Ukisoma Asia unarudi Bongo na stress tu

Ukisoma Asia unarudi Bongo na stress tu

Watanzania wengi waliosoma vyuo ambavyo vipo nchi za Asia wana msongo wa mawazo/stress, umaskini wa mali na akili mwisho hufa maskini.

Mfano wa hizo nchi ni kama Japan, China , India, Korea etc ambazo lifestyle yao kuanzia vyakula, malazi, socialization nk ni tofauti sana na Afrika/Bongo.

Nimeshuhudia vijana wanarudi na electronic appliances, vigari na simu tu kama faida ya kuwa huko. Mbali na hazo wengi huwa ni watu wenye jazba, tension, woga, msongo wa mawazo na kuogopa ogopa kufanya maamuzi.

Angalia watu waliosoma US, UK, Canada, Australia wako tofauti kabisa. Hata hawa viongozi wetu wewe wachunguze tu.

Hawakai chungu kimoja.

Asia twendeni tukatembee tu, siyo kula kitabu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mtoa Mada unachosema kinaweza kuwa na ukweli kama itatokea mwanafunzi husika ameenda chuo feki... Katika maeneo uliyotaja.

Kwa mfani India pekee ina vyuo fekia zaidi ya 14,000(yani elfu kumi na nne) Sasa pale inapotokea umekosea ukaenda huko lazima ukirudi ulie... Kwa ushauri ingekuwa ni vizuri sana kama wahusika waotaka kwenda kusoma huko wakafanya research kuhusu chuo husika.

Kusoma vyuo vya nchi za Asia kunafaida kubwa moja ya faida ni kusoma Short courses inayo husiana na degree yako kwa gharama ya chini tofauti na nchi za ulaya, ambapo kama unaakili itakupasa ukomae na zile ambazo hazipo Bongo... Ili ukirudi pamoja na degree yako uwe na potential zaidi.

Inakupasa kuwa makini kwenye kuchagua vyuo... Hata UK pia vyuo feki vipo.

Bongo stress tunaishi nazo kama hujiongezi itakula kwako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii elimu yao inabidi ichunguzwe wanawafundisha nn raia wa kigeni hadi wanakuwa mazwazwa lakini ,hadi vyakula wanavyokula watu wetu vichunguzwe, tusiwalaumu xana raia wetu labda nao hawajui wanapewa makitu gan hadi mtu unakuwa na Phd au Masters lakin unapigwa mkwara mdogo unatulia
 
Double P
Nina rafiki yangu anasemaga akifanikiwa kupata scholarship ya kusoma nje ya Tanzania hata kama ni 'sudan', ndio harudi tena Tanzania[emoji4][emoji4].
Nimesoma hii nikamkumbuka, nikahisi ikitokea ikashindikana kubaki akarudishwa Tz ataungana na 'hao' wenye stress kwa sababu malengo yake yatakuwa hayajatimia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyie ndugu punguzeni tabia isiyofaa. Tujenge tabia ya kutiana moyo. Nachukulia mfano hapo kwetu Tanzania, kuna baadhi ya wanafunzi hufeli ktk level tofauti tofauti, kuanzia elimu ya msingi, form two, form four, form six na hata vyuo watu wana disco ktk shule na vyuo tunavyoamini ni bora, kinachofanyika watu hutafuta namna rahisi zaidi ya kuendelea ndiposa wanatafuta vyuo mbadala au shule inayoweza kumchukua,kuna shule mbovu sana huko nyumbani, kuna vyuo vibovu sana huko nyumbani tena taasisi hizi nyingi ni za private, wao wanajali sana pesa. Vivyo hivyo hata huku China, kuna vyuo vya namna hiyo, unakuta karo ni ndogo na elimu ya hovyo, vinazoa kila mtu hii ipo hasa kwa wanafunzi wanaosoma undergraduates wengi vyuo sio vizuri.Hii haina maana kwamba China nzima wanatoa elimu mbovu,hapana. Mimi nikilinganisha elimu niliyopata huko bongo na hapa hasa ya vitendo, huku wamepiga hatua sana huenda mara 4 na zaid,tatizo ninaloliona kwa post graduates, kama utasoma kizembe, walimu hawana shida kabisa watakuacha umalize,urudi nchini kwako ila kwa wanafunzi wao wako very strick hawana mchezo,lakini kama ukiamua kusoma kwa bidii, kwanakupa support yote, utapata kila kitu na utajua vitu vingi sana. Watu wengi wamemaliza elimu za masters ulaya mfano Norway, Uholanzi hata marekani hawajui hata kuandika scientific papers wala hawajwahi kupublish kazi yake aliyowahi kuifanya hata ukimuuliza Sci. ni nini hajui kabisa.Mimi najivunia kusoma nchini China. Kuna issue ya kurudi nyumbani ukiwa na hela au unarudi bila kitu, kabla ya kwenda kusoma nchi yoyote lazima ufikiri sana unaenda kwa sababu unataka kwenda kusoma na umepata ufadhili wa kusoma elimu ya juu au unaenda kutafuta pesa. Swali hilo litakuongoza kuchagua nchi ya kwenda. Kwa china baadhi ya majimbo watu wanaruhusiwa kufanya kazi, pengine wanaruhusiwa kufanya kazi na kuishi mpka miaka minne baada ya kuhitimu (yaani hawawezi kukupa visa ya kazi na ya kusoma pamoja, lazima ucancel mojawapo). Ukija kusoma huku unawaza pesa unaweza kurudi nyumbani umechanganyikiwa. Kuna vijana wengi wamefanikiwa kwa kufanya biashara kati ya China na DSM, wengine wana makampuni n.k . China ina vyuo vikubwa tu bora mfano Tsinghua University, Peking University n.k elimu bora inaambatana na maendeleo, tujipime maendeleo yetu na China kisha turudi kudharau elimu yao.
 
Nyie ndugu punguzeni tabia isiyofaa. Tujenge tabia ya kutiana moyo. Nachukulia mfano hapo kwetu Tanzania, kuna baadhi ya wanafunzi hufeli ktk level tofauti tofauti, kuanzia elimu ya msingi, form two, form four, form six na hata vyuo watu wana disco ktk shule na vyuo tunavyoamini ni bora, kinachofanyika watu hutafuta namna rahisi zaidi ya kuendelea ndiposa wanatafuta vyuo mbadala au shule inayoweza kumchukua,kuna shule mbovu sana huko nyumbani, kuna vyuo vibovu sana huko nyumbani tena taasisi hizi nyingi ni za private, wao wanajali sana pesa. Vivyo hivyo hata huku China, kuna vyuo vya namna hiyo, unakuta karo ni ndogo na elimu ya hovyo, vinazoa kila mtu hii ipo hasa kwa wanafunzi wanaosoma undergraduates wengi vyuo sio vizuri.Hii haina maana kwamba China nzima wanatoa elimu mbovu,hapana. Mimi nikilinganisha elimu niliyopata huko bongo na hapa hasa ya vitendo, huku wamepiga hatua sana huenda mara 4 na zaid,tatizo ninaloliona kwa post graduates, kama utasoma kizembe, walimu hawana shida kabisa watakuacha umalize,urudi nchini kwako ila kwa wanafunzi wao wako very strick hawana mchezo,lakini kama ukiamua kusoma kwa bidii, kwanakupa support yote, utapata kila kitu na utajua vitu vingi sana. Watu wengi wamemaliza elimu za masters ulaya mfano Norway, Uholanzi hata marekani hawajui hata kuandika scientific papers wala hawajwahi kupublish kazi yake aliyowahi kuifanya hata ukimuuliza Sci. ni nini hajui kabisa.Mimi najivunia kusoma nchini China. Kuna issue ya kurudi nyumbani ukiwa na hela au unarudi bila kitu, kabla ya kwenda kusoma nchi yoyote lazima ufikiri sana unaenda kwa sababu unataka kwenda kusoma na umepata ufadhili wa kusoma elimu ya juu au unaenda kutafuta pesa. Swali hilo litakuongoza kuchagua nchi ya kwenda. Kwa china baadhi ya majimbo watu wanaruhusiwa kufanya kazi, pengine wanaruhusiwa kufanya kazi na kuishi mpka miaka minne baada ya kuhitimu (yaani hawawezi kukupa visa ya kazi na ya kusoma pamoja, lazima ucancel mojawapo). Ukija kusoma huku unawaza pesa unaweza kurudi nyumbani umechanganyikiwa. Kuna vijana wengi wamefanikiwa kwa kufanya biashara kati ya China na DSM, wengine wana makampuni n.k . China ina vyuo vikubwa tu bora mfano Tsinghua University, Peking University n.k elimu bora inaambatana na maendeleo, tujipime maendeleo yetu na China kisha turudi kudharau elimu yao.
Asilimia 99.7 ya Watanzania wanaosoma China husoma vyuo vya ajabu. Peking unaweza kuta watz 3 au hakuna kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katika mahala ambako shule inapigwa hapa duniani ,INDIA ,KOREA na CHINA huwezi ukaziacha kwenye list,Huko nje inategemea umeenda kusoma chuo gani,india wana INDIAN INSTITUTE OF TECHLONOLOGIES hizo vyuo ni world class na wengi wakimaliza hapo wanakimbilia USA wengi ni ma CEO wa makampuni makubwa ,Nenda NASA,GOOGLE ,APPLE hakuna mahala utamkosa muhindi tena kwenye Vitenge,
Ndio maana tukiugua maradhi yakishindikana hapo muhimbili kwenye elimu ngumu tunakimbilia INDIA,CHINA nk Elimu ipo huko ila inategemea umefuata nini

Sent using Jamii Forums mobile app
Tunakimbilia India kwa aababu being in ndogo, ulaya tiba ipo juu
 
Wadada waliosoma China wamekua slay queens tu insta. Trips za hong kong nyingi wakirudi bongo hamna wanachojua. TZ Ukiondoa Kampala University Dar es salaam hakuna chuo kinachukua failures. Failures wote wapo China na India.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hivi unajua utaratibu wa kuingia chuo chochote na ukasoma MD au unachangia mada kuchangamsha gengee??
 
Masters yangu nitachukulia kati ya Nchi ya Norway au Sweden basi!
Umenena mkuu, kuna kipindi nilitaka nichukue masters ya accounting pale mzumbe nikakuta waalimu wataotufundisha nao wameishia masters za hapa hapa hawana phd vyuo vya bongo, yaani kiufupi nilipchunguza nikaona hakuna utofauti wa masters na anaesomea degree..,,,Ikija tokea nimesoma masters basi itakua ni ulaya (uk, noway ama sweden), marekani au makerere ...FULLSTOP!!!
 
Ivi nifafanuloeni apa ukisoma certificate apa bongo unaweza soma chuo chochote nje ya nchi ?
Mie mzazi Nina mwanangu kamaliza form 4 mwaka wa jana ana d 8 ya f ya commercia na Arabic anataka kusomea account ebu nielewesheni kwa uelewa wenu Nina ndoto akasome nje ya nchi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom