USIMWAMINI MWANAMKE KWA 100% HATA SIKU MOJA
PART FOUR
Ilipoishia
Kama nilivosema mwanzo, kwa miaka yote 7 niliyokuwa Sharifa toka 2015 mpaka leo (BADO TUPO WOTE KAZAA NA MTOTO MWINGINE MWAKA HUU), hajawahi kuchelewa kupokea simu yangu, hata awe anafanya nini, hajawahi kukosa kujibu meseji yangu, hajawahi kufuta meseji yangu wala simu yangu, hajawahi kuacha kunitumia picha nikidai popote alipo, hajawahi kuficha simu yake nikiwepo. Yani nikifika tu kama kuna changamoto ya simu atanipa nishughulike nayo, kama kuna kitu interesting cha kunionyesha humo kwenye simu atanikabidhi simu yake niendelee kucheki yeye anaenda zake nje kupika. Simu yangu ikizima chaji halafu yeye anapika sina kampani, atanipa simu yake nicheki cheki instagram na FB bila hofu yoyote. YEYE NDIYE MTU AMBAYE NIKIWEKEWA BASTOLA KICHWANI NIKAAMBIWA NIMPIGIE MTU MMOJA TU ASIPOPOKEA WANANIPIGA RISASI, NTAMPIGIA YEYE.
Basi nikaamua kuachana na yaliyopita tusonge mbele. Sikuwahi kuuliza kitu tena kuhusu jamaa Ex husband mpaka mwaka huu 2022.
Tuendelee
Siku moja, mwezi sikumbuki lakini mwanzoni mwa mwaka huu (Sharifa akiwa tayari amejifungua mtoto wa pili - tumwite Venance) nilimpigia simu kumpa hai na watoto. Akaniambia Ex msumbufu kampigia simu kwa namba tofauti alivopokea akaanza kumwongelesha vitu havieleweki yeye akamkatia simu. Alivokata simu jamaa akarekodi audio kama 4 akamtumia na meseji nyingi (Hawezi kupiga kwa namba yake kwa sababu alishamblock). Akanitumia audio clip 2 mimi nikazisikiliza. Muda huo huo nikaenda. Nilivofika tu akanipa simu yake nisome mwenyewe na nisikilize clip zote. Kwa kifupi jamaa anamuambia amemmisi sana ila hana la kufanya, anaomba tu kama kuna kitu alimlisha arudi kwa mganga akakitoe kwa sababu anapata mateso makubwa. Atakuja kupata ajali. Muda wote akiwa anaendesha gari anamuwaza yeye, amejaribu kujifariji na wanawake wengine kadhaa ili amsahau Sharifa ameshindwa.
Kwenye moja ya hizo clip jamaa akaweka mtego, akamkumbusha tu kuwa mimi ni mkristo kwa hiyo siji kumuoa kamwe, huu ni mwaka wa 7 mbona sijamuoa bado?. Nadhani ndio maana Sharifa alinipa nisikilize.
Zile clip alizonitumia Sharifa (Mama Lisa na Venance) nikaziforward kwa jamaa Ex ajue kuwa meseji zake natumiwaga. Huko nyuma amewahi kutuma zingine kama mara 2 hivi, hazikuwa na uzito kama hizi. Nikamwambia ujumbe wake nimeupata. Na yeye akaniambia anajua nampotezea tu muda mwanamke wa watu baada ya kumpora yeye, sina mpango wa kumuoa, anaamini kwamba nishaujua ukweli kuwa Sharifa alinichezea akili miaka mitatu, naye ye alivomkataa kabisa mtoto ndio mwanamke akaamua kuja kwangu mazima.
Ila angekubali mtoto, asingefuatilia vile vyeti wangekuwa pamoja mpaka leo na yeye bado anampenda sana sana. Daaa! Tukarudi kule kuleeeeeeeeeeee!
Nikataka kuthibitisha zaidi kama kweli mtoto wangu alishakuwa amepewa yeye, kwamba angekubali tu, sasa hivi mtoto asingekuwa wangu!!! Ninavokapenda kabinti kangu hivi jamaniii! Nikasema sasa naingia kwenye misheni ya kujua ukweli mwenyewe hata kama yamepita. Ila moyoni kwangu nikajiahidi chochote nitakachogundua simuachi Sharifa (Mama Lisa na Venance) kamwe wala simwambii. Mtu pekee anayeweza kunithibitishia kuwa waliendelea na mahusiano mpaka Sharifa alivohama kule Temeke na kama kuna uwezekano mtoto Lisa akawa sio wangu ni wa yule jamaa, ni mtu mmoja tu.
Aliyejifanya dada yake kumbe mpangaji mwenzie. Na namna ya kupata hiyo Habari kutoka kwa yule ni kumsogeza karibu na kumpa mpa vihela hapa na pale halafu siku moja nimuite sehemu nimuahidi kitu kikubwa halafu nimdodose kama kweli toka 2015 mpaka 2018 yule Ex wa Sharifa alikuwa anakuja pale na je yule tuliyekutana pale siku ileee akagombagomba alikuwa nani. Si ni shoga yake, atakuwa alimsimulia.
Basi nikaanza misheni impossible mnamo mwezi wa 4 hivi. Nikampigia simu siku moja huyo shoga wa Sharifa (dada feki) kumsalimia, yeye akawa yuko poa ila mtoto wake anaumwa. Nikauliza kama kampeleka hospitali akasema hana hela. Mpesa chap bila kuchelewa nikamrushia elfu 20. Akaenda hospitali akanitumia kile kicheti wamemuandikia dawa za elfu 40. Nikajiongeza, kumwona daktari buku 5 nauli buku 5 atakuwa kabaki na buku 10. Chapa nikamrushia elsu 30. Alishukuru sana sana sana. Sasa ikawa mara moja moja tu namtumia buku 10 namwambia awanunulie watoto wake chips. Anafurahi balaa. Ikafika wakati akawa yeye ndio anaomba na wala hamwambii shoga yake chochote kuhusu tunavowasiliana. Mwanzo alikuwa anamwambia kila tukiongea, na Sharifa hana shida sisi kuwasiliana kwa sababu mara nyingi tu shoga yake akipiga simu wapeane udaku, yeye mwenye huwa ananipa simu nimsalimu. Sasa juzi kati nikasema ameshakuwa karibu sasa nimwite nimuulize zile maishu. Nikampigia simu tuonane akauliza wapi nikamtajia maeneo, akasema poa. Siku hiyo hakuja, akatoa sababu. Tukapanga siku nyingine hakuja. Nikajua misheni imefeli. Nikasema nijaribu mara ya mwisho.
Nilivompigia akasema naonaje tukionana keshokutwa yake, kwa sababu siku hiyo hayuko vizuri, yuko kwenye siku zake ndio anamalizia! KHAAAAAAAAA!
Nikawazaaaaaa yamekuwa hayooooooo!!!!! Nikashangaa sana kwa sababu wazo hilo mimi halikuwepo kichwani. Japo limewahi kunijia wakati ananipiga chenga kuonana, niliwaza labda anajua nataka mapenzi. Anyway, shetani ana nguvu sana, nikaamua kutembea nae kwenye reli yake hiyo hiyo.
Keshokutwa yake tukakutana, itoshe tu kusema shetani alinishinda nguvu, tukajikuta tu tuko lodge. Kilichojiri mungu anisamehe.
Sasa siku hiyo hata sikumuuliza chochote ili asijeshtuka akajidharau kuwa mimi lengo la kukutana lilikuwa lingine, humo kwenye lodge kajichomeka mwenyewe. Tukaachana kwa minajiri ya kukutana siku nyingine. Tukakutana tena mara ya pili, sikuongea chochote. Mara ya 3 ndio nikamuuliza. YEYE NDIO AKATHIBITISHA KUWA NI KWELI TOKA 2015 MPAKA 2018 JAMAA ALIKUWEPO KWENYE PICHA JAPO RAFIKI YAKE ALIKUWA HAMTAKI LAKINI ALIKUA HANA JINSI KWA SABABU ALIKUWA ANAKAA MWENYE NYUMBA AMBAYO JAMAA NDIO KAMPANGISHIA. Na akasisitiza kuwa wakati Sharifa anapata hiyo mimba jamaa alikuwa hajawahi kuonekana pale miezi mitatu, jamaa mwenyewe alimlalamikia sana yeye kuwa rafiki yake kamsaliti mpaka kashika mimba. Na jamaa alimwambia kuwa mimba haitambui ila bado anamtambua Sharifa kama mke wake. Mpaka mtoto LISA anazaliwa jamaa aliendelea kumsisitizia kuwa mtoto hamtambui ila Sharifa hamuachi. Mpaka Sharifa alivohama pale jamaa akamkosa yeye ndio alikuwa jamaa anamdai maelezo kama vile yeye ndio kamtorosha. Kwa hiyo akaniambia ukweli wote, kwa sababu yeye ndio anaujua vizuri na wameishi vyumba jirani kwa muda mrefu wakisaidiana kwenye kila kitu. Walikuwa wanapika pamoja kama familia moja. Kila kitu walikuwa wanashirikiana.
Kwa kifupi stori ndio iko hivo.
Na sasa hivi nafsi yangu imetulia baada ya kuujua ukweli wote. Kumbuka kwenye majadiliano yote, Sharifa au mama Lisa au mama Venance hajawahi kukiri popote kuwa na mahusiano yoyote na mtu yoyote kwa kipindi chote cha miaka 7 tuliyokuwa pamoja. Hata siku rafiki yake aliponiambia ukweli wote niliongea nae kuwa ukweli wote nimeshaujua lakini sina mpango wowote wa kumuacha. Nikamuuliza kwanini alitaka kumpa yule jamaa mtoto wangu?? Akasema hajawahi kufanya hiyo kitu.
BADO ALIENDELEA KUKATAA KUWA HAJAWAHI KUNISALITI. Swali lake kubwa hizo taarifa natafuta za nini? Ni sijiulizi wanaoniambia wanataka nini? Sioni kuwa Ex wake anawatumia wanaonimbia ili tuachane?? Ukiachilia mbali kuwa ana watoto wangu wawili, yeye mwenyewe nampenda sana sana sana (Inawezekana nimelishwa alicholishwa Ex).
SASA NILICHOTAKA KUSEMA NI KWAMBAAAAA, USIMUAMNI MTU KWA ASILIMIA 100. Maisha tuliyoishi na Sharifa 2015-2018 nilikuwa namwamini kupita maelezo. Ningeweza kufanya chochote kwa ajili yake. Alitengeneza mazingira ambayo ilikuwa lazima nimuamini asilimia zote. Yani na mawasiliano yote, na ukaribu wote, na kukutana kote, bado aliweza kunificha kitu kikubwa hivo, na jamaa yake aliendelea kuja pale kwake na yeye aliendelea kukutana na mimi kwenye lodge akihofia tutakutana wanaume wawili. Nilikuwa nikitaka tukosane siku hiyo nimuulize tu kuhusu huyo jamaa, nikisisitiza kuongelea mpaka analia machozi. Utasikia
”Alichonifanyia yule mtu, sitaki kabisa kumsikia kwenye maisha yangu, bora nife kuliko kurudi kwake. Ukiniacha wewe bora nirudi kijijini kwanza nikajipange kuliko kurudi kwake”
MWISHO