Umeshawahi kumsikia nyoka aitwaye Kifutu?

Umeshawahi kumsikia nyoka aitwaye Kifutu?

Nikimuona huyo kifutu hata muda wa kunichekea hataupata,, maana nitatimua vumbi la hatari..
 
Kwani ushawahi kuona nyoka akimkimbiza mtu ?

Kwani amekuwa simba au chui huyo ?

Mkuu mbona niliambiwa kuwa kuna nyoka anaitwa black mamba anakimbiza mtu kama simba, yaani ukikutana naye kitaani kwake ukipona ni majaaliwa eti akili yake ni kwasababu anatumia sana mmea ule pendwa lakini haramu.
 
Actually africa hakuna nyoka nkuu..! Nyoka wapo asia..! Especially the indian subcontinent..! Kule ndo kunaongoza kwa kuwa na nyoka wengi na wakali zaidi..! Wanasema watafiti kuwa mtu mmoja hufa kila baada ya dakika sita kutokana na kung'atwa na nyoka...!

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa ule wingi wao ni sawa kabisa kila dakika mtu kupotea

Psalm 133:1 "Behold, how good and how pleasant it is for brethren to dwell together in unity."
 
Nyoka hata kama ni Swila ama Koboko huwa ni wapole kinachotokea tu wakati mwingine ni kujihami...nyoka wengi hata wale wakali akimuona binadamu hutoka nduki ila kama kwa bahati mbaya ukaingia kwenye anga zake ndipo pale atakapokomaa na wewe kwa kusimamia mkia na ukijifanya mtaalamu wa kumpiga au kukimbia anakumaliza

Kumbe wanakimbiza, si umesema nyoka wanakimbia binadamu?
 
Akili finyu hizi

Naomba waungwana tumpuuze huyu jamaa.
Sasa wewe wadanganganye halafu wajifanye marafiki wa nyoka, then wataleta feedback!

Sent from my Nokia-tochi using JamiiForums mobile app
 
Mimi na nyoka ni vitu viwili tofauti, awe mpole au mkali ila mimi NYOKA yoyote yule NINAUA.
Kuna watu wasiojua shida wanazoleta nyoka. Wanadai tuwapende nyoka wakati wao hawatupendi! Ni kuponda vichwa vyao tu maandiko yatimie. Yeye akikuwahi tu anatimiza maandiko.

Sent from my Nokia-tochi using JamiiForums mobile app
 
Mkuu Fernando; Nyoka hakushambulii kwa lengo la kukushambulia tuu. La hasha. Mara zote nyoka anajihami mathalani umemkanyaga, umemfikia karibu mno na hana pa kukimbilia au kujificha au umeng'ngana kumuua. Sumu yake ni kwa ajili ya kujipatia chakula au tuseme kukamata mawindo yake. Tena ukumbuke anapokung'ata hakupi "Full Dose" kwani anaihitaji sumu hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa. Tena nyoka kifutu (na wengineo) wanafaida ya kula panya kama afanyavyo paka tunayemfuga. Kumbuka Tanzania(By then Tanganyika) tuliwahi ku-import vifutu from Malawi kwa ajili ya kudhibiti panya waharibifu kwenye ule mradi mkubwa wa Karanga Kongwa.
Mimi nyoka sikai naye, hao panya bora wajazane humo ndani nitakomaa nao kwa namna nyingine. Kuna nyoka wakorofi mkuu, hizi stori za kusimuliana na kufundishana katika taasisi za elimu hazifanani sana na uhalisia.

Kipindi cha vita ya Nduli Idd Amin Dadah kuna familia moja ya jirani ilikuwa imelala usiku kwenye handaki, baba, mama & watoto 11. Black mamba katika pitapita zake akadondokea humo, alitoa dozi moja moja kwa kila mmoja na kuwaua 12. Alipona mmoja tu! Kila nikiyatizama yale makaburi yalivyopangana nasema kwa herufi kubwa,,, SHIKAMOO BLACK MAMBA...

Sent from my Nokia-tochi using JamiiForums mobile app
 
Huyu nyoka mpole sana wanapatikana sana maeneo ya baridi , siku moja nikiwa mafinga jkt nilitoroka mkesha nikaenda kulala porini nilikuwa na blanket nikiwa nmelala kumbe likaja likifutu na kuingia kwenye blanket asubuhi nashtuka linanitekenya...
Wala halikunidhuru
Duh!

post using my macbook air using jamiiforums app
 
Mimi nyoka sikai naye, hao panya bora wajazane humo ndani nitakomaa nao kwa namna nyingine. Kuna nyoka wakorofi mkuu, hizi stori za kusimuliana na kufundishana katika taasisi za elimu hazifanani sana na uhalisia.

Kipindi cha vita ya Nduli Idd Amin Dadah kuna familia moja ya jirani ilikuwa imelala usiku kwenye handaki, baba, mama & watoto 11. Black mamba katika pitapita zake akadondokea humo, alitoa dozi moja moja kwa kila mmoja na kuwaua 12. Alipona mmoja tu! Kila nikiyatizama yale makaburi yalivyopangana nasema kwa herufi kubwa,,, SHIKAMOO BLACK MAMBA...

Sent from my Nokia-tochi using JamiiForums mobile app
Mkuu; hata mimi sikushauri kabisa ukae naye. Na akiingia ndani ya nyumba unayoishi yaani nyumbani kwako jitahidi umwondoshe haraka kwani anaweza kukudhuru wewe au familia yako. Nyoka huyo aliyeingia ndani mara nyingi ni kuwinda panya au kutafuta maji au kujihifadhi dhidi ya hali mbaya ya hewa (joto kali au baridi kali) hatajua kwamba huna nia mbaya naye ila atajihami tu. Na kwa mantiki hiyo atakuwa ameingia kwenye anga zako. Ninachosema hapa mkuu, ni kwa mtu yule bila sababu ya maana kumsaka au pengine mtu anatembea porini(ambako ndo nyumbani kwake nyoka) na akimwona nyoka anasitisha au anaacha shughuli iliyompeleka huko porini na kuanzisha kazi ya kumwua huyo nyoka. Walioumwa na Black mamba ilikuwa ni ajali kama zilivyo ajali nyingine. Watu wanapata ajali kwenye magari lakini bado hawaachi kuyatumia.
 
Na je nikimkanyaga bahati mbaya? Unadhani atanisamehe!??

Sent from my Nokia-tochi using JamiiForums mobile app
Aisee!! utakuwa tayar umeshafanya mistake, so kukusamehe ni pale atakapo kutanisha meno yake kwenye mguu wako..!

post using my macbook air using jamiiforums app
 
Kuna watu wasiojua shida wanazoleta nyoka. Wanadai tuwapende nyoka wakati wao hawatupendi! Ni kuponda vichwa vyao tu maandiko yatimie. Yeye akikuwahi tu anatimiza maandiko.

Sent from my Nokia-tochi using JamiiForums mobile app
Mkuu Fernando; hata mm nilikuwa na mawazo kama hayo esp. baada ya kuumwa na nyoka wale wenye rangi ya kijani na wanapenda sana kukaa juu ya miti - green mamba almaarufu kama boomslag. Lakini baada ya kuujua ukweli kuhusu viumbe hawa sina tatizo nao yaani chuki kali kihivyo.Ninajitahidi kuwaepuka lakini sio kila nyoka nimwonaye kazi ni moja tu KUUA. Kumbuka hata nyuki wanaleta shida, Nge wanaleta shida, Manyigu wanaleta shida ...ni shida kwani wana sumu. Basi bro.legeza vigezo na masharti - Usiwaue nyoka bila sababu ya msingi.
 
Aisee!! utakuwa tayar umeshafanya mistake, so kukusamehe ni pale atakapo kutanisha meno yake kwenye mguu wako..!

post using my macbook air using jamiiforums app
Sasa kiumbe asiyejua bahati mbaya hafai, mbaya zaidi hana shambulizi la kutoa onyo, ni kumaliza kazi kwa sumu

Sent from my Nokia-tochi using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom