Kama nilivyosema hapo juu, shida yako ni kwenye kutofautisha mambo, wewe unapomuangalia mtu aliyevaa nguo fupi, huwezi kusema ameingilia uhuru wako wa kuona kwa sababu hajakulazimisha, umehiari mwenyewe kumuangalia.
Waarabu wameenda na falsafa ya mavazi hadi inataka kuwafikisha pabaya, wanajifanya wao wana ashki sana, wanasema hata nywele za mwanamke ni utupu, hivyo azifunike, mwishowe wakabaini macho ya mwanamke nacho ni kishawishi, nayo wakamtaka aweke wavu, mwisho wamegundua hata akijifunika mwili mzima hadi macho, bado ni kishawishi. Saudia wameamua kujenga mji ambao wanawake watakaa huko peke yao ili wasionekane kabisa. Ni ujinga tu, vishawishi vinaanzia kwrnye fikra zako mwenyewe.