Heaven Seeker
JF-Expert Member
- May 12, 2017
- 478
- 1,047
Heshima kwenu Wakuu.
Nimebahatika kuishi Nchi za wenzetu kwa Mabeberu, kiasi fulani nimejifunza mambo kadhaa.
Sisi Wabongo tunaishi maisha ya ujamaa, yaani kugawana kidogo tunachokuwa nacho ili kila mtu apate japo mkate. Hali hii inatokana na ukweli kuwa idadi kubwa ya sisi wabongo bado maisha yetu yapo chini sana hivyo idadi ya wategemezi kwenye familia zetu bado ni kubwa sana hivyo tunaishi kwa kutegemeana.
Hata hivyo, hali ni tofauti kwa wenzetu mabeberu. Nadhani hii inatokana na kuwa, wao kiwango cha ukosefu wa ajira ni kiasi kidogo sana, hivyo kila familia ina uwezo wa kujiingizia kipato chake na kumudu gharama za maisha. Jambo lingine ni kuwa, wenzetu hawana maisha ya kijamaa kiviile. Yaani ni yeye na familia yake full stop. Mnaweza kuwa mnaishi nyumba moja ila mkawa mnasalimiana tu hakuna stories zaidi ya hapo. Msamiati wa kukopana pesa sijauona, ukiwa na shida unaweza kuomba msaada kwenye serikali ya jimbo lako. Kwa nchi kama Sweden, serikali ya mahali unapoishi inaweza kugharamia gharama za kuishi kwa vijana wasiokuwa na ajira ama kupoteza ajira. Unaweza kupata pesa ya kujikimu na ukalipiwa rent. Hi ni kwa raia pekee. Siyo kama sie wakuja.
Nirudi kwenye mada sasa.
Vibwagizo kidogo
1. Nilipokuwa nasoma wakati flani, kutokana na maisha yetu ya uduni, nilikuwa nikiomba masaada kwa ndugu yangu (binamu) hapa na pale ili kukidhi mahitaji muhimu. Huyu binamu yangu, kwa maoni yangu, alikuwa na unafuu kidogo wa maisha kwa maana ya kuwa na ajira, nyumba yake na kiusafiri. Hivyo kwa kuwaza kwangu kipindi hicho nikajua atakuwa na maisha bora na ana mpunga wa kutosha. Chakushangaza, wakati mmoja nikamuomba msaada nilikuwa chuoni wakati boom limekata akawa amenitumia kiasi cha pesa kidogo sana kuliko nilivyotarajia. Niwe muwazi kuwa nilifadhaika, nikasema, yaani kweli binamu ananitumia elfu 10 tu kweli? na nimemweleza kuwa nina shida na sina kitu kabisa?
2. Huyohuyo binamu yangu, wakati nipo mdogo kwa shangazi yangu, nilikuwa nashangaa, iweje tunaishi maisha magumu pale home pengine pesa ya kula inakata na wakati yeye ana kazi huko Dar na anakula maisha? (mawazo yangu). Na pesa ilipokuwa inakata, binamu alikuwa hatumi pesa mpaka Shangazi apige simu na akipiga alikuwa anatuma kiasi kidogo sana. Kwakweli niliwaza sana nikajisemea kuwa kwanini watu waliofanikiwa kupata vijisenti hawatumi pesa kwa wazazi wao mpaka waambiwe? Ina maana hawajui wajibu wao?
3. Kumbe buana, yale yalikuwa nawazo ya utoto tu. Ukubwani sasa nimegundua kuwa Binamu yangu alikuwa ameajiriwa na pengine kipato chake kilikuwa cha kawaida sana na kutokana na majukumu ya familia yake na maisha ya mjini tena Dar, basi kipato chake si chochote kivile kumudu maisha na kutuma mapesa mengi kwao kama nilivyokuwa nawaza nikiwa mdogo.
4. Mawazo yangu hapo juu, yametokana na ukweli kuwa, pamoja na kipato changu kuongezeka karibia mara mbili ya kipato changu cha awali, nimegundua kuwa hata mie wazazi wangu sijawatosheleza kwa kuwasaidia mahitaji yao kwa kiwango cha kuridhisha sana. Yaani wanaishi maisha yenye unafuu kidogo ila bado wana ganga ganga tu. Pamoja na kujitahidi kutokuwa mbinafsi na kuishi maisha ya kawaida, bado naona kabisa hata msaada wangu wa kwa ndugu na jamaa bado ni kidogo sana pamoja na kipato changu kuongezeka kidogo. Najua huwezi kumfurahisha kila mtu na huwezi kuacha kulaumiwa, ila naamini wapo watu wanaoniona kama mtu niliyefanikiwa na nimeshindwa kuwasaidia. Kumbe bado naganga ganga tu.
Naomba nijielekeze kwenye hoja ya msingi baada ya vibwagizo hapo juu.
Naomba kulizungumzia kundi la wale ambao vipato vyao huweza kugharamia mahitaji ya msingi kama chakula, mavazi na kulipia kodi ya nyumba ama pengine anaishi kwenye nyumba yake. Kundi hili baadhi ya watu huliita kama middle class family. Kwa uchunguzi wangu, kundi hili lina mzigo mkubwa kwenye jamii maana jamii yetu hasa wale wanaotoka kwenye extended families na jamaa zao hawawezi kumudu mahitaji muhimu, hulitazama kundi hili kama kundi lenye unafuu kimaisha, hivyo hutegemea kupata msaada kutoka kwao. Hata hivyo, kutokana na kipato chao kulingana na matumizi, tena yale ya lazima tu, kiukweli kundi hili hujikuta kwenye changamoto kubwa kimaisha na kushindwa kukidhi matarajio ya jamaa zake na kuonekana kama mtu mbinafsi, hivyo hutupiwa lawama kwa kiasi kikubwa ilihali vipato vyao pengine vinatosheleza tu kula chakula na kulipia kodi ya nyumba.
Je, wewe kama kipato chako kina balance na matumizi yale ya lazima pekee, yaani chakula, mavazi na makazi. Huwa unatumia njia gani kusaidia ndugu na jamaa zako ambao wana maisha duni na wana matarajio makubwa kutoka kwako? Kumbuka nazungumzia mtu ambaye akipata kipato chake kinalingana na matumizi kwa mwezi husika na hawezi kufanya hata savings. Nyongeza, namzungumzia mtu ambaye si mbinafsi, ana moyo wa kuwasaidia wahitaji ila uwezo wake upo chini zaidi ya kile anachotakiwa kufanya katika jamii yake. Wahitaji wanaweza kuwa ndugu wa karibu wa tumbo moja, mabinamu, wajomba, mashangazi, baba mkubwa, mama mkubwa, rafiki wa karibu sana n.k.
1) Je, ni sahihi kukubali lawama kwa muda flani ili ubakie kwenye mapambano kwanza na usitoe msaada mpaka utoboe kwanza kufikia hatua ya kipato kuwa juu ya gharama za maisha? Natambua kuwa kadri kipato kinavyoongezeka mtu anaweza kuchagua maisha ya juu zaidi hivyo isifike siku ambapo atabakiza savings na kuwasaidia wahitaji, ila hapa nazungumzia wale ambao wana nia ya dhati ya kuwasaidia jamaa zao na pengine wangependa kuridhika na maisha waliyonayo hasa anapokuwa amefikia kwenye lifestyle inayomwezesha kula na kubakisha savings kila mwezi.
2) Au Je, kama maisha ya swali hapo juu ni ubinafsi, unadhani ni sahihi kupunguza gharama za maisha yako ili ukubali kurudi nyuma kidogo ili kubakiza savings, ziweze kuwasaidia jamaa zako wanaokutegemea? Kama kweli tunataka kutekeleza msemo wa kwamba kutoa ni moyo na si utajiri..?
3) Je, jambo hilo namba 2 hapo juu ni practical in real sense?
Nini maoni yako? Karibu ku-share mawazo ili tuelimishhane..
Nimebahatika kuishi Nchi za wenzetu kwa Mabeberu, kiasi fulani nimejifunza mambo kadhaa.
Sisi Wabongo tunaishi maisha ya ujamaa, yaani kugawana kidogo tunachokuwa nacho ili kila mtu apate japo mkate. Hali hii inatokana na ukweli kuwa idadi kubwa ya sisi wabongo bado maisha yetu yapo chini sana hivyo idadi ya wategemezi kwenye familia zetu bado ni kubwa sana hivyo tunaishi kwa kutegemeana.
Hata hivyo, hali ni tofauti kwa wenzetu mabeberu. Nadhani hii inatokana na kuwa, wao kiwango cha ukosefu wa ajira ni kiasi kidogo sana, hivyo kila familia ina uwezo wa kujiingizia kipato chake na kumudu gharama za maisha. Jambo lingine ni kuwa, wenzetu hawana maisha ya kijamaa kiviile. Yaani ni yeye na familia yake full stop. Mnaweza kuwa mnaishi nyumba moja ila mkawa mnasalimiana tu hakuna stories zaidi ya hapo. Msamiati wa kukopana pesa sijauona, ukiwa na shida unaweza kuomba msaada kwenye serikali ya jimbo lako. Kwa nchi kama Sweden, serikali ya mahali unapoishi inaweza kugharamia gharama za kuishi kwa vijana wasiokuwa na ajira ama kupoteza ajira. Unaweza kupata pesa ya kujikimu na ukalipiwa rent. Hi ni kwa raia pekee. Siyo kama sie wakuja.
Nirudi kwenye mada sasa.
Vibwagizo kidogo
1. Nilipokuwa nasoma wakati flani, kutokana na maisha yetu ya uduni, nilikuwa nikiomba masaada kwa ndugu yangu (binamu) hapa na pale ili kukidhi mahitaji muhimu. Huyu binamu yangu, kwa maoni yangu, alikuwa na unafuu kidogo wa maisha kwa maana ya kuwa na ajira, nyumba yake na kiusafiri. Hivyo kwa kuwaza kwangu kipindi hicho nikajua atakuwa na maisha bora na ana mpunga wa kutosha. Chakushangaza, wakati mmoja nikamuomba msaada nilikuwa chuoni wakati boom limekata akawa amenitumia kiasi cha pesa kidogo sana kuliko nilivyotarajia. Niwe muwazi kuwa nilifadhaika, nikasema, yaani kweli binamu ananitumia elfu 10 tu kweli? na nimemweleza kuwa nina shida na sina kitu kabisa?
2. Huyohuyo binamu yangu, wakati nipo mdogo kwa shangazi yangu, nilikuwa nashangaa, iweje tunaishi maisha magumu pale home pengine pesa ya kula inakata na wakati yeye ana kazi huko Dar na anakula maisha? (mawazo yangu). Na pesa ilipokuwa inakata, binamu alikuwa hatumi pesa mpaka Shangazi apige simu na akipiga alikuwa anatuma kiasi kidogo sana. Kwakweli niliwaza sana nikajisemea kuwa kwanini watu waliofanikiwa kupata vijisenti hawatumi pesa kwa wazazi wao mpaka waambiwe? Ina maana hawajui wajibu wao?
3. Kumbe buana, yale yalikuwa nawazo ya utoto tu. Ukubwani sasa nimegundua kuwa Binamu yangu alikuwa ameajiriwa na pengine kipato chake kilikuwa cha kawaida sana na kutokana na majukumu ya familia yake na maisha ya mjini tena Dar, basi kipato chake si chochote kivile kumudu maisha na kutuma mapesa mengi kwao kama nilivyokuwa nawaza nikiwa mdogo.
4. Mawazo yangu hapo juu, yametokana na ukweli kuwa, pamoja na kipato changu kuongezeka karibia mara mbili ya kipato changu cha awali, nimegundua kuwa hata mie wazazi wangu sijawatosheleza kwa kuwasaidia mahitaji yao kwa kiwango cha kuridhisha sana. Yaani wanaishi maisha yenye unafuu kidogo ila bado wana ganga ganga tu. Pamoja na kujitahidi kutokuwa mbinafsi na kuishi maisha ya kawaida, bado naona kabisa hata msaada wangu wa kwa ndugu na jamaa bado ni kidogo sana pamoja na kipato changu kuongezeka kidogo. Najua huwezi kumfurahisha kila mtu na huwezi kuacha kulaumiwa, ila naamini wapo watu wanaoniona kama mtu niliyefanikiwa na nimeshindwa kuwasaidia. Kumbe bado naganga ganga tu.
Naomba nijielekeze kwenye hoja ya msingi baada ya vibwagizo hapo juu.
Naomba kulizungumzia kundi la wale ambao vipato vyao huweza kugharamia mahitaji ya msingi kama chakula, mavazi na kulipia kodi ya nyumba ama pengine anaishi kwenye nyumba yake. Kundi hili baadhi ya watu huliita kama middle class family. Kwa uchunguzi wangu, kundi hili lina mzigo mkubwa kwenye jamii maana jamii yetu hasa wale wanaotoka kwenye extended families na jamaa zao hawawezi kumudu mahitaji muhimu, hulitazama kundi hili kama kundi lenye unafuu kimaisha, hivyo hutegemea kupata msaada kutoka kwao. Hata hivyo, kutokana na kipato chao kulingana na matumizi, tena yale ya lazima tu, kiukweli kundi hili hujikuta kwenye changamoto kubwa kimaisha na kushindwa kukidhi matarajio ya jamaa zake na kuonekana kama mtu mbinafsi, hivyo hutupiwa lawama kwa kiasi kikubwa ilihali vipato vyao pengine vinatosheleza tu kula chakula na kulipia kodi ya nyumba.
Je, wewe kama kipato chako kina balance na matumizi yale ya lazima pekee, yaani chakula, mavazi na makazi. Huwa unatumia njia gani kusaidia ndugu na jamaa zako ambao wana maisha duni na wana matarajio makubwa kutoka kwako? Kumbuka nazungumzia mtu ambaye akipata kipato chake kinalingana na matumizi kwa mwezi husika na hawezi kufanya hata savings. Nyongeza, namzungumzia mtu ambaye si mbinafsi, ana moyo wa kuwasaidia wahitaji ila uwezo wake upo chini zaidi ya kile anachotakiwa kufanya katika jamii yake. Wahitaji wanaweza kuwa ndugu wa karibu wa tumbo moja, mabinamu, wajomba, mashangazi, baba mkubwa, mama mkubwa, rafiki wa karibu sana n.k.
1) Je, ni sahihi kukubali lawama kwa muda flani ili ubakie kwenye mapambano kwanza na usitoe msaada mpaka utoboe kwanza kufikia hatua ya kipato kuwa juu ya gharama za maisha? Natambua kuwa kadri kipato kinavyoongezeka mtu anaweza kuchagua maisha ya juu zaidi hivyo isifike siku ambapo atabakiza savings na kuwasaidia wahitaji, ila hapa nazungumzia wale ambao wana nia ya dhati ya kuwasaidia jamaa zao na pengine wangependa kuridhika na maisha waliyonayo hasa anapokuwa amefikia kwenye lifestyle inayomwezesha kula na kubakisha savings kila mwezi.
2) Au Je, kama maisha ya swali hapo juu ni ubinafsi, unadhani ni sahihi kupunguza gharama za maisha yako ili ukubali kurudi nyuma kidogo ili kubakiza savings, ziweze kuwasaidia jamaa zako wanaokutegemea? Kama kweli tunataka kutekeleza msemo wa kwamba kutoa ni moyo na si utajiri..?
3) Je, jambo hilo namba 2 hapo juu ni practical in real sense?
Nini maoni yako? Karibu ku-share mawazo ili tuelimishhane..