
Muendelezo.....
Jamaa akabamiza mlango akaondoka, alipofika nje akachukua boda, boda alimpeleka buguruni alipokuwa ame park lory aina ya Benz likiwa na container la 40FT, basi akapanda kwenye gari akawasha huyo motoo, safari ikaanza ya kwenda Burundi, ameenda mpaka kibaha akapigwa mkono na matrafki, si unajua tena wanataka tozo za kubrashia viatu akamwachia trafki yule aftatu, trafki akasema huku akitabasam unyama sanaa akimpungia jamaa.
Mwisho![]()


Endelea tu kuandikaUSIMWAMINI MWANAMKE KWA 100% HATA SIKU MOJA
TRUE STORY
PART TWO
__Stori ilipoishia
Kwa namna yule jamaa alivoingia nikawa na maswali mengi kichwani nikawa nimeghairi kuondoka ili jamaa aondoke nimuulize demu yule ni nani. Kwa hiyo nikamjibu kuwa nimeghairi kuondoka ntaondoka jioni (Hiyo ilikuwa saa 5 hivi asubuhi). Kwa unyonge akarudi kule ndani, nikasikia jamaa sasa linatukana matusi, kuwa halipendi ujinga na u.s.e.n.g.e u.s.e.n.g.e, na maneno mengine makali makali. Mengine nikawa sisikii mengine nasikia, kama dakika 2 hivi. Halafu jamaa likatoka likabamiza mlango kwa nguvu huku linaondoka linamwambia demu aache upumbavu wake kabisa. Hilooooooo likapotea zake……
Tuendelee
Jamaa alivoondoka demu akaanza kupika. Nikasubiri apike akamaliza tukala. Lakini akawa hana amani kabisa kwa sababu sijauliza chochote. Baadae tukaenda kukaa nje ndio nikamuuliza yule alikuwa nani. Akaniambia yule ni mume wa dada yake ambaye anaishi Dodoma, yuko Dar kikazi, dada yake alimuomba aje amletee hela kwa sababu yeye (demu) alimuomba dada yake. Kule kugomba ni kwa sababu alikuwa anampigia simu hapokei saa nzima alikuwa anataka demu ndio afuate hiyo hela mahali sasa yeye hakuiona simu. Nikauliza mbona kaingia ndani bila hodi kama shimoni tu, akasema pale ni sebleni kwa hiyo akitaka kuvaa anaenda chumbani kwa dada yake kuvaa (KUMBUKA SIO DADA YAKE NI MPANGAJI MWENZIE). Akasema watu wamezoea kuingia tu pale. Sikuridhika kabisa na maelezo yake lakini sikutaka kumkwaza nikapotezea. Upendo niliokuwa nao kwake ulikuwa mkubwa kuliko hilo tukio.
Alipokaribia kujifungua akaniambia akijifungua ataenda kukaa kwa dada ake mwingine yule wa Mbagala mpaka arobaini ikipita ndio atarudi (KUMBE YULE SASA NDIO DADA YAKE). Nikamuuliza kwa nini? Pale si yupo kwa dada yake? Akasema huyu hana upendo kama yule na ni mvivu, akikaa hapo atateseka, kujifungua kwenye daktari alishamwambia lazima atajifungua kwa operesheni. Halafu pia akasema akijifungua asingependa kuendelea kukaa pale, kama vipi nimpangishie kwingine. Mimi nikaelewa. KUMBE KUNA PICHA ANAICHEZA BANA. Kwanza huyu sio dada yake, pili lile jamaa ambalo ndio baba mwenye nyumba litakuwa linakuja kuvizia likutane na baba wa mtoto, japo lilishamwambia kwamba ile mimba sio yake, na demu akakomaa mimba ni yake. Lakini pia anataka akijifungua ahame pale kwa kutoroka, asimwambie jamaa kuwa anahama ili siku jamaa akija kama anavotokeaga bila kupiga simu akute hakuna mtu!!!
Siku ikafika akajifungua kwa operation alivoruhusiwa kutoka nikampeleka huko kwa dada yake (Ambaye siku zote 3 alikuwa anashinda hapo hospitali, ndio tukaweza kufahamiana sasa. Mtu poa sana yule shemeji!!). Arobaini ilivokaribia Sharifa akanikumbusha kuhusu kuhama pale Temeke. Kesho yake tu nikatafuta nyumba nikapata sehemu tatu tofauti tofauti, nikamtaarifu. Tukapanga aje aangalie achague atakapopapenda. Keshokutwa yake akamuacha mtoto chap akaja akachagua nyumba aliyoipenda nikalipa kodi ikawa wanafanya ukarabati wakimaliza aingie. Arobaini ikafika ikapita, akarudi kule Temeke sasa kwa ajili ya kujiweka sawa kuhama. Wiki hiyo hiyo kabla hajahama jamaa (ex husband) akatokea kujadili mustakabali wa mahusiano yao, nasikia ilikuwa ugomvi flani jamaa akaondoka kwa hasira lakini hakufanya fujo (HII SASA ALIKUJA KUNISUMULIA JAMAA MWEYEWE BAADAE wakati ananitafuta kuniambia nimetorosha mke wake. Alikuwa ashamtolea posa amuoe mke wa pili na posa ilipokelewa. Walikuwa washakuwa kwenye mahusiano miaka nane, yani toka demu anafika Dar tu. Jamaa ni muislam na demu muislam, mimi mkristo). Chanzo cha ugomvi wao siku hiyo ni kwamba jamaa alikuwa anakomaa kuwa huyo mtoto sio wake na Sharifa anakomaa ni wake, jamaa akasakura mpaka akapata kadi ya hospitali ya mtoto na tangazo la kuzaliwa, mtoto ana majina yangu (ya kikristu) na hata la mtoto ni la kikristu (tumuite LISA humu kwenye hii stori). Kwa hiyo jamaa aliondoka kwa hasira akiogopa atafanya kitu kibaya.
Siku demu aliyopanga kuhama ikafika tukafanya mipango yote akabeba vyombo akahama. Na alikuwa na vyombo vingi. Chumba alichokuwa anakaa kilikuwa kikubwa lakini kimejaa hakuna hata pa kupita. Na mimi nilikuwa sijanunua hata kimoja, nilimkuta na kila kitu. Sasa hapo nyuma alikuwa ananitaarifu kidogo kidogo kwamba litu flani ni chake, sio cha dadake mpaka akawa ametaja vyoooote vilivyomo mle ni vyake. Nikamuuliza mbona anavyombo vyote kama mke wa mtu kabisa? Akasema alijua ataolewa kwa sababu yule jamaa yake waliyeachana alishamtoleaga posa. Kwa hiyo akabeba vyombo vyake akahamia makazi mapya. Chumba na sebule na vyombo vilijaa, na hapo kochi moja kubwa la watu watatu nilimwambia aliache tu ntanunua lingine.
Baada ya wiki moja Sharifa akaniambia jamaa yake wa zamani kampigia (MPAKA WAKATI HUO MI NAJUA WALIACHANA KITAMBO NA HAWAWASIALIANI) kamtukana sana na kamuambia atahakikisha anamharibia kwangu. Nikauliza kivipi amharibie sasa hivi na miaka 3 imeshapita toka wameachana? Akasema hata yeye hajui kwanini, hawezi kuwa kichwani kwa mtu akajua mawazo yake. Akaniweka kwenye mtego eti nikiamua kumsikiliza yule jamaa basi yeye hana cha kusema, ila chochote atakachoniambia nijue ni kwa lengo la kumharibia tu. Kumbe yule jamaa ashaenda pale alipokuwa kampangishia na kakuta demu alishahama. Akauliza kahamia wapi hakuna anayejua, na yeye hata hakuwaambia majirani anahamia wapi. Hata yule alikuwa anajifanya dada ake hakumwambia anahamia wapi (MPAKA WAKATI HUO MIMI NILIKUWA NAJUA YULE NI DADA YAKE KABISA. Basi ndio jamaa akampigia simu demu na vitisho kibao kuwa atamharibia kwa sababu kitu alichomfanyia ni cha kinyama, wamekuwa wote miaka kibao kamfanyia mambo mengi, katoa posa, kashika mimba kamsamehe, lakini Sharifa bado kamtoroka. Nikauliza jamaa kanijuaje akasema kule alikokuwa anafanya kazi kabla hajashika mimba wamempa data zangu zote, na kweli kule walitokea kunifahamu karibu wote na nilikuwa nikienda wananichangamkia sana kama shemeji. Na wengi kati yao walikuwa wanajua Facebook account yangu. Na mimi kwenye bio yangu ya FB nimeweka taarifa zangu zote. Naishi wapi, nafanya kazi wapi, familia yangu, na kuna posts kama 500 hivi etc.
Siku hiyo hiyo nikaingia Facebook jioni nikakuta kuna mtu kanitafuta Facebook mesenja kanisalimu tu halafu kaniambia anaomba kuonana na mimi. Muda huo niko kwangu home sasa, si jioni. Nikampigia simu Sharifa kumuuliza huyo Ex wake anaitwa nani na anajiita nani FB. Akaniambia. Basi nikamjibu yule jamaa kuwa uwezekano wa mimi kuonana nay eye haupo kabisa. Najua yeye ndio ex wa Sharifa. Kwa hiyo kama kuna kitu anataka kwa Sharifa wawasiliane wenyewe mpaka mwisho wasiniingize mimi. Akasema nakosea nikisema Sharifa ni Ex wake, yeye ashamtolea posa na alishapangiwa mahari anataka kupeleka sasa anashangaa Sharifa katoroka nyumbani na yeye kaambiwa yuko kwangu. Akasema kimsingi nimemtorosha mke wake, kwa sababu moyoni kwake ni kama alishafunga nae ndoa. Daaaah, jasho lilinitoka. Kwa hiyo aksisitiza tuonane. Jioni hiyo akili yote ikawa haipo home, wife ananiongelesha hata sieleweki vitu ninavojibu. Akawa anashangaa tu. Kumbe mi nawaza asubuhi ifike chap niende kwa sharifa akanifafanulie vizuri hii ishu ya pos ana mahari na makila kitu. Iliyonichanganya Zaidi ni jamaa kuniambia bado wako wote, hata juzi kati alivorudi kutoka kwa dadake baada ya arobaini kupita mbona alikuwa nyumbani kwa sharifa na walikwazana kidogo ndio akaondoka kwa hasira. Kesho ikafika asubuhi na mapema nikawahi, kufika Sharifa kanidaka juu juu kuuliza jamaa alisemaje, wakati mi nilitaka nile kamoja chap baadae ndio niulize hizo habari. Nikamwambia alinitumia meseji mbili mesenja na zinasema hivi na hivi. Akasema MPENZI WANGU UNANIAMNI? HUYO MTU KAAHIDI ANATAKA KUNIHARIBIA KWAKO, UKIMSIKILIZA UKANIACHA LENGO LAKE LITAKUWA LIMETIMIA. ILA NTATESEKA SANA NA MWANANGU. BASI WE MSIKILIZE TU. Nikamwambia kaaaaaamwe siwezi kumsikiliza jamaa nikamuacha yeye, over.
Naendelea kuandika_
Cc: monde arabe 😂 Mzee wa Noma sanaNoma saana
Afu mbona penzi likinoga ni kimya likifa ndo Uzi jf?
Kwa hio wanaume wapo Arusha na Rombo Mashati au sio?Dar es salaam hakuna wanaume, kuna makabeji(cabbages).
Hovyo kabisa.
Upo vizuri.USIMWAMINI MWANAMKE HATA SIKU MOJA!
TRUE STORY
Nilikutana na Sharifa mwaka 2015 akiwa anafanya kazi mgahawani maeneo ya posta ya zamani. Nilipomuona tu siku ya kwanza nikampenda. Baada ya siku 3 za kwenda kula pale tukazoeana nikamuomba namba akanipa tukaanza mawasiliano ya mara kwa mara. Baada ya mwezi tukaanza mahusiano. Mapenzi yalikuwa motomoto, karibu kutwa zima tunachati. Muda wote ambao haudumii wateja na mimi nikiwa free tunachati tu, mpaka wenzake wakawa wanamshangaa wanamwambia huyo aliyempata safari hii kanasa pabaya (Nikienda pale kazini kwake kuna rafiki yake alikuwa ananipa udaku).
Nikamuuliza ilikuwaje akawa singo, akasema AMEACHANA NA JAMAA YAKE SIKU SI NYINGI KABLA HAJAKUTANA NA MIMI. Penzi lilikolea hakuna mfano, baada ya miezi miwili tu alikuwa muda wote yupo kichwani mwangu (naamini hata yeye kwake ilikuwa hivo kwa sababu nisipomtafuta masaa mawili mfululizo ni kesi). Nakumbuka kuna siku sijui kulitokea nini sikumtafuta toka asubuhi mpaka jioni, nikampigia saa 3 usiku video call, hicho kilio alicholia ni kama amefiwa.
Toka siku hiyo nikaahidi haitatokea tena kutomtafuta kutwa nzima. (Kumbuka yeye hawezi kunitafuta kwa sababu hajui niko kwenye mazingira gani, nina mke na mtoto). NILIPOMUULIZA ANAKAA WAPI AKASEMA ANAKAA KWA DADA YAKE TEMEKE. Kwamba huyo ni dada yake wa pili kuzaliwa ndani mwao (KUMBE NI MPANGAJI MWENZIE). Wa kwanza yupo kijijini, wa pili ndio huyo anaekaa kwake, wa tatu anakaa Mbagala, wa nne kaka yake anakaa Mbezi na wa tano ni yeye (wa mwisho).
Mapenzi yakapamba moto, kukutana ni jumamosi au jumapili, au wiki zingine jumamosi na jumapili. Tukikutana tunashinda ndani (lodge) mpaka usiku ndio anaondoka kwenda kwao na mimi naenda kwangu. Kwa miaka miwili mfululizo nadhani hatujawahi kuruka jumamosi hata moja bila kukutana. Sijawahi kutaka kufika anakokaa kwa sababu niliona ni mapema kuanza kutaka kwenda kwa dadake, na kuna namna ni kama alikuwa anapotezea nikiuliza habari za anakokaa na mimi nikawa sitilii maanani sana Kwenda kwao.
Lakini kidogo kidogo akawa ananipa maelezo ambayo naweza kufika mpaka mtaani anakokaa. Ila hakuwahi kunikaribisha huko kwao. Tulipendana mnooo, kwa siku alikuwa ananitumia picha hata kumi akiwa kwenye mazingira tofauti. Nikiuliza yuko wapi anafanya nini muda huo jibu lake inakuja picha (selfie). Halafu tunaendelea kuchati. Siku za kukutana mara nyingi yeye ndio alikuwa anakuja maeneo ya Sinza ndio tunakutania huko, ikafika kipindi nikawa naenda maeneo ya Temeke tunaingia gesti za huko, sio mbali sana na anakokaa. Ratiba ikawa inabadilika badilika.
Pamoja na kukutania lodge za maeneo ya kwao, hakuwahi kunikaribisha nikapajue kwao. Ila alinionyesha kwa mbali sana mnara wa simu (vodacom) akasema anakaa karibu kabisa na huo mnara, akanitajia na rangi ya nyumba wanayokaa.
Picha lilikuja kuanza mwaka 2017. Nilipata safari ya kuzunguka mikoa mitano ya Tanzania bara nikaamua kusafiri nae tukale Maisha. Hizo zilikuwa wiki 3 za furaha kubwa kuliko kipindi chochote kwenye maisha yangu, siji kuzisahau.
Baada ya kurudi safari haikupita wiki mbili akaniambia ni mjamzito. Nikafurahi sana, kwa sababu nilikuwa natamani siku zote anizalie mtoto na kama sio kipingamizi cha ndoa nadhani ningemuoa haraka sana tulivokutana. Tatizo nilikuwa na mke tayari. Kuna siku nilienda kufanya mishe Mbagala na yeye asubuhi alikuwa ameniambia anaumwa (mimba ilikuwa inamsumbua sana ile), basi nikaamua kwenda pale bila kumwambia.
Nikafika mpaka pale bila yeye kunielekeza, nilipofika koridoni nikamkuta jirani yao akanionyesha chumba chao nikaingia. Akashangaa sana kwa sababu hakujua kuwa naenda pale, lakini akanipokea vizuri tu tukapiga stori tukatoka wote tukaenda duka la madawa tukanunua dawa akarudi kwao mi nikarudi zangu ofisini.
Sasa humo alimonikaribisha aliniambia ndio sebuleni kwa dada ake, chumba cha pili ndio cha kulala. Ila yeye analala sebuleni (kulikuwa na kila kitu mpaka kitanda). KUMBE NI CHUMBA CHAKE alichopangishiwa na yule jamaa aliyeniambia waliachana (MPAKA WAKATI HUO WALIKUWA BADO WAKO PAMOJA na sikuwahi kushtuka kuwa yuko na mtu na jamaa hajawahi kushtuka kuwa anaibiwa). Jamaa nae alikuwa na mke wake hivo anakujaga mara moja moja sana. Akija anapiga zake bao chap anarudi kwake, halafu haonekani tena mpaka baada ya mwezi au miwili (alikuwa dereva wa magari ya safari ndefu).
Kilichofanya nisishtuke kabisa kuwa tuko wawili ni kwamba jamaa yake hanaga mawasiliano ya simu ya mara kwa mara. Nadhani akimhitaji alikuwa anaenda tu geto alikompangishia bila kupiga simu wala kutuma meseji. Na akienda hakagui simu hata mara moja kwa sababu angekuwa anakagua angeshajua kitambo kuwa demu wake yuko na mimi. Demu hajawahi kufuta meseji yangu hata moja toka tulipokutana. Na picha zote alizonitumia wasap hajawahi kufuta kwenye simu yake hata moja hata zangu nilizomtumia mimi.
Na kumbukumbu ya simu nilizompigia hajawahi kufuta hata moja. Kitu kingine, nikiwa nae lodge simu yake inakaa hapo mezani muda wote haigusi hata mara moja, na ikipigwa au ikiingia meseji na mimi niko karibu nayo, ataniuliza mimi ni nani anapiga au nani katuma meseji. Yani alikuwa demu ambaye hana mambo mengi kabisa, nilimpenda mnooo na alijenga mazingira ya mimi kumuamini asilimia 100 (sipendi kabisa madem ambaye ukiwa naye muda wote yuko na simu mkononi, huyu alikuwa wa kwanza kukutana nae wa aina ya pekee). Kama mara mbili imewahi kupigwa simu tukiwa pamoja, aliempigia akamfokea sana, halafu yeye hakujibu. Nilipokuwa namuuliza huyo nani akawa anasema ni yule jamaa waliyeachana siku hizi anamsumbua sana anataka warudiane, na yeye hataki kwa sababu ameshakuwa na mimi. (KUMBUKA MPAKA HAPO WALIKUWA HAWAJAACHANA ila mimi nilikuja kujua baadae sana walipochana kweli baada ya demu kujifungua na mimi kumuhamisha demu kutoka pale (”KWA DADA YAKE”) nikamleta maeneo ya jirani na ninakokaa ili iwe rahisi kuwaona na mtoto kila siku).
Kuna wakati akaniambia dadake amesafiri kaenda nyumbani Iringa. Basi siku moja asubuhi tu kabla hajaamka nikaenda pale (Kazi alikuwa ashasimama kwa ajili ya ujauzito). Toka siku hiyo tukaacha kwenda lodge, mambo yote tunamalizia hapo (KUMBUKA KAPANGISHIWA NA MWANAUME ila mimi najua ni kwa dada yake). Nikawa naenda mara kwa mara naingiaga tu kama kwangu.
Aliyejifanya dada ake ananipokea fresh nashinda hapo. Wanapika misosi tunakula kila nikienda. Tunakaa chumbani tukitosheka tunakaa koridoni tukichoka tunakaa nje, yani nikawa huru mno. ILA KUNA MACHO WAPANGAJI WENZIE WALIKUWA WANANIANGALIA KAMA YA KUNIAMBIA KITU mi sina hili wala lile, nimezama kwenye penzi zito. Kabla ya hapo nilikuwa nishaanza hata kuchangia kodi, kwamba mle sebleni anamolala kodi nalipa mimi, nikamwambia amwambie kabisa dadake. Na alikuwa na mtoto yuko darasa la sita huko kijijini kwao (kwa bibi yake huyo mwanamke wangu) nikawa nasaidia kumhudumia.
Picha likaendelea. Siku moja akaniambia anaumwa, mimi mapema tu nikatokea pale. Nikaingia chumbani nikavua zangu shati nikabaki na singlet, akaniandalia chai nikanywa baadae tukatoka tukakaa koridoni, nikamwambia sikai sana ntaondoka muda si mrefu.
Tukiwa hapo koridoni akaingia jamaa, alipofika karibu na chumba cha demu (WAKATI HUO MI NAJUA NI SEBLENI KWA DADAKE) akanisalimia mimi HALAFU BILA KUPIGA HODI WALA NINI akaingia humo chumbani. Demu akasimama akamfuata huko ndani, nikasikia jamaa anaunguruma kama analalamika kitu kama dakika moja nzima, ila maneno nilikuwa siyasikii. Halfu demu akatoka akamuacha jamaa huko ndani. Akaniuliza kama anisindikize au vipi kwa sababu nilikuwa nimemwambia naondoka sasa hivi.
Kwa namna yule jamaa alivoingia nikawa na maswali mengi kichwani nikawa nimeghairi kuondoka ili jamaa aondoke nimuulize demu yule ni nani. Kwa hiyo nikamjibu kuwa nimeghairi kuondoka ntaondoka jioni (Hiyo ilikuwa saa 5 hivi asubuhi). Kwa unyonge akarudi kule ndani, nikasikia jamaa sasa linatukana matusi, kuwa halipendi ujinga na u.s.e.n.g.e u.s.e.n.g.e, na maneno mengine makali makali. Mengine nikawa sisikii mengine nasikia, kama dakika 2 hivi. Halafu jamaa likatoka likabamiza mlango kwa nguvu huku linaondoka linamwambia demu aache upumbavu wake kabisa. Hilooooooo likapotea zake……
ITAENDELEA KESHO***
Sasa hapo wa kutoaminiwa ni wewe bro!!una mke,harsfu unampanga Binti wa watu!!USIMWAMINI MWANAMKE HATA SIKU MOJA!
TRUE STORY
Nilikutana na Sharifa mwaka 2015 akiwa anafanya kazi mgahawani maeneo ya posta ya zamani. Nilipomuona tu siku ya kwanza nikampenda. Baada ya siku 3 za kwenda kula pale tukazoeana nikamuomba namba akanipa tukaanza mawasiliano ya mara kwa mara. Baada ya mwezi tukaanza mahusiano. Mapenzi yalikuwa motomoto, karibu kutwa zima tunachati. Muda wote ambao haudumii wateja na mimi nikiwa free tunachati tu, mpaka wenzake wakawa wanamshangaa wanamwambia huyo aliyempata safari hii kanasa pabaya (Nikienda pale kazini kwake kuna rafiki yake alikuwa ananipa udaku).
Nikamuuliza ilikuwaje akawa singo, akasema AMEACHANA NA JAMAA YAKE SIKU SI NYINGI KABLA HAJAKUTANA NA MIMI. Penzi lilikolea hakuna mfano, baada ya miezi miwili tu alikuwa muda wote yupo kichwani mwangu (naamini hata yeye kwake ilikuwa hivo kwa sababu nisipomtafuta masaa mawili mfululizo ni kesi). Nakumbuka kuna siku sijui kulitokea nini sikumtafuta toka asubuhi mpaka jioni, nikampigia saa 3 usiku video call, hicho kilio alicholia ni kama amefiwa.
Toka siku hiyo nikaahidi haitatokea tena kutomtafuta kutwa nzima. (Kumbuka yeye hawezi kunitafuta kwa sababu hajui niko kwenye mazingira gani, nina mke na mtoto). NILIPOMUULIZA ANAKAA WAPI AKASEMA ANAKAA KWA DADA YAKE TEMEKE. Kwamba huyo ni dada yake wa pili kuzaliwa ndani mwao (KUMBE NI MPANGAJI MWENZIE). Wa kwanza yupo kijijini, wa pili ndio huyo anaekaa kwake, wa tatu anakaa Mbagala, wa nne kaka yake anakaa Mbezi na wa tano ni yeye (wa mwisho).
Mapenzi yakapamba moto, kukutana ni jumamosi au jumapili, au wiki zingine jumamosi na jumapili. Tukikutana tunashinda ndani (lodge) mpaka usiku ndio anaondoka kwenda kwao na mimi naenda kwangu. Kwa miaka miwili mfululizo nadhani hatujawahi kuruka jumamosi hata moja bila kukutana. Sijawahi kutaka kufika anakokaa kwa sababu niliona ni mapema kuanza kutaka kwenda kwa dadake, na kuna namna ni kama alikuwa anapotezea nikiuliza habari za anakokaa na mimi nikawa sitilii maanani sana Kwenda kwao.
Lakini kidogo kidogo akawa ananipa maelezo ambayo naweza kufika mpaka mtaani anakokaa. Ila hakuwahi kunikaribisha huko kwao. Tulipendana mnooo, kwa siku alikuwa ananitumia picha hata kumi akiwa kwenye mazingira tofauti. Nikiuliza yuko wapi anafanya nini muda huo jibu lake inakuja picha (selfie). Halafu tunaendelea kuchati. Siku za kukutana mara nyingi yeye ndio alikuwa anakuja maeneo ya Sinza ndio tunakutania huko, ikafika kipindi nikawa naenda maeneo ya Temeke tunaingia gesti za huko, sio mbali sana na anakokaa. Ratiba ikawa inabadilika badilika.
Pamoja na kukutania lodge za maeneo ya kwao, hakuwahi kunikaribisha nikapajue kwao. Ila alinionyesha kwa mbali sana mnara wa simu (vodacom) akasema anakaa karibu kabisa na huo mnara, akanitajia na rangi ya nyumba wanayokaa.
Picha lilikuja kuanza mwaka 2017. Nilipata safari ya kuzunguka mikoa mitano ya Tanzania bara nikaamua kusafiri nae tukale Maisha. Hizo zilikuwa wiki 3 za furaha kubwa kuliko kipindi chochote kwenye maisha yangu, siji kuzisahau.
Baada ya kurudi safari haikupita wiki mbili akaniambia ni mjamzito. Nikafurahi sana, kwa sababu nilikuwa natamani siku zote anizalie mtoto na kama sio kipingamizi cha ndoa nadhani ningemuoa haraka sana tulivokutana. Tatizo nilikuwa na mke tayari. Kuna siku nilienda kufanya mishe Mbagala na yeye asubuhi alikuwa ameniambia anaumwa (mimba ilikuwa inamsumbua sana ile), basi nikaamua kwenda pale bila kumwambia.
Nikafika mpaka pale bila yeye kunielekeza, nilipofika koridoni nikamkuta jirani yao akanionyesha chumba chao nikaingia. Akashangaa sana kwa sababu hakujua kuwa naenda pale, lakini akanipokea vizuri tu tukapiga stori tukatoka wote tukaenda duka la madawa tukanunua dawa akarudi kwao mi nikarudi zangu ofisini.
Sasa humo alimonikaribisha aliniambia ndio sebuleni kwa dada ake, chumba cha pili ndio cha kulala. Ila yeye analala sebuleni (kulikuwa na kila kitu mpaka kitanda). KUMBE NI CHUMBA CHAKE alichopangishiwa na yule jamaa aliyeniambia waliachana (MPAKA WAKATI HUO WALIKUWA BADO WAKO PAMOJA na sikuwahi kushtuka kuwa yuko na mtu na jamaa hajawahi kushtuka kuwa anaibiwa). Jamaa nae alikuwa na mke wake hivo anakujaga mara moja moja sana. Akija anapiga zake bao chap anarudi kwake, halafu haonekani tena mpaka baada ya mwezi au miwili (alikuwa dereva wa magari ya safari ndefu).
Kilichofanya nisishtuke kabisa kuwa tuko wawili ni kwamba jamaa yake hanaga mawasiliano ya simu ya mara kwa mara. Nadhani akimhitaji alikuwa anaenda tu geto alikompangishia bila kupiga simu wala kutuma meseji. Na akienda hakagui simu hata mara moja kwa sababu angekuwa anakagua angeshajua kitambo kuwa demu wake yuko na mimi. Demu hajawahi kufuta meseji yangu hata moja toka tulipokutana. Na picha zote alizonitumia wasap hajawahi kufuta kwenye simu yake hata moja hata zangu nilizomtumia mimi.
Na kumbukumbu ya simu nilizompigia hajawahi kufuta hata moja. Kitu kingine, nikiwa nae lodge simu yake inakaa hapo mezani muda wote haigusi hata mara moja, na ikipigwa au ikiingia meseji na mimi niko karibu nayo, ataniuliza mimi ni nani anapiga au nani katuma meseji. Yani alikuwa demu ambaye hana mambo mengi kabisa, nilimpenda mnooo na alijenga mazingira ya mimi kumuamini asilimia 100 (sipendi kabisa madem ambaye ukiwa naye muda wote yuko na simu mkononi, huyu alikuwa wa kwanza kukutana nae wa aina ya pekee). Kama mara mbili imewahi kupigwa simu tukiwa pamoja, aliempigia akamfokea sana, halafu yeye hakujibu. Nilipokuwa namuuliza huyo nani akawa anasema ni yule jamaa waliyeachana siku hizi anamsumbua sana anataka warudiane, na yeye hataki kwa sababu ameshakuwa na mimi. (KUMBUKA MPAKA HAPO WALIKUWA HAWAJAACHANA ila mimi nilikuja kujua baadae sana walipochana kweli baada ya demu kujifungua na mimi kumuhamisha demu kutoka pale (”KWA DADA YAKE”) nikamleta maeneo ya jirani na ninakokaa ili iwe rahisi kuwaona na mtoto kila siku).
Kuna wakati akaniambia dadake amesafiri kaenda nyumbani Iringa. Basi siku moja asubuhi tu kabla hajaamka nikaenda pale (Kazi alikuwa ashasimama kwa ajili ya ujauzito). Toka siku hiyo tukaacha kwenda lodge, mambo yote tunamalizia hapo (KUMBUKA KAPANGISHIWA NA MWANAUME ila mimi najua ni kwa dada yake). Nikawa naenda mara kwa mara naingiaga tu kama kwangu.
Aliyejifanya dada ake ananipokea fresh nashinda hapo. Wanapika misosi tunakula kila nikienda. Tunakaa chumbani tukitosheka tunakaa koridoni tukichoka tunakaa nje, yani nikawa huru mno. ILA KUNA MACHO WAPANGAJI WENZIE WALIKUWA WANANIANGALIA KAMA YA KUNIAMBIA KITU mi sina hili wala lile, nimezama kwenye penzi zito. Kabla ya hapo nilikuwa nishaanza hata kuchangia kodi, kwamba mle sebleni anamolala kodi nalipa mimi, nikamwambia amwambie kabisa dadake. Na alikuwa na mtoto yuko darasa la sita huko kijijini kwao (kwa bibi yake huyo mwanamke wangu) nikawa nasaidia kumhudumia.
Picha likaendelea. Siku moja akaniambia anaumwa, mimi mapema tu nikatokea pale. Nikaingia chumbani nikavua zangu shati nikabaki na singlet, akaniandalia chai nikanywa baadae tukatoka tukakaa koridoni, nikamwambia sikai sana ntaondoka muda si mrefu.
Tukiwa hapo koridoni akaingia jamaa, alipofika karibu na chumba cha demu (WAKATI HUO MI NAJUA NI SEBLENI KWA DADAKE) akanisalimia mimi HALAFU BILA KUPIGA HODI WALA NINI akaingia humo chumbani. Demu akasimama akamfuata huko ndani, nikasikia jamaa anaunguruma kama analalamika kitu kama dakika moja nzima, ila maneno nilikuwa siyasikii. Halfu demu akatoka akamuacha jamaa huko ndani. Akaniuliza kama anisindikize au vipi kwa sababu nilikuwa nimemwambia naondoka sasa hivi.
Kwa namna yule jamaa alivoingia nikawa na maswali mengi kichwani nikawa nimeghairi kuondoka ili jamaa aondoke nimuulize demu yule ni nani. Kwa hiyo nikamjibu kuwa nimeghairi kuondoka ntaondoka jioni (Hiyo ilikuwa saa 5 hivi asubuhi). Kwa unyonge akarudi kule ndani, nikasikia jamaa sasa linatukana matusi, kuwa halipendi ujinga na u.s.e.n.g.e u.s.e.n.g.e, na maneno mengine makali makali. Mengine nikawa sisikii mengine nasikia, kama dakika 2 hivi. Halafu jamaa likatoka likabamiza mlango kwa nguvu huku linaondoka linamwambia demu aache upumbavu wake kabisa. Hilooooooo likapotea zake……
ITAENDELEA KESHO***