Kubota na co salaams, sisi tupo tunaendelea vizuri tu. Ukipita nymba yenye makelele ukaona kimya ujue tunakula! Sasaivi tunaongelea masoko kule kulikuwa na uzi wa Eliphas. Masoko ya reja reja ni ya kubahatisha. Wateja wangu wote wa kuku wa kisasa wanajibu kama kasuku "nitafute ukiwa na kuku 400 kuendelea....' wakati mie nauza jogoo 10 au 20 kufanya kuwapunguza tu ila nimecheck soko liko poa sana tu. Kingine wengi wanawataka kwa ajili ya kufuga na hivyo wanangangania tetea wasioanza kutaga sasa kwa vile hii ni stock ya kwanza imebidi niwanyime. Kuhusu Chakula cha vifaranga mimi sijaka tama na endapo nitachukua vifaranga karibuni nitajaribu hata ikibidi nihamie mashine nijifunze mbona wengi hawana uchoyo ni sisi tu kukosa mtaji mkubwa wa kusaga chakula kingi na kupenda kununua mfuko kila ukipata kidogokidogo. Niwatakie siku na kazi njema
Mama Timmy, Mama Joe, Asigwa, LiverpoolFC, Guta, n.k, upweke umenizidi, mko wapi wakubwa? Feedback zije wajameni!
 
hahaaaaaaaaa umenikumbusha mbali kweli mimi mbwa wamefugwa nyumbani utotoni sikuwa karibu nao sana. Nilipoanza kufuga mtu alimpa motto wangu kambwa kadogo kiasi kwa kweli sikuwa na mind kanakula nini hasa ingawa dagaa wanakanunulia nilichokuja shtuka kukuta miguu ya kuku nyuma ya banda ilibidi nikarudisha fasta. Kweli inabidi utafute mbwa mzuri sio kila mbwa anafaa.
Asante sana,dog nlpata mdogo akala kuku akazaa watoto nao wakala kuku,nkawachapa usku wanenda kuvnja mabanda ya majiran
 
Wakuu wote (Kubota, Mama-Timmy, Mama-Joe, Asigwa, LiverpoolFC, Guta, n.k, n.k, n.k); Jamani Mwenyezi Mungu awabariki sana sana sana. Wajasiriamali tunaelimika sana.
Mie nilitaka nikasome certificate ya vet ili niweze kufuga kuku wa asili/kienyeji vizuri, lakini kwa kusoma uzi huu, pamoja na nyuzi nyingine hapa JF, basi mie ni mfugaji bora sasa wa Kuku wa asili/kienyeji.
Narudia tena. Mwenyezi Mungu awabariki sana.
 
Wadau nataka kumuanzishia mama mradi wa kuku wa kienyeji. Napataje breed nzuri ya hao kuku?nimeskia hapa watu mnataja mbegu za kiisrael,ndo nawapata wapi hao?
 
Mama Timmy, Mama Joe, Asigwa, LiverpoolFC, Guta, n.k, upweke umenizidi, mko wapi wakubwa? Feedback zije wajameni!
Tupo mkuu hatujapotea tupo sana aisee...nilikuomba unitag kwenye uzi mpaka leo hujanitag mkuu..ndio maana someties inakua kazi kuufuatilia na kutoa mrejesho wa uzi...

Ubarikiwe lakini katika kila ulifanyalo mpaga uduwae...
 
Mama Timmy, Mama Joe, Asigwa, LiverpoolFC, Guta, n.k, upweke umenizidi, mko wapi wakubwa? Feedback zije wajameni!
Kubota kaka yangu natumai umzima wa afya!kwa upande wangu namshukuru Mungu kwa afya na hatua nipigazo kila siku ktk maisha yangu.kuku wangu wanaendelea vzr na kwa sasa niko kwenye zoezi la kutotolesha kwa kutumia kuku wachache mara mbili.changamoto ni nyingi sana ila na jaribu kuzigeuza kuwa ni shule kwangu.
 
Kubota na co salaams, sisi tupo tunaendelea vizuri tu. Ukipita nymba yenye makelele ukaona kimya ujue tunakula! Sasaivi tunaongelea masoko kule kulikuwa na uzi wa Eliphas. Masoko ya reja reja ni ya kubahatisha. Wateja wangu wote wa kuku wa kisasa wanajibu kama kasuku "nitafute ukiwa na kuku 400 kuendelea....' wakati mie nauza jogoo 10 au 20 kufanya kuwapunguza tu ila nimecheck soko liko poa sana tu. Kingine wengi wanawataka kwa ajili ya kufuga na hivyo wanangangania tetea wasioanza kutaga sasa kwa vile hii ni stock ya kwanza imebidi niwanyime. Kuhusu Chakula cha vifaranga mimi sijaka tama na endapo nitachukua vifaranga karibuni nitajaribu hata ikibidi nihamie mashine nijifunze mbona wengi hawana uchoyo ni sisi tu kukosa mtaji mkubwa wa kusaga chakula kingi na kupenda kununua mfuko kila ukipata kidogokidogo. Niwatakie siku na kazi njema
Safi sana mwanamke hapaswi kukata tamaa Kirahisi.ninaamini safari hii unamaliza mchezo nasi tutajifunza kupitia kwako.nakutakia mafanikio makubwa.
 
Mkuu asante sana kwa kutujuza. Hapa tena tunashuhudia jinsi feed back ilivyokitu chenye thamani kubwa kwenye kuelimishana. Asante mkuu kwa kushea nasi uzoefu huo, kuanguka daima ni darasa kubwa na hasara ni ada ya shule. Kusema kweli sijawahi kufuga chotara ila niliwahi kuwaona chotara wa broiler kwa jirani yangu, ukweli kuku walikuwa wanakua kwa kasi kubwa sana kuliko kuku wa kikwetu lakini ukweli unabaki pale pale kwamba kuku halisi wa kienyeji wanahimili mikiki mikiki kuliko kuku wa kisasa na chotara. Ukweli umeuona mwenyewe, hata hivyo ukiwamudu kuku wa kienyeji baadae unaweza kurudia hao chotara maana wanakua haraka na utagaji mkubwa sinauhakika kama huwa wanauwezo wa kuatamia mayai, wadau tuelimishane kwa hili.
Chotara hawaatamii japo niliwahi ona mmoja mmoja wanaatamia..chotara anahitaji mtu mwenye muda wa kuwahudumia vinginevyo utakula hasara kila siku.kwangu mimi chotara ni chuma ulete kwani wana gharama kubwa sana kwenye utunzaji wao.ukianzia chakula,madawa na kikubwa ni muda utakaoutumia kuwahudumia.ila Kama vyote hivi unavimudu basi utapata faida
 
Namshukuru Mungu na ushauri wenu ni kweli tukikazana tutaweza tu, changamoto kubwa ni magonjwa ya ghafla kutokea ila nashukuru yaani kila likija hili unakuta mwingine hapa kesha leta na ufumbuzi umejadiliiwa yaani imenisaidia sana sikuwa na Dr yoyote wa mifugo zaidi ya kupata ushauri hapa, kwa RETI na kwenye phamarcy. Sikutaka kuchukua mkopo nilitaka niende taratibu kwa kujibana tu na kupunguza matumizi yasiyo lazima. Naomba nikutie moyo mama Timmy kuku chotara hawana tofauti na hawa kienyeji kwa kulisha na dawa, mimi nimefuga wale wa kisasa ndio nimehamia kwa hawa, ukuaji wa hawa chotara ni wa haraka wakati hawahitaji gharama kubwa kihivyo maana hawali chakula kingi kama wakisasa wala hawahitaji vitamin isipokuwa wiki chache 2 za mwanzo. Kwavile wanakua haraka tayari wakifika kiezi 5 tu unauza kwa 10000 lakini ukiwaacha hadi miezi 8 jogoo ni wakubwa sana na wanauzwa 15000 -20000. Unakuwa huna pressure ya kukubali bei ndogo maana hawali chakula kingi. Faida ya pili wanataga mapema kuliko wa kienyeji hivyo wanaanza kujilisha wenyewe wakiwa na miezi 6 kuendelea na vilevile waweza kuwatumia mayai yao kutotoa vifaranga aidha kwa kuwatumia tetea wa kienyeji pure au incubator na hivyo kutokuwa na haja ya kununua tena vifaranga wengine. Nitajaribu kuweka mchanganuo wa gharama na faida ingawa nikiangalia sio tofauti na iliyowekwa na RETI hapahapa. Lengo langu ni kuongeza aina nyingine ya kuku chotara ili kuwa na aina tofautitofauti, kuanza kutengeneza chakula changu mwenyewe kupitia formula nilipewa na ex SUA lecture na Dr mifugo sasaivi yuko wizarani yeye na mkewe wameitumia na waliniambia inafaa sana ingawa itabidi nipate ushauri wa mwenye mashine kiwango cha usagaji na uchanganyaji wa chakula nitaleta feedback hapa. Nawashukuru wote kwa michango yenu Mungu azidi kuwafanikisha zaidi ktk malengo yenu.
Safi sana mwanamke hapaswi kukata tamaa Kirahisi.ninaamini safari hii unamaliza mchezo nasi tutajifunza kupitia kwako.nakutakia mafanikio makubwa.
 
Wana JF natumaini hamjambo, ni siku nyingine naomba niendelee na simulizi ya mihangaiko yangu ya ufugaji wa Kuku wa Kienyeji!

Naomba nisisitize kutokana na nilichoshuhudia ni kuwa wafugaji wengi huishia kubaki na idadi ndogo ya kuku, hii hasa kutokana na utotoaji duni au vifo vingi sana vya vifaranga. Mbinu ya kuwatenganisha vifaranga na mama zao na kuwakuza peke yao ikifanywa kwa uangalifu hupanua kundi la kuku kwa haraka sana. Kuna utenganishaji ambao hufanyika mara tu vifaranga wanapototolewa aina hii huwezesha kuku kuwa na awamu nyingi za utagaji na uatamiaji kufikia hadi awamu 6 kwa mwaka. Kwa wale wenye mashine za kutotolesha vifaranga ambako kuku hawaachwi kuatamia kabisa, kuku hao huweza kutaga mayai mengi zaidi kwa mwaka kulingana na uwezo wa aina ya kuku.


Mimi sikuwa na mashine ya kutotolesha na wala sikuweza kuwatenganisha vifaranga mara baada ya kutotolewa kwa kuwa sikuwa na miundo mbinu yenye kuwezesha kufanya hivyo. Niliwategemea kuku hao hao kuatamia na kukuza vifaranga. Isipokuwa sasa tofauti na kawaida, mimi nilipunguza idadi ya kuku wa kuatamia kwa kuwapa mayai mengi kuku wachache wayaatamie ili wengine badala ya kuatamia mayai machache wakaendelee kutaga, pia baada ya hawa kuku wachache kutotolesha, vifaranga vyao nilivikabidhi kwa kuku wachache zaidi kama nilivyosimulia jana, ili na hawa nao warudi kundini kutaga! Kuwa na kuku wengi wanaotaga kulisaidia kupata lishe na kuuza mayai ambapo nilikuwa napata pesa ya kununulia chakula na dawa za kulea vifaranga na kuku wote.


Baada ya kumudu kuweza kutotolesha vifaranga kwa wingi liliibuka tatizo la vifo vya vifaranga kiasi ambacho kilianza kunikatisha tamaa kabisa! Ilinichukua muda sana nikijiuliza kwa nini? Hadi kufikia napata ufumbuzi nilikuwa nimeshatupa vifaranga wengi sana, nitalielezea hili vizuri wakati wake ukifika hapo baadae.
Hawa vifaranga WAJE kutaga wanachukuwa siku ngapi?
 
Namshukuru Mungu na ushauri wenu ni kweli tukikazana tutaweza tu, changamoto kubwa ni magonjwa ya ghafla kutokea ila nashukuru yaani kila likija hili unakuta mwingine hapa kesha leta na ufumbuzi umejadiliiwa yaani imenisaidia sana sikuwa na Dr yoyote wa mifugo zaidi ya kupata ushauri hapa, kwa RETI na kwenye phamarcy. Sikutaka kuchukua mkopo nilitaka niende taratibu kwa kujibana tu na kupunguza matumizi yasiyo lazima. Naomba nikutie moyo mama Timmy kuku chotara hawana tofauti na hawa kienyeji kwa kulisha na dawa, mimi nimefuga wale wa kisasa ndio nimehamia kwa hawa, ukuaji wa hawa chotara ni wa haraka wakati hawahitaji gharama kubwa kihivyo maana hawali chakula kingi kama wakisasa wala hawahitaji vitamin isipokuwa wiki chache 2 za mwanzo. Kwavile wanakua haraka tayari wakifika kiezi 5 tu unauza kwa 10000 lakini ukiwaacha hadi miezi 8 jogoo ni wakubwa sana na wanauzwa 15000 -20000. Unakuwa huna pressure ya kukubali bei ndogo maana hawali chakula kingi. Faida ya pili wanataga mapema kuliko wa kienyeji hivyo wanaanza kujilisha wenyewe wakiwa na miezi 6 kuendelea na vilevile waweza kuwatumia mayai yao kutotoa vifaranga aidha kwa kuwatumia tetea wa kienyeji pure au incubator na hivyo kutokuwa na haja ya kununua tena vifaranga wengine. Nitajaribu kuweka mchanganuo wa gharama na faida ingawa nikiangalia sio tofauti na iliyowekwa na RETI hapahapa. Lengo langu ni kuongeza aina nyingine ya kuku chotara ili kuwa na aina tofautitofauti, kuanza kutengeneza chakula changu mwenyewe kupitia formula nilipewa na ex SUA lecture na Dr mifugo sasaivi yuko wizarani yeye na mkewe wameitumia na waliniambia inafaa sana ingawa itabidi nipate ushauri wa mwenye mashine kiwango cha usagaji na uchanganyaji wa chakula nitaleta feedback hapa. Nawashukuru wote kwa michango yenu Mungu azidi kuwafanikisha zaidi ktk malengo yenu.
Nashukuru kwa kunitoa woga mama joe.nikiwa tayari kufuga chotara nitakutafuta kwanza ndugu yangu.
 
Naombeni msaada wenu, nina vifaranga vya kuku chotara ambavyo vina umri wa wiki 7.
Tatizo ni kwamba miguu yao inakosa nguvu, wanashndwa kutembea.
Nilimpeleka mmoja kwenye duka la dawa za mifugu, wakamchunguza na kunipatia dawa ya vitamin kwa kuwa walinieleza kuwa miili yao imeshndwa kutengeneza vitamin B plus.
Tatizo bado linaendelea japokuwa nilianza kuwapatiwa vitamin hao vifaranga wote. Nasubiri ushauri wenu wanajamvi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom