Hatua na Taratibu za Kufungua Maombi ya kusimamia Mirathi Mahakamani

Apr 26, 2022
64
99
HATUA NA TARATIBU ZA KUFUNGUA MAOMBI YA KUSIMAMIA MIRATHI

Ni jambo lingine kwenda Mahakamani na ni jambo lingine kuzijua taratibu za Mahakama. Kuna namna ya kuwasiliana na Mahakama, ukikosea utaratibu au nyaraka utakosa haki yako, sio kwa sababu hauna haki ila kwa sababu hujui utaratibu (procedures) na documents.

Je, mtu akifa na ameacha mali, haijalishi kuna wosia au hakuna wosia, zipi ni hatua za kufata ukitaka kufungua shauri la mirathi?

Imeandaliwa na kuletwa kwako nami Zakaria Maseke - Advocate / Wakili
zakariamaseke@gmail.com
(0746575259 - WhatsApp).

Kwa kusoma makala hii utafahamu mambo yafuatayo:

(i) Jinsi ya kufungua shauri la mirathi Mahakamani kuomba kusimamia mirathi kukiwa na wosia na kukiwa hakuna wosia.
(ii) Nyaraka (documents) za kufungulia mirathi.
(iii) Vitu vya kuambatanisha.
(iv) Mahakama zinazosikiliza mirathi.
(v) Jinsi ya kupinga Mahakamani mtu asiteuliwe kusimamia mirathi.
(vi) Jinsi ya kumuondoa msimamizi wa mirathi ambaye tayari ameshateuliwa na Mahakama.
(vii) Jinsi ya kufanya kama umeondolewa miongoni mwa warithi halali, mfano mke au mtoto wa marehemu n.k.
(viii) Jinsi ya kufanya kama mali zako zimechanganywa kwenye mirathi ya marehemu.
(ix) Jinsi ya kufanya kama umechelewa kupinga mirathi mpaka kesi ya mirathi imeisha na jalada limefungwa n.k.

Kiujumla, utaratibu wa kufungua mirathi, inategemeana kama marehemu aliacha wosia au hakuacha wosia.* (Whether the deceased person died testate i.e left a will or died intestate i.e without leaving a will).

If the deceased person left a will appointing the name of a person to be an ‘EXECUTOR,’ you petition/apply for ‘GRANT OF PROBATE.’ (Namaanisha kwamba, kama marehemu aliacha wosia akiwa amekuchagua kusimamia na kugawa mirathi yake baada ya yeye kufariki, utaomba Mahakamani UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE)).

But if the deceased person died intestate or the will has been nullified by the Court, you will apply for ‘GRANT OF LETTERS OF ADMINISTRATION.’ (Lakini kama marehemu hakuacha wosia kabisa au aliacha wosia lakini wosia umebatilishwa na Mahakama, utaomba BARUA YA USIMAMIZI WA MIRATHI* (LETTERS OF ADMINISTRATION)).

Or there's a will, but it does not appoint the executor, or the executor(s) appointed by a will have renounced, or if no executor survives the testator, etc., you apply for ‘GRANT OF LETTERS OF ADMINISTRATION.’* (Wosia upo ila kuna mapungufu, mfano hautaji jina la msimamizi, au aliyechaguliwa kwenye wosia amekataa au hapatikani au ametangulia kufa kabla ya marehemu au kabla ya kuthibitishwa Mahakamani, au hana vigezo kisheria vya kuwa msimamizi wa mirathi (mfano bado ni mtoto au ana ugonjwa wa akili), n.k., utaomba BARUA YA USIMAMIZI WA MIRATHI ukiambatanisha na huo wosia (LETTERS OF ADMINISTRATION WITH THE WILL ANNEXED).

Soma kifungu cha 24 na 29 cha Sheria ya Uthibitisho wa Wosia na Usimamizi wa Mirathi. Kwa kiingereza, inaitwa the ‘Probate and Administration of Estates Act’, ambayo ili Kuepuka usumbufu, nitakuwa nairejea kwa kifupi kama PAEA kwenye andiko hili lote.

Swali: What if the deceased before death he wrote a will and later on acquired properties but forgot to include them in a will, e.t.c., how will you apply? (Kama kuna baadhi ya mali za marehemu hazijatajwa kwenye wosia utaombaje Mahakamani kufungua hiyo mirathi?) Tuendelee!

Labda unajiuliza, kwani kuna utofauti gani kati ya ‘ADMINISTRATOR’ na ‘EXECUTOR,’ au kati ya ‘UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE)’ na ‘BARUA ZA USIMAMIZI WA MIRATHI (LETTERS OF ADMINISTRATION?’

Kwa kifupi, Administrator na Executor wote ni wasimamizi wa mirathi, lakini ‘ADMINISTRATOR’ anateuliwa na Mahakama baada ya kupendekezwa na ukoo au familia, wakati ‘EXECUTOR’ ni yule aliyetajwa kwenye wosia na marehemu mwenyewe.

Vivyo hivyo, unaomba ‘UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE)’ au kuthibitishwa kutekeleza wosia kama kuna wosia (section 24(1) PAEA) na unaomba ‘BARUA ZA USIMAMIZI WA MIRATHI (LETTERS OF ADMINISTRATION)’ au kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi kama marehemu hakuacha wosia kabisa au wosia upo lakini una mapungufu, au aliyechaguliwa kwenye wosia amekataa, au hapatikani au hana vigezo, au ametangulia kufa kabla ya marehemu au kabla ya kuthibitishwa Mahakamani, n.k. Section 29 PAEA.

HATUA ZA KUFUNGUA MIRATHI:

1. FAMILY (CLAN) MEETING TO APPOINT THE ADMINISTRATOR OF ESTATES (KIKAO CHA FAMILIA AU UKOO KUMCHAGUA MSIMAMIZI WA MIRATHI).
Kama hakuna wosia, hatua ya kwanza ni kuchagua msimamizi wa mirathi. Ndugu wa marehemu wanatakiwa kupendekeza jina la mtu ambaye wanapenda asimamie mirathi.

(Ingawa sio lazima muitishe kikao cha familia/ukoo. Sheria haisemi kuwe na kikao, lakini kikao cha familia au ukoo ni muhimu kitawasaidia kubainisha mali na madeni ya marehemu, warithi halali na mambo mengine).

Kazi ya msimamizi wa mirathi ni kufungua Mahakamani shauri la maombi ya kusimamia mirathi, kubainisha, kukusanya na kuhifadhi mali za marehemu, kulipa madeni yaliyoachwa na marehemu na kugawa kilichobaki kwa warithi halali n.k.

2: APPLICATION/PETITION FOR GRANT OF PROBATE OR LETTERS OF ADMINISTRATION (KUPELEKA MAHAKAMANI MAOMBI YA KUOMBA KUTEULIWA AU KUTHIBITISHWA KUWA MSIMAMIZI WA MIRATHI):

Kama kuna wosia au kama hakuna wosia na familia imeshakaa kikao imependekeza msimamizi, basi mtu aliyetajwa kwenye wosia au aliyechaguliwa kwenye kikao cha wanafamilia (ukoo) atafungua maombi ya mirathi Mahakamani kuomba kuteuliwa au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi.

Labda kwanza tufahamu, ni MAHAKAMA ipi unaweza kupeleka kesi au kufungua maombi ya kusimamia MIRATHI? (Maana sio kila Mahakama unayoiona inasikiliza mirathi yoyote). Mirathi inasikilizwa kwenye Mahakama zifuatazo:

{i} Primary Court (Mahakama ya Mwanzo).
{ii} District Court (Mahakama ya Wilaya).
{iii} Court of District Delegate (Mahakama ya Hakimu Mteule).
{iv} Mahakama Kuu (High Court).

Sasa uende Mahakama ipi, itategemeana na sheria inayotumika au thamani ya mirathi yenyewe na mahali marehemu alipokuwa anaishi.

{i}: MAHAKAMA YA MWANZO:


Unaenda Mahakama ya Mwanzo kama mirathi inahusisha sheria za Kimila au za Kiislam (where the law applicable is customary or Islamic law), haijalishi AINA au THAMANI ya mirathi. Hata iwe million ngapi.

(Kwa hiyo kama wewe ni Mkristo, usiende Mahakama ya Mwanzo, utaenda Mahakama ya Mwanzo kama sheria inayotumika kwenye hiyo mirathi ni ya Kimila au Kiislam na sio vinginevyo).

SHERIA ZINAZOTUMIKA KWENYE MIRATHI MAHAKAMA YA MWANZO:

Sheria inayotumika kwenye mashauri ya mirathi katika Mahakama ya Mwanzo ni the Primary Courts (Administration of Estates) Rules G.N. No 49 of 1971 (Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama ya Mwanzo) Tangazo la Serikali Na. 49 la mwaka 1971 na MCA kifungu cha 18(1)(a)(i), 19(1)(c) & paragraph 1(1) ya Jedwali la tano la MCA (Fifth Schedule to the MCA).

DOCUMENT (NYARAKA) YA KUFUNGULIA MIRATHI KWA MAHAKAMA YA MWANZO:


Kwa Mahakama ya Mwanzo maombi ya kuteuliwa au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi hufanyika kupitia FOMU NAMBA I. Soma Kanuni ya 3 ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama ya Mwanzo) na Paragraph 2(a) & (b) ya Jedwali la tano la MCA.

NB: Hizi fomu zinazotumika kufungua mirathi unaweza kuziona nyuma ya sheria ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi kwa Mahakama ya Mwanzo, au kwenye Sheria inayotoa fomu zinazotumika katika mashauri ya Mahakama za Mwanzo (the Magistrates Court (Approved Forms for the Primary Court) GN. No. 943 za mwaka 2020.

Kwa Mahakama zingine, forms zao zipo kwenye Kanuni za Mirathi zinaitwa Probate Rules za mwaka 1963. (Sheria hizi zote zipo mtandaoni unaweza kupakua (download) na kusoma).

{ii} MAHAKAMA YA WILAYA (DISTRICT COURT):

Mahakama ya Wilaya inasikiliza mashauri ya mirathi midogo (small estate). Small estate ni mirathi ambayo haizidi shilling 100,000,000/= Kwa hiyo chochote chenye thamani ya kuanzia sifuri (0) mpaka million mia /100,000,000 ni small estate. Usiende Mahakama ya Mwanzo, hata kama mirathi ni shilling moja. Utaenda Mahakama ya Mwanzo kama tu, sheria inayotumika ni ya kimila au kiislam haijalishi ni million ngapi.

Lakini kama mirathi haina uhusiano na sheria ya Kimila au Kiislam, (na thamani yake haizidi million 100,000,000) nenda Mahakama ya Wilaya. Soma section 6(1) PAEA.

DOCUMENT (NYARAKA) INAYOTUMIKA KUFUNGUA MIRATHI MAHAKAMA YA WILAYA:

Kwa Mahakama ya Wilaya maombi ya kuteuliwa kuwa msimamizi au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi hufanyika kupitia FOMU NAMBA 76 ya Probate Rules. (Zaidi Kuhusu Mahakama ya Wilaya soma section 73-87 ya PAEA).

{iii} MAHAKAMA YA HAKIMU MTEULE WA WILAYA (COURT OF DISTRICT DELEGATE):

Kabla ya kuendelea, tufahamu kwanza who is a district delegate (Hakimu mteule wa wilaya ni nani?) Huyu zamani alikuwa ni hakimu mkazi (resident magistrate) ambaye amefanya kazi kufikia mwaka mmoja.

Iko hivi, kabla ya mwaka 2008, Jaji Mkuu (Chief Justice) alikua anawateua Mahakimu kadhaa kuwa Mahakimu wateule wa Wilaya. Kwa hiyo zamani sio Mahakimu wote walikua wateule wa wilaya (district delegates).

Mwaka 2008, Jaji Mkuu akatoa tangazo linalowateua au kuwatambua (recognizing) Mahakimu wote Wakazi (Resident Magistrates) kuwa Mahakimu wateule wa wilaya (district delegates).

Sasa kwa sababu Mahakama ya Wilaya pia inao Mahakimu Wakazi (Resident Magistrates), Mahakimu hao hao wanaokaa ndani ya Mahakama ya Wilaya pia ni wateule wa wilaya (district delegates). Kimsingi hakuna tofauti ya District delegate na Resident Magistrate ni mtu huyo huyo.

Sasa ni wakati gani Hakimu anakaa kama Hakimu mkazi na wakati gani anakaa kama mteule wa wilaya (district delegate)? What determines that this matter is before a District Delegate or a Resident Magistrate in District Court? INATEGEMEA NA WEWE UMEFUNGUA MIRATHI KWA KUTUMIA NJIA IPI (THE WAY YOU GO).

Ukiandika document (petition/maombi) yako in the DISTRICT COURT of… Hiyo ni small estate (mirathi midogo), lakini ukiandika in the COURT OF DISTRICT DELEGATE OF…itakua umeenda kwa District Delegate (Hakimu mteule wa wilaya). (Hata hivyo, hiyo petition haijalishi umeandikaje, bado utaipeleka pale pale Mahakama ya Wilaya na kwa hakimu yule yule (au mwingine kama yeye) anayesikiliza kesi zingine za small estate.

Kwamba, kama Hakimu Mkazi akiwa amekaa kuamua kwenye Mahakama ya Wilaya, ukafungua kesi ya mirathi inayohusu mirathi midogo/small estate), huyo Hakimu ataiamua hiyo kesi kama Hakimu Mkazi ambaye yupo Mahakama ya Wilaya, lakini huyo huyo anaweza kutumika pia kama mteule wa wilaya (district delegate) hapo hapo Mahakama ya Wilaya.

Na ikiletwa kesi ya mirathi ya DISTRICT DELEGATE, Hakimu Mkazi (resident magistrate) huyo huyo aliyepo Mahakama ya Wilaya, ataisikiliza awamu hii kama District delegate, hapo hapo Mahakama ya Wilaya. Kwa sababu hatuna majengo tofauti ya Mahakama ya district delegate ila majengo ni hayo hayo.

Sasa tuendelee na MAMLAKA ya hii mahakama (COURT OF DISTRICT DELEGATE/MAHAKAMA YA HAKIMU MTEULE WA WILAYA) kwenye mirathi.

Generally, thamani ya mirathi ya marehemu ikizidi 100,000,000 ndo unaenda Mahakama ya Hakimu mteule wa wilaya (District Delegate) kama hiyo mirathi haina ubishani (non contentious).

Iko hivi: Mamlaka ya hii Mahakama (District Delegate) inategemeana na vitu viwili.

(i) Kama mirathi inabishaniwa (ni contentious)
(ii) Kama mirathi haibishaniwi (ni non contentious).

CONTENTIOUS inatokea pale ambapo umefungua shauri la mirathi alafu anakuja mtu anaweka pingamizi (caveat).
Mfano, umefungua shauri la mirathi kuomba uteuliwe au uthibitishwe kusimamia mirathi, Mahakama ikatoa tangazo (general citation) kwamba kuna mirathi imefunguliwa Mahakamani, yeyote ambaye anadhani ana maslahi aje, mtu akaja akaweka pingamizi. Tayari hiyo mirathi itakuwa contentious, lakini NON CONTENTIOUS ni pale ambapo umeomba kufungua mirathi na hakuna mtu aliyejitokeza kupinga.

Sasa kama hakuna pingamizi au mabishano yoyote, mamlaka ya kifedha ya hii Mahakama (ya District Delegate) ni unlimited (hayana mipaka ya HELA). Pecuniary Jurisdiction of district delegate is unlimited if the matter is non contentious.

Lakini kama kuna ubishani (contention), ukomo wa hii Mahakama ya District Delegate ni shilling elfu kumi na tano (15,000)/= (If the matter is contentious the district delegate jurisdiction is limited only to 15,000/=).

Ikitokea kuna pingamizi, Hakimu ataangalia kama thamani ya hiyo mirathi ni 15,000 kushuka chini au inazidi 15,000? Kama inazidi 15,000 ina maana Mahakama ya District Delegate haitakua na mamlaka, hilo shauri itabidi lipelekwe Mahakama kuu Kuomba mwongozo. Kisha Mahakama Kuu itaamua ama kusikiliza yenyewe hiyo mirathi au iwaruhusu district delegate kuendelea.

Lakini kama hakuna pingamizi (no caveat lodged) tangu tangazo litoke mpaka muda wa tangazo kuisha, hiyo mirathi haina ubishani ni non contentious, na mteule wa wilaya (District Delegate) ataendelea nayo hata kama thamani yake ni billions. Soma section 5 ya PAEA.

In summary:
-Kama hakuna pingamizi, district delegate haitakua na ukomo wa mamlaka kwenye kiwango cha hela.
-Kama kuna pingamizi, mamlaka yake yanaishia mwisho 15,000. Weka full stop usiongeze neno.

{iv} MAHAKAMA KUU (HIGH COURT):

Mamlaka ya Mahakama Kuu ni unlimited (hayana mipaka). Mahakama Kuu inaweza kusikiliza kesi ya mirathi yoyote ile, iwe ya kimila, Kiislam, ya Mkristo na mtu yeyote. (Ila utaratibu wa kisheria unatakiwa kuanzia chini kabla ya kwenda Mahakama Kuu).

DOCUMENTS ZA KUFUNGULIA MIRATHI

KAMA KUNA WOSIA, maombi ya kuomba kusimamia mirathi (au kuthibitisha wosia) hufanyika kupitia fomu maalum iliyowekwa kisheria, FORM NUMBER 18. soma section 55(1) PAEA & Rule 33 ya Probate Rules. (NB: Wosia wa mdomo form ni no. 20, wosia uliopotea form no. 21, ukiwa na kopi/nakala ya wosia tu form no. 22). Rejea section 25 PAEA.

-Kama wosia una hitilafu maombi ya kuteuliwa kuwa msimamizi (letters of administration) hufanyika kupitia FORM NUMBER 26 (soma Section 55(1) PAEA & Rule 40 ya Probate Rules) au kama hakuna wosia kabisa FOMU NAMBA 27, soma section 56 PAEA & Rule 39.

VITU VYA KUAMBATANISHA UNAPOOMBA KUTHIBITISHWA AU KUTEULIWA KUWA MSIMAMIZI WA MIRATHI

Ni muhimu kuambatanisha vitu vifuatavyo (ambapo inategemeana na marehemu aliacha wosia au hakuacha wosia)

KAMA KUNA WOSIA UTAAMBATANISHA:

{i} WILL (WOSIA),
ikiwa marehemu aliacha wosia. Rule 33(1)(a) ya Probate Rules

{ii} UTHIBITISHO WA KIFO CHA MAREHEMU: Unaweza kuthibitisha kwa kuambatanisha vitu vifuatavyo;
-Cheti cha kifo (death certificate). As per Rule 33(1)(b) & 63.
-Hati ya kiapo (affidavit) ya ndugu wa marehemu au ya mtu aliyeshuhudia mazishi ya marehemu au
-Letter from the village or ward executive Secretary (barua kutoka ofisi ya mtendaji wa serikali ya kijiji au kata - kama hakuna cheti cha kifo).

{iii} kiapo cha msimamizi wa mirathi/executor’s oath, (aliyetajwa kwenye wosia) kwamba atasimamia mirathi kwa uaminifu. Section 66 of PAEA, rule 33(1)(d), form no. 47.

{iv} kiapo cha kuthibitisha makazi ya mwisho ya marehemu (an affidavit as to the deceased’s domicile at the time of his death. Rule 33(1)(c), form number 45.

{v} Verification of the petition (uthibitisho kutoka kwa mashahidi walioshuhudia huo wosia wakati unaandikwa) - Unajaza Form number 19, section 57 PAEA.

KAMA HAKUNA WOSIA UTAAMBATANISHA:

{i} MINUTES FROM THE CLAN/FAMILY MEETING (DONDOO AU MUHTASARI WA KIKAO CHA FAMILIA AU UKOO)
kilichomteua (kumpendekeza) muombaji kuwa msimamizi wa mirathi ikiwa marehemu hakuacha wosia au aliacha wosia lakini hakutaja jina la msimamizi, au aliyetajwa amekataa au amefariki n.k.

Zingatia: Sio lazima upeleke dondoo za kikao Mahakamani, hiki kitu hakipo kwenye sheria ni utaratibu tu wa mazoea (practice). Hata usipopeleka haina shida.

{ii} UTHIBITISHO WA KIFO CHA MAREHEMU: Unaweza kuthibitisha kwa kuambatanisha vitu vifuatavyo;
-Cheti cha kifo (death certificate). As per Rule 39(a) & 63
-Na vingine nilivyokwisha kutaja huko juu.

{iii} kiapo cha kuthibitisha makazi ya mwisho ya marehemu
(an affidavit as to the deceased’s domicile at the time of his death. Rule 39(b) & Rule 64, form number 45.

{iv} kiapo cha msimamizi wa mirathi/administrator’s oath (aliyependekezwa na ukoo) kwamba atasimamia mirathi kwa uaminifu (administrator's oath). Section 66, rule 39(c), form number 46.

{v} Dhamana ya mtu atakayemdhamini msimamizi wa mirathi (administration bond) kama kuna umuhimu wa kufanya hivyo, section 67, rule 39(d), 66 & 68 form no. 48 or 49 (au fomu namba 3 kama ni Mahakama ya Mwanzo - Rejea Kanuni ya 7(1) na (3) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi katika Mahakama za Mwanzo.

{vi} Hati ya hali ya fedha ya wadhamini wa msimamizi wa mirathi/administrator (certificate as to the financial position of the sureties). Rule 39(e) & 69, form no. 54.

{vii} Ridhaa ya warithi na ndugu au watu wenye maslahi katika mali za marehemu (consent of all heirs). Rule 39(f), 71 & 72, form 56

{viii} Kama ni mtu mmoja amefungua mirathi, weka na kiapo. Rule 39(g) na Rule 32.

{ix} Kiasi na aina ya mali za marehemu (amount and nature of assets)

{x) Na mengineyo.

Baada ya hapo utalipia gharama zinazotakiwa, na shauri lako litapewa namba na kuingizwa kwenye kitabu cha kufungulia mirathi

MUDA (UKOMO) WA KUFUNGUA MIRATHI:

Unatakiwa kufungua mirathi ndani ya muda gani? Je, kuna ukomo wa kufungua shauri la mirathi?

Kiufupi, hakuna muda maalumu wa kufungua shauri la mirathi, lakini kama utachelewa kwa muda wa MIAKA MITATU (3) tangu kifo cha marehemu, itakubidi utoe na maelezo au sababu za kuchelewa. Usipoambatanisha maelezo, maombi yako yatatupiliwa mbali.
Soma Rule 31 ya Probate Rules.

3: NOTICE OR GENERAL CITATION (TANGAZO AU WITO WA KUFIKA MAHAKAMANI).

Baada ya maombi ya kufungua mirathi kupokelewa, Mahakama itatoa tangazo kwamba kuna mtu amefungua mirathi pamoja na wito wa kufika Mahakamani kwa watu wote wanaohusika au wenye maslahi au uchungu na mirathi ya marehemu. Tangazo hutolewa kwenye mbao za matangazo za Mahakama au kwenye gazeti la serikali linalosomwa na watu wengi au sehemu za wazi zenye mikusanyiko ya watu. Section 61(1)(c) & (2) PAEA, Rule 75, form no. 58.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo CITATION hutolewa kupitia Fomu Namba II.

Lengo la matangazo ya mirathi ni kuwapa taarifa watu wote wanaohusika na mali za marehemu waweze kufika Mahakamani tarehe, siku na muda uliopangwa kufatilia maombi ya mirathi au ikiwa kuna mwenye dukuduku au pingamizi lolote aweze kuwasilisha kabla muombaji hajateuliwa au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi.

Mfano labda hamuelewani na anayetaka kusimamia mirathi, inawezekana amechaguliwa na familia lakini wewe humtaki, au hana sifa za kuwa msimamizi, au wosia uliopo ni feki (wa kughushi), au wosia uliandaliwa kwa udanganyifu, au wosia hautaji mtoto wa marehemu, au wosia hautaji mke wa marehemu n.k.

MUDA (UKOMO) WA WITO (CITATION)


-Zamani tangazo la mirathi lilidumu kwa muda wa siku 90. Kuna kesi Moja Jaji alisema, inatakiwa iwe walau si chini ya week nne (4), chini ya hapo ni “Vodafasta” na ni hatari kuharakisha (Kesi ya Beatrice Brighton Kamanga and Amanda Brighton Kamanga v. Ziada William Kamanga, 2020), hata hivyo muda umepunguzwa mpaka siku 21.

-Mahakama zinahamasishwa kutoa matangazo ya mirathi kwa muda mfupi kadri iwezekanavyo, cha muhimu ni watu wote wanaohusika wapate taarifa.

4: OBJECTION/ENTERING CAVEAT (KUWASILISHA PINGAMIZI KAMA LIPO).


Kama una pingamizi lolote utawasilisha kupitia form no. 62 au hata kwa mdomo. Section 58(1), Rule 82(1).

Pingamizi linadumu miezi minne Section 58(5) PAEA. Pingamizi ni kama onyo, linaisimamisha Mahakama isiendelee kufanya chochote au isiendelee kusikiliza maombi ya kufungua mirathi mpaka itakapomaliza kusikiliza pingamizi.

Kukiwa na pingamizi hiyo ndo inaitwa CONTENTIOUS MATTER na kama hakuna pingamizi inaitwa NON CONTENTIOUS MATTER.

-Mahakama ya Mwanzo pia ina mamlaka ya kupokea na kusikiliza pingamizi. Ambapo ukiwa na pingamizi utaenda kama ni Mahakama ya Mwanzo, utajieleza wewe ni nani, utawaambia umeona tangazo la mirathi kwa hiyo unapinga alafu watakusikiliza, watatoa maamuzi.

5: CITATION TO CAVEATOR

Kama kuna pingamizi, yule mleta maombi ya mirathi anatakiwa kuiomba Mahakama itoe wito (citation) kumuita aliyeweka pingamizi (caveator) afike Mahakamani. Maombi yanatakiwa kufanyika ndani ya siku 30. Section 59(2) PAEA, Rule 75, rule 82(2), form number 63.

Ukishindwa kuiomba Mahakama imuite caveator (muweka pingamizi), Mahakama itakukumbusha kwa kukupa notice ya kukutaka umuite caveator ndani ya siku zingine 21. Notice hiyo inatolewa kupitia form no. 63A. Ukishindwa tena kufanya application ndani ya hizo siku 21 za nyongeza, basi Mahakama itachukulia kwamba umeondoa mwenyewe Mahakamani maombi yako ya kuomba kusimamia mirathi. Rule 82(2A) & (2B). Ukitaka kuendelea na maombi ya mirathi yako utaomba yarudishwe (restoration). Soma Rule 82(2D).

6: ISSUANCE OF CITATION

Mleta maombi ya mirathi ukimaliza kuiomba Mahakama itoe wito (citation) kumuita aliyeweka pingamizi (caveator) aje Mahakamani, Msajili wa Mahakama atatoa wito (citation) kupitia form number 64 kumuita aliyeweka pingamizi aje atoe maelezo ndani ya siku 30, kama anakubali au anapinga maombi yako ya mirathi. Na kama anapinga kwa nini anapinga uthibitisho wa wosia au kutolewa kwa barua za usimamizi wa mirathi kwa muombaji. Rule 82(3).

Pamoja na wito huo, muweka pingamizi utapewa na documents (nyaraka) zote za mwenendo wa shauri la mirathi Mahakamani, ili uone kama kila kitu kiko sawa, mali zilizotajwa ndo zenyewe au kuna zingine sio za marehemu, n.k., ili ujiridhishe kama dukuduku au wasiwasi wako ni kweli au la!

7: APPEARANCE BY CAVEATOR

Aliyeweka pingamizi baada ya kupokea wito (citation) atafika Mahakamani na kujibu kupitia form number 65, akiambatanisha na affidavit au kiapo cha maelezo ya maslahi aliyo nayo na sababu za kupinga. Mfano labda umeona mali zako zimechanganywa kwenye mirathi ya marehemu, au umeondolewa kwenye orodha ya warithi n.k. Rule 82(4). Nakala itapelekwa kwa mfungua shauri la mirathi. Rule 82(5).

Baada ya mtu kuweka pingamizi, maombi ya kufungua mirathi hugeuka kuwa kama KESI YA MADAI, muombaji anakuwa Mlalamikaji (Plaintiff) na Caveator anakuwa kama Defendant (Mshtakiwa). Section 52(b) PAEA, Rule 82(6).

8: HEARING & RULING (KUSIKILIZA PINGAMIZI NA KUTOA UAMUZI MDOGO). Pingamizi litasikilizwa na kutolewa uamuzi, ambapo Mahakama inaweza kukubali au kukataa kukuteua kuwa msimamizi wa mirathi au kuthibitisha wosia wako.

Kama ikitokea caveat au pingamizi lako limetupiliwa mbali na Mahakama, (yaani umeshindwa kesi) kata rufaa Mahakama ya Juu.

9: KUSIKILIZA MAOMBI NA KUTEUA/KUTHIBITISHA MSIMAMIZI WA MIRATHI.

Kama hakuna pingamizi au pingamizi limekataliwa, Mahakama itaendelea mbele kusikiliza maombi ya mirathi na kuthibitisha wosia au kumteua msimamizi wa mirathi na kumkabidhi barua ya kuhalalisha kugawa mirathi.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo, hati ya kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi hutolewa kupitia form no. IV.

NB: Hata kama hukuwepo wakati mtu anafungua shauri la mirathi kuomba kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi (labda ulisafiri au hukujua n.k), ukaja ukakuta ameshateuliwa na Mahakama, hapo huwezi tena kuweka pingamizi (caveat) ila unaweza kuomba kutenguliwa kwa msimamizi wa mirathi (revocation) kama unaona haeleweki au hafanyi kazi yake ipasavyo.

Jinsi ya kuomba revocation (kutenguliwa) kwa msimamizi wa mirathi kuna form maalum za kujaza zinaitwa chamber summons na affidavit (kiapo). Soma Rule 29 & section 49 PAEA. Kwa Mahakama ya Mwanzo utajaza fomu ya mirathi namba 7.

10: TO FILE INVENTORIES (KUWASILISHA ORODHA YA MALI)

Msimamizi wa mirathi ukishateuliwa na Mahakama, unatakiwa ndani ya miezi sita, kuwasilisha Mahakamani orodha ya mali za marehemu unazotarajia kugawa, na aina zake mfano ni mali isiyohamishika au inayohamishika, eneo ilipo, thamani yake, madeni, gharama nyinginezo kama vile gharama za mazishi, matibabu, gharama za usimamizi n.k. Section 107(1) PAEA, Rule 106, form number 80.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo orodha ya mali huwasilishwa kupitia fomu namba V ndani ya miezi minne. Rejea Kanuni ya 10(1) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi katika Mahakama za Mwanzo.

11: DIVISION OF ASSETS TO HEIRS (KUGAWA MALI KWA WARITHI).

Ukishalipa madeni na gharama za msiba, unagawanya kilichobaki kwa warithi halali. Section 110 PAEA.

12: TO FILE STATEMENTS OF ACCOUNTS (KUTOA HESABU YA MIRATHI)

-Baada ya kugawa mali, msimamizi wa mirathi anatakiwa ndani ya mwaka mmoja (miezi sita tangu upeleke orodha ya mali na madeni), kurudisha Mahakamani hesabu kamili au taarifa ya ugawaji mali za marehemu, namna alivyotekeleza majukumu yake tangu alipoteuliwa na alivyogawa mirathi kwa warithi ili Mahakama ifunge jalada (kesi). Section 107(1) PAEA, Rule 107, form number 81.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo hesabu ya mirathi huwasilishwa kupitia fomu namba VI ndani ya miezi minne. Rejea Kanuni ya 10(1) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama za Mwanzo.

(Ni kosa kwa msimamizi kutoa hesabu au taarifa za uongo na kama akisababisha hasara yoyote anatakiwa alipe).

13: CLOSING OF PROBATE PROCEEDINGS (KUFUNGWA KWA SHAURI LA MIRATHI)

Msimamizi wa mirathi akiiambia Mahakama amemaliza kazi yake, baada ya Mahakama kuridhika kwamba msimamizi wa mirathi ametekeleza wajibu wake ipasavyo, shauri la mirathi litafungwa.

14: RE OPENING OF PROBATE PROCEEDINGS (KUFUNGULIWA KWA MIRATHI ILIYOFUNGWA):
Je, mirathi iliyofungwa inawezekana kufunguliwa tena? Sio rahisi ila inawezekana.

Mirathi iliyofungwa inaweza kufunguliwa tena kama mtagundua kuna mali (mpya) zingine za marehemu mliziacha.

Mnapeleka maombi Mahakamani, Mahakama itateua msimamizi yule yule wa awali au mwingine, ambapo hiyo mali mpya nayo ikishagawiwa mirathi itafungwa tena rasmi.

Zingatia: Mahakama haziruhusiwi kujihusisha na ugawaji wa mirathi (hiyo ni kazi ya Msimamizi wa mirathi). Pia kama hujaridhika na ugawaji wa mirathi, msimamizi ameshamaliza kazi yake na jalada limeshafungwa, labda na wewe ni mrithi ila walikusahau, njia pekee ni kumshtaki aliyekua msimamizi wa mirathi kwa kufungua kesi ya kawaida ya madai (sio ya mirathi tena)

Hizo ndo hatua za kufungua shauri la mirathi Mahakamani Nchini Tanzania. Nimetumia muda mrefu huu kuelimisha jamii bure kuhusu mirathi, kama mojawapo ya wajibu wangu kama mwanasheria. Mungu akubariki ndugu msomaji.

-----MWISHO----

Natoa angalizo, wale wazee wa kukopi machapisho ya watu na kuweka majina yenu. Ni kosa kisheria. Hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote atakayejimilikisha andiko hili. Unaruhusiwa tu kusambaza lakini usibadili yaliyomo. Ni heri uanze kuandika ya kwako mpya.


Disclaimer: Lengo la hii makala ni kutoa elimu kwa jamii. Huu sio ushauri wa kisheria kwa mtu yeyote. Kama unahitaji ushauri wa kisheria wasiliana na Mawakili Wasomi.

Mimi mwandishi wa makala hii naitwa Zakaria Maseke - Advocate/ Wakili.
zakariamaseke@gmail.com
(0746575259 - WhatsApp).
 
Ni jambo jingine kwenda Mahakamani na ni jambo jingine kuzijua taratibu za Mahakama. Kuna namna ya kuongea na Mahakama, ukikosea utapoteza haki zako, sio kwa sababu hauna haki ila kwa sababu hujui utaratibu (procedures).

Je, mtu akifa na ameacha mali, haijalishi kuna wosia au hakuna wosia, zipi ni hatua za kufuata ukitaka kufungua shauri la maombi ya mirathi?

(Imeandaliwa na kuletwa kwako na Zakaria - Lawyer by profession).

Kuna taratibu za kufungua mirathi, ambapo, inategemeana kama marehemu aliacha wosia au hakuacha wosia. (Whether the deceased person died testate i.e left a will or died intestate i.e without leaving will).

If the deceased person left a will appointing the name of person to be an ‘EXECUTOR,’ you petition/apply for ‘GRANT OF PROBATE,’ but if the deceased person died intestate, or the executor appointed by a will have renounced, or if no executor survives the testator etc, you apply for ‘GRANT OF LETTERS OF ADMINISTRATION.’ And a person so appointed is called Administrator (of estates).

-Namaanisha kwamba, kama marehemu aliacha wosia akiwa amekuchagua kusimamia na kugawa mirathi yake baada ya yeye kufariki, utaomba Mahakamani UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE).

-Kama marehemu hakuacha wosia au aliyechaguliwa kwenye wosia amekataa au ametangulia kufa kabla ya marehemu, au hana vigezo kisheria n.k., utaomba Mahakamani BARUA ya USIMAMIZI WA MIRATHI (LETTERS OF ADMINISTRATION)

Soma kifungu cha 24 na 29 cha Sheria ya Uthibitisho wa Wosia na Usimamizi wa Mirathi. Kwa kiingereza, inaitwa the ‘Probate and Administration of Estates Act’, ambayo ili Kuepuka usumbufu, nitakuwa nairejea kwa kifupi kama PAEA kwenye andiko hili lote.

Labda unajiuliza, kwani kuna utofauti gani kati ya ‘ADMINISTRATOR’ na ‘EXECUTOR,’ na kati ya ‘UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE)’ na ‘BARUA ZA USIMAMIZI WA MIRATHI (LETTERS OF ADMINISTRATION?’

Kwa kifupi sana, ‘ADMINISTRATOR’ anateuliwa na Mahakama baada ya kupendekezwa na ukoo au familia, wakati ‘EXECUTOR’ ni yule aliyetajwa kwenye wosia na marehemu mwenyewe.

Vivyo hivyo, unaomba ‘UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE)’ au kuthibishwa kutekeleza wosia kama kuna wosia (section 24(1) PAEA) na unaomba ‘BARUA YA USIMAMIZI WA MIRATHI (LETTERS OF ADMINISTRATION)’ au kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi kama marehemu hakuacha kabisa wosia au wosia upo lakini una mapungufu, au aliyechaguliwa kwenye wosia amekataa, au hana vigezo, au ametangulia kufa kabla ya marehemu au kabla ya kuthibitishwa Mahakamani, n.k. Section 29 PAEA.

HATUA ZA KUFUNGUA MIRATHI:

1. FAMILY (CLAN) MEETING TO APPOINT THE ADMINISTRATOR OF ESTATES (KIKAO CHA FAMILIA AU UKOO KUMCHAGUA MSIMAMIZI WA MIRATHI). Kama, hakuna wosia, hatua ya kwanza ni kuchagua msimamizi wa mirathi. Ndugu wa marehemu wanatakiwa kupendekeza jina la mtu ambaye wanapenda asimamie mirathi.

Kazi ya msimamizi wa mirathi ni kufungua Mahakamani shauri la maombi ya kusimamia mirathi, kubainisha, kukusanya na kulipa madeni yaliyoachwa na marehemu, kugawa mali za marehemu kwa warithi halali n.k.

2: APPLICATION/PETITION FOR GRANT OF PROBATE OR LETTERS OF ADMINISTRATION (KUPELEKA MAHAKAMANI MAOMBI YA KUOMBA KUTEULIWA AU KUTHIBITISHWA KUWA MSIMAMIZI WA MIRATHI)

Mtu aliyetajwa kwenye wosia au aliyechaguliwa kwenye kikao cha wanafamilia (ukoo) atafungua maombi ya mirathi Mahakamani kuomba kuteuliwa au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi.

Sasa hapa inategemea na Mahakama unayoenda kufungua Mirathi.

Labda kwanza tufahamu, ni MAHAKAMA IPI UNAWEZA KUPELEKA KESI YA MIRATHI? (Maana, sio kila Mahakama unayoiona inasikiliza mirathi yoyote).

Inategemeana na sheria inayotumika au thamani ya mirathi yenyewe na marehemu alipokuwa anaishi. Mfano, kama mirathi inahusisha sheria za Kimila au Kiislam (where the law applicable is customary or Islamic law), unatakiwa kwenda Mahakama ya Mwanzo (haijalishi aina na thamani ya mirathi hiyo).

Zingatia: Mahakama ya Mwanzo haina mamlaka ya kusikiliza mashauri ya mirathi ya Wakristo. Kwa nini? Kwa sababu kwanza, mamlaka ya Mahakama ya Mwanzo yanaishia kwenye mirathi inayoendeshwa kwa kutumia sheria za Kimila au Kiislam, (yaani mirathi ambayo marehemu wakati wa uhai wake aliishi kwa kufuata taratibu za kimila au taratibu za dini ya Kiislamu). Soma kifungu cha 18(1)(a)(i) cha Sheria ya Mahakama za Mahakimu (the Magistrates’ Courts Act), unaweza kuiita kwa kifupi kama ‘MCA.’

Pili, sheria inayotumika kwa Wakristo ni Indian Succession Act, ya mwaka 1865, ambayo sio miongoni mwa sheria zinazotumika Mahakama ya Mwanzo.

Sheria inayotumika kwenye mashauri ya mirathi katika Mahakama ya Mwanzo ni the Primary Courts (Administration of Estates) Rules G.N. No 49 of 1971 (Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama ya Mwanzo) Tangazo la Serikali Na. 49 la mwaka 1971 na MCA kifungu cha 18(1)(a)(i), 19(1)(c) & paragraph 1(1) ya Jedwali la tano la MCA (Fifth Schedule to the MCA).

Kwa Mahakama ya Mwanzo maombi ya kuteuliwa kuwa msimamizi au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi hufanyika kupitia FOMU NAMBA I. Soma Kanuni ya 3 ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama ya Mwanzo) na Paragraph 2(a) & (b) ya Jedwali la tano la MCA.

Kumbuka: Fomu hizi zote unaweza kuziona nyuma ya sheria ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama ya Mwanzo, au kwenye Sheria inayotoa fomu zinazotumika katika mashauri ya Mahakama za Mwanzo (the Magistrates Court (Approved Forms for the Primary Court) GN. NO. 943 za mwaka 2020.

Kwa Mahakama zingine, forms zao zipo kwenye Kanuni za Mirathi zinaitwa Probate Rules za mwaka 1963. Sheria hizi zote zipo mtandaoni unaweza kujisomea.

Tuendelee sasa. Kama mirathi ya marehemu haizidi million mia moja (100,000,000) utaenda Mahakama ya Wilaya. Section 6(1) PAEA. (Zingatia, kama ina uhusiano na sheria ya Kimila au Kiislam utarudi Mahakama ya Mwanzo haijalishi ni million ngapi. Ni kana kwamba Mahakama ya Wilaya wanaenda Wakristo tu ambao mirathi yao haizidi 100,000,000.
Zaidi Kuhusu Mahakama ya Wilaya soma section 73-87 ya PAEA.

Kwa upande wa Mahakama zingine (ukiacha Mahakama ya Mwanzo) kama kuna wosia;

Maombi ya kuthibitisha wosia hufanyika kupitia fomu maalum iliyowekwa kisheria, FORM NUMBER 18. soma section 55(1) PAEA & Rule 33 ya Probate Rules. (NB: Wosia wa mdomo form ni no. 20, wosia uliopotea form no. 21, ukiwa na kopi/nakala ya wosia tu form no. 22). Rejea section 25 PAEA.

-Kama wosia una hitilafu maombi ya kuteuliwa kuwa msimamizi (letters of administration) hufanyika kupitia FORM NUMBER 26 (soma Section 55(1) PAEA & Rule 40 ya Probate Rules) au kama hakuna wosia kabisa FOMU NAMBA 27, soma section 56 PAEA & Rule 39.

VITU VYA KUAMBATANISHA UNAPOOOMBA KUTHIBITISHWA AU KUTEULIWA KUWA MSIMAMIZI WA MIRATHI

Ni muhimu kuambatanisha vitu vifuatavyo (ambapo inategemeana na marehemu aliacha wosia au hakuacha wosia)

KAMA KUNA WOSIA UTAAMBATANISHA:

{i} WILL (WOSIA), ikiwa marehemu aliacha wosia. Rule 33(1)(a) ya Probate Rules

{ii} UTHIBITISHO WA KIFO CHA MAREHEMU: Unaweza kuthibitisha kwa kuambatanisha vitu vifuatavyo;
-Cheti cha kifo (death certificate). As per Rule 33(1)(b) & 63.
-Hati ya kiapo (affidavit) ya ndugu wa marehemu au ya mtu aliyeshuhudia mazishi ya marehemu au
-Letter from the village or ward executive Secretary (barua kutoka ofisi ya mtendaji wa serikali ya kijiji au kata - kama hakuna cheti cha kifo).

{iii} kiapo cha msimamizi wa mirathi/executor’s oath, (aliyetajwa kwenye wosia) kwamba atasimamia mirathi kwa uaminifu. Section 66 of PAEA, rule 33(1)(d), form no. 47.

{iv} kiapo cha kuthibitisha makazi ya mwisho ya marehemu (an affidavit as to the deceased’s domicile at the time of his death. Rule 33(1)(c), form number 45.

{v} Verification of the petition (uthibitisho kwamba ulishuhudia wosia wakati unaandikwa) - Form number 19, section 57 PAEA.

KAMA HAKUNA WOSIA UTAAMBATANISHA:

{i} MINUTES FROM THE CLAN/FAMILY MEETING (DONDOO AU MUHTASARI WA KIKAO CHA FAMILIA AU UKOO) kilichomteua (kumpendekeza) muombaji kuwa msimamizi wa mirathi ikiwa marehemu hakuacha wosia au aliacha wosia lakini hakutaja jina la msimamizi, au aliyetajwa amekataa au amefariki n.k.

NB: Sio lazima mpeleke dondoo za kikao Mahakamani, hiki kitu hakipo kwenye sheria ni utaratibu tu wa Mahakama. Hata usipopeleka haina shida.

{ii} UTHIBITISHO WA KIFO CHA MAREHEMU: Unaweza kuthibitisha kwa kuambatanisha vitu vifuatavyo;
-Cheti cha kifo (death certificate). As per Rule 39(a) & 63
-Na vingine nilivyokwisha kutaja huko juu.

{iii} kiapo cha kuthibitisha makazi ya mwisho ya marehemu (an affidavit as to the deceased’s domicile at the time of his death. Rule 39(b) & Rule 64, form number 45.

{iv} kiapo cha msimamizi wa mirathi/administrator’s oath (aliyependekezwa na ukoo) kwamba atasimamia mirathi kwa uaminifu (administrator's oath). Section 66, rule 39(c), form number 46.

{v} Dhamana ya mtu atakayemdhamini
msimamizi wa mirathi (administration bond) section 67, rule 39(d), 66 & 68 form no. 48 or 49 (au fomu namba 3 kama ni Mahakama ya Mwanzo - Rejea Kanuni ya 7(1) na (3) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi katika Mahakama za Mwanzo.

{vi} Hati ya hali ya fedha ya wadhamini wa
msimamizi wa mirathi/administrator (certificate as to the financial position of the sureties). Rule 39(e) & 69, form no. 54.

{vii} Ridhaa ya warithi na ndugu au watu wenye maslahi katika mali za marehemu (consent of all heirs). Rule 39(f), 71 & 72, form 56

{viii} Kama ni mtu mmoja amefungua mirathi, weka na kiapo. Rule 39(g) na Rule 32.

{ix} Mali za marehemu (amount and nature of assets)

{x) Na mengineyo.

Baada ya hapo utalipia gharama zinazotakiwa, na shauri lako litapewa namba na kuingizwa kwenye kitabu cha kufungulia mirathi

MUDA (UKOMO) WA KUFUNGUA MIRATHI:

Unatakiwa kufungua mirathi ndani ya muda gani? Je, kuna ukomo wa kufungua shauri la mirathi? Kiufupi, hakuna muda maalumu wa kufungua shauri la mirathi, lakini kama utachelewa kwa muda wa MIAKA MITATU (3) tangu kifo cha marehemu, itakubidi utoe na maelezo au sababu za kuchelewa. Usipoambatanisha maelezo, maombi yako yatatupiliwa mbali.
Soma Rule 31 ya Probate Rules.

3: NOTICE OR GENERAL CITATION (TANGAZO AU WITO WA KUFIKA MAHAKAMANI).

Baada ya maombi kupokelewa, Mahakama itatoa tangazo kwamba kuna mtu amefungua mirathi pamoja na wito wa kufika Mahakamani kwa watu wote wanaohusika au wenye maslahi na mirathi ya marehemu. Tangazo hutolewa kwenye mbao za matangazo za Mahakama au kwenye gazeti la serikali linalosomwa na watu wengi au sehemu za wazi zenye mikusanyiko ya watu.

Lengo ni kuwapa taarifa watu wote wanaohusika na mali za marehemu waweze kufika Mahakamani tarehe, siku na muda uliopangwa, kufatilia maombi ya mirathi na ikiwa kuna mwenye pingamizi lolote aweze kuwasilisha kabla muombaji hajateuliwa au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi. Section 61(1)(c) & (2) PAEA, Rule 75, form no. 1 & no. 58.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo CITATION hutolewa kupitia Fomu Namba II.

MUDA (UKOMO) WA WITO (CITATION)

-Zamani tangazo la mirathi lilidumu kwa muda wa siku 90. Kuna kesi Moja Jaji alisema, inatakiwa iwe walau si chini ya week nne (4), chini ya hapo ni “Vodafasta” na ni hatari kuharakisha (Beatrice Brighton Kamanga and Amanda Brighton Kamanga v. Ziada William Kamanga, 2020), hata hivyo muda umepunguzwa mpaka siku 21.

-Mahakama zinahamasishwa kutoa matangazo ya mirathi kwa muda mfupi kadri iwezekanavyo, cha muhimu ni watu wote wanaohusika wapate taarifa.

4: OBJECTION/ENTERING CAVEAT (KUWASILISHA PINGAMIZI KAMA LIPO).

Kama una pingamizi lolote utawasilisha kupitia form form no. 62 au hata kwa mdomo. Section 58(1), Rule 82(1).

Pingamizi linadumu miezi minne Section 58(5) PAEA. Pingamizi linaisimamisha Mahakama isiendelee kusikiliza maombi ya mirathi kwanza mpaka itakapomaliza kusikiliza pingamizi.

Kukiwa na pingamizi hiyo ndo inaitwa CONTENTIOUS MATTER na kama hakuna pingamizi inaitwa NON CONTENTIOUS MATTER.

-Mahakama ya Mwanzo pia ina mamlaka ya kupokea na kusikiliza pingamizi.

5: CITATION TO CAVEATOR

Mfungua maombi ya mirathi ataiomba Mahakama itoe wito (citation) kumuita aliyeweka pingamizi (caveator) afike Mahakamani. Maombi yanatakiwa kufanyika ndani ya siku 30. Section 59(2) PAEA, Rule 75, rule 82(2), form number 63.

Ukishindwa kuiomba Mahakama imuite caveator, Mahakama itakukumbusha kwa kukupa notice ya kukutaka umuite caveator ndani ya siku zingine 21. Notice hiyo inatolewa kupitia form no. 63A. Ukishindwa tena kufanya application ndani ya hizo siku 21 za nyongeza, basi Mahakama itachukulia kwamba umeondoa mwenyewe Mahakamani maombi yako ya kuomba kusimamia mirathi. Rule 82(2A) & (2B). Ukitaka kuendelea utaomba restoration. Rule 82(2D).

6: ISSUANCE OF A CITATION

Kisha Msajili wa Mahakama atatoa wito kupitia form number 64 kumuita aliyeweka pingamizi atoe maelezo ndani ya siku 30, kama anakubali au anapinga. Na kama anapinga kwa nini anapinga uthibitisho wa wosia au kutolewa kwa barua za usimamizi wa mirathi kwa muombaji. Rule 82(3).

7: APPEARANCE BY CAVEATOR

Aliyeweka pingamizi baada ya kupokea wito (citation) atafika Mahakamani na kujibu kupitia form number 65, akiambatanisha na kiapo cha maelezo ya maslahi aliyo nayo na sababu za kupinga. Rule 82(4). Nakala itapelekwa kwa mfungua shauri la mirathi. Rule 82(5).

Baada ya pingamizi, maombi ya kufungua mirathi hugeuka kuwa kama KESI YA MADAI, muombaji anakuwa Mlalamikaji (Plaintiff) na Caveator anakuwa kama Defendant (Mtuhumiwa). Section 52(b) PAEA, Rule 82(6).

8: HEARING & RULING (KUSIKILIZA PINGAMIZI NA KUTOA UAMUZI MDOGO). Pingamizi litasikilizwa na kutolewa uamuzi, ambapo Mahakama inaweza kukubali au kukataa kuteua msimamizi wa mirathi au kuthibitisha wosia.

9: KUSIKILIZA MAOMBI NA
KUTEUA/KUTHIBITISHA MSIMAMIZI WA MIRATHI.

Kama hakuna pingamizi au pingamizi limekataliwa, Mahakama itaendelea mbele kusikiliza maombi ya mirathi na kuthibitisha wosia au kumteua msimamizi wa mirathi na kumkabidhi barua ya kuhalalisha kugawa mirathi.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo, hati ya kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi hutolewa kupitia fomu namba 4.

NB: Unaweza kuomba kutenguliwa kwa msimamizi wa mirathi, kama unaona haeleweki au hafanyi kazi yake ipasavyo.

10: TO FILE INVENTORIES (KUWASILISHA ORODHA YA MALI)

Msimamizi wa mirathi anatakiwa ndani ya miezi sita, kuwasilisha Mahakamani orodha ya mali za marehemu, na aina zake mfano ni mali isiyohamishika au inayohamishika, eneo ilipo, thamani yake, madeni, gharama nyinginezo kama vile gharama za mazishi, matibabu, gharama za usimamizi n.k. Section 107(1) PAEA, Rule 106, form number 80.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo orodha ya mali huwasilishwa kupitia fomu namba V ndani ya miezi minne. Rejea Kanuni ya 10(1) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi katika Mahakama za Mwanzo.

11: DIVISION OF ASSETS TO HEIRS (KUGAWA MALI KWA WARITHI).

Cha kwanza unalipa madeni na gharama za msiba, alafu unagawanya kilichobaki kwa warithi.

12: TO FILE STATEMENTS OF ACCOUNTS (KUTOA HESABU YA MIRATHI)

-Baada ya kugawa mali, msimamizi wa mirathi anatakiwa ndani ya mwaka mmoja, kurudisha Mahakamani hesabu kamili au taarifa ya ugawaji mali za marehemu, namna alivyotekeleza majukumu yake tangu alipoteuliwa na alivyogawa (atakavyogawa) mirathi kwa warithi ILI MAHAKAMA IFUNGE JALADA (KESI). Section 107(1) PAEA, Rule 107, form number 81.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo hesabu ya mirathi huwasilishwa kupitia fomu namba VI ndani ya miezi minne. Rejea Kanuni ya 10(1) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama za Mwanzo.

(Ni kosa kwa msimamizi kutoa hesabu au taarifa za uongo na kama akisababisha hasara yoyote anatakiwa alipe).

14: CLOSING OF A CASE FILE (KUFUNGWA KWA SHAURI LA MIRATHI)
Baada ya Mahakama kuridhika kwamba msimamizi wa mirathi ametekeleza wajibu wake ipasavyo, shauri la mirathi litafungwa.

Na huo ndio mwisho.

Zingatia: Mahakama haziruhusiwi kujihusisha na ugawaji wa mirathi (hiyo ni kazi ya Msimamizi wa mirathi).

Imeandaliwa na kuletwa kwako nami Zakaria Wakili Mtarajiwa (0754575246 WhatsApp).

Hobby: Exceptional legal research, writing, organizational and analytical skills.
Congole msomi unaitendea haki field
 
Ni jambo jingine kwenda Mahakamani na ni jambo jingine kuzijua taratibu za Mahakama. Kuna namna ya kuongea na Mahakama, ukikosea utapoteza haki zako, sio kwa sababu hauna haki ila kwa sababu hujui utaratibu (procedures).

Je, mtu akifa na ameacha mali, haijalishi kuna wosia au hakuna wosia, zipi ni hatua za kufuata ukitaka kufungua shauri la maombi ya mirathi?

(Imeandaliwa na kuletwa kwako na Zakaria - Lawyer by profession).

Kuna taratibu za kufungua mirathi, ambapo, inategemeana kama marehemu aliacha wosia au hakuacha wosia. (Whether the deceased person died testate i.e left a will or died intestate i.e without leaving will).

If the deceased person left a will appointing the name of person to be an ‘EXECUTOR,’ you petition/apply for ‘GRANT OF PROBATE,’ but if the deceased person died intestate, or the executor appointed by a will have renounced, or if no executor survives the testator etc, you apply for ‘GRANT OF LETTERS OF ADMINISTRATION.’ And a person so appointed is called Administrator (of estates).

-Namaanisha kwamba, kama marehemu aliacha wosia akiwa amekuchagua kusimamia na kugawa mirathi yake baada ya yeye kufariki, utaomba Mahakamani UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE).

-Kama marehemu hakuacha wosia au aliyechaguliwa kwenye wosia amekataa au ametangulia kufa kabla ya marehemu, au hana vigezo kisheria n.k., utaomba Mahakamani BARUA ya USIMAMIZI WA MIRATHI (LETTERS OF ADMINISTRATION)

Soma kifungu cha 24 na 29 cha Sheria ya Uthibitisho wa Wosia na Usimamizi wa Mirathi. Kwa kiingereza, inaitwa the ‘Probate and Administration of Estates Act’, ambayo ili Kuepuka usumbufu, nitakuwa nairejea kwa kifupi kama PAEA kwenye andiko hili lote.

Labda unajiuliza, kwani kuna utofauti gani kati ya ‘ADMINISTRATOR’ na ‘EXECUTOR,’ na kati ya ‘UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE)’ na ‘BARUA ZA USIMAMIZI WA MIRATHI (LETTERS OF ADMINISTRATION?’

Kwa kifupi sana, ‘ADMINISTRATOR’ anateuliwa na Mahakama baada ya kupendekezwa na ukoo au familia, wakati ‘EXECUTOR’ ni yule aliyetajwa kwenye wosia na marehemu mwenyewe.

Vivyo hivyo, unaomba ‘UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE)’ au kuthibishwa kutekeleza wosia kama kuna wosia (section 24(1) PAEA) na unaomba ‘BARUA YA USIMAMIZI WA MIRATHI (LETTERS OF ADMINISTRATION)’ au kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi kama marehemu hakuacha kabisa wosia au wosia upo lakini una mapungufu, au aliyechaguliwa kwenye wosia amekataa, au hana vigezo, au ametangulia kufa kabla ya marehemu au kabla ya kuthibitishwa Mahakamani, n.k. Section 29 PAEA.

HATUA ZA KUFUNGUA MIRATHI:

1. FAMILY (CLAN) MEETING TO APPOINT THE ADMINISTRATOR OF ESTATES (KIKAO CHA FAMILIA AU UKOO KUMCHAGUA MSIMAMIZI WA MIRATHI). Kama, hakuna wosia, hatua ya kwanza ni kuchagua msimamizi wa mirathi. Ndugu wa marehemu wanatakiwa kupendekeza jina la mtu ambaye wanapenda asimamie mirathi.

Kazi ya msimamizi wa mirathi ni kufungua Mahakamani shauri la maombi ya kusimamia mirathi, kubainisha, kukusanya na kulipa madeni yaliyoachwa na marehemu, kugawa mali za marehemu kwa warithi halali n.k.

2: APPLICATION/PETITION FOR GRANT OF PROBATE OR LETTERS OF ADMINISTRATION (KUPELEKA MAHAKAMANI MAOMBI YA KUOMBA KUTEULIWA AU KUTHIBITISHWA KUWA MSIMAMIZI WA MIRATHI)

Mtu aliyetajwa kwenye wosia au aliyechaguliwa kwenye kikao cha wanafamilia (ukoo) atafungua maombi ya mirathi Mahakamani kuomba kuteuliwa au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi.

Sasa hapa inategemea na Mahakama unayoenda kufungua Mirathi.

Labda kwanza tufahamu, ni MAHAKAMA IPI UNAWEZA KUPELEKA KESI YA MIRATHI? (Maana, sio kila Mahakama unayoiona inasikiliza mirathi yoyote).

Inategemeana na sheria inayotumika au thamani ya mirathi yenyewe na marehemu alipokuwa anaishi. Mfano, kama mirathi inahusisha sheria za Kimila au Kiislam (where the law applicable is customary or Islamic law), unatakiwa kwenda Mahakama ya Mwanzo (haijalishi aina na thamani ya mirathi hiyo).

Zingatia: Mahakama ya Mwanzo haina mamlaka ya kusikiliza mashauri ya mirathi ya Wakristo. Kwa nini? Kwa sababu kwanza, mamlaka ya Mahakama ya Mwanzo yanaishia kwenye mirathi inayoendeshwa kwa kutumia sheria za Kimila au Kiislam, (yaani mirathi ambayo marehemu wakati wa uhai wake aliishi kwa kufuata taratibu za kimila au taratibu za dini ya Kiislamu). Soma kifungu cha 18(1)(a)(i) cha Sheria ya Mahakama za Mahakimu (the Magistrates’ Courts Act), unaweza kuiita kwa kifupi kama ‘MCA.’

Pili, sheria inayotumika kwa Wakristo ni Indian Succession Act, ya mwaka 1865, ambayo sio miongoni mwa sheria zinazotumika Mahakama ya Mwanzo.

Sheria inayotumika kwenye mashauri ya mirathi katika Mahakama ya Mwanzo ni the Primary Courts (Administration of Estates) Rules G.N. No 49 of 1971 (Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama ya Mwanzo) Tangazo la Serikali Na. 49 la mwaka 1971 na MCA kifungu cha 18(1)(a)(i), 19(1)(c) & paragraph 1(1) ya Jedwali la tano la MCA (Fifth Schedule to the MCA).

Kwa Mahakama ya Mwanzo maombi ya kuteuliwa kuwa msimamizi au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi hufanyika kupitia FOMU NAMBA I. Soma Kanuni ya 3 ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama ya Mwanzo) na Paragraph 2(a) & (b) ya Jedwali la tano la MCA.

Kumbuka: Fomu hizi zote unaweza kuziona nyuma ya sheria ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama ya Mwanzo, au kwenye Sheria inayotoa fomu zinazotumika katika mashauri ya Mahakama za Mwanzo (the Magistrates Court (Approved Forms for the Primary Court) GN. NO. 943 za mwaka 2020.

Kwa Mahakama zingine, forms zao zipo kwenye Kanuni za Mirathi zinaitwa Probate Rules za mwaka 1963. Sheria hizi zote zipo mtandaoni unaweza kujisomea.

Tuendelee sasa. Kama mirathi ya marehemu haizidi million mia moja (100,000,000) utaenda Mahakama ya Wilaya. Section 6(1) PAEA. (Zingatia, kama ina uhusiano na sheria ya Kimila au Kiislam utarudi Mahakama ya Mwanzo haijalishi ni million ngapi. Ni kana kwamba Mahakama ya Wilaya wanaenda Wakristo tu ambao mirathi yao haizidi 100,000,000.
Zaidi Kuhusu Mahakama ya Wilaya soma section 73-87 ya PAEA.

Kwa upande wa Mahakama zingine (ukiacha Mahakama ya Mwanzo) kama kuna wosia;

Maombi ya kuthibitisha wosia hufanyika kupitia fomu maalum iliyowekwa kisheria, FORM NUMBER 18. soma section 55(1) PAEA & Rule 33 ya Probate Rules. (NB: Wosia wa mdomo form ni no. 20, wosia uliopotea form no. 21, ukiwa na kopi/nakala ya wosia tu form no. 22). Rejea section 25 PAEA.

-Kama wosia una hitilafu maombi ya kuteuliwa kuwa msimamizi (letters of administration) hufanyika kupitia FORM NUMBER 26 (soma Section 55(1) PAEA & Rule 40 ya Probate Rules) au kama hakuna wosia kabisa FOMU NAMBA 27, soma section 56 PAEA & Rule 39.

VITU VYA KUAMBATANISHA UNAPOOOMBA KUTHIBITISHWA AU KUTEULIWA KUWA MSIMAMIZI WA MIRATHI

Ni muhimu kuambatanisha vitu vifuatavyo (ambapo inategemeana na marehemu aliacha wosia au hakuacha wosia)

KAMA KUNA WOSIA UTAAMBATANISHA:

{i} WILL (WOSIA), ikiwa marehemu aliacha wosia. Rule 33(1)(a) ya Probate Rules

{ii} UTHIBITISHO WA KIFO CHA MAREHEMU: Unaweza kuthibitisha kwa kuambatanisha vitu vifuatavyo;
-Cheti cha kifo (death certificate). As per Rule 33(1)(b) & 63.
-Hati ya kiapo (affidavit) ya ndugu wa marehemu au ya mtu aliyeshuhudia mazishi ya marehemu au
-Letter from the village or ward executive Secretary (barua kutoka ofisi ya mtendaji wa serikali ya kijiji au kata - kama hakuna cheti cha kifo).

{iii} kiapo cha msimamizi wa mirathi/executor’s oath, (aliyetajwa kwenye wosia) kwamba atasimamia mirathi kwa uaminifu. Section 66 of PAEA, rule 33(1)(d), form no. 47.

{iv} kiapo cha kuthibitisha makazi ya mwisho ya marehemu (an affidavit as to the deceased’s domicile at the time of his death. Rule 33(1)(c), form number 45.

{v} Verification of the petition (uthibitisho kwamba ulishuhudia wosia wakati unaandikwa) - Form number 19, section 57 PAEA.

KAMA HAKUNA WOSIA UTAAMBATANISHA:

{i} MINUTES FROM THE CLAN/FAMILY MEETING (DONDOO AU MUHTASARI WA KIKAO CHA FAMILIA AU UKOO) kilichomteua (kumpendekeza) muombaji kuwa msimamizi wa mirathi ikiwa marehemu hakuacha wosia au aliacha wosia lakini hakutaja jina la msimamizi, au aliyetajwa amekataa au amefariki n.k.

NB: Sio lazima mpeleke dondoo za kikao Mahakamani, hiki kitu hakipo kwenye sheria ni utaratibu tu wa Mahakama. Hata usipopeleka haina shida.

{ii} UTHIBITISHO WA KIFO CHA MAREHEMU: Unaweza kuthibitisha kwa kuambatanisha vitu vifuatavyo;
-Cheti cha kifo (death certificate). As per Rule 39(a) & 63
-Na vingine nilivyokwisha kutaja huko juu.

{iii} kiapo cha kuthibitisha makazi ya mwisho ya marehemu (an affidavit as to the deceased’s domicile at the time of his death. Rule 39(b) & Rule 64, form number 45.

{iv} kiapo cha msimamizi wa mirathi/administrator’s oath (aliyependekezwa na ukoo) kwamba atasimamia mirathi kwa uaminifu (administrator's oath). Section 66, rule 39(c), form number 46.

{v} Dhamana ya mtu atakayemdhamini
msimamizi wa mirathi (administration bond) section 67, rule 39(d), 66 & 68 form no. 48 or 49 (au fomu namba 3 kama ni Mahakama ya Mwanzo - Rejea Kanuni ya 7(1) na (3) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi katika Mahakama za Mwanzo.

{vi} Hati ya hali ya fedha ya wadhamini wa
msimamizi wa mirathi/administrator (certificate as to the financial position of the sureties). Rule 39(e) & 69, form no. 54.

{vii} Ridhaa ya warithi na ndugu au watu wenye maslahi katika mali za marehemu (consent of all heirs). Rule 39(f), 71 & 72, form 56

{viii} Kama ni mtu mmoja amefungua mirathi, weka na kiapo. Rule 39(g) na Rule 32.

{ix} Mali za marehemu (amount and nature of assets)

{x) Na mengineyo.

Baada ya hapo utalipia gharama zinazotakiwa, na shauri lako litapewa namba na kuingizwa kwenye kitabu cha kufungulia mirathi

MUDA (UKOMO) WA KUFUNGUA MIRATHI:

Unatakiwa kufungua mirathi ndani ya muda gani? Je, kuna ukomo wa kufungua shauri la mirathi? Kiufupi, hakuna muda maalumu wa kufungua shauri la mirathi, lakini kama utachelewa kwa muda wa MIAKA MITATU (3) tangu kifo cha marehemu, itakubidi utoe na maelezo au sababu za kuchelewa. Usipoambatanisha maelezo, maombi yako yatatupiliwa mbali.
Soma Rule 31 ya Probate Rules.

3: NOTICE OR GENERAL CITATION (TANGAZO AU WITO WA KUFIKA MAHAKAMANI).

Baada ya maombi kupokelewa, Mahakama itatoa tangazo kwamba kuna mtu amefungua mirathi pamoja na wito wa kufika Mahakamani kwa watu wote wanaohusika au wenye maslahi na mirathi ya marehemu. Tangazo hutolewa kwenye mbao za matangazo za Mahakama au kwenye gazeti la serikali linalosomwa na watu wengi au sehemu za wazi zenye mikusanyiko ya watu.

Lengo ni kuwapa taarifa watu wote wanaohusika na mali za marehemu waweze kufika Mahakamani tarehe, siku na muda uliopangwa, kufatilia maombi ya mirathi na ikiwa kuna mwenye pingamizi lolote aweze kuwasilisha kabla muombaji hajateuliwa au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi. Section 61(1)(c) & (2) PAEA, Rule 75, form no. 1 & no. 58.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo CITATION hutolewa kupitia Fomu Namba II.

MUDA (UKOMO) WA WITO (CITATION)

-Zamani tangazo la mirathi lilidumu kwa muda wa siku 90. Kuna kesi Moja Jaji alisema, inatakiwa iwe walau si chini ya week nne (4), chini ya hapo ni “Vodafasta” na ni hatari kuharakisha (Beatrice Brighton Kamanga and Amanda Brighton Kamanga v. Ziada William Kamanga, 2020), hata hivyo muda umepunguzwa mpaka siku 21.

-Mahakama zinahamasishwa kutoa matangazo ya mirathi kwa muda mfupi kadri iwezekanavyo, cha muhimu ni watu wote wanaohusika wapate taarifa.

4: OBJECTION/ENTERING CAVEAT (KUWASILISHA PINGAMIZI KAMA LIPO).

Kama una pingamizi lolote utawasilisha kupitia form form no. 62 au hata kwa mdomo. Section 58(1), Rule 82(1).

Pingamizi linadumu miezi minne Section 58(5) PAEA. Pingamizi linaisimamisha Mahakama isiendelee kusikiliza maombi ya mirathi kwanza mpaka itakapomaliza kusikiliza pingamizi.

Kukiwa na pingamizi hiyo ndo inaitwa CONTENTIOUS MATTER na kama hakuna pingamizi inaitwa NON CONTENTIOUS MATTER.

-Mahakama ya Mwanzo pia ina mamlaka ya kupokea na kusikiliza pingamizi.

5: CITATION TO CAVEATOR

Mfungua maombi ya mirathi ataiomba Mahakama itoe wito (citation) kumuita aliyeweka pingamizi (caveator) afike Mahakamani. Maombi yanatakiwa kufanyika ndani ya siku 30. Section 59(2) PAEA, Rule 75, rule 82(2), form number 63.

Ukishindwa kuiomba Mahakama imuite caveator, Mahakama itakukumbusha kwa kukupa notice ya kukutaka umuite caveator ndani ya siku zingine 21. Notice hiyo inatolewa kupitia form no. 63A. Ukishindwa tena kufanya application ndani ya hizo siku 21 za nyongeza, basi Mahakama itachukulia kwamba umeondoa mwenyewe Mahakamani maombi yako ya kuomba kusimamia mirathi. Rule 82(2A) & (2B). Ukitaka kuendelea utaomba restoration. Rule 82(2D).

6: ISSUANCE OF A CITATION

Kisha Msajili wa Mahakama atatoa wito kupitia form number 64 kumuita aliyeweka pingamizi atoe maelezo ndani ya siku 30, kama anakubali au anapinga. Na kama anapinga kwa nini anapinga uthibitisho wa wosia au kutolewa kwa barua za usimamizi wa mirathi kwa muombaji. Rule 82(3).

7: APPEARANCE BY CAVEATOR

Aliyeweka pingamizi baada ya kupokea wito (citation) atafika Mahakamani na kujibu kupitia form number 65, akiambatanisha na kiapo cha maelezo ya maslahi aliyo nayo na sababu za kupinga. Rule 82(4). Nakala itapelekwa kwa mfungua shauri la mirathi. Rule 82(5).

Baada ya pingamizi, maombi ya kufungua mirathi hugeuka kuwa kama KESI YA MADAI, muombaji anakuwa Mlalamikaji (Plaintiff) na Caveator anakuwa kama Defendant (Mtuhumiwa). Section 52(b) PAEA, Rule 82(6).

8: HEARING & RULING (KUSIKILIZA PINGAMIZI NA KUTOA UAMUZI MDOGO). Pingamizi litasikilizwa na kutolewa uamuzi, ambapo Mahakama inaweza kukubali au kukataa kuteua msimamizi wa mirathi au kuthibitisha wosia.

9: KUSIKILIZA MAOMBI NA
KUTEUA/KUTHIBITISHA MSIMAMIZI WA MIRATHI.

Kama hakuna pingamizi au pingamizi limekataliwa, Mahakama itaendelea mbele kusikiliza maombi ya mirathi na kuthibitisha wosia au kumteua msimamizi wa mirathi na kumkabidhi barua ya kuhalalisha kugawa mirathi.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo, hati ya kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi hutolewa kupitia fomu namba 4.

NB: Unaweza kuomba kutenguliwa kwa msimamizi wa mirathi, kama unaona haeleweki au hafanyi kazi yake ipasavyo.

10: TO FILE INVENTORIES (KUWASILISHA ORODHA YA MALI)

Msimamizi wa mirathi anatakiwa ndani ya miezi sita, kuwasilisha Mahakamani orodha ya mali za marehemu, na aina zake mfano ni mali isiyohamishika au inayohamishika, eneo ilipo, thamani yake, madeni, gharama nyinginezo kama vile gharama za mazishi, matibabu, gharama za usimamizi n.k. Section 107(1) PAEA, Rule 106, form number 80.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo orodha ya mali huwasilishwa kupitia fomu namba V ndani ya miezi minne. Rejea Kanuni ya 10(1) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi katika Mahakama za Mwanzo.

11: DIVISION OF ASSETS TO HEIRS (KUGAWA MALI KWA WARITHI).

Cha kwanza unalipa madeni na gharama za msiba, alafu unagawanya kilichobaki kwa warithi.

12: TO FILE STATEMENTS OF ACCOUNTS (KUTOA HESABU YA MIRATHI)

-Baada ya kugawa mali, msimamizi wa mirathi anatakiwa ndani ya mwaka mmoja, kurudisha Mahakamani hesabu kamili au taarifa ya ugawaji mali za marehemu, namna alivyotekeleza majukumu yake tangu alipoteuliwa na alivyogawa (atakavyogawa) mirathi kwa warithi ILI MAHAKAMA IFUNGE JALADA (KESI). Section 107(1) PAEA, Rule 107, form number 81.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo hesabu ya mirathi huwasilishwa kupitia fomu namba VI ndani ya miezi minne. Rejea Kanuni ya 10(1) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama za Mwanzo.

(Ni kosa kwa msimamizi kutoa hesabu au taarifa za uongo na kama akisababisha hasara yoyote anatakiwa alipe).

14: CLOSING OF A CASE FILE (KUFUNGWA KWA SHAURI LA MIRATHI)
Baada ya Mahakama kuridhika kwamba msimamizi wa mirathi ametekeleza wajibu wake ipasavyo, shauri la mirathi litafungwa.

Na huo ndio mwisho.

Zingatia: Mahakama haziruhusiwi kujihusisha na ugawaji wa mirathi (hiyo ni kazi ya Msimamizi wa mirathi).

Imeandaliwa na kuletwa kwako nami Zakaria Wakili Mtarajiwa (0754575246 WhatsApp).

Hobby: Exceptional legal research, writing, organizational and analytical skills.
Habar kwa mfano unataka kufungua mirathi je unatakiwa uambatanishe vitu gani
 
Habar kwa mfano unataka kufungua mirathi je unatakiwa uambatanishe vitu gani
Hatua ya kwanza unatakiwa uwe na Cheti cha Kifo(ukiwa na Cheti hiko)ni suala la siku moja,kikubwa uwe na kama 150,000 kwa ajili ya gharama za Mahakama,Tangazo Gazetini na Pesa ya Mwanasheria.Pia uwe na Muhtasari wa Kikao cha Familia uliokuchagua wewe kuwa Msimamizi wa Mirathi ya Marehemu B.Ukitaka sample ya Muhtasari/jinsi unavyoandikwa njoo PM. Na pia ukitaka Mwanasheria/Wakili wa kushughulikia suala lako naweza kukuunganisha na mmoja aliyenisaidia,yupo very smart
 
Ni jambo jingine kwenda Mahakamani na ni jambo jingine kuzijua taratibu za Mahakama. Kuna namna ya kuongea na Mahakama, ukikosea utapoteza haki zako, sio kwa sababu hauna haki ila kwa sababu hujui utaratibu (procedures).

Je, mtu akifa na ameacha mali, haijalishi kuna wosia au hakuna wosia, zipi ni hatua za kufuata ukitaka kufungua shauri la maombi ya mirathi?

(Imeandaliwa na kuletwa kwako na Zakaria - Lawyer by profession).

Kuna taratibu za kufungua mirathi, ambapo, inategemeana kama marehemu aliacha wosia au hakuacha wosia. (Whether the deceased person died testate i.e left a will or died intestate i.e without leaving will).

If the deceased person left a will appointing the name of person to be an ‘EXECUTOR,’ you petition/apply for ‘GRANT OF PROBATE,’ but if the deceased person died intestate, or the executor appointed by a will have renounced, or if no executor survives the testator etc, you apply for ‘GRANT OF LETTERS OF ADMINISTRATION.’ And a person so appointed is called Administrator (of estates).

-Namaanisha kwamba, kama marehemu aliacha wosia akiwa amekuchagua kusimamia na kugawa mirathi yake baada ya yeye kufariki, utaomba Mahakamani UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE).

-Kama marehemu hakuacha wosia au aliyechaguliwa kwenye wosia amekataa au ametangulia kufa kabla ya marehemu, au hana vigezo kisheria n.k., utaomba Mahakamani BARUA ya USIMAMIZI WA MIRATHI (LETTERS OF ADMINISTRATION)

Soma kifungu cha 24 na 29 cha Sheria ya Uthibitisho wa Wosia na Usimamizi wa Mirathi. Kwa kiingereza, inaitwa the ‘Probate and Administration of Estates Act’, ambayo ili Kuepuka usumbufu, nitakuwa nairejea kwa kifupi kama PAEA kwenye andiko hili lote.

Labda unajiuliza, kwani kuna utofauti gani kati ya ‘ADMINISTRATOR’ na ‘EXECUTOR,’ na kati ya ‘UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE)’ na ‘BARUA ZA USIMAMIZI WA MIRATHI (LETTERS OF ADMINISTRATION?’

Kwa kifupi sana, ‘ADMINISTRATOR’ anateuliwa na Mahakama baada ya kupendekezwa na ukoo au familia, wakati ‘EXECUTOR’ ni yule aliyetajwa kwenye wosia na marehemu mwenyewe.

Vivyo hivyo, unaomba ‘UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE)’ au kuthibishwa kutekeleza wosia kama kuna wosia (section 24(1) PAEA) na unaomba ‘BARUA YA USIMAMIZI WA MIRATHI (LETTERS OF ADMINISTRATION)’ au kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi kama marehemu hakuacha kabisa wosia au wosia upo lakini una mapungufu, au aliyechaguliwa kwenye wosia amekataa, au hana vigezo, au ametangulia kufa kabla ya marehemu au kabla ya kuthibitishwa Mahakamani, n.k. Section 29 PAEA.

HATUA ZA KUFUNGUA MIRATHI:

1. FAMILY (CLAN) MEETING TO APPOINT THE ADMINISTRATOR OF ESTATES (KIKAO CHA FAMILIA AU UKOO KUMCHAGUA MSIMAMIZI WA MIRATHI). Kama, hakuna wosia, hatua ya kwanza ni kuchagua msimamizi wa mirathi. Ndugu wa marehemu wanatakiwa kupendekeza jina la mtu ambaye wanapenda asimamie mirathi.

Kazi ya msimamizi wa mirathi ni kufungua Mahakamani shauri la maombi ya kusimamia mirathi, kubainisha, kukusanya na kulipa madeni yaliyoachwa na marehemu, kugawa mali za marehemu kwa warithi halali n.k.

2: APPLICATION/PETITION FOR GRANT OF PROBATE OR LETTERS OF ADMINISTRATION (KUPELEKA MAHAKAMANI MAOMBI YA KUOMBA KUTEULIWA AU KUTHIBITISHWA KUWA MSIMAMIZI WA MIRATHI)

Mtu aliyetajwa kwenye wosia au aliyechaguliwa kwenye kikao cha wanafamilia (ukoo) atafungua maombi ya mirathi Mahakamani kuomba kuteuliwa au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi.

Sasa hapa inategemea na Mahakama unayoenda kufungua Mirathi.

Labda kwanza tufahamu, ni MAHAKAMA IPI UNAWEZA KUPELEKA KESI YA MIRATHI? (Maana, sio kila Mahakama unayoiona inasikiliza mirathi yoyote).

Inategemeana na sheria inayotumika au thamani ya mirathi yenyewe na marehemu alipokuwa anaishi. Mfano, kama mirathi inahusisha sheria za Kimila au Kiislam (where the law applicable is customary or Islamic law), unatakiwa kwenda Mahakama ya Mwanzo (haijalishi aina na thamani ya mirathi hiyo).

Zingatia: Mahakama ya Mwanzo haina mamlaka ya kusikiliza mashauri ya mirathi ya Wakristo. Kwa nini? Kwa sababu kwanza, mamlaka ya Mahakama ya Mwanzo yanaishia kwenye mirathi inayoendeshwa kwa kutumia sheria za Kimila au Kiislam, (yaani mirathi ambayo marehemu wakati wa uhai wake aliishi kwa kufuata taratibu za kimila au taratibu za dini ya Kiislamu). Soma kifungu cha 18(1)(a)(i) cha Sheria ya Mahakama za Mahakimu (the Magistrates’ Courts Act), unaweza kuiita kwa kifupi kama ‘MCA.’

Pili, sheria inayotumika kwa Wakristo ni Indian Succession Act, ya mwaka 1865, ambayo sio miongoni mwa sheria zinazotumika Mahakama ya Mwanzo.

Sheria inayotumika kwenye mashauri ya mirathi katika Mahakama ya Mwanzo ni the Primary Courts (Administration of Estates) Rules G.N. No 49 of 1971 (Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama ya Mwanzo) Tangazo la Serikali Na. 49 la mwaka 1971 na MCA kifungu cha 18(1)(a)(i), 19(1)(c) & paragraph 1(1) ya Jedwali la tano la MCA (Fifth Schedule to the MCA).

Kwa Mahakama ya Mwanzo maombi ya kuteuliwa kuwa msimamizi au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi hufanyika kupitia FOMU NAMBA I. Soma Kanuni ya 3 ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama ya Mwanzo) na Paragraph 2(a) & (b) ya Jedwali la tano la MCA.

Kumbuka: Fomu hizi zote unaweza kuziona nyuma ya sheria ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama ya Mwanzo, au kwenye Sheria inayotoa fomu zinazotumika katika mashauri ya Mahakama za Mwanzo (the Magistrates Court (Approved Forms for the Primary Court) GN. NO. 943 za mwaka 2020.

Kwa Mahakama zingine, forms zao zipo kwenye Kanuni za Mirathi zinaitwa Probate Rules za mwaka 1963. Sheria hizi zote zipo mtandaoni unaweza kujisomea.

Tuendelee sasa. Kama mirathi ya marehemu haizidi million mia moja (100,000,000) utaenda Mahakama ya Wilaya. Section 6(1) PAEA. (Zingatia, kama ina uhusiano na sheria ya Kimila au Kiislam utarudi Mahakama ya Mwanzo haijalishi ni million ngapi. Ni kana kwamba Mahakama ya Wilaya wanaenda Wakristo tu ambao mirathi yao haizidi 100,000,000.
Zaidi Kuhusu Mahakama ya Wilaya soma section 73-87 ya PAEA.

Kwa upande wa Mahakama zingine (ukiacha Mahakama ya Mwanzo) kama kuna wosia;

Maombi ya kuthibitisha wosia hufanyika kupitia fomu maalum iliyowekwa kisheria, FORM NUMBER 18. soma section 55(1) PAEA & Rule 33 ya Probate Rules. (NB: Wosia wa mdomo form ni no. 20, wosia uliopotea form no. 21, ukiwa na kopi/nakala ya wosia tu form no. 22). Rejea section 25 PAEA.

-Kama wosia una hitilafu maombi ya kuteuliwa kuwa msimamizi (letters of administration) hufanyika kupitia FORM NUMBER 26 (soma Section 55(1) PAEA & Rule 40 ya Probate Rules) au kama hakuna wosia kabisa FOMU NAMBA 27, soma section 56 PAEA & Rule 39.

VITU VYA KUAMBATANISHA UNAPOOOMBA KUTHIBITISHWA AU KUTEULIWA KUWA MSIMAMIZI WA MIRATHI

Ni muhimu kuambatanisha vitu vifuatavyo (ambapo inategemeana na marehemu aliacha wosia au hakuacha wosia)

KAMA KUNA WOSIA UTAAMBATANISHA:

{i} WILL (WOSIA), ikiwa marehemu aliacha wosia. Rule 33(1)(a) ya Probate Rules

{ii} UTHIBITISHO WA KIFO CHA MAREHEMU: Unaweza kuthibitisha kwa kuambatanisha vitu vifuatavyo;
-Cheti cha kifo (death certificate). As per Rule 33(1)(b) & 63.
-Hati ya kiapo (affidavit) ya ndugu wa marehemu au ya mtu aliyeshuhudia mazishi ya marehemu au
-Letter from the village or ward executive Secretary (barua kutoka ofisi ya mtendaji wa serikali ya kijiji au kata - kama hakuna cheti cha kifo).

{iii} kiapo cha msimamizi wa mirathi/executor’s oath, (aliyetajwa kwenye wosia) kwamba atasimamia mirathi kwa uaminifu. Section 66 of PAEA, rule 33(1)(d), form no. 47.

{iv} kiapo cha kuthibitisha makazi ya mwisho ya marehemu (an affidavit as to the deceased’s domicile at the time of his death. Rule 33(1)(c), form number 45.

{v} Verification of the petition (uthibitisho kwamba ulishuhudia wosia wakati unaandikwa) - Form number 19, section 57 PAEA.

KAMA HAKUNA WOSIA UTAAMBATANISHA:

{i} MINUTES FROM THE CLAN/FAMILY MEETING (DONDOO AU MUHTASARI WA KIKAO CHA FAMILIA AU UKOO) kilichomteua (kumpendekeza) muombaji kuwa msimamizi wa mirathi ikiwa marehemu hakuacha wosia au aliacha wosia lakini hakutaja jina la msimamizi, au aliyetajwa amekataa au amefariki n.k.

NB: Sio lazima mpeleke dondoo za kikao Mahakamani, hiki kitu hakipo kwenye sheria ni utaratibu tu wa Mahakama. Hata usipopeleka haina shida.

{ii} UTHIBITISHO WA KIFO CHA MAREHEMU: Unaweza kuthibitisha kwa kuambatanisha vitu vifuatavyo;
-Cheti cha kifo (death certificate). As per Rule 39(a) & 63
-Na vingine nilivyokwisha kutaja huko juu.

{iii} kiapo cha kuthibitisha makazi ya mwisho ya marehemu (an affidavit as to the deceased’s domicile at the time of his death. Rule 39(b) & Rule 64, form number 45.

{iv} kiapo cha msimamizi wa mirathi/administrator’s oath (aliyependekezwa na ukoo) kwamba atasimamia mirathi kwa uaminifu (administrator's oath). Section 66, rule 39(c), form number 46.

{v} Dhamana ya mtu atakayemdhamini
msimamizi wa mirathi (administration bond) section 67, rule 39(d), 66 & 68 form no. 48 or 49 (au fomu namba 3 kama ni Mahakama ya Mwanzo - Rejea Kanuni ya 7(1) na (3) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi katika Mahakama za Mwanzo.

{vi} Hati ya hali ya fedha ya wadhamini wa
msimamizi wa mirathi/administrator (certificate as to the financial position of the sureties). Rule 39(e) & 69, form no. 54.

{vii} Ridhaa ya warithi na ndugu au watu wenye maslahi katika mali za marehemu (consent of all heirs). Rule 39(f), 71 & 72, form 56

{viii} Kama ni mtu mmoja amefungua mirathi, weka na kiapo. Rule 39(g) na Rule 32.

{ix} Mali za marehemu (amount and nature of assets)

{x) Na mengineyo.

Baada ya hapo utalipia gharama zinazotakiwa, na shauri lako litapewa namba na kuingizwa kwenye kitabu cha kufungulia mirathi

MUDA (UKOMO) WA KUFUNGUA MIRATHI:

Unatakiwa kufungua mirathi ndani ya muda gani? Je, kuna ukomo wa kufungua shauri la mirathi? Kiufupi, hakuna muda maalumu wa kufungua shauri la mirathi, lakini kama utachelewa kwa muda wa MIAKA MITATU (3) tangu kifo cha marehemu, itakubidi utoe na maelezo au sababu za kuchelewa. Usipoambatanisha maelezo, maombi yako yatatupiliwa mbali.
Soma Rule 31 ya Probate Rules.

3: NOTICE OR GENERAL CITATION (TANGAZO AU WITO WA KUFIKA MAHAKAMANI).

Baada ya maombi kupokelewa, Mahakama itatoa tangazo kwamba kuna mtu amefungua mirathi pamoja na wito wa kufika Mahakamani kwa watu wote wanaohusika au wenye maslahi na mirathi ya marehemu. Tangazo hutolewa kwenye mbao za matangazo za Mahakama au kwenye gazeti la serikali linalosomwa na watu wengi au sehemu za wazi zenye mikusanyiko ya watu.

Lengo ni kuwapa taarifa watu wote wanaohusika na mali za marehemu waweze kufika Mahakamani tarehe, siku na muda uliopangwa, kufatilia maombi ya mirathi na ikiwa kuna mwenye pingamizi lolote aweze kuwasilisha kabla muombaji hajateuliwa au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi. Section 61(1)(c) & (2) PAEA, Rule 75, form no. 1 & no. 58.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo CITATION hutolewa kupitia Fomu Namba II.

MUDA (UKOMO) WA WITO (CITATION)

-Zamani tangazo la mirathi lilidumu kwa muda wa siku 90. Kuna kesi Moja Jaji alisema, inatakiwa iwe walau si chini ya week nne (4), chini ya hapo ni “Vodafasta” na ni hatari kuharakisha (Beatrice Brighton Kamanga and Amanda Brighton Kamanga v. Ziada William Kamanga, 2020), hata hivyo muda umepunguzwa mpaka siku 21.

-Mahakama zinahamasishwa kutoa matangazo ya mirathi kwa muda mfupi kadri iwezekanavyo, cha muhimu ni watu wote wanaohusika wapate taarifa.

4: OBJECTION/ENTERING CAVEAT (KUWASILISHA PINGAMIZI KAMA LIPO).

Kama una pingamizi lolote utawasilisha kupitia form form no. 62 au hata kwa mdomo. Section 58(1), Rule 82(1).

Pingamizi linadumu miezi minne Section 58(5) PAEA. Pingamizi linaisimamisha Mahakama isiendelee kusikiliza maombi ya mirathi kwanza mpaka itakapomaliza kusikiliza pingamizi.

Kukiwa na pingamizi hiyo ndo inaitwa CONTENTIOUS MATTER na kama hakuna pingamizi inaitwa NON CONTENTIOUS MATTER.

-Mahakama ya Mwanzo pia ina mamlaka ya kupokea na kusikiliza pingamizi.

5: CITATION TO CAVEATOR

Mfungua maombi ya mirathi ataiomba Mahakama itoe wito (citation) kumuita aliyeweka pingamizi (caveator) afike Mahakamani. Maombi yanatakiwa kufanyika ndani ya siku 30. Section 59(2) PAEA, Rule 75, rule 82(2), form number 63.

Ukishindwa kuiomba Mahakama imuite caveator, Mahakama itakukumbusha kwa kukupa notice ya kukutaka umuite caveator ndani ya siku zingine 21. Notice hiyo inatolewa kupitia form no. 63A. Ukishindwa tena kufanya application ndani ya hizo siku 21 za nyongeza, basi Mahakama itachukulia kwamba umeondoa mwenyewe Mahakamani maombi yako ya kuomba kusimamia mirathi. Rule 82(2A) & (2B). Ukitaka kuendelea utaomba restoration. Rule 82(2D).

6: ISSUANCE OF A CITATION

Kisha Msajili wa Mahakama atatoa wito kupitia form number 64 kumuita aliyeweka pingamizi atoe maelezo ndani ya siku 30, kama anakubali au anapinga. Na kama anapinga kwa nini anapinga uthibitisho wa wosia au kutolewa kwa barua za usimamizi wa mirathi kwa muombaji. Rule 82(3).

7: APPEARANCE BY CAVEATOR

Aliyeweka pingamizi baada ya kupokea wito (citation) atafika Mahakamani na kujibu kupitia form number 65, akiambatanisha na kiapo cha maelezo ya maslahi aliyo nayo na sababu za kupinga. Rule 82(4). Nakala itapelekwa kwa mfungua shauri la mirathi. Rule 82(5).

Baada ya pingamizi, maombi ya kufungua mirathi hugeuka kuwa kama KESI YA MADAI, muombaji anakuwa Mlalamikaji (Plaintiff) na Caveator anakuwa kama Defendant (Mtuhumiwa). Section 52(b) PAEA, Rule 82(6).

8: HEARING & RULING (KUSIKILIZA PINGAMIZI NA KUTOA UAMUZI MDOGO). Pingamizi litasikilizwa na kutolewa uamuzi, ambapo Mahakama inaweza kukubali au kukataa kuteua msimamizi wa mirathi au kuthibitisha wosia.

9: KUSIKILIZA MAOMBI NA
KUTEUA/KUTHIBITISHA MSIMAMIZI WA MIRATHI.

Kama hakuna pingamizi au pingamizi limekataliwa, Mahakama itaendelea mbele kusikiliza maombi ya mirathi na kuthibitisha wosia au kumteua msimamizi wa mirathi na kumkabidhi barua ya kuhalalisha kugawa mirathi.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo, hati ya kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi hutolewa kupitia fomu namba 4.

NB: Unaweza kuomba kutenguliwa kwa msimamizi wa mirathi, kama unaona haeleweki au hafanyi kazi yake ipasavyo.

10: TO FILE INVENTORIES (KUWASILISHA ORODHA YA MALI)

Msimamizi wa mirathi anatakiwa ndani ya miezi sita, kuwasilisha Mahakamani orodha ya mali za marehemu, na aina zake mfano ni mali isiyohamishika au inayohamishika, eneo ilipo, thamani yake, madeni, gharama nyinginezo kama vile gharama za mazishi, matibabu, gharama za usimamizi n.k. Section 107(1) PAEA, Rule 106, form number 80.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo orodha ya mali huwasilishwa kupitia fomu namba V ndani ya miezi minne. Rejea Kanuni ya 10(1) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi katika Mahakama za Mwanzo.

11: DIVISION OF ASSETS TO HEIRS (KUGAWA MALI KWA WARITHI).

Cha kwanza unalipa madeni na gharama za msiba, alafu unagawanya kilichobaki kwa warithi.

12: TO FILE STATEMENTS OF ACCOUNTS (KUTOA HESABU YA MIRATHI)

-Baada ya kugawa mali, msimamizi wa mirathi anatakiwa ndani ya mwaka mmoja, kurudisha Mahakamani hesabu kamili au taarifa ya ugawaji mali za marehemu, namna alivyotekeleza majukumu yake tangu alipoteuliwa na alivyogawa (atakavyogawa) mirathi kwa warithi ILI MAHAKAMA IFUNGE JALADA (KESI). Section 107(1) PAEA, Rule 107, form number 81.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo hesabu ya mirathi huwasilishwa kupitia fomu namba VI ndani ya miezi minne. Rejea Kanuni ya 10(1) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama za Mwanzo.

(Ni kosa kwa msimamizi kutoa hesabu au taarifa za uongo na kama akisababisha hasara yoyote anatakiwa alipe).

14: CLOSING OF A CASE FILE (KUFUNGWA KWA SHAURI LA MIRATHI)
Baada ya Mahakama kuridhika kwamba msimamizi wa mirathi ametekeleza wajibu wake ipasavyo, shauri la mirathi litafungwa.

Na huo ndio mwisho.

Zingatia: Mahakama haziruhusiwi kujihusisha na ugawaji wa mirathi (hiyo ni kazi ya Msimamizi wa mirathi).

Imeandaliwa na kuletwa kwako nami Zakaria Wakili Mtarajiwa (0754575246 WhatsApp).

Hobby: Exceptional legal research, writing, organizational and analytical skills.
Asante mkuu.
 
Hi
Ni jambo jingine kwenda Mahakamani na ni jambo jingine kuzijua taratibu za Mahakama. Kuna namna ya kuongea na Mahakama, ukikosea utapoteza haki zako, sio kwa sababu hauna haki ila kwa sababu hujui utaratibu (procedures).

Je, mtu akifa na ameacha mali, haijalishi kuna wosia au hakuna wosia, zipi ni hatua za kufuata ukitaka kufungua shauri la maombi ya mirathi?

(Imeandaliwa na kuletwa kwako na Zakaria - Lawyer by profession).

Kuna taratibu za kufungua mirathi, ambapo, inategemeana kama marehemu aliacha wosia au hakuacha wosia. (Whether the deceased person died testate i.e left a will or died intestate i.e without leaving will).

If the deceased person left a will appointing the name of person to be an ‘EXECUTOR,’ you petition/apply for ‘GRANT OF PROBATE,’ but if the deceased person died intestate, or the executor appointed by a will have renounced, or if no executor survives the testator etc, you apply for ‘GRANT OF LETTERS OF ADMINISTRATION.’ And a person so appointed is called Administrator (of estates).

-Namaanisha kwamba, kama marehemu aliacha wosia akiwa amekuchagua kusimamia na kugawa mirathi yake baada ya yeye kufariki, utaomba Mahakamani UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE).

-Kama marehemu hakuacha wosia au aliyechaguliwa kwenye wosia amekataa au ametangulia kufa kabla ya marehemu, au hana vigezo kisheria n.k., utaomba Mahakamani BARUA ya USIMAMIZI WA MIRATHI (LETTERS OF ADMINISTRATION)

Soma kifungu cha 24 na 29 cha Sheria ya Uthibitisho wa Wosia na Usimamizi wa Mirathi. Kwa kiingereza, inaitwa the ‘Probate and Administration of Estates Act’, ambayo ili Kuepuka usumbufu, nitakuwa nairejea kwa kifupi kama PAEA kwenye andiko hili lote.

Labda unajiuliza, kwani kuna utofauti gani kati ya ‘ADMINISTRATOR’ na ‘EXECUTOR,’ na kati ya ‘UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE)’ na ‘BARUA ZA USIMAMIZI WA MIRATHI (LETTERS OF ADMINISTRATION?’

Kwa kifupi sana, ‘ADMINISTRATOR’ anateuliwa na Mahakama baada ya kupendekezwa na ukoo au familia, wakati ‘EXECUTOR’ ni yule aliyetajwa kwenye wosia na marehemu mwenyewe.

Vivyo hivyo, unaomba ‘UTHIBITISHO WA WOSIA (PROBATE)’ au kuthibishwa kutekeleza wosia kama kuna wosia (section 24(1) PAEA) na unaomba ‘BARUA YA USIMAMIZI WA MIRATHI (LETTERS OF ADMINISTRATION)’ au kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi kama marehemu hakuacha kabisa wosia au wosia upo lakini una mapungufu, au aliyechaguliwa kwenye wosia amekataa, au hana vigezo, au ametangulia kufa kabla ya marehemu au kabla ya kuthibitishwa Mahakamani, n.k. Section 29 PAEA.

HATUA ZA KUFUNGUA MIRATHI:

1. FAMILY (CLAN) MEETING TO APPOINT THE ADMINISTRATOR OF ESTATES (KIKAO CHA FAMILIA AU UKOO KUMCHAGUA MSIMAMIZI WA MIRATHI). Kama, hakuna wosia, hatua ya kwanza ni kuchagua msimamizi wa mirathi. Ndugu wa marehemu wanatakiwa kupendekeza jina la mtu ambaye wanapenda asimamie mirathi.

Kazi ya msimamizi wa mirathi ni kufungua Mahakamani shauri la maombi ya kusimamia mirathi, kubainisha, kukusanya na kulipa madeni yaliyoachwa na marehemu, kugawa mali za marehemu kwa warithi halali n.k.

2: APPLICATION/PETITION FOR GRANT OF PROBATE OR LETTERS OF ADMINISTRATION (KUPELEKA MAHAKAMANI MAOMBI YA KUOMBA KUTEULIWA AU KUTHIBITISHWA KUWA MSIMAMIZI WA MIRATHI)

Mtu aliyetajwa kwenye wosia au aliyechaguliwa kwenye kikao cha wanafamilia (ukoo) atafungua maombi ya mirathi Mahakamani kuomba kuteuliwa au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi.

Sasa hapa inategemea na Mahakama unayoenda kufungua Mirathi.

Labda kwanza tufahamu, ni MAHAKAMA IPI UNAWEZA KUPELEKA KESI YA MIRATHI? (Maana, sio kila Mahakama unayoiona inasikiliza mirathi yoyote).

Inategemeana na sheria inayotumika au thamani ya mirathi yenyewe na marehemu alipokuwa anaishi. Mfano, kama mirathi inahusisha sheria za Kimila au Kiislam (where the law applicable is customary or Islamic law), unatakiwa kwenda Mahakama ya Mwanzo (haijalishi aina na thamani ya mirathi hiyo).

Zingatia: Mahakama ya Mwanzo haina mamlaka ya kusikiliza mashauri ya mirathi ya Wakristo. Kwa nini? Kwa sababu kwanza, mamlaka ya Mahakama ya Mwanzo yanaishia kwenye mirathi inayoendeshwa kwa kutumia sheria za Kimila au Kiislam, (yaani mirathi ambayo marehemu wakati wa uhai wake aliishi kwa kufuata taratibu za kimila au taratibu za dini ya Kiislamu). Soma kifungu cha 18(1)(a)(i) cha Sheria ya Mahakama za Mahakimu (the Magistrates’ Courts Act), unaweza kuiita kwa kifupi kama ‘MCA.’

Pili, sheria inayotumika kwa Wakristo ni Indian Succession Act, ya mwaka 1865, ambayo sio miongoni mwa sheria zinazotumika Mahakama ya Mwanzo.

Sheria inayotumika kwenye mashauri ya mirathi katika Mahakama ya Mwanzo ni the Primary Courts (Administration of Estates) Rules G.N. No 49 of 1971 (Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama ya Mwanzo) Tangazo la Serikali Na. 49 la mwaka 1971 na MCA kifungu cha 18(1)(a)(i), 19(1)(c) & paragraph 1(1) ya Jedwali la tano la MCA (Fifth Schedule to the MCA).

Kwa Mahakama ya Mwanzo maombi ya kuteuliwa kuwa msimamizi au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi hufanyika kupitia FOMU NAMBA I. Soma Kanuni ya 3 ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama ya Mwanzo) na Paragraph 2(a) & (b) ya Jedwali la tano la MCA.

Kumbuka: Fomu hizi zote unaweza kuziona nyuma ya sheria ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama ya Mwanzo, au kwenye Sheria inayotoa fomu zinazotumika katika mashauri ya Mahakama za Mwanzo (the Magistrates Court (Approved Forms for the Primary Court) GN. NO. 943 za mwaka 2020.

Kwa Mahakama zingine, forms zao zipo kwenye Kanuni za Mirathi zinaitwa Probate Rules za mwaka 1963. Sheria hizi zote zipo mtandaoni unaweza kujisomea.

Tuendelee sasa. Kama mirathi ya marehemu haizidi million mia moja (100,000,000) utaenda Mahakama ya Wilaya. Section 6(1) PAEA. (Zingatia, kama ina uhusiano na sheria ya Kimila au Kiislam utarudi Mahakama ya Mwanzo haijalishi ni million ngapi. Ni kana kwamba Mahakama ya Wilaya wanaenda Wakristo tu ambao mirathi yao haizidi 100,000,000.
Zaidi Kuhusu Mahakama ya Wilaya soma section 73-87 ya PAEA.

Kwa upande wa Mahakama zingine (ukiacha Mahakama ya Mwanzo) kama kuna wosia;

Maombi ya kuthibitisha wosia hufanyika kupitia fomu maalum iliyowekwa kisheria, FORM NUMBER 18. soma section 55(1) PAEA & Rule 33 ya Probate Rules. (NB: Wosia wa mdomo form ni no. 20, wosia uliopotea form no. 21, ukiwa na kopi/nakala ya wosia tu form no. 22). Rejea section 25 PAEA.

-Kama wosia una hitilafu maombi ya kuteuliwa kuwa msimamizi (letters of administration) hufanyika kupitia FORM NUMBER 26 (soma Section 55(1) PAEA & Rule 40 ya Probate Rules) au kama hakuna wosia kabisa FOMU NAMBA 27, soma section 56 PAEA & Rule 39.

VITU VYA KUAMBATANISHA UNAPOOOMBA KUTHIBITISHWA AU KUTEULIWA KUWA MSIMAMIZI WA MIRATHI

Ni muhimu kuambatanisha vitu vifuatavyo (ambapo inategemeana na marehemu aliacha wosia au hakuacha wosia)

KAMA KUNA WOSIA UTAAMBATANISHA:

{i} WILL (WOSIA), ikiwa marehemu aliacha wosia. Rule 33(1)(a) ya Probate Rules

{ii} UTHIBITISHO WA KIFO CHA MAREHEMU: Unaweza kuthibitisha kwa kuambatanisha vitu vifuatavyo;
-Cheti cha kifo (death certificate). As per Rule 33(1)(b) & 63.
-Hati ya kiapo (affidavit) ya ndugu wa marehemu au ya mtu aliyeshuhudia mazishi ya marehemu au
-Letter from the village or ward executive Secretary (barua kutoka ofisi ya mtendaji wa serikali ya kijiji au kata - kama hakuna cheti cha kifo).

{iii} kiapo cha msimamizi wa mirathi/executor’s oath, (aliyetajwa kwenye wosia) kwamba atasimamia mirathi kwa uaminifu. Section 66 of PAEA, rule 33(1)(d), form no. 47.

{iv} kiapo cha kuthibitisha makazi ya mwisho ya marehemu (an affidavit as to the deceased’s domicile at the time of his death. Rule 33(1)(c), form number 45.

{v} Verification of the petition (uthibitisho kwamba ulishuhudia wosia wakati unaandikwa) - Form number 19, section 57 PAEA.

KAMA HAKUNA WOSIA UTAAMBATANISHA:

{i} MINUTES FROM THE CLAN/FAMILY MEETING (DONDOO AU MUHTASARI WA KIKAO CHA FAMILIA AU UKOO) kilichomteua (kumpendekeza) muombaji kuwa msimamizi wa mirathi ikiwa marehemu hakuacha wosia au aliacha wosia lakini hakutaja jina la msimamizi, au aliyetajwa amekataa au amefariki n.k.

NB: Sio lazima mpeleke dondoo za kikao Mahakamani, hiki kitu hakipo kwenye sheria ni utaratibu tu wa Mahakama. Hata usipopeleka haina shida.

{ii} UTHIBITISHO WA KIFO CHA MAREHEMU: Unaweza kuthibitisha kwa kuambatanisha vitu vifuatavyo;
-Cheti cha kifo (death certificate). As per Rule 39(a) & 63
-Na vingine nilivyokwisha kutaja huko juu.

{iii} kiapo cha kuthibitisha makazi ya mwisho ya marehemu (an affidavit as to the deceased’s domicile at the time of his death. Rule 39(b) & Rule 64, form number 45.

{iv} kiapo cha msimamizi wa mirathi/administrator’s oath (aliyependekezwa na ukoo) kwamba atasimamia mirathi kwa uaminifu (administrator's oath). Section 66, rule 39(c), form number 46.

{v} Dhamana ya mtu atakayemdhamini
msimamizi wa mirathi (administration bond) section 67, rule 39(d), 66 & 68 form no. 48 or 49 (au fomu namba 3 kama ni Mahakama ya Mwanzo - Rejea Kanuni ya 7(1) na (3) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi katika Mahakama za Mwanzo.

{vi} Hati ya hali ya fedha ya wadhamini wa
msimamizi wa mirathi/administrator (certificate as to the financial position of the sureties). Rule 39(e) & 69, form no. 54.

{vii} Ridhaa ya warithi na ndugu au watu wenye maslahi katika mali za marehemu (consent of all heirs). Rule 39(f), 71 & 72, form 56

{viii} Kama ni mtu mmoja amefungua mirathi, weka na kiapo. Rule 39(g) na Rule 32.

{ix} Mali za marehemu (amount and nature of assets)

{x) Na mengineyo.

Baada ya hapo utalipia gharama zinazotakiwa, na shauri lako litapewa namba na kuingizwa kwenye kitabu cha kufungulia mirathi

MUDA (UKOMO) WA KUFUNGUA MIRATHI:

Unatakiwa kufungua mirathi ndani ya muda gani? Je, kuna ukomo wa kufungua shauri la mirathi? Kiufupi, hakuna muda maalumu wa kufungua shauri la mirathi, lakini kama utachelewa kwa muda wa MIAKA MITATU (3) tangu kifo cha marehemu, itakubidi utoe na maelezo au sababu za kuchelewa. Usipoambatanisha maelezo, maombi yako yatatupiliwa mbali.
Soma Rule 31 ya Probate Rules.

3: NOTICE OR GENERAL CITATION (TANGAZO AU WITO WA KUFIKA MAHAKAMANI).

Baada ya maombi kupokelewa, Mahakama itatoa tangazo kwamba kuna mtu amefungua mirathi pamoja na wito wa kufika Mahakamani kwa watu wote wanaohusika au wenye maslahi na mirathi ya marehemu. Tangazo hutolewa kwenye mbao za matangazo za Mahakama au kwenye gazeti la serikali linalosomwa na watu wengi au sehemu za wazi zenye mikusanyiko ya watu.

Lengo ni kuwapa taarifa watu wote wanaohusika na mali za marehemu waweze kufika Mahakamani tarehe, siku na muda uliopangwa, kufatilia maombi ya mirathi na ikiwa kuna mwenye pingamizi lolote aweze kuwasilisha kabla muombaji hajateuliwa au kuthibitishwa kuwa msimamizi wa mirathi. Section 61(1)(c) & (2) PAEA, Rule 75, form no. 1 & no. 58.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo CITATION hutolewa kupitia Fomu Namba II.

MUDA (UKOMO) WA WITO (CITATION)

-Zamani tangazo la mirathi lilidumu kwa muda wa siku 90. Kuna kesi Moja Jaji alisema, inatakiwa iwe walau si chini ya week nne (4), chini ya hapo ni “Vodafasta” na ni hatari kuharakisha (Beatrice Brighton Kamanga and Amanda Brighton Kamanga v. Ziada William Kamanga, 2020), hata hivyo muda umepunguzwa mpaka siku 21.

-Mahakama zinahamasishwa kutoa matangazo ya mirathi kwa muda mfupi kadri iwezekanavyo, cha muhimu ni watu wote wanaohusika wapate taarifa.

4: OBJECTION/ENTERING CAVEAT (KUWASILISHA PINGAMIZI KAMA LIPO).

Kama una pingamizi lolote utawasilisha kupitia form form no. 62 au hata kwa mdomo. Section 58(1), Rule 82(1).

Pingamizi linadumu miezi minne Section 58(5) PAEA. Pingamizi linaisimamisha Mahakama isiendelee kusikiliza maombi ya mirathi kwanza mpaka itakapomaliza kusikiliza pingamizi.

Kukiwa na pingamizi hiyo ndo inaitwa CONTENTIOUS MATTER na kama hakuna pingamizi inaitwa NON CONTENTIOUS MATTER.

-Mahakama ya Mwanzo pia ina mamlaka ya kupokea na kusikiliza pingamizi.

5: CITATION TO CAVEATOR

Mfungua maombi ya mirathi ataiomba Mahakama itoe wito (citation) kumuita aliyeweka pingamizi (caveator) afike Mahakamani. Maombi yanatakiwa kufanyika ndani ya siku 30. Section 59(2) PAEA, Rule 75, rule 82(2), form number 63.

Ukishindwa kuiomba Mahakama imuite caveator, Mahakama itakukumbusha kwa kukupa notice ya kukutaka umuite caveator ndani ya siku zingine 21. Notice hiyo inatolewa kupitia form no. 63A. Ukishindwa tena kufanya application ndani ya hizo siku 21 za nyongeza, basi Mahakama itachukulia kwamba umeondoa mwenyewe Mahakamani maombi yako ya kuomba kusimamia mirathi. Rule 82(2A) & (2B). Ukitaka kuendelea utaomba restoration. Rule 82(2D).

6: ISSUANCE OF A CITATION

Kisha Msajili wa Mahakama atatoa wito kupitia form number 64 kumuita aliyeweka pingamizi atoe maelezo ndani ya siku 30, kama anakubali au anapinga. Na kama anapinga kwa nini anapinga uthibitisho wa wosia au kutolewa kwa barua za usimamizi wa mirathi kwa muombaji. Rule 82(3).

7: APPEARANCE BY CAVEATOR

Aliyeweka pingamizi baada ya kupokea wito (citation) atafika Mahakamani na kujibu kupitia form number 65, akiambatanisha na kiapo cha maelezo ya maslahi aliyo nayo na sababu za kupinga. Rule 82(4). Nakala itapelekwa kwa mfungua shauri la mirathi. Rule 82(5).

Baada ya pingamizi, maombi ya kufungua mirathi hugeuka kuwa kama KESI YA MADAI, muombaji anakuwa Mlalamikaji (Plaintiff) na Caveator anakuwa kama Defendant (Mtuhumiwa). Section 52(b) PAEA, Rule 82(6).

8: HEARING & RULING (KUSIKILIZA PINGAMIZI NA KUTOA UAMUZI MDOGO). Pingamizi litasikilizwa na kutolewa uamuzi, ambapo Mahakama inaweza kukubali au kukataa kuteua msimamizi wa mirathi au kuthibitisha wosia.

9: KUSIKILIZA MAOMBI NA
KUTEUA/KUTHIBITISHA MSIMAMIZI WA MIRATHI.

Kama hakuna pingamizi au pingamizi limekataliwa, Mahakama itaendelea mbele kusikiliza maombi ya mirathi na kuthibitisha wosia au kumteua msimamizi wa mirathi na kumkabidhi barua ya kuhalalisha kugawa mirathi.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo, hati ya kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi hutolewa kupitia fomu namba 4.

NB: Unaweza kuomba kutenguliwa kwa msimamizi wa mirathi, kama unaona haeleweki au hafanyi kazi yake ipasavyo.

10: TO FILE INVENTORIES (KUWASILISHA ORODHA YA MALI)

Msimamizi wa mirathi anatakiwa ndani ya miezi sita, kuwasilisha Mahakamani orodha ya mali za marehemu, na aina zake mfano ni mali isiyohamishika au inayohamishika, eneo ilipo, thamani yake, madeni, gharama nyinginezo kama vile gharama za mazishi, matibabu, gharama za usimamizi n.k. Section 107(1) PAEA, Rule 106, form number 80.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo orodha ya mali huwasilishwa kupitia fomu namba V ndani ya miezi minne. Rejea Kanuni ya 10(1) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi katika Mahakama za Mwanzo.

11: DIVISION OF ASSETS TO HEIRS (KUGAWA MALI KWA WARITHI).

Cha kwanza unalipa madeni na gharama za msiba, alafu unagawanya kilichobaki kwa warithi.

12: TO FILE STATEMENTS OF ACCOUNTS (KUTOA HESABU YA MIRATHI)

-Baada ya kugawa mali, msimamizi wa mirathi anatakiwa ndani ya mwaka mmoja, kurudisha Mahakamani hesabu kamili au taarifa ya ugawaji mali za marehemu, namna alivyotekeleza majukumu yake tangu alipoteuliwa na alivyogawa (atakavyogawa) mirathi kwa warithi ILI MAHAKAMA IFUNGE JALADA (KESI). Section 107(1) PAEA, Rule 107, form number 81.

-Kwa Mahakama ya Mwanzo hesabu ya mirathi huwasilishwa kupitia fomu namba VI ndani ya miezi minne. Rejea Kanuni ya 10(1) ya Kanuni za Usimamizi wa Mirathi Mahakama za Mwanzo.

(Ni kosa kwa msimamizi kutoa hesabu au taarifa za uongo na kama akisababisha hasara yoyote anatakiwa alipe).

14: CLOSING OF A CASE FILE (KUFUNGWA KWA SHAURI LA MIRATHI)
Baada ya Mahakama kuridhika kwamba msimamizi wa mirathi ametekeleza wajibu wake ipasavyo, shauri la mirathi litafungwa.

Na huo ndio mwisho.

Zingatia: Mahakama haziruhusiwi kujihusisha na ugawaji wa mirathi (hiyo ni kazi ya Msimamizi wa mirathi).

Imeandaliwa na kuletwa kwako nami Zakaria Wakili Mtarajiwa (0754575246 WhatsApp).

Hobby: Exceptional legal research, writing, organizational and analytical skills.
Hivi ikatokea mzazi wa kiume amefariki na hajaacha mali kuna ulazima wa kuapply hiyo probate?
 
Hivi Kwa Mfano Dhamira ya Mali ni kuuzwa Lakini Mteja Bado hajapatikana Je Nini Kinaanza
Kugawa Kwa Kufata Asilimia na Mtapouza Mnakamilisha Au Sheria inataka Kwanza ziuzwe Ndipo Mgawane ?
 
Back
Top Bottom