Umeshawahi kumsikia nyoka aitwaye Kifutu?

Umeshawahi kumsikia nyoka aitwaye Kifutu?


Basi leo ngoja nikueleze habari ya kufurahisha kuhusu nyoka huyu, kwanza ni miongoni mwa viumbe ambao wamesaidia lugha ya kiswahili kukua, kwa waliosoma kiswahili wanaweza kufahamu vyema kuwa miongoni mwa mambo ambayo husaidia kukua kwa lugha ni pamoja na lugha kukopa maneno, misimu pia kufananisha umbo la kitu na maneno, ikiwa pamoja na mambo mengine mengi,

Basi nyoka kifutu amefananishwa umbo lake na jina alilopewa, ukimuona kichwani ni mwembamba na mkia mwembamba lakini mwili wa kati ni kibonge mbaya.

Nyoka huyu hatagi bali anazaa ! Sasa usitoe macho, kama ulikuwa hujui nakufahamisha hivi nyoka katika masuala ya uzazi wamegawanyika katika makundi matatu, kundi la kwanza hutaga, kundi la pili huzaa na kundi la tatu huwa wanataga na kuzaa (hapa ndio utashangaa yaani anataga na akitotoa akabaini watoto bado dhaifu basi atawameza na kuwazaa hapo baadaye, au akiwa na mayai akabaini kwamba mazingira hayo si rafiki atameza mayai na kuzaa baadaye).

Turudi kwa kifutu wetu yeye huzaa watoto 20 na kuendelea huko, na watoto huendelea na maisha yao punde tuu baada ya kuzaliwa, Chakula kikuu cha mnyama huyu ni pamoja na wadudu, panya, mayai ya ndege, wanyama wadodo wadogo kama sungura nk, hapa hutegemea sana na umri, wapo katika makundi mawili moja wale ambao hujitokeza sehemu ambazo binadamu hufanya shughuli zake kama shambani nk.

Hawa huwa na sumu lakini si kali sana, ila waishio polini akikuuma una hatari ya kufa mapema sana na nyoka huyu ni miongoni mwa nyoka ambao wapo katika kundi la nyoka walioua sana binadamu.

Ana meno mawili juu na makali sana yaliyochongoka kama ambayo huonekana kwa simba au chui, na meno ya chini ni madogo na hujipanga kwa wingi sana lakini hayazidi kumi.

SIFA ZAKE
  1. Bingwa sana wa kujificha, watu wengi humkanyaga kwakuwa ni ngumu kumuona kwa urahisi.
  2. Si mkorofi pamoja na ukatili alionao, lakini akiona binadamu humkimbia, pamoja kwamba atakukimbia lakini atarudi mara kwa mara kuangalia je umeondoka ! Lengo likiwa ni kuendelea na shughuli zake, hivyo akikupa heshima na wewe uwe mstarabu kumpisha.
  3. Akikuona sura yake huitengeneza kama anatabasamu, sasa sio anataka kukuchekea anaweka meno sawa.
  4. Ana aibu pia.
  5. Anapowinda akiwa penye ardhi laini hujifukia, sasa kanyaga.
  6. Ana urefu wa mita moja na kilo sita au zaidi.
  7. Akikuuma utapatwa na yafuatayo, kutwoka sana na jasho, kutapika na kuishiwa nguvu.

Je umeshawahi kujua nyoka akikuuma yatakiwa ufanye nini ?

[HASHTAG]#wasalaam[/HASHTAG].
=======

Nimekopi nikiamini humu ntapata ufafanuz wa kutaalam zaidi hasa kwenye kuzaa hapo
Ana tofauti gani na chatu au koboko?
 
Kwanza huyu nyoka ni mpole.

Kinachomfanya aue sana na harak ni sumu yake kuwa nyepesi sio nZito so inasafiri kwa urahisi sana

Kingine huyu jamaa ni mlain sana, nimewah wapiga na jembe unawakat vizuri, wana body laini
Vipi kuhusu chatu?
 

Basi leo ngoja nikueleze habari ya kufurahisha kuhusu nyoka huyu, kwanza ni miongoni mwa viumbe ambao wamesaidia lugha ya kiswahili kukua, kwa waliosoma kiswahili wanaweza kufahamu vyema kuwa miongoni mwa mambo ambayo husaidia kukua kwa lugha ni pamoja na lugha kukopa maneno, misimu pia kufananisha umbo la kitu na maneno, ikiwa pamoja na mambo mengine mengi,

Basi nyoka kifutu amefananishwa umbo lake na jina alilopewa, ukimuona kichwani ni mwembamba na mkia mwembamba lakini mwili wa kati ni kibonge mbaya.

Nyoka huyu hatagi bali anazaa ! Sasa usitoe macho, kama ulikuwa hujui nakufahamisha hivi nyoka katika masuala ya uzazi wamegawanyika katika makundi matatu, kundi la kwanza hutaga, kundi la pili huzaa na kundi la tatu huwa wanataga na kuzaa (hapa ndio utashangaa yaani anataga na akitotoa akabaini watoto bado dhaifu basi atawameza na kuwazaa hapo baadaye, au akiwa na mayai akabaini kwamba mazingira hayo si rafiki atameza mayai na kuzaa baadaye).

Turudi kwa kifutu wetu yeye huzaa watoto 20 na kuendelea huko, na watoto huendelea na maisha yao punde tuu baada ya kuzaliwa, Chakula kikuu cha mnyama huyu ni pamoja na wadudu, panya, mayai ya ndege, wanyama wadodo wadogo kama sungura nk, hapa hutegemea sana na umri, wapo katika makundi mawili moja wale ambao hujitokeza sehemu ambazo binadamu hufanya shughuli zake kama shambani nk.

Hawa huwa na sumu lakini si kali sana, ila waishio polini akikuuma una hatari ya kufa mapema sana na nyoka huyu ni miongoni mwa nyoka ambao wapo katika kundi la nyoka walioua sana binadamu.

Ana meno mawili juu na makali sana yaliyochongoka kama ambayo huonekana kwa simba au chui, na meno ya chini ni madogo na hujipanga kwa wingi sana lakini hayazidi kumi.

SIFA ZAKE
  1. Bingwa sana wa kujificha, watu wengi humkanyaga kwakuwa ni ngumu kumuona kwa urahisi.
  2. Si mkorofi pamoja na ukatili alionao, lakini akiona binadamu humkimbia, pamoja kwamba atakukimbia lakini atarudi mara kwa mara kuangalia je umeondoka ! Lengo likiwa ni kuendelea na shughuli zake, hivyo akikupa heshima na wewe uwe mstarabu kumpisha.
  3. Akikuona sura yake huitengeneza kama anatabasamu, sasa sio anataka kukuchekea anaweka meno sawa.
  4. Ana aibu pia.
  5. Anapowinda akiwa penye ardhi laini hujifukia, sasa kanyaga.
  6. Ana urefu wa mita moja na kilo sita au zaidi.
  7. Akikuuma utapatwa na yafuatayo, kutwoka sana na jasho, kutapika na kuishiwa nguvu.

Je umeshawahi kujua nyoka akikuuma yatakiwa ufanye nini ?

[HASHTAG]#wasalaam[/HASHTAG].
=======

Nimekopi nikiamini humu ntapata ufafanuz wa kutaalam zaidi hasa kwenye kuzaa hapo
Ninaishi naye huyu. Nina viatu na mkanda wake.
 
Mleta mada, huyo nyoka kweli anaitwa Kifutu au Moma?.
Kwa uelewa wangu na miaka yote ambayo niko porini, namfahamu kama Moma.
Kifutu ni nyoka wengine wana rangi ya brown ambao nao ni wapole lakini wana sumu kali zaidi.
Moma ni huyo huyo kifutu- ( kiswahili ni kifutu).

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Wakati mdogo nko chimala mbeya nlikuwa nakutana nao sana
Kuna siku nlikuwa naenda mafundisho tuko chaka tukakutana naye wacha atubaraze
Ukienda Kyle mtoni sasa huko ndiko kuna michatu kibao,chatu akishiba sasa anakuwa kama bwege tu
Sema ile nyumba nliyokuwa nakaa walikuwa na dawa za nyoka
Nyoka kuingia ndani ilikuwa kawaida tu

Ova
 
Back
Top Bottom