Umemsikia MUGABE alichomwambia OBAMA.?

Umemsikia MUGABE alichomwambia OBAMA.?

Waafrika wengi kuwapoteza lengo ni kazi rahisi sana.

Watajie habari za wakoloni, wazungu, utumwa, new world order, ushoga, maadui wa nje, maadui wa ndani, wasaliti, waliokosa uzalendo etc etc.

Utawaibia mabilioni kwa mabilioni huku wanakupigia makofi.

Wengi wanataka waigizaji na vitongozi.

Hawataki viongozi.

Sasa mtu kama Mugabe baada ya mauaji yote na economic mismnagement aliyoifanya Zimbabwe naye ni wa kusifiwa?

Kisa?

Kawatongoza waafrika masikini vizuri na kujipa image ya mpinga wazungu!

Wanaomsifia Mugabe wanajua jinsi gani alivyoua wa Ndebele?

Someni Gukurahundi

http://en.m.wikipedia.org/wiki/Gukurahundi

aaaaah subiri kwanza wewe ushoga unauonaje....
 
Mugabe alishajua vizuri saikolojia ya waafrika.
Toa matamshi makali dhidi ya wazungu, hata ikibidi kuwatukana, watakuita Simba wa Afrika, shujaa, kidume, True son of Afrika, Mzalendo wa kweli na majina mengine kibao, wakikuambia umekaa muda mrefu madarakani jilinganishe na malkia, kwamba na yeye mbona amekaa muda mrefu, kwa sababu anajua kabisa hakuna mtu mwenye akili za kutofautisha mfumo wa utawala wa Ungereza na Zimbabwe.

Atakayekuchallenge kwenye madaraka sema tu ni kibaraka wa wazungu, umemaliza mchezo.

Hizi mbinu za kujifanya una hasira na wazungu alitumiaga sana Marehemu Qaddaf, and he was honoured.
Mshairi na mchekeshaji wa Kirumi aliyeitwa Juvenal alikuwa na msemo wake uliotoka katika "Satire X", akisema kuwatawala watu wasiofikiri kama hawa wa populations za nchi za Africa unahitaji kuwapa mkate na sarakasi tu.

Sasa sisi huku Afrika tunapewa sarakasi tupu bila mkate, tena sarakasi mbaya. Watu wanapigwa "kipara" bila maji halafu wanashangilia.

From Juvenal



Ndiyo maana watu wakisikia Mugabe kapiga sarakasi bila ya ku address matatizo ya kiuchumi na kujibu kuhusu damu aliyomwaga, watu wanamshangilia.

Watu hawatafuti uongozi tena, wanatafuta sarakasi tu.

Hata huo mkate wamekosa matumaini nao!
 
"If Obama wants me to allow gays marriage in Zimbabwe,I should marry him first to show the good example"-Robert Mugabe..

Ndio huyu huyu mzee,ambaye alipoulizwa na wanahabari wa Uingereza kuwa kwanini asiachie ngazi ilhali ameshazeeka, aliwauliza kama walishawahi kumuuliza swali kama hilo malkia wao..

Salute kwako uncle mugabe..
Hawa viongozi wa magharibi hawana adabu kabisa. Wanatafuta tu sababu ya kutudhalilisha kwa unyonge wetu. Kwani nani kawaambia huku afrika mashoga wanauliwa zaidi ya kudharauliwa wanapojitambulisha hadharani. Kwa mila na desturi kote ulimwenguni ushoga ni jambo la aibu na kudharauliwa. Kama wao wana uchungu na haki za binaadamu kwanza waache kutunyonya rasilimali zetu hadi tumebakia fukara wa kutupa. Sasa kama wao wanaona ushoga ni tabia ya kawaida Obama amjibu Mzee Mugabe ombi lake.
 
"If Obama wants me to allow gays marriage in Zimbabwe,I should marry him first to show the good example"-Robert Mugabe..

Ndio huyu huyu mzee,ambaye alipoulizwa na wanahabari wa Uingereza kuwa kwanini asiachie ngazi ilhali ameshazeeka, aliwauliza kama walishawahi kumuuliza swali kama hilo malkia wao..

Salute kwako uncle mugabe..

huyu ndie Kiongozi wa Africa ... na ndii maana anaing'ang:ania Zimbabwe ... anajua upimbavu wa wazungu .. he really know them

big up Mugabe .
 
aaaaah subiri kwanza wewe ushoga unauonaje....

Mimi si suala la ushoga tu, mambo yote ambayo yanahusiana na watu wazima wawili ni juu yao. Falsafa yangu ni, mambo ya Ngoswe, muachie Ngoswe mwenyewe.

As long as mashoga hawanilazimishi mimi niwe shoga, sitaki kuwalazimisha wawe straight.

Hao wazungu/ wamagharibi wanaojidai wana mind sana haki za binadamu kuna namna ya kuwabana, lakini sijasikia bado kiongozi wa kiafrika akiwabana inavyotakiwa.

kwa mfano, sijawahi kusikia kiongozi wa Kiafrika akisema sisi kwetu Afrika mwanamme anaweza kuoa wake wawili au watatu au wanne (waislam) au hata zaidi katika mila zetu. Kwa nini nyie mnatukataza kuoa wake wawili na zaidi tukiwa kwenu?

Angalia ukewenza ulivyo kosa katika nchi nyingi za magharibi

Bigamy - Wikipedia, the free encyclopedia

Sasa kama mtu anataka kukataa cultural imperialism, kupewa utamaduni wa kuufuata, hili swali kama pale kwenye interview ya Kikwete na Amanpour ndipo lilikuwa sehemu yake.

Ningekuwa mimi Kikwete ningemuuliza Amanpour, haya mambo ni mambo ya utamaduni, mbona huku kwetu Afrika mwanamme anaweza kuoa wake wengi kisheria (rais wa South Africa ana wake zaidi ya mmoja, Rais Mwinyi alikuwa na wake wenza, mfalme Mswati ndiyo usiseme tena) halafu huko kwenu Marekani na Ulaya kuwa na wake wengi ni kosa la jinai na sisi hatuwalazimishi msilifanye kosa?

Kama mnataka kuhalalisha ushoga kwetu, basi na kwenu halalisheni ukewenza tujue mnachotaka si kututupia tamaduni zenu tu, bali mnataka kwenda na a progressive world (progressive in the sense kwamba mtu mzima yeyote asipangiwe cha kufanya )

Kwa hiyo kuna namna ya kuhoji haya mambo in a statesmanlike manner, sio Kikwete anaulizwa wewe unaonaje anajiumauma kama kigoli aliyejaa haiba.

Mimi ningekuwa na uamuzi, mtu mwenyewe awe na uamuzi wake. Akitaka kuwa shoga kivyake. Mwanamme akitaka kuoa wake kumi na nane kivyake. mwanamke akitaka kuolewa na wanaume kumi na nane kivyake. Mradi mtu mzima asipangiwe maisha.

Na huko Marekani wanakojifanya maliberali waruhusu wanaume kuoa wake wengi. na sie tunaotaka kuanzisha vyama vya kikomunisti Marekani tupewe uhuru wa kufanya hivyo.

Sio Mmarekani anajifanya mpenda uhuru wakati mtu hawezi kuoa wake wawili, au kuwa mwanachama wa chama cha Kikomunisti.

Hawa viongozi wa Afrika utawasikia sana kuongelea mambo kama haya ya ushoga kwa sababu hawana kingine cha kuongea.

Ukiwapeleka kwenye uchumi, elimu, maendeleo wengi wao ni failures.
 
aaaaah subiri kwanza wewe ushoga unauonaje....
Kwani ushoga ni nini?
Mbona wanaume kibao wanawafanya wake zao kinyume na maumbile hamuoni kama ni kitu cha ajabu?
Kuonyesha kuwa waafrika akili zina hitlafu, wanamuona shoga ni muovu kuliko mwizi na hata muuaji.

Mijadala kibao ilishafanyika bungeni kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo ufisadi na vitu kem kem, lakini Wenje alipoibua hoja kuwa chama kimoja cha siasa nchini, itikadi yake inatambua haki za mtu mmoja mmoja wakiwemo mashoga moto uliwaka haijawahi kutokea, Wenje akazuiwa kusoma hadi atoe hicho kipengele. Mwandishi Ezekiel Kamwaga alishawahi kuuliza katika makala zake iwapo ushoga ni mbaya kuliko ufisadi.

Ni ufinyu wa fikra unaoashiria hitlafu katika akili kuamini kuwa ushoga ni jambo baya kuliko yote katika nchi na ni kitu ambacho watawala wanatakiwa kutoa kipaumbele katika kupambana nacho.
 
Nafikiri unajua kusoma so acha kulazimisha ambayo sijaandika na pia sina tatizo na ndoa za mashoga
Sasa si ungesema tu kuwa unaunga mkono hizo ndoa kuliko kuzungu zunguka bila mpango au na wewe muoga??!! Unaogopa hadi huku kwenye keyboard!!!!
 
Mkuu Kiranga, waafrika tutaendelea kuwa wa mwisho kwa kila kitu hadi kiyama kwa sababu inawezekana kabisa akili zetu zina hitlafu.
Hiyo kauli ina nini cha maana hadi isifiwe?, bora hata angejenga hoja nzuri juu ya huo ushoga anaopinga kuliko kutoa kauli ya kipuuzi tu isiyo na staha, Ni ajabu kwa mpinga ushoga kutaka kuonyesha mfano kwa kuoa mwanaume mwenziye halafu wapinga ushoga wenzie wakashangilia.

Kweli huyu jamaa amewateka akili watu wa kauli za kipuuzi tu zisizokuwa na tija yeyote kwa taifa lake.
We huwezi kumwelewa mtu kama Mugabe labda uingie darasani kwanza!!! Kuna kauli huwa zinaeleweka na waliokusudiwa tu, ndio maana wanaomuunga mkono wamemwelewa. Wewe kakaa pembeni waachie yao hao.
 
Duh,

Nilivyokuwa namjibu Mjuni Lwambo nilikuwa sijakusoma mkuu.

Sasa napitia posts za karibuni naona kwamba kumbe hili swali la authenticity ya hii habari si langu tu, kuna wengine wameliona.

Hatuwezi kupewa habari tu tukaimeza nzima nzima bila kuichunguza kama ni ya kweli au vipi.

Nimegoogle combinations kadhaa za hii habari sijaona lolote zaidi ya vi blog, vi website vya wanaija na twitter/ facebook.

Kama hii habari si ya kweli, itadhihirisha jinsi watu walivyo rahisi kuamini mambo bila kuthibitisha.
Kiranga bwana, umeimeza kwanza ndio unakumbuka ku-google, kwa hili mtu wako Ngabu yuko sahihi kuwa "miafrika ndivyo tulivyo" teh teh teh!
 
Hata kama hakuna chanzo cha uhakika cha hii habari, binafsi sitashangaa sana kama ikiwa ni kweli kwa sababu Mugabe ni mtu wa kurusha madongo sana hususan dhidi ya viongozi wa nchi za Magharibi.



Siyo Waganda tu. Hata Wabongo. Hivi umeona anavyopewa heko na watu humu JF? Halafu cha kushangaza zaidi ni kwamba anaungwa mkono mpaka na wanawake (at least kulingana na IDs zao humu na jinsi wanavyojiwasilisha).

Ndo maana nimekuwa nikisema kwamba Waafrika wengi sana ni wepesi wa kuhadaiwa na kuvutika. Jambo dogo tu hawakawii kukupachika sifa kede kede...'fulani ni kichwa'....'fulani ni jembe'.

Viwango vyetu ni vya chini sana sisi.
Kwa hiyo kutohadaiwa ni kukubaliana na kile unachofikiri wewe kuwa ni sahihi??!!! Kama wanawake wanamuunga mkono wewe unashangaa nini?? Umeambiwa kuwa wanawake wote ni lazima waunge mkono uvaaji wa vimini??!! Kwani kama unaona kuvaa chupi barabarani ni sawa, kuna tatizo gani mwingine akiona si sawa?? Iweje utake watu wote wawe na maoni kama yako??
 
Mwana wa Ngabu, mimi huwa naenda mbali sana hadi kudhani kuwa labda waafrika tuna hitlafu katika akili zetu.
Hebu fikiria tu hata hilo la nguo fupi, mtu anaitwa shujaa eti kwa kuzuia mtindo fulani ya mavazi!!, Ndiyo. Kwani nguo fupi ni nini hasa zaidi tu ya mitindo ya mavazi!??, ndio ushujaa wa Afrika huo!??, hivyo tu!!!.
Inawezekana kweli una hitilafu kichwani. Ninyi watu mna tatizo gani na watu kuamua jinsi ya kuishi katika jamii??!!! Kama hampendi si mseme tu, eti tuna hitilafu!!!
 
Kiranga bwana, umeimeza kwanza ndio unakumbuka ku-google, kwa hili mtu wako Ngabu yuko sahihi kuwa "miafrika ndivyo tulivyo" teh teh teh!

Nimeimeza wapi? Umesoma hiyo post yangu ya kwanza? Umeona nilichoandika ni nini na kinachotiliwa shaka ni nini?

Unataka kudandia rocket launcher kwa mbele?
 
We huwezi kumwelewa mtu kama Mugabe labda uingie darasani kwanza!!! Kuna kauli huwa zinaeleweka na waliokusudiwa tu, ndio maana wanaomuunga mkono wamemwelewa. Wewe kakaa pembeni waachie yao hao.
Mimi Mugabe namuelewa, ni mjanja tu,
Anajua ukitaka kuwawini waafrika we pinga wazungu, vitu kama ushoga nakadhalisha, baasi. Hauhitaji kuumiza kichwa.
Niambie kama kuna kitu kingine ambacho wewe unampendea Mugabe zaidi ya kupinga wazungu na ushoga, sema!!
 
Mimi Mugabe namuelewa, ni mjanja tu,
Anajua ukitaka kuwawini waafrika we pinga wazungu, vitu kama ushoga nakadhalisha, baasi. Hauhitaji kuumiza kichwa.
Niambie kama kuna kitu kingine ambacho wewe unampendea Mugabe zaidi ya kupinga wazungu na ushoga, sema!!
Mimi wapi nimesema nampenda mugabe?! Pili kuna ubaya gani kuwapinga wazungu kama wanakosea?? We ulitaka awasifie tu kama unavyofanya wewe?? Kuwasifia wazungu ndio akili?
 
Nimeimeza wapi? Umesoma hiyo post yangu ya kwanza? Umeona nilichoandika ni nini na kinachotiliwa shaka ni nini?

Unataka kudandia rocket launcher kwa mbele?
Naona ukisikia rocket launcher unaogopa sana, ila kwa bahati mbaya wewe ndiye umeidandia. Wewe kule juu si umechangia kwa kuwananga waafrika, halafu baada ya kuona watu wanahoji eti na wewe unajidai umeliona hilo. We kubali tu umekumbuka shuka asubuhi. Tatizo lako unadhani huwezi kukosea.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom