Unakumbuka nini miaka ya 90's kushuka chini?

Unakumbuka nini miaka ya 90's kushuka chini?

Pia nakumbuka Michael Jackson alikuja tz akasema dar inanukaaaaa!
Hiyo mbona ni juzi juzi tu mkuu kama ndo zamani yako basi tuache watu wazima tuendelee, hyo ni 94 au 95 alipokuja pale sinza shule mahalum akawapa bus tulikuwa wakubwa kabisa mkuu.
 
tapatalk_1470173411156.jpeg

Naomba niishie hapa tafadhali
 
Nakumbuka JKT Bulombola 1980 wenzetu wapo front line halafu tunawapongeza, nakumbuka Mugabe anapata uhuru tunaimba kumsifu (najuta), nakumbuka kupanga foleni kununua sukari kwa kutumia kadi ya meneja wa kijiji, kg. moja tu basi. Nakumbuka kulala guest kwenda kuchukua mshahara halafu unaambiwa muda umeisha inabidi ulale siku mbili na nauli umekopa kwa meneja wa kijiji. Nakumbuka Katambuga au Arusha to Moshi unachagua ile nzuri ya tyre za East Africa ambazo baadaye kiwanda kiliuzwa na Makonde, nakumbuka nipo Moro Sokoine amefariki baada ya wahujumu uchumi, mmoja wao alikuwa RPC wa Moro, watu wake walishangilia saana siku hiyo sababu Kantabula alikuwa amefukuzwa kazi na Nyerere mhanga namba moja. Nakumbuka kutumia nguo za kuzikia kusitiri watoto kama nepi. Hakukuwa na nepi nchini tulizifua vizuri na kuzipamba sababu shuleni enzi zetu tulisoma needlework hivyo tulijua jinsi ya kupendezesha vitu. Siwezi maliza yote hayo yanatosha.
 
Nakumbuka JKT Bulombola 1980 wenzetu wapo front line halafu tunawapongeza, nakumbuka Mugabe anapata uhuru tunaimba kumsifu (najuta), nakumbuka kupanga foleni kununua sukari kwa kutumia kadi ya meneja wa kijiji, kg. moja tu basi. Nakumbuka kulala guest kwenda kuchukua mshahara halafu unaambiwa muda umeisha inabidi ulale siku mbili na nauli umekopa kwa meneja wa kijiji. Nakumbuka Katambuga au Arusha to Moshi unachagua ile nzuri ya tyre za East Africa ambazo baadaye kiwanda kiliuzwa na Makonde, nakumbuka nipo Moro Sokoine amefariki baada ya wahujumu uchumi, mmoja wao alikuwa RPC wa Moro, watu wake walishangilia saana siku hiyo sababu Kantabula alikuwa amefukuzwa kazi na Nyerere mhanga namba moja. Nakumbuka kutumia nguo za kuzikia kusitiri watoto kama nepi. Hakukuwa na nepi nchini tulizifua vizuri na kuzipamba sababu shuleni enzi zetu tulisoma needlework hivyo tulijua jinsi ya kupendezesha vitu. Siwezi maliza yote hayo yanatosha.
Mkuu si ajabu ulivaa Pima juu chini kadilia nadhani " pekosi"
 
Mkuu si ajabu ulivaa Pima juu chini kadilia nadhani " pekosi"
Mimi flaire ambazo zilikuwa soro kipindi cha seventies. Hizo zilikuwa za mabitoz kumbuka kamanyola wakati huo unaliza watu, Moro jazz, Tabora Jazz na Vijana jazz. Zilikuwa nyingi nashangaa sasa wanasema wanamziki wasiimbe siasa wakati siasa tuliisoma kwenye music.
 
Nakumbuka nilikua na pair nyingi za viatu nyumbani lakini bado shuleni bado naenda peku peku
 
Nakumbuka mwaka 1985 tukiwa darasa la 6 Muhimbili Primary school na akina Dj Bonny love na Kibonde, alikuja Mwl. Nyerere shuleni kwa shuhuli ya mwenge. Tukaambiwa usipoimba wimbo wa taifa utakufa.. hiyo bidii ya kukariri huo wimbo sitakaa nisahau..
 
Nakumbuka kuangalia video za kina Shozniga na Bolo Yangi kwenye mabanda
 
Back
Top Bottom