Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 13,226
- 26,048
Kwanza napenda kumpongeza Tundu Antipass Lissu kwa kuwa Mtanzania pekee hadi sasa aliyekuja na uchambuzi wa kihoja kwenye suala la Makubaliano ya Tanzania na Dubai kuhusu masuala ya Bandari.
Namfahamu Tundu Antipass Lissu kama mwanasheria mzuri sana. Nimeshiriki nae kwenye kazi kadhaa hivyo sina mashaka na ujuzi wake kwenye masuala ya Sheria.
Pamoja na haya leo napenda kupingana na Mwanasheria huyu mwenzangu katika uchambuzi wake katika masuala ya Bandari na hii ni kwa sababu najua anajua kuwa amepotosha na ni kweli na hakika kuwa katika suala hili ndugu yangu Lissu amepotosha sana.
Kwa nini Tundu Antipass Lissu amepotosha?
Kuhusu suala la Muda wa ukomo wa Mkataba
Lissu amesema kabisa huu mkataba unafuatiwa na Mkataba wa Host Government Agreement ila bado anajichanganya kwa kusema kuwa endapo hakutakuwa na Host Government Agreement mkataba huu utakuwa wa milele. Hapa Wakili wangu amepotosha vibaya sana. Katika Mkataba huu, Ibara ya Kwanza Ibara ndogo ya 2 ( Article 1(2))inaelezea ulazima wa pande zote ikiwemo Tanzania kuingia katika makubaliano ya Host Government Agreement!
Katika ibara hii kuanzia vipengele a, but hadi c vimeelezea wazi kabisa kuhusu HGA zitakazoingiwa kuhusu maeneo husika.
Sasa swali langu kwa Lissu tuseme hakuona hiki kifungu cha mkataba? Anapotosha kwa maslahi gani?
Kuhusu Mkataba kutosema faida tunazopata na uwekezaji unaofanyika ni wa kiasi gani?
Kusema kweli hapa Wakili msomi Lissu kama hafanyi upotoshaji wa makusudi basi atakuwa ameanza kuzeeka.
Article 1(2) c ya Mkataba huu inasema wazi na nakinukuu hapa,
" Tanzania agrees each relevant HGA and each relevant project agreement to which it or state authority is a party shall be the contractual framework for Tanzania and the State Authority's contractual rights, obligations and undertakings under or in connection with the relevant project"
Maana ya hiki kifungu ni kwamba kutika makubaliano ya HGA kuhusu mradi husika mfano iyo sehemu ya Bandari atakayopewa mwekezaji haki zote na wajibu wote ndo vitaelezwa humo ikiwemo uwekezaji ni kiasi gani, faida kwa Tanzania kuhusu uwekezaji huo ni kiasi gani na kila kitu kingine.
Logic behind kifungu hiki ni kuwa kabla pande mbili hazijaingia mkataba wa HGA hapo lazima wataalamu wa actuary wakae wapige hesabu kuhusu gharama za uwekezaji , faida zitakuwaje na mgawanyo wa kodi na malipo mengine yaweje. Haya yote kimsingi hayawezi kuwekwa katika mkataba huu ila yanapaswa kuwekwa kwenye HGA husika. Sasa Lissu kama mwanasheria najua anajua kuwa haya mambo hayapaswi kuwa katika IGA maana IGA inakuwa general ila HGA inakuwa specific katika mradi husika.
Kuhusu masuala ya Kodi
Hapa Wakili msomi Tundu Lissu kusema kweli amekosea kwa sababu anadai itakuwa kama kwenye masuala ya madini wakati hata hajajua kwenye HGA husika wajibu wa mwekezaji utawekwaje na ushiriki wetu kwenye huo uwekezaji utakuwaje??? Ibara ya 18 ya Mkataba huu imesisitiza kuzingatiwa na Sheria na masharti kama yalivyowekwa kwenye HGA. Sasa hapa zijaelewa kabisa hoja za Lissu?
Kwenye kipengele hiki hoja za Lissu zingekuwa na mashiko kama HGA zingekuwa zimeshakamilika na wataalamu wa Actuary hawajahusika katika kuweka hesabu za uwekezaji na faida vizuri. Hivyo sioni kama ana hoja ya msingi kwenye hili
Kuhusu kwenye Bandari za kuuzwa ingawa nakubaliana na Lissu kuwa muungano wetu una changamoto kwa kuwa naamini kama kweli ni muungano basi ulitakiwa kuwa wa serikali moja ila bado sikubaliani na Lissu kuhusu kusema Bandari zetu zimeuzwa.
Nimesoma mkataba wote, nimepitia kifungu kwa kifungu na kusema kweli hakuna sehemu mkataba huu umewapa watu wa Dubai Bandari. Mkataba huu umeonesha kuwa tutashirikiana katika masuala ya Bandari katika maeneo yatakayokubaliwa kwenye mkataba mwingine wa HGA ambapo sisi tutasema tushirikiane nao katika Bandari ipi au eneo lipi la uwekezaji na kwa masharti yapi. Hakuna sehemu imesemwa Bandari zote wamepewa au wanapewa. Lissu amepotosha sana.
Kuhusu Uzanzibari wa Samia na Prof Mbarawa hapa napo naona Lissu ameongea kama mwanasiasa ila sio kama mwanasheria. Unapohoji uraia wa mtu lazima uwe na msingi wa kuhoji. Kwa nini hakuhoji alipoamua alipwe posho zake alizozurumiwa kipindi cha awamu ya 5? Hapo hakuona kama anafanya kwa Uzanzibari wake?
Kwa nini hakuhoji wakati mazungumzo yake na Rais yalifanya afutiwe kesi zote na kupewa passport yake?
Kusema kweli hapa Lissu anapotosha kwa sababu hakuna Bandari yeyote iliyouzwa au kugawiwa hadi sasa. Hizi ni siasa za majitaka
Namfahamu Tundu Antipass Lissu kama mwanasheria mzuri sana. Nimeshiriki nae kwenye kazi kadhaa hivyo sina mashaka na ujuzi wake kwenye masuala ya Sheria.
Pamoja na haya leo napenda kupingana na Mwanasheria huyu mwenzangu katika uchambuzi wake katika masuala ya Bandari na hii ni kwa sababu najua anajua kuwa amepotosha na ni kweli na hakika kuwa katika suala hili ndugu yangu Lissu amepotosha sana.
Kwa nini Tundu Antipass Lissu amepotosha?
Kuhusu suala la Muda wa ukomo wa Mkataba
Lissu amesema kabisa huu mkataba unafuatiwa na Mkataba wa Host Government Agreement ila bado anajichanganya kwa kusema kuwa endapo hakutakuwa na Host Government Agreement mkataba huu utakuwa wa milele. Hapa Wakili wangu amepotosha vibaya sana. Katika Mkataba huu, Ibara ya Kwanza Ibara ndogo ya 2 ( Article 1(2))inaelezea ulazima wa pande zote ikiwemo Tanzania kuingia katika makubaliano ya Host Government Agreement!
Katika ibara hii kuanzia vipengele a, but hadi c vimeelezea wazi kabisa kuhusu HGA zitakazoingiwa kuhusu maeneo husika.
Sasa swali langu kwa Lissu tuseme hakuona hiki kifungu cha mkataba? Anapotosha kwa maslahi gani?
Kuhusu Mkataba kutosema faida tunazopata na uwekezaji unaofanyika ni wa kiasi gani?
Kusema kweli hapa Wakili msomi Lissu kama hafanyi upotoshaji wa makusudi basi atakuwa ameanza kuzeeka.
Article 1(2) c ya Mkataba huu inasema wazi na nakinukuu hapa,
" Tanzania agrees each relevant HGA and each relevant project agreement to which it or state authority is a party shall be the contractual framework for Tanzania and the State Authority's contractual rights, obligations and undertakings under or in connection with the relevant project"
Maana ya hiki kifungu ni kwamba kutika makubaliano ya HGA kuhusu mradi husika mfano iyo sehemu ya Bandari atakayopewa mwekezaji haki zote na wajibu wote ndo vitaelezwa humo ikiwemo uwekezaji ni kiasi gani, faida kwa Tanzania kuhusu uwekezaji huo ni kiasi gani na kila kitu kingine.
Logic behind kifungu hiki ni kuwa kabla pande mbili hazijaingia mkataba wa HGA hapo lazima wataalamu wa actuary wakae wapige hesabu kuhusu gharama za uwekezaji , faida zitakuwaje na mgawanyo wa kodi na malipo mengine yaweje. Haya yote kimsingi hayawezi kuwekwa katika mkataba huu ila yanapaswa kuwekwa kwenye HGA husika. Sasa Lissu kama mwanasheria najua anajua kuwa haya mambo hayapaswi kuwa katika IGA maana IGA inakuwa general ila HGA inakuwa specific katika mradi husika.
Kuhusu masuala ya Kodi
Hapa Wakili msomi Tundu Lissu kusema kweli amekosea kwa sababu anadai itakuwa kama kwenye masuala ya madini wakati hata hajajua kwenye HGA husika wajibu wa mwekezaji utawekwaje na ushiriki wetu kwenye huo uwekezaji utakuwaje??? Ibara ya 18 ya Mkataba huu imesisitiza kuzingatiwa na Sheria na masharti kama yalivyowekwa kwenye HGA. Sasa hapa zijaelewa kabisa hoja za Lissu?
Kwenye kipengele hiki hoja za Lissu zingekuwa na mashiko kama HGA zingekuwa zimeshakamilika na wataalamu wa Actuary hawajahusika katika kuweka hesabu za uwekezaji na faida vizuri. Hivyo sioni kama ana hoja ya msingi kwenye hili
Kuhusu kwenye Bandari za kuuzwa ingawa nakubaliana na Lissu kuwa muungano wetu una changamoto kwa kuwa naamini kama kweli ni muungano basi ulitakiwa kuwa wa serikali moja ila bado sikubaliani na Lissu kuhusu kusema Bandari zetu zimeuzwa.
Nimesoma mkataba wote, nimepitia kifungu kwa kifungu na kusema kweli hakuna sehemu mkataba huu umewapa watu wa Dubai Bandari. Mkataba huu umeonesha kuwa tutashirikiana katika masuala ya Bandari katika maeneo yatakayokubaliwa kwenye mkataba mwingine wa HGA ambapo sisi tutasema tushirikiane nao katika Bandari ipi au eneo lipi la uwekezaji na kwa masharti yapi. Hakuna sehemu imesemwa Bandari zote wamepewa au wanapewa. Lissu amepotosha sana.
Kuhusu Uzanzibari wa Samia na Prof Mbarawa hapa napo naona Lissu ameongea kama mwanasiasa ila sio kama mwanasheria. Unapohoji uraia wa mtu lazima uwe na msingi wa kuhoji. Kwa nini hakuhoji alipoamua alipwe posho zake alizozurumiwa kipindi cha awamu ya 5? Hapo hakuona kama anafanya kwa Uzanzibari wake?
Kwa nini hakuhoji wakati mazungumzo yake na Rais yalifanya afutiwe kesi zote na kupewa passport yake?
Kusema kweli hapa Lissu anapotosha kwa sababu hakuna Bandari yeyote iliyouzwa au kugawiwa hadi sasa. Hizi ni siasa za majitaka