu kubwa kwa taifa la Kenya, ukilaza unaposhabikiwa na kuungwa mkono.

Poleni Wakenya kwa hii aibu.

Hili tatizo
 
Back
Top Bottom