Ukisoma Asia unarudi Bongo na stress tu

Ukisoma Asia unarudi Bongo na stress tu

Nafikiri hapa wachangiaji wengi hamjaelewa nini hasa mnachokiongelea. Huko China na India kuna makundi mawili ya wanafunzi wa kitanzania.

1: Wanaokwenda kwa udhamini binafsi

Hawa huwa wanaunganishwa vyuoni kupitia hizi taasisi zilizofurika mitaani. Mimi pia nina mashaka kiasi fulani na ufaulu wao. Na wengi wao huwa ni undergraduates (Shahada ya kwanza) kama sio wote.Hawa binafsi naomba serikali pia uwamulikie jicho kali kuangalia vigezo kama vinafikiwa.

2: Wanaokwenda kupitia ufadhiri wa nchi husika na organizations kubwa duniani.

Hawa wengi wao huwa wanaufaulu mkubwa maana mchakato wa kuwapata huwa unazingatia ufaulu wa mtahiniwa (pia wapo viazi wanaobebwa kwa kujuana) na huwa wanakwenda vyuo vya serikali na vyenye heshima, mara nyingi huwa ni graduates (yaani masters na PhD). Binafsi sina mashaka sana na hawa.

Elimu katika kila nchi inategemea na aina ya chuo utakachokisomea, vyuo vingi vya private wanajali maslahi tu wakati vya serikali vinapambana zaidi kulinda heshima yake na kuendelea zaidi. Hivyo mleta mada yupo sahihi kwa asilimia fulani lakini pia hayupo sahihi kwa asilimia kadhaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom