Utajiri wa damu

Utajiri wa damu

UTAJIRI WA DAMU - 11-
ILIPOISHIA
“Anasemaje huyo Mmakonde?” aliniuliza.
“Anazungumzia dawa aliyokupa.”
“Achananaye. Nitakupa zawadi kubwa sana kwa kunifichia siri kwa polisi…kuhusu mbwa na mkono wa mtu kwenye friji,” alisema akiniangalia.
SONGA NAYO...


Kimya kilitawala kwa dakika kadhaa kisha akaingia ndani na kutoka na bunda.
“Cheprisca, hizi ni shilingi milioni tano. Ni zako. Umetumia akili sana kuficha siri zangu. Kwanza kwa kuwadanganya polisi kwamba mimi naumwa wakati siumwi chochote.”
“Nakushukuru sana mzee Mitimingi lakini na wewe ulikuwa unatetemeka, ilikuwa unavunga au?”
“Hapana. Nilikuwa natetemeka kweli kwa woga. Kulikuwa na mambo mengi sana ambayo umenisaidia leo, ungekuwa na roho ya kuniangamiza leo ningekwisha.”
“Sawa. Pamoja na kukushukuru lakini jambo moja kubwa ukumbuke kwamba natakiwa kwenda polisi kesho asubuhi.”Nilimuambia huku nikipokea ‘mzigo’ wangu.
“Hilo nakumbuka.”
“Sasa kabla ya hilo ni lazima twende hospitali ili niwe na vyeti vyako kuonesha kuwa hukuwa unawadanganya polisi kwa ugonjwa wako.”
“Ushauri wako ni mzuri sana lakini kabla ya kwenda huko kuna mambo ya kukuambia ambayo utapaswa kuyazingatia,”
Nilimsikiliza, nikawa namtazama usoni. Alikunja sura na kuniangalia. Aliangalia kwenye geti lake na kuona mlinzi wake yule wa Kimakonde yupo palepale getini.
“Tuingie ndani kwanza maana kuna mambo ya siri sana nataka kukumegea.”
Tuliinua na kuingia ndani huku nikiwa nimeshika shilingi zangu milioni tano. Kwangu mimi ilikuwa kama ni ndoto kushika fedha nyingi kiasi kile, tena kwa wakati mmoja.
Nilipoingia ndani niliketi kwenye sofa kubwa na mzee Mitimingi aliamua kukaa karibu na mimi.
“Sikiliza kwa makini habari hii ninayokupa na nakuomba sana hii ni siri kubwa. Sijawahi kumuambia mtu yeyote na kama utathubutu kuitoa nje basi kichwa chako ni halali yangu.”
Baada ya kusema maneno hayo alikaa kimya huku akiniangalia usoni ili asikie ningemjibu nini. Nami kichwa kilifanya kazi haraka nikapangusa uso wangu kwa kitambaa cheupe kisha nikamuambia.
“Sikiliza mzee Mitimingi. Mimi nimesoma hadi chuo kikuu. Kama unaona kuwa hiyo siri yako mimi nitaivujisha, ya nini kuniambia?”
“Ni lazima nikuambie. Unamuona yule mlinzi wa Kimakonde? Hajawahi kumuona yule mbwa mtu hata mara moja. Wewe pia ulikiona kiganja cha mtu kwenye friji, jambo ambalo hakuna mtu aliyewahi kuona kitu kama hicho.”
Alitulia kwa sekunde kama kumi hivi, akazidi kuniangalia machoni nami nikainamisha kichwa kisha akasimama.
“Ngoja kidogo, nakuja.”
Aliinuka kuelekea kwenye friji, nilidhani anakwenda kuniongezea kinywaji kwa sababu juisi niliyokuwa nakunywa ilikuwa imekwisha.
Badala yake alichukua mfuko akaweka kitu. Nilifikiri haraka nikagundua kuwa alikuwa akihamisha kile kiganja na kukipeleka chumbani kwake baada ya sekunde chache akaja kuketi palepale alipokuwa amekaa awali.
“Sikiliza Cheprispa. Nilikwenda kukihamisha kiganja kile kutoka kwenye friji na kukiweka chumbani kwa sababu sikutegemea hata siku moja kuwa kuna mtu angefungua friji leo lakini wewe ulifungua. Ulifungua kwa nia nzuri ya kuwapa wageni, yaani wale polisi vinywaji.”
“Kwani mzee nilikosea?”
“Hapana. Hujafanya kosa kabisa tena mimi nakusifu sana kwa jinsi ulivyotumia akili na kuwazubaisha polisi. Ilikuwa ni hatari sana.”
Alichukua bilauri yake iliyokuwa na juisi akainywa.
“Nataka kukusimulia kuhusu yule mbwa mtu. Umemuona jinsi alivyofanana na sura ya mtu? Yule ni mtu. Nilimpa masharti akayakosea akajikuta anageuka mbwa.”
“Masharti gani hayo?”
“Ni kwamba nilimuambia kama ninavyokuambia wewe leo kwamba usitoe siri, yeye akatoa siri kwa mpenzi wake kwamba mimi utajiri wangu unapatikana kwa njia ya damu.”
“Ina maana wewe umemfanya binadamu awe vile?”
“Siyo mimi ni masharti ya mganga ndiyo yamemfanya awe vile! Mimi nilimuonya kuwa jambo hili usiliseme kwa watu yeye akamwaga mchele kwenye kuku wengi, yakampata yale.”
“Sasa kwani huyo mganga hana dawa ya kumfanya arejee awe binadamu?”
“Kwanza mimi aliniudhi sana na sikuwa na mpango wa kumrejesha kabisa katika hali ya kawaida kwani alichokuwa akinifanyia ni sawa na kuniua. Wewe unaweza kumsamehe mtu anayekuua?”
“Hapana mzee Mitimingi, kama ni mateso umemtesa sana. Naomba chondechonde msamehe na mrejeshee ubinadamu wake.”
“Naweza kumrejeshea lakini hadithi ya jambo hili ni ndefu na nzito siyo kama unavyofikiri. Kwanza ni lazima nimpige viboko kila siku vitano. Ndiyo masharti yenyewe la sivyo mimi nitakuwa kama yeye.”
Je, Mitimingi atamsamehe mbwa mtu na kumrudisha awe binadamu? Fuatilia Jumatano ijayo.
 
duuu mi mvivu kusoma Riwaya ila naona nimevutwa toka mwanzo hadi mwisho...................Big up tunakungoja uendelee au umesha chukuliwa na Afande Ado?
 
UTAJIRI WA DAMU - 12-

ILIPOISHIA

"Hapana mzee Mitimingi, kama ni mateso umemtesa sana. Naomba chondechonde msamehe na mrejeshee ubinadamu wake."
"Naweza kumrejeshea lakini hadithi ya jambo hili ni ndefu na nzito siyo kama unavyofikiri. Kwanza ni lazima nimpige viboko vitano kila siku . Ndiyo masharti yenyewe la sivyo mimi nitakuwa kama yeye."
SONGA NAYO...


Mzee Mitimingi baada ya kuyasema hayo aliniambia kwa kuwa hadithi ya mbwa mtu ni ndefu aliona ni vema kama nitakwenda kwanza polisi kuripoti kisha nirudi anisimulie kwa urefu.
"Chepriska hadithi hii inahitaji muda mrefu ili uelewe na usiwe na maswali."
"Lakini mzee nimekuambia kuwa twende kwanza hospitali ukapate vyeti kwa sababu wale polisi wakijua kuwa hatukwenda hospitali wanaweza kudhani tulikuwa na jambo tulikuwa tumelificha."
"Sawa. Mimi nitakwenda hospitali peke yangu, wewe nenda polisi."
"Hapana twende sote polisi."
Mzee Mitimingi hakuwa na la kufanya isipokuwa kukubaliana na Chepriska hasa kwa kuwa alijua kwamba ana upeo au uwezo wa kutabiri kitakachotokea.
"Chambilecho," aliita mzee Mitimingi.
Mara aliingia ndani kijana mmoja ambaye alikuwa amevaa Kaunda suti.
"Ndiyo mzee."
"Gari lako lina mafuta ya kutosha?"
"Ndiyo mzee. Jana jioni niliweka ya shilingi elfu hamsini na hatukuzunguka sana."
"Sawa. Tungoje tunatoka."
Mzee Mitimingi alichukua begi na kunipa.
"Huo mzigo wako tumbukiza humo."
Nilichukua ule mfuko wa nailoni uliokuwa na shilingi milioni tano na kuziweka kwenye lile begi. Baadaye tuliinuka na kuingia kwenye gari aina ya GMC la Kimarekani.
"Tupitie Hospitali ya Misheni kwa Buruda John."
Ndani ya gari hakuna hata mtu mmoja aliyezungumza na hatukuchukua muda mrefu tukawa tumefika kwa Buruda John.
"Nisubirini, nakuja," alisema mzee Mitimingi akaingia hospitali huku mimi na dereva Chambilecho tukimsindikiza kwa macho.
Alikaa ndani ya hospitali hiyo kwa dakika kumi na mbili kisha alitoka akiwa na rundo la makaratasi.
"Nimeandikiwa ED 3 (mapumziko ya siku tatu)."
"ED ya nini kwani wewe unafanya kazi ya mtu?"
"Napita kulekule kwenye ushauri wako kwamba hii ni kuonesha kuwa naumwa sana. Wakija wale jamaa wakiona hii, watajua naugua kweli."
"Sawa."
"Chambilecho sasa elekea polisi."
"Lakini kama hujali si ni bora tungeenda kukushusha wewe nyumbani kisha polisi niende na dereva?"
"Hapana , polisi ni polisi, unaweza kwenda wakakung'ang'ania."
"Sasa wakining'ang'ania wewe utafanyaje? Si wanajua kwamba wewe upo taabani?"
""Hapana, nitatumia ujanja kwa kuwaambia kuwa nimepata nafuu lakini nimeambiwa nisifanye kazi yoyote na ndiyo maana nina ED."
Niliona kuwa wazo lake ni zuri, nikaamua twende naye polisi. Kutoka pale hospitali ya Buruda hadi polisi ilituchukua dakika kumi na tano.
Nilikwenda moja kwa moja kwa Inspekta Ado ambaye nilimkuta akisoma majalada yaliyokuwa juu ya meza yake.
"Karibu Chepriska."
"Ahsante."
Niliingia na kuketi kwenye kiti kilichokuwa kando ya meza yake kubwa. Nilitulia kusubiri ataniambia nini lakini badala yake akawa anaendelea kupekua yale majalada.
Mara moja akachukua alilokuwa akilitafuta.
"Nimekuita nilitaka kuongeza mambo kadhaa humu kwenye jalada lako."
"Sawa."
"Kwanza pole kwa kuuguza maana askari waliokuja kwako jana waliambiwa upo kwa mzee wako Mitimingi. Kwani yule ni baba yako mzazi?"
"Hapana, ni baba wa kunilea tu."
"Oke."
"Kuna habari kwamba mzee yule anapenda sana ushirikina. Hiyo ni kweli?"
"Hilo mimi silijui."
"Wewe umewahi kuishi pale kwake?"
"Hapana. Mimi huwa namtembelea tu, sijawahi kuishi pale."
"Kwa nini?"
"Kwa sababu mimi nilipoingia hapa mjini kwa nauli ya yule mzee niliamua kuwa nijitegemee. Nikapanmga chumba. Siku za kwanza alinilazimisha sana niishi pale kwake nikakataa katakata."
"Ulikataa kwa kuwa ulikuwa unajua kuwa huyo mzee ni mshirikina siyo?"
"Hapana, nilipenda niwe huru."
"Kwani ulipofika hapa mjini alikuambia atakupa kazi gani?
"Aliniambia kazi yangu ni kusimamia magari yake.


Je, kiliendelea nini? Fuatilia Tena Jumatano ijayo......
 
UTAJIRI WA DAMU - 13-


ILIPOISHIA
"Kuna habari kwamba mzee yule anapenda sana ushirikina. Hiyo ni kweli?"
"Hilo mimi silijui."
"Wewe umewahi kuishi pale kwake?"
"Hapana. Mimi huwa namtembelea tu, sijawahi kuishi pale."
"Kwa nini?"
"Kwa sababu mimi nilipoingia hapa mjini kwa nauli ya yule mzee niliamua kujitegemea. Nikapanga chumba. Siku za kwanza alinilazimisha sana niishi pale kwake nikakataa katakata."
"Ulikataa kwa kuwa ulikuwa unajua kuwa huyo mzee ni mshirikina siyo?"
"Hapana, nilipenda niwe huru."
"Kwani ulipofika hapa mjini alikuambia atakupa kazi gani?
SASA SONGA NAYO...


"Aliniambia kazi yangu ni kusimamia magari yake.
"Kwani yule mzee hana watoto au mke?"
Moyo wangu ulienda mbio kwa sababu niliona kama askari yule aliyekuwa akinihoji pale kwenye kituo cha polisi kama alikuwa ananitega.
Lakini pia nilikuwa nawaza kwamba kama wakiamua kwenda kuikagua nyumba ya mzee Mitimingi ni wazi mbwamtu watamuona na kile kiganja cha mtu watakiona.
Nikawa najiuliza ikitokea hivyo moja kwa moja nitaingia matatani. Sikujua hawa polisi waliambiwa na nani kuhusu ushirikina wa yule mzee.
"Kwani nyinyi nani amewaambia kuwa mzee Mitimingi ni mshirikina?" Nilijikakamua kumuuliza yule askari.
Aliacha kuandika, akaniangalia kama vile alikuwa akitafakari kitu. Unajua askari wa upelelezi wana akili ya kwenda mbele zaidi kwa kila kitu.
"Nakuona kama una wasiwasi."
"Wasiwasi wa nini? Nakuuliza ili niweze kujua na mimi, mbona wewe unanihoji."
"Kwa kawaida mtuhumiwa ndiye anayehojiwa polisi na kazi yake kujibu siyo kuuliza tena suala linalohusu alichoitiwa. Unaweza kunihoji ili nikikupa jibu ukwepeshe ukweli."
"Haya endelea kunihoji." Nilisema huku nikibongesha simu yangu ya kiganjani, nilipolifikia jina la mzee Mitimingi nikabofya ili iite, iliita akaipokea. Nilifanya hivyo ili asikie yale mahojiano. Simu yangu nikaiweka kwenye shavu kama vile nilikuwa naitumia kukuna shavu langu.
"Mzee Mitimingi alikuambia kazi yako ni kusimamia magari yake, kwani wewe ni fundi makenika?"
"Hapana, hakuniambia kusimamia mambo ya ufundi."
"Sasa alikuambia usimamie nini kama wewe siyo fundi makenika."
"Mimi kazi yangu ni kukusanya fedha zake, yaani kwenye mabasi na kwenye malori nilikuwa nakusanya fedha na kuzipeleka benki."
"Ahaaa kwani wewe umesomea uhasibu?"
"Hapana. Kazi yangu hiyo nilijifunza nyumbani tu na pale nimepata uzoefu zaidi."
"Sawa. Hujawahi kusikia lolote kuhusu mzee Mitimingi kuua watu?"
"Ningesikia kuwa anaua watu nisingeweza kukaa pale na kufanyanaye kazi."
"Niambie pale nyumbani kwake ni nani hasa wanaopenda kwenda na kwa muda gani?"
"Pale wanaofika ni madereva wake na mara nyingine hawamkuti wananikuta mimi."
"Anakuwa amekwenda wapi?"
"Ana mambo mengi, siwezi kujua labda siku ambazo ananiaga."
"Siku ambazo amekuwa akikuaga, huwa anasema anakwenda wapi?"
"Huwa anasema anakwenda kutembea au anakwenda kwenye mipango yake."
"Mipango gani?"
"Huwa haniambii."
"Mke wa mzee Mitimingi yupo wapi?"
"Aliniambia ni mgonjwa na amelazwa."
"Wapi?"
"Hospitali ya Dk. Mei Chilungoli."
"Kwa nini ameamua mkewe alazwe huko?"
"Daktari yule ni mtu wa kwao, tena ana utaalam wa hali ya juu kwa magonjwa ya akina mama."
"Wewe unamfahamu Dk. Mei?"
"Namfahamu kwa kuwa siku nyingine huwa anakuja nyumbani kumtibia huyo mama."
Baada ya mahojiano hayo yule askari alikwenda kumuona mkuu wake ambaye ni Inspekta Ado.
"Subiri nikamuambie afande haya uliyoyasema tuone atashauri nini."
Aliinuka na kuniacha nikitafakari, kisha nikakata simu.
Baada ya dakika chache niliitwa kwenye ofisi ya Inspekta Ado. Niliingia nikamkuta akipekuapekua lile jalada lenye maelezo yangu.
"Binti nimesoma maelezo yako hapa nadhani subiri tumuhoji mlinzi wenu. Nimetuma askari wamemleta hapa."
Baada ya dakika mbili niliona mzee Chambilecho akiingizwa katika ofisi ile. Shati lake lilikuwa limelowa jasho kama vile alikuwa anafanya mazoezi ya viungo na alikuwa na wasiwasi.
Sikujua kwa nini alikuwa na wasiwasi kiasi kile kama kwamba kaambiwa ana kesi ya kujibu inayohusu mauaji. Aligeuka kuangalia nilipokuwa nami nikajifanya kutabasamu ili kumuondoa hofu.
Hakuonekana kubadilika muonekano wa sura yake kwani bado alikuwa kama vile ananishangaa kuwepo pale. Nilihisi inawezekana yule mzee wa Kimakonde alikuwa anajua siri za mzee Mitimingi.

Je, siri za mzee Mitimingi zitafichuliwa na mzee huyo? Fuatilia alkhamisi ijayo...
 
UTAJIRI WA DAMU - 13-


ILIPOISHIA
"Kuna habari kwamba mzee yule anapenda sana ushirikina. Hiyo ni kweli?"
"Hilo mimi silijui."
"Wewe umewahi kuishi pale kwake?"

"Hapana. Mimi huwa namtembelea tu, sijawahi kuishi pale."
"Kwa nini?"
"Kwa sababu mimi nilipoingia hapa mjini kwa nauli ya yule mzee niliamua kujitegemea. Nikapanga chumba. Siku za kwanza alinilazimisha sana niishi pale kwake nikakataa katakata."

"Ulikataa kwa kuwa ulikuwa unajua kuwa huyo mzee ni mshirikina siyo?"
"Hapana, nilipenda niwe huru."
"Kwani ulipofika hapa mjini alikuambia atakupa kazi gani?

SASA SONGA NAYO...
"Aliniambia kazi yangu ni kusimamia magari yake.
"Kwani yule mzee hana watoto au mke?"
Moyo wangu ulienda mbio kwa sababu niliona kama askari yule aliyekuwa akinihoji pale kwenye kituo cha polisi kama alikuwa ananitega.

Lakini pia nilikuwa nawaza kwamba kama wakiamua kwenda kuikagua nyumba ya mzee Mitimingi ni wazi mbwamtu watamuona na kile kiganja cha mtu watakiona.
Nikawa najiuliza ikitokea hivyo moja kwa moja nitaingia matatani. Sikujua hawa polisi waliambiwa na nani kuhusu ushirikina wa yule mzee.

"Kwani nyinyi nani amewaambia kuwa mzee Mitimingi ni mshirikina?" Nilijikakamua kumuuliza yule askari.
Aliacha kuandika, akaniangalia kama vile alikuwa akitafakari kitu. Unajua askari wa upelelezi wana akili ya kwenda mbele zaidi kwa kila kitu.
"Nakuona kama una wasiwasi."

"Wasiwasi wa nini? Nakuuliza ili niweze kujua na mimi, mbona wewe unanihoji."
"Kwa kawaida mtuhumiwa ndiye anayehojiwa polisi na kazi yake kujibu siyo kuuliza tena suala linalohusu alichoitiwa. Unaweza kunihoji ili nikikupa jibu ukwepeshe ukweli."

"Haya endelea kunihoji." Nilisema huku nikibongesha simu yangu ya kiganjani, nilipolifikia jina la mzee Mitimingi nikabofya ili iite, iliita akaipokea. Nilifanya hivyo ili asikie yale mahojiano. Simu yangu nikaiweka kwenye shavu kama vile nilikuwa naitumia kukuna shavu langu.
"Mzee Mitimingi alikuambia kazi yako ni kusimamia magari yake, kwani wewe ni fundi makenika?"
"Hapana, hakuniambia kusimamia mambo ya ufundi."

"Sasa alikuambia usimamie nini kama wewe siyo fundi makenika."
"Mimi kazi yangu ni kukusanya fedha zake, yaani kwenye mabasi na kwenye malori nilikuwa nakusanya fedha na kuzipeleka benki."
"Ahaaa kwani wewe umesomea uhasibu?"

"Hapana. Kazi yangu hiyo nilijifunza nyumbani tu na pale nimepata uzoefu zaidi."
"Sawa. Hujawahi kusikia lolote kuhusu mzee Mitimingi kuua watu?"
"Ningesikia kuwa anaua watu nisingeweza kukaa pale na kufanyanaye kazi."
"Niambie pale nyumbani kwake ni nani hasa wanaopenda kwenda na kwa muda gani?"
"Pale wanaofika ni madereva wake na mara nyingine hawamkuti wananikuta mimi."

"Anakuwa amekwenda wapi?"
"Ana mambo mengi, siwezi kujua labda siku ambazo ananiaga."
"Siku ambazo amekuwa akikuaga, huwa anasema anakwenda wapi?"
"Huwa anasema anakwenda kutembea au anakwenda kwenye mipango yake."
"Mipango gani?"

"Huwa haniambii."
"Mke wa mzee Mitimingi yupo wapi?"
"Aliniambia ni mgonjwa na amelazwa."
"Wapi?"
"Hospitali ya Dk. Mei Chilungoli."

"Kwa nini ameamua mkewe alazwe huko?"
"Daktari yule ni mtu wa kwao, tena ana utaalam wa hali ya juu kwa magonjwa ya akina mama."
"Wewe unamfahamu Dk. Mei?"
"Namfahamu kwa kuwa siku nyingine huwa anakuja nyumbani kumtibia huyo mama."
Baada ya mahojiano hayo yule askari alikwenda kumuona mkuu wake ambaye ni Inspekta Ado.

"Subiri nikamuambie afande haya uliyoyasema tuone atashauri nini."
Aliinuka na kuniacha nikitafakari, kisha nikakata simu.
Baada ya dakika chache niliitwa kwenye ofisi ya Inspekta Ado. Niliingia nikamkuta akipekuapekua lile jalada lenye maelezo yangu.

"Binti nimesoma maelezo yako hapa nadhani subiri tumuhoji mlinzi wenu. Nimetuma askari wamemleta hapa."
Baada ya dakika mbili niliona mzee Chambilecho akiingizwa katika ofisi ile. Shati lake lilikuwa limelowa jasho kama vile alikuwa anafanya mazoezi ya viungo na alikuwa na wasiwasi.

Sikujua kwa nini alikuwa na wasiwasi kiasi kile kama kwamba kaambiwa ana kesi ya kujibu inayohusu mauaji. Aligeuka kuangalia nilipokuwa nami nikajifanya kutabasamu ili kumuondoa hofu.
Hakuonekana kubadilika muonekano wa sura yake kwani bado alikuwa kama vile ananishangaa kuwepo pale. Nilihisi inawezekana yule mzee wa Kimakonde alikuwa anajua siri za mzee Mitimingi.

Je, siri za mzee Mitimingi zitafichuliwa na mzee huyo? Fuatilia alkhamisi ijayo...
kiongozi ni znuri ila sana ila ni fupi sana jaribu kurefusha wakati mwingine
 
Back
Top Bottom