mkuu ukiwa unachunga mifugo porini kuonana na nyoka mnapishana kama swila, kifutu, chatu ni vitu vya kawaida na ikitokea chatu kakamata mbuzi inabidi upambane nae ile mbaya, kuna kitu nakumbuka chatu alikosea step akaenda mdaka ng'ombe sasa ng'ombe nahisi alimuona, chatu kufyatuka na ng'ombe karuka hivyo chatu akaambulia kudaka miguu, ili amuangushe si ng'ombe akakojoa, ule mkojo kumdondokea chatu, aisee alifyatuka kama radi, nikahisi mkojo wa ng'ombe inawezekana ni sumu kwa joka lile, nilitafuta sehemu nyingine yenye jani nikachamba, ukiwa mwoga porini huwezi kwenda, yani inafikia kipindi unaona kawaida tu, kuna nyoka wengine nao sijawahi kuwaona mpaka leo lakini kule wapo, sijui siku hizi manake naona mapori mengi watu wamelima na yashakuwa makazi ya watu,