UK Visas To Be Processed In Nairobi

Hata Ubalozi wa Canada wana utaratibu wa kupeleka Passport Nairobi kwa ajili ya visa stamp,lakini huduma yao ni ya haraka zaidi,inachukua siku tatu passport inakuwa imekwisharudishwa Dar.
 
Nasubiri wasabato wakikwea pipa bila papers najiunga kanisani kwao sina haja ya kwenda Nairobi.
 
Tunako kwenda itabidi baadae kwanza Passport zote zitumwe kwa Malkia kisha yeye ndio aseme umepata visa or no.

Lakini all in all hawa jamaa wana kila haki ya kubana mfumo wao mzima wa visa. Mimi naangalia kutoka kwenye conservatism point of view, Wahamiaji wengine wametumia hizi loop hole kuabuse visa. Hii includes kuzamia, kwenda nchi za watu na kujiingiza kwenye welfare, na mengine mengi.

Uncle Sam is gonna getchu
 
Hii naona sio kitu cha ajabu, 2 years ago Kenyans nao walikuwa wanprocess Visa za USA kupitia ubalozi wa Dar sasa hivi sijui kama hiyo process inaendelea. Kikubwa ni efficiency ya kutoa visa yao na gharama hasa kwa upande wao tho kwetu ina-matter but wao ndio wauzaji hivyo wanajifikiria wao kwanza.
 
Mimi sina haja ya kwenda kwao. Kwani nakwenda kutafuta nini wakati nina kwetu?
Nikitakwenda mbali nakwetu nakwenda Mtwara au Lindi au Songea. Je huko pia nahitaji wiki 6 ili niruhusiwe kwenda?
Come on nyinyi waingereza msitusumbue vichwa. Hata mkisema mnatoa visa kwa miaka 10 hakuna shida. Poleni mnaotaka kwenda UK sasa ni wakati wenu wa kubadilisha mawazo au vipi?
 
Malipizo ya obama ni ni kazi kweli kweli!!!
Ukate tiket mpaka nairobi jmani ukakose 's
 
Watu wa Ulaya washenzi sana wanazidi kuongenza masharti ya sisi kwenda kwao!wanatumia umaskini wetu kutunyanyasa!wanafanya hivyo kwa sababu wengi wanaokwenda huko ni kutumia resources za wazungu!wenzetu wakija huku ni kuwekeza!halo halo na bado WAZUNGU ongenzeni masharti hadi hawa waafrica wajifunze kujitgemea wamezidi kila kitu wanataka waende ulaya!kusoma ulaya!kwenda kusafisha vyoo na kuosha vibibi ulaya!
 
We might give it names but may be we are using our system as a bench mark! This is a wrong approach, you can't use an inefficient system like the one we have in Tz to set pace for others.

Restructuring of systems is a common thing and I don't think there is a problem as long as the new system is just as efficient as the old one. We don't need to ask why Nrb and not Dar because even Kenyans would be asking the same questions if it was the other way. But if you listened to the Officer, NRB has more applicants than Dar!

kama NRB wana applicants wengi kuliko hapa... kwa kupeleka kule huoni kuwa ndio wanacomplicate ndo matokeo ya kuchukua muda mrefu???

hiyo inefficient sys unayoiongelea ni ya inchi au ya wao??? sisi kuwa na inefficient sys haiwazuii wao kufanyakazi yao....labda uniambie ni kwa muda tuu ni takuelewa lkn kama ndo for good basi hiyo haiko sawa.. maana ada pekee ni kubwa sana plus kusafirikwenda nrb na huna uhakika wa kupata hivo visa yenyewe...

nasikitika sana watz na serikali yetu kwa kuwa maboga (kama nitakuwa sijaa muumiza mtu) wao wakija hapa wanajazia form pale airport na kuilipa ADA KIDOGO.. tofauti na kwetu... jamani watu hawa wanatuchezea nchini mwetu huku tukiwachekelea..
 
Muhimu hapa wasiongeze gharama za visa tu. Ikiwa wataweza gharama za kuDHL hizo passport hapo sasa ndio noma vinginevyo ni sawa tu kilichoongezeka hapo ni muda tu.

Jamani waombaji hawatahitajika kwenda NRB process zote ni Dar
 
Muhimu hapa wasiongeze gharama za visa tu. Ikiwa wataweza gharama za kuDHL hizo passport hapo sasa ndio noma vinginevyo ni sawa tu kilichoongezeka hapo ni muda tu.

Jamani waombaji hawatahitajika kwenda NRB process zote ni Dar

Masatu, hawa jamaa huwa wanataka applicants kufanya mahojiano ambayo mara nyingi huwa ya ana kwa ana, kama utaratibu huo utaendlea basi kabla ya kupata visa itawapasa waombaji waende Nairobi kwa mahojiano.

Kaazi kwelikweli, safari ya UK utadhani ni ya kwenda mbinguni!
 
Masatu, hawa jamaa huwa wanataka applicants kufanya mahojiano ambayo mara nyingi huwa ya ana kwa ana, kama utaratibu huo utaendlea basi kabla ya kupata visa itawapasa waombaji waende Nairobi kwa mahojiano.

Kaazi kwelikweli, safari ya UK utadhani ni ya kwenda mbinguni!


Ibrah isome tena taarifa hakuna mahala afisa aliposema habari kwenda NRB ila maombi yatakuwa online na process zitafanyika Dar wakati last procedure (ie stamping) ndio Nairobi.

kumbuka mambo ya interview wanaya phase out na wanafunzi hawana interview siku hizi zinazungumza karatasi tu
 
Masatu, hawa jamaa huwa wanataka applicants kufanya mahojiano ambayo mara nyingi huwa ya ana kwa ana, kama utaratibu huo utaendlea basi kabla ya kupata visa itawapasa waombaji waende Nairobi kwa mahojiano.

Kaazi kwelikweli, safari ya UK utadhani ni ya kwenda mbinguni!

Ibrah siku hizi hakuna mahojiano hata kidogo mwakajana niliomba na mwakahuu tena ni j3 iliopita na zote nilipata hata sikuhijiwa na mtu isipokuwa na docs zako tu zinaongea
 
Naona watu wamepanic.....Hakuna kusafiri kwenda Nairobi ila kugongewa visa ndio PASSPORT zinapelekwa Nairobi....isijekuwa watu walikuwa wanajaribu kutengeneza kanjanja lol.
 
HIVI this kind of colonial-master behavior will ever come to an end.

Kwani ni lazima twende Uingereza. Hatuwezi kufanya jambo ambalo litawaonesha sisi hatuna shida nao hata kidogo.

Kwa mfano, kila Mtanzania akilenga kumpeleka mtoto wake kusoma Uchina, Uarabuni, India, Korea kusini, Japani, Malaysia, Australia, New Zealand jamaa wataendelea kutunyanyasa hivi kwa visa kweli?

Waingereza wanatufanyia dharau ya wazi kwa kuona sisi masikini, wenye shida, tunawahitaji wao. Na wao eti hawatuhitaji sisi. Ni ushuuuzi tu kwao!


Kama ndio hivyo tukae mkao wa Rwanda basi. Kwanza, tuamue kuwa lugha ya kufundishia sasa ni Kijapani na Kiarabu.

Lugha zinazofuatia ni Kihindi, Kichina, Kireno na Kihispania halafu Kiarabu.

Na lugha ya shughuli zote za kitaifa na kimataifa ikiwa kupata cheti cha chekechea hadi Chuo Kikuu ni Kiswahili au Kizaramo au Kinyamwezi au Kigogo au.....


TUONE MPAKA hapo kama ni wao waingereza watatuhitaji sisi au sisi ndio tutawahitaji wao!!!


HAPA wanataka kutuambia wenzao ni Kenya na sisi ni watumwa tu kwao!

Wafanya kama vile Microsoft walivyofanya kuwatumia Watanzania kuandaa software zake kwa Kiswahili na kisha kuzipa software hizo hadhi na heshima ya kwamba ni za Kenya na sio Tanzania. Upuuzi mtupu!!!
 
Akili,
Mambo si marahisi kiasi hicho kwa kubadili lugha. Pia Kiingereza si maarufu kwa sababu ni lugha ya UK. Ni maarufu kwa sababu ni lugha ya Marekani (USA). Nafikiri kama Mrusi angelishinda basi leo hii tungelikuwa tunasema KHARASHOO wote hapa. Kitu kingine lazima ujuwe kuwa Kiingereza ndiyo official lugha ya Europian Union. Kwa wale wanasema tujifunze Kijeruman, basi wajue hata Wajeruman wenyewe sasa inabidi wajue Kiingereza maana hayo ma EuroCode na takataka nyingine yanakwenda kwa Kiingereza.
Labda ni vema wanaanza kuwa wakali. Kwenye nia pana njia. Mwisho wa kudekezwa watu duniani unakwisha. Hata wao kubebana sasa mwisho. Wameshaanza kusema ni lini wataacha kuwapa pesa za bure wakulima, makampuni, mashirika nk ili yapunguze uzalishaji na kuweka bei ya bidhaa kuwa chini sana.
Ila kwa upande mwingine, Tanzania kuna kitu kibaya kinaendelea. Tunajiona wakali sana lakini Kenya wanatufunga magoli. Juzijuzi nilisikia kuwa hata nchi kama Poland wamefunga ubalozi wao Tanzania na sasa ukitaka VISA badi inabidi uende wapi???? Nairobi - KENYA. Tusubiri na nchi nyingine iseme kufuta VISA inabidi uende Nairobi. Kama tungelikuwa na uchumi imara, na maendeleo ya kutosha kama tunavyofikiri ingawa sivyo, hawa jamaa wasingelifunga au kupunguza nguvu ya hizi balozi zao. Nafikiri kinachofanyika sasa ni kubana matumizi. Watapunguza wafanyakazi nakuwaweka sehemu moja. Ila hii itatokea sehemu ambazo kwao hazina umuhimu sana. Sidhani kama watafanya hivyo South Africa, Japan, Korea, Hong Kong, New Zeland nk. Hata kama ni mie inabidi nibane matumizi kutokana na hali ngumu ya uchumi wa dunia, Tanzania naanzia bila wasiwasi ingawa ni kwetu. Haya, tuache uvivu twende kazini tubadili heshima ya Tanzania duniani.
 
Acheni ku-panic! Mambo yakawaida haya!

Hapa ninapoishi, whenever I apply for UK Visa, natumia process kama ya japo juu, na kuipata si chini ya wiki moja, sasa tatizo liko wapi! Tulieni vijana!

Kisura kabla ya haya mabadiliko visa ilikuwa inapatikana kwa siku tano tu, sasa ni wiki sita. Kwa maoni yangu hii ni kuongeza bureaucracy na gharama kwa waombaji hasa ukitilia maanani wataotakiwa kufanyiwa interview itabidi waingie gharama nyingine za kwenda Nairobi ambazo kabla ya mabadiliko hazikuweko.
 
Ukweli ni kwamba....Sio kama Kenya imeendelea kuliko TZ, Wakenya ni wachapa kazi sana. They get things done. Watanzania tumezidi uzembe. Kazi ya siku moja TZ inafanywa kwa wiki mbili. Hongo mbele....Mafisadi nao....ndio hivyo tena......
Hawa wazungu wana haki ya kutuweka benchi na kuchukua wachezaji bora.
Kama TZ tutarekebisha myenendo yetu kikazi....then ....tutakuwa na argument
ya hii topic.......otherwise......tulie tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom