Kubota na co salaams, sisi tupo tunaendelea vizuri tu. Ukipita nymba yenye makelele ukaona kimya ujue tunakula! Sasaivi tunaongelea masoko kule kulikuwa na uzi wa Eliphas. Masoko ya reja reja ni ya kubahatisha. Wateja wangu wote wa kuku wa kisasa wanajibu kama kasuku "nitafute ukiwa na kuku 400 kuendelea....' wakati mie nauza jogoo 10 au 20 kufanya kuwapunguza tu ila nimecheck soko liko poa sana tu. Kingine wengi wanawataka kwa ajili ya kufuga na hivyo wanangangania tetea wasioanza kutaga sasa kwa vile hii ni stock ya kwanza imebidi niwanyime. Kuhusu Chakula cha vifaranga mimi sijaka tama na endapo nitachukua vifaranga karibuni nitajaribu hata ikibidi nihamie mashine nijifunze mbona wengi hawana uchoyo ni sisi tu kukosa mtaji mkubwa wa kusaga chakula kingi na kupenda kununua mfuko kila ukipata kidogokidogo. Niwatakie siku na kazi njema
Mama Timmy, Mama Joe, Asigwa, LiverpoolFC, Guta, n.k, upweke umenizidi, mko wapi wakubwa? Feedback zije wajameni!