MjuviKitambo
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 711
- 817
Aseme tuu tumudonetie tuuu
MziziMkavu ujue tunakungoja tu.
usikate tamaa kiurahisi namna hiyo,stahamili japo unaumia.du! Mpaka nimekata tamaa.
ILIKUWA ni kazi nzito kwa polisi waliokuwa wakisumbuliwa na wimbi la mauaji ya kimyakimya yaliyokuwa yakifanywa na mtu ambaye hawakumjua.
Polisi walijua kuwa mtu huyo hakuwa wa kawaida kutokana na aina ya vifo vilivyokuwa vikiwakumba watu katika Jiji la Dar es Salaam.
Maiti ya kwanza waliikuta imeninginizwa kwenye mti lakini inawezekana wauaji kwa harakaharaka walimtundika marehemu mtini wakiamini watu watadhani amejinyonga bila kujua kwamba uzito wa mtu huyo waliyemuua na mti ni tofauti.
Mara baada ya kumtundika marehemu huyo kwenye tawi la mti, lilipinda na maiti ikawa imegusa chini baada ya muda mfupi ikawa imepiga magoti ardhini.
Hali hiyo ilimfanya Inspekta Ado aliyekuwa akifuatilia kifo hicho, aamini kwamba mtu huyo hakujiua kwa kujinyonga bali aliuawa kusikojulikana na pale aliletwa akiwa ameshafariki dunia akatundikwa mtini.
Wauaji hawa walidhani mti huu ni imara, hivyo asubuhi watu wangemkuta ananinginia, kumbe tawi lenyewe siyo imara hivyo limepinda, alisema Inspekta Ado huku akiwaangalia askari kanzu wake aliokuwanao eneo la tukio jirani kabisa na kota za wafanyakazi wa machimbo ya madini wa Kampuni ya Lumesule.
Kulikuwa na kundi kubwa la watu waliokuwa wameizunguka maiti wakati askari wakifanya uchunguzi wao na hakuna hata mmoja aliyekuwa akionekana kumfahamu marehemu huyo.
Inspekta Ado aliwageukia raia waliokuwepo na kuwaangalia mmoja baada ya mwingine kabla ya kuwauliza.
Ndugu zangu, kuna mtu yeyote hapa ambaye anamjua marehemu huyu?
Hakuna, alijibu mtu mmoja aliyekuwa amevaa kofia aina ya pama.
Jibu lako unawakilisha watu wote au ni wewe ndiye humjui huyu marehemu?
Afande nimejibu hivyo kutokana na sababu ninazozijua.
Sababu gani hizo?
Kwa vyovyote kungekuwa na watu ambao wanamjua au ndugu wa marehemu kwanza kama ni wanawake basi wangeangua kilio na usingekuwa na sababu ya kutuhoji na kama ni mwanaume, asingesita kujitokeza na kujitambulisha, alisema mtu huyo.
Inspekta Ado alijiuliza kimoyomoyo busara za mtu huyo kama zinagonga ubongo wake? Akajijibu kuwa alikuwa sahihi.
Akaachana naye na kugeukia umati.
Ndugu zangu kuna yeyote ambaye atatusaidia yaani kama kuna mtu wa jirani na hapa ambaye aliliona gari likileta mwili huu usiku?
Swali hilo liliwafanya watu kuangaliana bila kujibu lolote.
Inspekta Ado alichomoa simu yake ya upepo ambayo alikuwa ameininginiza kwenye mkanda mkubwa kiunoni.
Haloo, hebu hakikisheni mnatuma gari la wagonjwa hapa haraka liwe na daktari, aliamuru.
Wakati hayo yanafanyika mimi Che-Priska Ajigale nilikuwa naangalia kwa umakini mkubwa na nilikuwa nimesimama jirani kabisa na Inspekta Ado.
Nilikuwa natetemeka kwa mbali sana lakini nilijitahidi ili watu wasiweze kugundua mwili wangu unatetemeka.
Nilikuwa nimeshika tawi la mti huohuo ambao maiti ilikuwa imeninginizwa kumbe Inspekta Ado akagundua natetemeka baada ya kuona majani yakitikisika, aligeuka kabla na kuniangalia kwa macho makali.
Wewe msichana kwa nini unatetemeka na unaitwa nani? aliniuliza Inspekta Ado.
Naitwa Che-Priska Ajigale
Kwa nini unatetemeka?
Haya tena kwa wale wanaopenda kuwa ni Matajiri wasome hii hadithi ya kusisimuwa kama utapenda niendelee weka ( Like)