Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,741
- Thread starter
- #41
UTAJIRI WA DAMU - 8-
ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA
Chepriska baada ya kupokea simu ya polisi akajiona ni mnyonge sana hali iliyomfanya mzee Mitimingi kuwa na wasiwasi.
"Kwani hiyo simu imetoka wapi? Maana baada ya kuipokea umekuwa mnyonge, kulikoni?," Akamuuliza.
"Hii simu imetoka polisi. Wananiita ."
"Polisi wanakuita? Tafadhali sana usiwaambie kuhusu huyu mbwa mtu, ukiwaeleza tu, umeniua, umeelewa?" Mzee Mitimingi alisema huku akiwa ametoa macho.
SONGA NAYO...
"Lakini mzee umeniambia kuwa utaniambia jambo zito, kabla ya hujasema simu imeingia, kwani huwezi kuniambia kwa kifupi?"
Aliniangalia akiwa amekunja sura kisha akasimama.
"Nilichokuambia hukielewi, kwamba nimekuongezea shilingi laki moja kwa ajili ya kuficha siri hii. Mbwa huyu hajawahi kuonwa na mtu yeyote isipokuwa wewe na mimi."
"Ni hilo tu?"
"Wee mtoto, kwani katika maisha yako umewahi kumuona mbwa kama huyu?"
"Sijawahi, kwani huyu ni mbwa au jini?"
"Swali gani hilo unauliza? Nilichokueleza umeelewa?" Alifoka huku akifuta jasho usoni.
"Samahani mzee."
"Nimepata wazo jipya. Hebu wapigie hao polisi na uwaambie kuwa leo huna nafasi kwa kuwa kuna dharura, waombe uende kesho."
"Lakini mzee nikifanya hivyo wanaweza kudhani kuwa nataka kutoroka?"
"Wewe waombe kama watakataa basi, nitakupeleka mimi."
"Sawa."
Nilichukua simu na kuipiga namba ya yule mpelelezi, baada ya kuita ikapokelewa.
"Inspekta Ado hapa."
"Aaah, nilifikiri ni simu ya mpelelezi wa kesi ya marehemu Mpepechere."
"Nani anaongea?"
"Ni mimi Chepriska."
"Aaah binti, ni mimi niliagiza wakuite, nahitaji kukuona."
"Nilikuwa nampigia mpelelezi wangu ili kumuomba nije kesho kwa sababu saa hizi nampeleka mzee wangu hospitali anaumwa," nilimdanganya.
"Kwani sasa hivi upo wapi?"
"Nipo Mtaa wa Mizambarauni nyumba namba kumi na mbili."
"Sawa lakini mpelelezi atakuja kukuona jioni nyumbani kwako."
"Sawa mzee na nashukuru kwa kuniruhusu."
Nilikata simu na kumuangalia mzee Mitimingi.
"Wanasemaje? Wamekuruhusu?" aliuliza mzee Mitimingi huku akinikodolea macho.
"Wameniruhusu. Nimeongea na bosi wao."
"Mbona umeitaja namba ya nyumba yangu?"
"Nimewaambia wewe mzee wangu unaumwa, nakupeleka hospitali."
"Una akili sana binti wewe na ndiyo maana napenda sana uwe unafanya kazi zangu na safari hii ni lazima nibadili maisha yako yawe ya kifahari."
Alifikiri kwa dakika kama moja hivi kisha akachukua juisi na kuinywa, akaniangalia, akasema:
"Kumbe ulikuwa na namba ya bosi wa wale wapelelezi?"
"Nilikuwa sina kumbe yule mpelelezi alitumia simu ya bosi wake kunipigia."
Wakati wanaendelea na mazungumzo yao walipigwa butwaa baada ya kuliona gari la polisi ‘Defender' likipiga honi kwenye geti.
Bahati nzuri mlinzi ambaye sikujua awali alikuwa wapi, alifungua geti na taratibu gari likaingia ndani.
"Jifanye mgonjwa," nilimnong'oneza mzee Mitimingi.
Naye kisanii akawa ameegesha shingo yake upande pale kwenye kiti cha sofa alichokuwa amekalia.
Lile gari lilisimama hatua chache kutoka pale tulipokuwa tumeketi na mzee Mitimingi.
"Karibuni sana," nilisema huku nikijifanya sina hofu nao. Askari watatu walishuka, miongoni mwao alikuwepo askari wa kike. Nilihisi kwamba wamekuja kunikamata kwa sababu kwa sheria za polisi mwanamke hukamatwa na askari wa jinsia yake.
"Huyu ni mzee wangu, lakini siyo baba yangu mzazi ni wa kunilea."
"Sawa. Mimi ni Sajenti Mbegu na hawa ni wapelelezi bila shaka huyu wa kike unamkumbuka."
"Namkumbuka, ndiye aliyekuwa akinihoji pale kituo cha polisi."
"Huyu mzee wako anaitwa nani?"
"Ni mzee Mitimingi."
"Haah kumbe mzee Mitimingi ndiye huyu? Ni maarufu sana kwa sababu huwa naona mabasi na malori yake sehemu mbalimbali hapa mjini yakiwa yameandikwa jina lake."
"Bahati mbaya mmekuta anaumwa."
"Siyo mbaya kwa sababu yote ni mipango ya Mungu."
"Karibuni, sijui mnatumia kinywaji gani?"
"Wewe tuletee juisi tu, hakuna mnywaji wa pombe hapa."
Niliingia katika nyumba ya mzee Mitimingi japokuwa sikuwa mwenyeji mle ndani lakini nilikwenda moja kwa moja jikoni nikakuta friji.
"Khaaaa" nilisema kwa sauti. Nikafunga mdomo kwa mikono yangu kushangaa kile nilichokiona ndani ya friji.Niliona kuna kiganja cha mtu!!
Nilitaka kutimua mbio kurudi walipo askari lakini nikaona nikifanya hivyo tutakuwa tumejipalia mkaa maana hata mimi nitajiingiza katika matatizo.
Nilishika boksi moja la juisi nikaipasua na kumwaga kiasi chini kisha nyingine nikaweka kwenye trei na kuwaletea wageni.
"Vipi mbona tumesikia ukisema khaa?" aliniuliza yule askari wa kike.
Kabla sijajibu chochote nilimuona mzee Mitimingi akitetemeka, bila shaka alijua polisi wakikagua wataona maajabu ya mbwa-mtu na kiganja kwenye friji.
Je, nini kitatokea? Fuatilia leo jioni tena
ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA
Chepriska baada ya kupokea simu ya polisi akajiona ni mnyonge sana hali iliyomfanya mzee Mitimingi kuwa na wasiwasi.
"Kwani hiyo simu imetoka wapi? Maana baada ya kuipokea umekuwa mnyonge, kulikoni?," Akamuuliza.
"Hii simu imetoka polisi. Wananiita ."
"Polisi wanakuita? Tafadhali sana usiwaambie kuhusu huyu mbwa mtu, ukiwaeleza tu, umeniua, umeelewa?" Mzee Mitimingi alisema huku akiwa ametoa macho.
SONGA NAYO...
"Lakini mzee umeniambia kuwa utaniambia jambo zito, kabla ya hujasema simu imeingia, kwani huwezi kuniambia kwa kifupi?"
Aliniangalia akiwa amekunja sura kisha akasimama.
"Nilichokuambia hukielewi, kwamba nimekuongezea shilingi laki moja kwa ajili ya kuficha siri hii. Mbwa huyu hajawahi kuonwa na mtu yeyote isipokuwa wewe na mimi."
"Ni hilo tu?"
"Wee mtoto, kwani katika maisha yako umewahi kumuona mbwa kama huyu?"
"Sijawahi, kwani huyu ni mbwa au jini?"
"Swali gani hilo unauliza? Nilichokueleza umeelewa?" Alifoka huku akifuta jasho usoni.
"Samahani mzee."
"Nimepata wazo jipya. Hebu wapigie hao polisi na uwaambie kuwa leo huna nafasi kwa kuwa kuna dharura, waombe uende kesho."
"Lakini mzee nikifanya hivyo wanaweza kudhani kuwa nataka kutoroka?"
"Wewe waombe kama watakataa basi, nitakupeleka mimi."
"Sawa."
Nilichukua simu na kuipiga namba ya yule mpelelezi, baada ya kuita ikapokelewa.
"Inspekta Ado hapa."
"Aaah, nilifikiri ni simu ya mpelelezi wa kesi ya marehemu Mpepechere."
"Nani anaongea?"
"Ni mimi Chepriska."
"Aaah binti, ni mimi niliagiza wakuite, nahitaji kukuona."
"Nilikuwa nampigia mpelelezi wangu ili kumuomba nije kesho kwa sababu saa hizi nampeleka mzee wangu hospitali anaumwa," nilimdanganya.
"Kwani sasa hivi upo wapi?"
"Nipo Mtaa wa Mizambarauni nyumba namba kumi na mbili."
"Sawa lakini mpelelezi atakuja kukuona jioni nyumbani kwako."
"Sawa mzee na nashukuru kwa kuniruhusu."
Nilikata simu na kumuangalia mzee Mitimingi.
"Wanasemaje? Wamekuruhusu?" aliuliza mzee Mitimingi huku akinikodolea macho.
"Wameniruhusu. Nimeongea na bosi wao."
"Mbona umeitaja namba ya nyumba yangu?"
"Nimewaambia wewe mzee wangu unaumwa, nakupeleka hospitali."
"Una akili sana binti wewe na ndiyo maana napenda sana uwe unafanya kazi zangu na safari hii ni lazima nibadili maisha yako yawe ya kifahari."
Alifikiri kwa dakika kama moja hivi kisha akachukua juisi na kuinywa, akaniangalia, akasema:
"Kumbe ulikuwa na namba ya bosi wa wale wapelelezi?"
"Nilikuwa sina kumbe yule mpelelezi alitumia simu ya bosi wake kunipigia."
Wakati wanaendelea na mazungumzo yao walipigwa butwaa baada ya kuliona gari la polisi ‘Defender' likipiga honi kwenye geti.
Bahati nzuri mlinzi ambaye sikujua awali alikuwa wapi, alifungua geti na taratibu gari likaingia ndani.
"Jifanye mgonjwa," nilimnong'oneza mzee Mitimingi.
Naye kisanii akawa ameegesha shingo yake upande pale kwenye kiti cha sofa alichokuwa amekalia.
Lile gari lilisimama hatua chache kutoka pale tulipokuwa tumeketi na mzee Mitimingi.
"Karibuni sana," nilisema huku nikijifanya sina hofu nao. Askari watatu walishuka, miongoni mwao alikuwepo askari wa kike. Nilihisi kwamba wamekuja kunikamata kwa sababu kwa sheria za polisi mwanamke hukamatwa na askari wa jinsia yake.
"Huyu ni mzee wangu, lakini siyo baba yangu mzazi ni wa kunilea."
"Sawa. Mimi ni Sajenti Mbegu na hawa ni wapelelezi bila shaka huyu wa kike unamkumbuka."
"Namkumbuka, ndiye aliyekuwa akinihoji pale kituo cha polisi."
"Huyu mzee wako anaitwa nani?"
"Ni mzee Mitimingi."
"Haah kumbe mzee Mitimingi ndiye huyu? Ni maarufu sana kwa sababu huwa naona mabasi na malori yake sehemu mbalimbali hapa mjini yakiwa yameandikwa jina lake."
"Bahati mbaya mmekuta anaumwa."
"Siyo mbaya kwa sababu yote ni mipango ya Mungu."
"Karibuni, sijui mnatumia kinywaji gani?"
"Wewe tuletee juisi tu, hakuna mnywaji wa pombe hapa."
Niliingia katika nyumba ya mzee Mitimingi japokuwa sikuwa mwenyeji mle ndani lakini nilikwenda moja kwa moja jikoni nikakuta friji.
"Khaaaa" nilisema kwa sauti. Nikafunga mdomo kwa mikono yangu kushangaa kile nilichokiona ndani ya friji.Niliona kuna kiganja cha mtu!!
Nilitaka kutimua mbio kurudi walipo askari lakini nikaona nikifanya hivyo tutakuwa tumejipalia mkaa maana hata mimi nitajiingiza katika matatizo.
Nilishika boksi moja la juisi nikaipasua na kumwaga kiasi chini kisha nyingine nikaweka kwenye trei na kuwaletea wageni.
"Vipi mbona tumesikia ukisema khaa?" aliniuliza yule askari wa kike.
Kabla sijajibu chochote nilimuona mzee Mitimingi akitetemeka, bila shaka alijua polisi wakikagua wataona maajabu ya mbwa-mtu na kiganja kwenye friji.
Je, nini kitatokea? Fuatilia leo jioni tena