Usafiri enzi zile Mwanza yetu

Usafiri enzi zile Mwanza yetu

Umeona eeh! Sie tulikuwa tunasagia kirumba, unapeleka mzigo leo, kesho yake ndio unaenda kuchukua unga


Mashine ya kusaga Pasiansi na nyananoro ilikuwa nyamanoro kwenye mashine ya maji,aliyekuwa anasaga aliitwa Mashauli, ikiharibika mnachapa lapa maka Kirimba au Sahara kata ya Pamba
 
Umeona eeh! Sie tulikuwa tunasagia kirumba, unapeleka mzigo leo, kesho yake ndio unaenda kuchukua unga

We ram kama ulikuwa unakaa muelekeo wa Pasiansi kwa nini uende hadi kirumba badala ya kwenda kwenye mashine ya mama John maeneo ya Kariakoo kubwa?
 
Last edited by a moderator:
Nyegezi,ILOVE MANORI.

Dah umenikumbusha mbali sana na hii I Love Manori aisee...Mwenye haya Mabasi tulikuwa tunaishi naye jirani Kilimahewa kipindi hichi sehemu kubwa ukiwa ni majaruba ya Mpunga.Mtoto wake Peter Manori tukasoma naye Nyanza Primary alikuwa na hela huyo...Akija shule na shilingi Mia Tano tunamshangaa mno inawezekanaje mtoto mdogo akawa na kiasi hiki cha pesa.
 
Huo sijui mwaka gani unouongelea, lakini nnajuwa aliyekuwa mwanzilishi wa basi za mjini Mwanza alianza kibasi kimoja tu kinaitwa Wahiwahi mwaka 1973 ilikuwa Nissan Bus ya passenger 24 na 1974 ikaongezeka ya pili Bus Leyland 52 passengers zikienda Igoma, 1974 ndio zikaanza kuongezeka za watu wengine. Siku hizo gari zilikuwa nyang'anyang'a mpya zilikuwa ni hizo za Wahiwahi tu.

Sijui kama ulikuwa umeshazaliwa wakati huo.

Kwi kwi kwi teh teh teh!

Shkamoo.. faizafox
 
Last edited by a moderator:
Wakati mwingine tulitembea mpaka,nyegezi kilimo

Mkuu ulisoma Nyegezi KILIMO? mwaka gani huo? Wakati huo express zilikuwa zinaishia kona ya Butimba, tunapiga lapa kupitia magereza, fisheries, Nyamalango mpaka chuoni!
 
Kashekulu alikuwa na hoteli na kuja karibu na nganza sec,tulikuwa tunatoroka kwenda hapo,kununua mkate na juice
Kashekulo alikuwa mwalimu pale MATI Nyegezi wakati huo!
 
Ndugu mashine za kariakoo kubwa zilianza kama sikosei miaka ya tisini, hapa naongelea miaka ya 86, 85 kurudi nyuma

We ram kama ulikuwa unakaa muelekeo wa Pasiansi kwa nini uende hadi kirumba badala ya kwenda kwenye mashine ya mama John maeneo ya Kariakoo kubwa?
 
Last edited by a moderator:
Ndugu mashine za kariakoo kubwa zilianza kama sikosei miaka ya tisini, hapa naongelea miaka ya 86, 85 kurudi nyuma

Aliye anzisha jina la soko la Kariakoo ni mme wa mama yangu mkubwa, kwasasa ni marehemu alijulikana kwa jina la baba Chale, nahuyo mwanae alikuwa chautundu hakuna mfano, sarakasi yumo,ngumi usiseme,hataungekuwa na ndevu utaliatu. ikabidi aitwe Chale sugu. hata shule aliishia darasa la nne shule ya Makongoro ,alikuwa anajificha mlima kwasasa panaitwa mjimwema .hiloeneo la mjimwema tulikuwa tunagombanishia Mbwa kila j.mosi tukitoka josho KAUMA ya zamani, ilikuwa kama mbwa wako unamuamini kwa ukali unamuleta mlimani,mbwa wa Chale sugu walikuwa wakali baraa ila ikitokea mbwa wake akapigwa basi mbwa aliyeshinda atapigwa mawe na wewe ukileta za kuleta unapigwa, mimi nilikuwa natumia kule kuwa ndugu na Chale sugu nami naonekana mtemi mkwala wangu ilikuwa sarakasi na mabreka dansi,Enzi za Kabibi Hotel
 
Nimefurahi sana jinsi watu tunavyoifahamu mwanza kila mtu kwa wakati wake;
Mm nakumbuka,
Siku ya mechi tunapanda gola kuangalia mpira ccm kirumba, goli moja unaliona nusu huku ukisikiliza redioni,
Movie mwaloni kwa kabago, kariakoo kubwa kulikuwa na chekechea ya mtaa, miaka y tisini bati lilipaa likamuangukia mtoto anatoka mashineni akafa na shule ikafa, sungusungu ghana ilikuwa balaa alichapwa bakora jamaa mmoja hadi akafa.
Shule ya msingi nyamanoro saa saba mchana haukatizi eti kuna majini yanapiga vibao.
 
Mimi nakbuka usafiri ulivyokuwa wa shida wakati huo mkuyuni - mjini mwanza kulikuwa na mabasi matatu tu yenye vichwa vya Bedford yakiitwa; mwanza Pernel, mantaline na black mamba! Du! Kipindi hicho igoma na usagara ni mwendo wa 109 tu da! Kweli tumetoka mbali!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom