Ufafanuzi na Mchanganuo Kuhusu Biashara ya Vipodozi na Urembo

Mugaji

Member
Jan 26, 2012
13
17

Wana JF naombeni ushauri wenu zikiwemo changamoto zake.



WADAU WENGINE WANAOHITAJI KUELEWA BIASHARA HII
Habari wana jamvi,

Natarajia kufanya biashara hii ya duka la vipodozi kwa mkoa wa arusha, naomba kufahamu angalau kidogo kwa wenzangu wanao fanya biashara hii, mzigo huwa mnachukulia wapi, na changamoto zake pia zikoje.



MICHANGO YA WADAU KUHUSU BIASHARA HII
 
Fanya biashara ya vipodozi vya bei nafuu. Ukitarget akina mama wa nyumbani, wanafunzi wa vyuoni uta win. Sehemu yako ya soko iwe ni ya mkusanyiko wa watu wengi kama stendi ya basi, sokoni n.k
 
Habari zenu wadau. Nafikiria kuanzisha biashara ya kuuza vipodozi sehemu ya Sinza Madukani. Lakini sina uzoefu na biashara hii.Nina mtaji wa shilingi milioni tano. Bahati nzuri fremu sio ya kupangisha, nimepewa na father. Naomba mnichangie mawazo Je inalipa kweli? Changamoto zake zipi? Au kama kuna wazo zuri zaidi ya biashara hii tujuzane wadau.Naombeni mawazo yenu wadau.
 
Biashara hiyo siyo mbaya inategemea na location na aina ya vipodozi unavyotaka kuuza coz kuna mapambo ya kike kuna mafuta na lotion na kuna pafryum na urembo mwengine so unataka kuweka kipi ama vyote.
 
Baada ya kukaa na kufikiria kwa muda mrefu na kupata maoni mbalimbali hasa kutoka humu JF sasa nahisi ni wakati wa kuweka wazo langu hapa mnipe ushauri. Nafikiria kufanya biashara ya kuuza vipodozi kwa jumla na rejareja. Sehemu ninayofikiria kufungua ni Mbeya. Sasa nahitaji kusaidiwa ktk mambo ya fuatayo:

1. Utaratibu wa kuprocess kibali unaanzia wapi.
2. Sehemu (miji) za kuchukulia mzigo kwa kuzingatia unafuu wa kuchukulia na kusafirisha.
3. At least mtaji kwa kuanzia (kwa sasa nina 10M)
4. Napenda pia kujua rate ya profit
5. Nahitaji kujua risks ninazotarajia ku-encounter mbele ya safari.

Naomba kuwasilisha.
 
Mimi nakushauri tafuta fedha ya maana ya kufungulia biashara, 10m inaweza kuwa nyingi lakini si kwa magnitude hiyo, badala ya kutaka kuagizishia nunua wanaponunua wenzio slowly mtaji utakua na tayari itakuwa ushapata na akili yako mwenyewe.
 
Mimi nakushauri tafuta fedha ya maana ya kufungulia biashara, 10m inaweza kuwa nyingi lakini si kwa magnitude hiyo, badala ya kutaka kuagizishia nunua wanaponunua wenzio slowly mtaji utakua na tayari itakuwa ushapata na akili yako mwenyewe.

Thanks bro.
 
Vipodozi pia ukikamatwa na customs siku moja tu, unafilisika.

Mkuu kwa kuanzia nilikusudia kuchukulia hapa hapa nchini na nilidhani natakiwa kupata kibali cha kufanya biashara hiyo,so mambo ya customs sikuyaconsider sana.Mimi pia nafikiri biashara ya vipodozi haina tofauti sana na biashara ya dawa za binadamu.
 
Wakuu za wikiendi,

Poleni mfungo wale ndugu waislam na pia wale wenzetu wa upande pili najua mnaburudika jumapili hii. Nipo maeneo ya Dar es Salaam nilikuwa naomba kujua location gani ipo vizuri kwa ajili ya kufungua duka la vipodozi nina mtaji wangu wa millioni tatu nahitaji kujua wakuu manake kuajiriwa ni utumwa.
 
Nahitaji eneo la nje ya kariakoo na mwenge kuepuka ushindani kwa kuwa nina mtaji mdogo.
 
Mjasiriamali usikwepe ushindani, maeneo ntayokushauri ni buguruni, tandika, mwananyamala, na mtongani na mbagala mwisho,
 
Ujasiliamali ndiyo maisha ya leo, ukizingatia kuwa ajira ni janga kwa Tanzania na Dunia kwa ujumla. Nisiwachoshe sana kwa maneno mengi mnayoyajua.

Nina pesa kiasi cha Tshs milion 5 (Tshs. 5,000,000/-). Ambayo ninafikiria kuitumia kuanzisha biashara ya "VIPODOZI" DODOMA MJINI, ili wife apate pakutokea badala ya kukaa nyumbani tu. Hapa lengo ni kuchanga nguvu ili tujikwamue kwa namna moja ama nyingine.

Ninaomba ushauri wenu wadau kwa mambo yafuatayo:-

1. Je, kiasi hiki cha pesa kinafaa kwa kuanzia?

2. Na kama 1 ni ndiyo, je, vitu gani vya mhimu kuvifanya ktk kuanzisha hiyo biashara? (namaanisha kama kuna documents za mhimu ninazopaswa kuwa nazo kama watu wa afya i.e maduka ya dawa)

3. Kama 1 ni ndiyo, ni wapi naweza nunua mzigo(bidhaa) nami nikapata chochote kama lengo lilivyo?

NB: Ushauri wako ni mhimu sana, pia kama hicho kiasi kitakuwa hakitoshi nishauri ni kiasi gani niongeze/nitafute ili kufikia lengo.

NAWASILISHA.
 
Habari wana JF napenda kuuliza na kupata ushauri toka kwenu kuhusu soko la vipodozi nataka kuchukua toka Tunduma nilete Dar kuuza kwa jumla kwa maduka nitakayochukua oda. Je, naweza pata mchanganuo wa hii biashara maana ndio nataka nijalibu na mtaji wangu wa kuunga unga. Natanguliza shukrani na mawazo yenu.
 

Mkuu hii biashara inatakiwa ujue aina ya vipodozi.vile vinavyolipa ni vile ambavyo serikali imepiga marufuku. Vingine ambavyo vinaruhusiwa havilipi ila ukivileta vile vinavyolipa biashara yake ni kama kuuza unga vile.kuanzia kuvisafirisha toka huko mpaka dar.wenye mabasi ndiyo, wanaoongoza kuchomea kwa police halafu wanapatagao. Kiufupi tafuta biashara nyingine mkuu. Maana unaweza kata mtaji wako trip ya kwanza tu.
 
Hiyo biashara inalipa sana cha muhimu ujue vipodozi vilivyoruhusiwa ili usishikwe na kuchomewa. Cha kwanza zunguka maduka ya vipodozi uhulize vip vinavyouzika. zunguka kwa zahidi ya maduka 40 ili ujue.

Kuna mdada namjua ila yeye alikuwa anatoa Congo ya mashariki akipitia Uganda, kisha anapanda bus za Dar kupitia Bukoba, sasa hiv ni tajiri mkubwa.

Fanya nilivyokwambia utafanikiwa.
 
Mimi nina saloon ya kike niko Kilimanjaro vipi unaweza kufanya bussnes na mm, saloon kwangu nauza urembo na vipondozi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…