Ubungo DSM, Kibesa S/Msingi wanafunzi darasa la nne waamuliwa kuchangia sh. 1,000/ mfululizo mpaka watakapofanya mtihani wa taifa

Mtu wa kwanza

New Member
Sep 14, 2018
3
0
Kibesa S/msingi wilaya ya Ubungo, jijini Dar Es Salaam, wanafunzi wa darasa la nne waamuliwa kufanya mtihani mfululizo kwa gharama ya sh. 1,000 kila mwanafunzi na kwa darasa zima lenye wanafunzi 120 linalazimika kuchanga kiasi cha sh.120,000/ ikitajwa kuwa ni posho ya Mwalimu na gharama ya kuchapisha mitihani.

Wazazi wamelalamika mbali na hizo gharama, michango mingine mingi ikiendelea hali ambayo inalazimu wazazi kushindwa kumudu gharama.

Walimu wamekuwa wakiitisha vikao kujadili na wazazi huku maoni yanayotolewa na wazazi kulalamikia gharama hizo yakipuuzwa.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Nestory Masunga, amekuwa akitoa vitisho kuwa mzazi asiyechangia, mtoto atatengwa na hatopewa mtihani na anaweza asifanye vyema mtihani wa taifa.

Wazazi wanaiomba serikali kupitia rais Samia S. Hassan kuwasaidia kwani kufanya mtihani kila siku hakutamsaidia mtoto kuelewa badala yake walimu wajikite na kutoa muda wa kutosha kuwafundisha watoto kwenye masomo ambayo hawafanyi vizuri badala ya kuwapa mitihani kila siku mfululizo.

Wanaiomba Serikali iingilie kati na ifuatilie na itoe muongozo kwani michango ni mingi na inazidi kuratibiwa katika shule hii ya Kibesa.
 
Kwa nini wasiende kulalamika.kwa.viongozi? Na uhakika hiyo michango walipitisha wao na wanalalamikia walilaidi kwenda kwenye kikao.
 
Kama vikao vinaitishwa, na niny wenyewe mlipitisha bas hamna haja ya kuja kulalamika huku,
Nendeni kwenye vikao tena,

Kama wameanzisha from no where, naomba nikemee kwa sana hii tabia ovu, serikali ya wilaya iingilie kati,
Huwez mpa mitihani mtoto kila siku
 
Unaposema mfululizo unamaanisha nini? Kikawaida ninavyojua weekly test ni sawa,na hii sisi tulikuwa tunaandikiwa ubaoni hamna mchango wowote.Mitihani mingine, ni midterm , terminal na mock .

Sema siku hizi walimu wamekuwa na njaa kali sana, wala lengo sio kusaidia watoto..kinacholengwa hapo ni maokoto tu!
 
Kibesa S/msingi wilaya ya Ubungo, jijini Dar Es Salaam, wanafunzi wa darasa la nne waamuliwa kufanya mtihani mfululizo kwa gharama ya sh. 1,000 kila mwanafunzi na kwa darasa zima lenye wanafunzi 120 linalazimika kuchanga kiasi cha sh.120,000/ ikitajwa kuwa ni posho ya Mwalimu na gharama ya kuchapisha mitihani.

Wazazi wamelalamika mbali na hizo gharama, michango mingine mingi ikiendelea hali ambayo inalazimu wazazi kushindwa kumudu gharama.

Walimu wamekuwa wakiitisha vikao kujadili na wazazi huku maoni yanayotolewa na wazazi kulalamikia gharama hizo yakipuuzwa.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Nestory Masunga, amekuwa akitoa vitisho kuwa mzazi asiyechangia, mtoto atatengwa na hatopewa mtihani na anaweza asifanye vyema mtihani wa taifa.

Wazazi wanaiomba serikali kupitia rais Samia S. Hassan kuwasaidia kwani kufanya mtihani kila siku hakutamsaidia mtoto kuelewa badala yake walimu wajikite na kutoa muda wa kutosha kuwafundisha watoto kwenye masomo ambayo hawafanyi vizuri badala ya kuwapa mitihani kila siku mfululizo.

Wanaiomba Serikali iingilie kati na ifuatilie na itoe muongozo kwani michango ni mingi na inazidi kuratibiwa katika shule hii ya Kibesa.
Mtamkumbuka dikteta.

Na bado
 
hahahhaa kuna shule inaitwa diplomasia sekondary iko temeke nayo ina balaa kwenye masuala ya hela aisee afu naona sku hz wanafundi wao wanatoka saa 2 usiku sjui wansoma nn waalimu wa diplomasia sec mtuambie
 
Kibesa S/msingi wilaya ya Ubungo, jijini Dar Es Salaam, wanafunzi wa darasa la nne waamuliwa kufanya mtihani mfululizo kwa gharama ya sh. 1,000 kila mwanafunzi na kwa darasa zima lenye wanafunzi 120 linalazimika kuchanga kiasi cha sh.120,000/ ikitajwa kuwa ni posho ya Mwalimu na gharama ya kuchapisha mitihani.

Wazazi wamelalamika mbali na hizo gharama, michango mingine mingi ikiendelea hali ambayo inalazimu wazazi kushindwa kumudu gharama.

Walimu wamekuwa wakiitisha vikao kujadili na wazazi huku maoni yanayotolewa na wazazi kulalamikia gharama hizo yakipuuzwa.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Nestory Masunga, amekuwa akitoa vitisho kuwa mzazi asiyechangia, mtoto atatengwa na hatopewa mtihani na anaweza asifanye vyema mtihani wa taifa.

Wazazi wanaiomba serikali kupitia rais Samia S. Hassan kuwasaidia kwani kufanya mtihani kila siku hakutamsaidia mtoto kuelewa badala yake walimu wajikite na kutoa muda wa kutosha kuwafundisha watoto kwenye masomo ambayo hawafanyi vizuri badala ya kuwapa mitihani kila siku mfululizo.

Wanaiomba Serikali iingilie kati na ifuatilie na itoe muongozo kwani michango ni mingi na inazidi kuratibiwa katika shule hii ya Kibesa.
 
Hii nilikua namuachia wife aende kwenye hivyo vikao,, na hili la kuchangia mitihani kila wiki darasa la nne nilipinga sana ingawa sikumzuia kulipa,, siku moja nikasema kwa kuwa nipo tu home ngoja leo niende mwenyewe kwenye hivyo vikao vya shule,, aisee nyinyi acheni tu,, hii elimu bure ni mateso kwa walimu usiombe,, tuchangeni tu ingawa na wao kuna sehemu wanazidi,,
 
Back
Top Bottom