Una Degree na unafanya kazi ambayo ungeweza kuifanya hata kama ungeishia darasa la saba

666 chata

JF-Expert Member
Mar 14, 2013
1,688
3,816
Wakuu kwema!

Huyu Rafiki wa zamani tulipotezana miaka mingi kidogo, enzi za chuo chuo miaka ile mwamba akisomea moja ya fani ya Engineering pale DIT. Miaka hiyo tukiongelea future jamaa alikuwa akijiweka katika nafasi kama tisa hivi za juu za nchi vile akiamini uinjinia utakapo mweka.

Juzi nipo chimbo moja hapa mjini, namkuta yeye ndio mpishi mkuu wa eneo hilo, akiwauzia watu supu na vyakula vingine, kavaa nguo zile za ki chef, nilishtuka ila sikujisikia vibaya maana pesa inatafutwa bwana! Ikabidi tuzungumze na nijue what happened? Chief Engineer imekuwaje kuaje mpaka uwe chef cooker?

Mwamba alistuka lakini akawa mkweli tu mzee na vile tumeshakuwa watu wazima, akasema ni mchakato tu wa maisha, ila aka kazia 'anachosikitika kitu alichokisomea hajawahi kukifanyia kazi, miaka minne yote aliyosomea uinjinia imepotea bure tu na sasa anafanya kazi ambayo hata kama angeishia darasa la saba angeifanya tu'.

Anasema, maisha yalikuwa magumu kweli kweli, kazi hakuna so akaomba kazi ya u dj bar flan sababu alikuwa anapenda sana muziki. Baadaye kwenye u dj kukawa kugumu basi akaona kuna bar imeanzishwa maeneo jirani yake akaomba kazi pale wakampa chaka la jiko, na amekuwa akihama toka bar flan kwenda nyingine na sasa ndo kabobea hapo kwenye karia ya majiko.

Maswali ya kujiuliza, hivi watu hua wanazingatia kweli muda walioupoteza kwenye masomo yao? Kweli hustles zile zimeenda bure? Wanazingatia mamilioni waliyoyalipa vyuoni kwa ajili ya icho walichokuwa wanakisomea? au shida ni kwamba watu wengi walienda kusomea vitu ambavyo sio kusudi lao ambalo Mungu aliliweka ndani yao so degree zao zinakua ni gabage?

Watoto wetu tunawaandaa vp na tunawaambia vipi kwamba baba ako mimi usinione ni chef mimi nina degree ya uinjinia. So hatuwezi kuwa ving'ang'anizi kwenye vile tulivyovisomea kwa miaka mingi na kulipia fedha nyingi?
 
Kama wewe ni great thinker wala usingewaza hivyo. Lazima ungegusa pande zote ili ndiyo tujadili ni kwanini, sasa kwa ulipoishia kuandika mimi nashindwa kujadili maana pia wapo darasa la saba wanaofanya kazi za wenye degree eidha kwa kupeana kindugu ama kijuana kwa namna moja aau nyingine.

Sasa kama wa degree kazi yake imepatiwa mtu wa la saba aifanye kisa tu baba yake anajuana na watu flani ni lazima nae jamaa wa degree apige U_Turn moja matata akapige kazi ya jamaa wa darasa la saba sasa.... Na hapo sasa ndiyo utakuta jamaa wa degree anachimba mitaro, Anavuta mkokoteni, yeye ni fundi saidia analipwa 5,000 per day... sasa atafanyaje jamaa wawatu hana jinsi.

Nafikiri tuishie hapa. Ingawa nimejibu kwa kusoma tittle tu. Ngoja niupitie uzi sasa.

Habari za asubuhi lakini.
 
Hii inatokana na mifumo mbovu Kwanza WA jinsi labour inavyokuwa organised kwenye nchi , hii nchi ni ya kipumbavu Sana , utakuta mtu kaishia la pili kaajiriwa anafanya kazi ya qualifications za mtu WA degree , it's so messy + nepotism +bribery .
Plus uchumi mbovu usiozalisha ajira leaving people unemployed and destitute . Ni dalili mbaya Sana hii , mnabaki na uchumi WA kwenye makaratasi Ila wananchi hoi bin taabani , watu wanaishi kama wapo vitani .
 
Maisha ni vita.
Elimu ni silaha, na haipo yenyewe zipo silaha zingine Kama Nguvu, Mtaji, Rasilimali, n.k.

Ukienda vitani unaenda na silaha zote kwani haujui ni ipi itakayokusaidia kulingana na adui atakavyokuja.

Ni ujinga ukienda vitani alafu uone vita haihitaji Bunduki alafu ukalazimisha kutumia Bunduki ilhali vita inahitaji Labda mawe na visu
 
Hii inatokana na mifumo mbovu Kwanza WA jinsi labour inavyokuwa organised kwenye nchi , hii nchi ni ya kipumbavu Sana , utakuta mtu kaishia la pili kaajiriwa anafanya kazi ya qualifications za mtu WA degree , it's so messy + nepotism +bribery .
Plus uchumi mbovu usiozalisha ajira leaving people unemployed and destitute . Ni dalili mbaya Sana hii , mnabaki na uchumi WA kwenye makaratasi Ila wananchi hoi bin taabani , watu wanaishi kama wapo vitani .
Kama kampuni ya baba au mjomba, mwache aajiriwe kwenye nafasi hiyo, maana watajuwa namma ya kurekebisha mapungufu yatakayojitokeza. Lakini kwa serikalini, hilo litakuwa janga kubwa sana!
 
Yeye si wa kwanza, kuna watu famous kama Mr bean, Wenger nao walipitia hiyo hali. Anachotakiwa kufanya ni kutengeneza pesa halafu atasifiwa kuwa yeye ni injinia mpishi. Elimu ni muhimu ila usiisotee ukiwaza hilo karatasi ndo likupe kazi.
 
Hizo kazi zote anazofanya ukute hakuwa competent hata moja. Mtu aliyetoka Engineering DIT ukamkabidhi masaani ya DJ hawezi kuwa perfect kwenye hiyo kazi labda awe aliwekeza muda wake mwingi uko kabla ili awe master. Vilevile huwezi fyatua mtu mtaani ukampa jiko la bar apike akawa vizuri kisa ana degree ya miaka minne. Lazima alipata tabu kwenye kazi hizo mpaka kuzoea.

Kuna chefs wanapigwa hela ndefu na wanagombaniwa kwenye mahoteli hasa ya kitalii. Ila kuanzia engineering na kuwa master chef unachelewa kiasi
 
Cha maana, mwisho wa siku unaingiza ngapi? Alipiga mahesabu akaona anapata zaidi ya professor, maisha ni mchezo na anacheza vizuri.
 
Kuna mwamba maeneo fulani asubuhi unamkuta amekaa kwenye kigoda pembeni ana jiko la mkaa anachoma vitumbua nikasema hii vita ni ngumu sana na mwamba sidhani kama sio graduate.
 
hii comment imefunga uzi, point tupu. huyo chef mwenye degree hawezi kufanya kazi kama la 7. na ikitokea connection yoyote anamuacha wa la 7 amesimama.
Kuna Jamaa mmoja nilimsikia redioni anasimulia. Ana elimu ya degree mbili,alianza kazi kubeba mizigo duka la fenicha baada ya kukosa kazi muda mrefu. Alikuja client mzungu jamaa akamuhudumia vizuri huku Kiingereza kimenyooka. Mzungu akanote jamaa ni smart, akamtoa pale. The rest is history. Jamaa sasa hivi ni one of influential people in Tz.
 
Back
Top Bottom