UTAJIRI WA DAMU - 7-
Mama yenu mgonjwa.
Tangu lini? mmoja wa madereva alihoji.
Wiki moja sasa! Mzee Mitimingi alijibu.
Anasumbuliwa na nini?
Ana presha ya kupanda na analalamika miguu inamuuma sana asubuhi na jioni.
Madereva hao waliahidi kwenda kumuona siku iliyofuata kwani walichoka sana kisha wakaaga na kuondoka.
Nilibaki na mzee Mitimingi na nilipomuaga kwamba naondoka akasema anataka kuniambia jambo gumu.
Kuna jambo gumu sana na zito nataka kukuambia kuhusu yule mbwa mwenye sura ya mtu, nataka uitunze siri hiyo.
ENDELEA
Niliwaza, ni nini anataka kuniambia mzee huyo, lakini akili ikagonga kuwa ni lazima itakuwa kuhusu mbwa-mtu.
Katika maisha yangu sijawahi kuona mbwa akiwa na sura ya binadamu. Niliwahi kusoma katika vitabu kitu kama hicho na nilikuwa nadhani ni mambo ya utunzi tu lakini sasa nimejionea laivu.
Mzee Mitimingi aliingia ndani na kutoka na begi jeusi, aliketi kisha akalifungua.
Alitoa noti nyekundunyekundu na kuzihesabu kisha kunipa.
Chepriska, shika hizi ni fedha zako, alisema. Niliona kama amechanganyikiwa kwa sababu alikwishanipa shilingi laki moja na shilingi elfu thelathini za kinyozi aliyekuwa akinikusanyia nywele za watoto wadogo.
Mzee ulishanipa fedha zangu na za kinyozi, sikudai chochote, nilimkumbusha.
Hapana, si nimekuambia kuwa nataka kukuambia jambo gumu na zito? Chukua kwanza huu mzigo.
***
Katika kituo cha polisi, Inspekta Ado alikuwa amejifungia akichambua majalada lakini yote yalihusiana na vifo vya watu mbalimbali.
Huyu Josefu Kumusi, alinyongwa kwa kuninginizwa mtini, Paulo Gunia naye hivyohivyo lakini Hamisi Mpepechere yeye kifo chake siyo cha kunyongwa kwa kuninginizwa bali aliuawa huko alikokuwa na kuninginizwa mtini ili ionekane alinyongwa, alijisemea Inspekta Ado kama vile kulikuwa na mtu aliyezungumzanaye.
Kifupi mezani kwake kulikuwa na majalada tisa na yote yalikuwa yakihusu watu kuuawa na watu wasiojulikana.
Mbaya zaidi ni kwamba hakuna hata mtuhumiwa aliyetiwa mbaroni.
Hili ni tatizo sana. Kwa nini wahusika hawapatikani? Ina maana wapelelezi wangu wana walakini? aliendelea kujihoji.
Baadaye alichukua jalada la mauaji ya Mpepechere na kuanza kulisoma.
Huyu Chepriska anaweza kujua kitu, kwa nini hawa wapelelezi wamemuachia? alijiuliza na kuamua kupiga simu chumba cha wapelelezi.
Haloo. Inspekta Ado hapa. Naomba mpelelezi anayeshughulikia kesi ya kifo cha Mpepechere aje ofisini kwangu, aliamuru.
Baada ya dakika tatu hivi, askari mpelelezi aliingia katika ofisi yake na kunyooka huku akiwa amekakamaa.
Jambo afande? akasalimia.
Jambo. Keti.
Askari yule aliketi na kusubiri bosi wake atampa maelekezo gani.
Nilikuwa napitia hili jalada la kesi unayoipeleleza nikaaona yule binti Chepriska umemuachia.
Ndiyo afande.
Kigezo gani kilikufanya umuachie?
Kama umesoma vizuri afande maelezo yake, sijagundua lolote la kumhusisha ndiyo maana siku iliyofuata tukaamua kumuachia lakini tulimuambia kuwa tukimhitaji tutamuita.
Kwani hukufanya uamuzi huu peke yako?
Ndiyo afande tulikaa jopo la wapelelezi na tukagundua kuwa huyu binti alikuwa mlevi tu ambaye alikuwa akikutana na marehemu baa lakini alikuwa hakujui nyumbani wala kazini kwake.
Mlifuatilia huko baa?
Nilifuatilia usiku uleule na mwenye baa ya Chambilecho alinihakikishia kuwa wote hao ni wateja wake ambao hawana uhusiano wowote.
Uliaminije hilo?
Niliamini kwa sababu mwenye baa alisema marehemu siku nyingine alikuwa akija na mkewe au mpenzi wake na kukutana na msichana Chepriska na kukawa hakuna malumbano wala ugomvi na binti huyo naye kwa siku kadhaa alikuwa akija na boifrendi wake na marehemu hakuwa akionesha kuchukia.
Inspekta Ado aliuma kalamu yake akawa anamuangalia yule askari wake wa upelelezi kisha akafunua jalada la kesi na kutoa simu yake ya kiganjani. Akabofya namba kadhaa, simu ikawa inaita kwani aliitegesha kwenye spika ya nje.
Akiipokea mwambie anahitajika hapa polisi.
Sawa afande.
Haloo, ni Chepriska anayeongea?
Ndiyo.
Tafadhali sana unahitajika hapa kituoni.
Sawa nakuja lakini nipe dakika ishirini kwa kuwa siko nyumbani na ni lazima nifike nyumbani kufunga mlango maana nyinyi polisi hamuaminiki.
Hatuaminiki kwani sisi wezi?
Hapana. Naweza kuja hapo mkanishikilia.
***
Chepriska baada ya kupokea simu akajiona ni mnyonge sana hali iliyomfanya mzee Mitimingi kuwa na wasiwasi.
Kwani hiyo simu imetoka wapi? Maana baada ya kuipokea umekuwa mnyonge sana, kulikoni?, akamuuliza.
Hii simu imetoka polisi. Wananiita .
Polisi wanakuita? Tafadhali sana usiwaambie kuhusu huyu mbwa mtu, ukiwaeleza tu, umeniiua, umeelewa? Mzee Mitimingi alisema hayo huku akiwa ametoa macho.
Je, nini kitatokea?
Fuatilia baadae usiku mwingi......