Umemsikia MUGABE alichomwambia OBAMA.?

Umemsikia MUGABE alichomwambia OBAMA.?

Mnamsifia mjinga huyo alichukuwa nchi ikiwa first world kaifanya third world na nusu ya wananchi wake wameishia ukimbizini kuwa manamba..poleni kwa ujinga
h

nakuambia southern Africa ni first world, mm nimeenda South Africa na Swaziland, wao walishasahau matatatizo madogo madogo kama maji, umeme, barabara, reli, huduma za afya, tena kwao wananchi wana haki ya kusimamisha gari ya polisi ili impeleke mgonjwa hospitali na lazima polisi wasimame na wamchukue mgonjwa vinginevyo wanapoteza kazi. mm naona wewe umeaminishwa na wazungu kwa wao kutamka kuwa imekuwa third world

hii haina tofauti na waandishi feki ambao wamekuwa kwa muda mrefu wakiandika kuwa Askofu Kakobe ametoroka nchini, matokeo yake walipokutana naye katika msiba wa Askofu Mkuu kulola na maeneo ya jinsi hiyo walishindwa kutuambia amerudi lini?

nenda kajionee usisubiri kuambiwa,
 
Mwana wa Ngabu, mimi huwa naenda mbali sana hadi kudhani kuwa labda waafrika tuna hitlafu katika akili zetu.
Hebu fikiria tu hata hilo la nguo fupi, mtu anaitwa shujaa eti kwa kuzuia mtindo fulani ya mavazi!!, Ndiyo. Kwani nguo fupi ni nini hasa zaidi tu ya mitindo ya mavazi!??, ndio ushujaa wa Afrika huo!??, hivyo tu!!!.
Hata kama hakuna chanzo cha uhakika cha hii habari, binafsi sitashangaa sana kama ikiwa ni kweli kwa sababu Mugabe ni mtu wa kurusha madongo sana hususan dhidi ya viongozi wa nchi za Magharibi.



Siyo Waganda tu. Hata Wabongo. Hivi umeona anavyopewa heko na watu humu JF? Halafu cha kushangaza zaidi ni kwamba anaungwa mkono mpaka na wanawake (at least kulingana na IDs zao humu na jinsi wanavyojiwasilisha).

Ndo maana nimekuwa nikisema kwamba Waafrika wengi sana ni wepesi wa kuhadaiwa na kuvutika. Jambo dogo tu hawakawii kukupachika sifa kede kede...'fulani ni kichwa'....'fulani ni jembe'.

Viwango vyetu ni vya chini sana sisi.
 
Hahahahahahaaaaa

Majibu ya mugabe
Lazima uondoke umenunaaaaaa.
 
"If Obama wants me to allow GAYS marriage in Zimbabwe. I should Marry him first to
show the good example" -Robert Mugabe"

Haa haa haaaa haaa Mugabe ni shidaaa!
 
Hivi Rais wa JMT alijibu vipi vile interview ya CNN:flypig:
 
Maskini Mzee Mugabe anaathirika name uzee tumhurumie!
 
Hivi Rais wa JMT alijibu vipi vile interview ya CNN:flypig:

Kimsingi alichosema JK kwenye kujibu swali lile ni kwamba, watu wa magharibi msiende kasi sana, watu wetu hawakubali tamaduni zenu, lakini ni suala la muda tu watakubali.

Amanpour akamuumua hapo hapo, akamuuliza, vipi wewe unakubali?

JK akajibalaguza akajibu siwezi kusema kwa sasa.

Rais mzima wa nchi kashindwa kutoa msimamo ajulikane anakubali ushoga au hakubali.

Kwa wachunguzi wa mambo ya kisiasa jibu hilo, ukiliangalia katika mtiririko wa alivyojibu kuanzia mwanzo, ni kwamba anakubali ila anaogopa akisema anakubali huku nyumbani itakuwa mtafaruku. Ndiyo maana katika kuwapoza wamagharibi maliberali anasema wasiwe na shaka baada ya muda haya mambo yatakubalika tu, lakini alipoulizwa kama yeye anayakubali akagwaya kisiasa kwa kuogopa mlumbano atakaozua nyumbani.
 
Mwana wa Ngabu, mimi huwa naenda mbali sana hadi kudhani kuwa labda waafrika tuna hitlafu katika akili zetu.
Hebu fikiria tu hata hilo la nguo fupi, mtu anaitwa shujaa eti kwa kuzuia mtindo fulani ya mavazi!!, Ndiyo. Kwani nguo fupi ni nini hasa zaidi tu ya mitindo ya mavazi!??, ndio ushujaa wa Afrika huo!??, hivyo tu!!!.

Mshairi na mchekeshaji wa Kirumi aliyeitwa Juvenal alikuwa na msemo wake uliotoka katika "Satire X", akisema kuwatawala watu wasiofikiri kama hawa wa populations za nchi za Africa unahitaji kuwapa mkate na sarakasi tu.

Sasa sisi huku Afrika tunapewa sarakasi tupu bila mkate, tena sarakasi mbaya. Watu wanapigwa "kipara" bila maji halafu wanashangilia.

From Juvenal

Already long ago, from when we sold our vote to no man, the People have abdicated our duties; for the People who once upon a time handed out military command, high civil office, legions - everything, now restrains itself and anxiously hopes for just two things: bread and circuses

Ndiyo maana watu wakisikia Mugabe kapiga sarakasi bila ya ku address matatizo ya kiuchumi na kujibu kuhusu damu aliyomwaga, watu wanamshangilia.

Watu hawatafuti uongozi tena, wanatafuta sarakasi tu.

Hata huo mkate wamekosa matumaini nao!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom