Ubabe hadi Canada? This time you're done

Ehh Mwenyezi Mungu umtangulie mkulima Stern apate haki yake.πŸ™πŸΎ
Na mwanga wa milele umwangazie eee Bwana

Mamilioni ya Watanzania tunamwombea Mkulima!

Ukija na Swiss Air, KLM 80% wanashuka Nairobi, dege linakuja KIA na DAR tupu toka Ulaya!

Ni data gani zinazowaonyesha watalii hatuna kwa sababu hakuna ndege ya kuwaleta???

Mpaka British Airways wakafunga biashara baada ya kuja DAR miaka 50 mfululizo...

leo mnasema mnanunua ndege kuleta watalii... Kutoka wapi, Katavi? Kule mlikosema kuanzia leo nataka kuona ndege inatua Katavi???

Kwani wangesema tunataka kufufua ATC, kuendesha biashara ya ndani na nje, watalii wawepo wasiwepo, tumerekebisha hiki na kile, daftari la mahesabu ya hasara na faida hili hapa, mwenye maoni ya kuponda na kujenga apeleke maandishi kwa mdhibiti mkuu TCAA, kama tunavyopeleka malalamiko EWURA, TCRA, SUMATRA, au akaongee viwanja vya Mwembeyanga saa sita mchana mpaka sauti ikauke, sisi tunajaribu biashara... nani angewaombea mabaya?? nani duniani anaanzisha biashara na uhakika wa mafanikio??
 
Ndege zenyewe wala hazina routes za uhakika bado wanaongeza nyingine. Hapa unaona kabisa kuwa kuna anaenufaika na manunuzi si matumizi.
 

Nimeongelea kubadili katiba?

Nimeongelea kuvunja katiba!

Na kuvunja katiba ni KOSA!

Halafu upo hapa kushabikia uvunjifu wa katiba ambayo ni supreme law of the land!??

Hivi una habari anakuja rais mwingine 2025 anaweza fungilia mbali hilo limawe lenu kwa haya makosa anayofanya leo?

Hivi unadhani crime ina statue of limitation?

Wait and see!
 
Nadhani wengi hawatambui kwamba kuombea mtu kifo ni tamaa ya kuua mtu.
Mtu wa hivyo akipata nafasi ya kuuwa basi anatekeleza tamaa yake.
 
Ukiona hadi ma drug deals kama mtoa mada wanampiga jpm jua kuna kazi nzuri kafanya


State agent
 
Pasco huna Baba hata umwite Magufuli kuwa Baba yako?
Magufuli ni Dikteta wa Tanzania, full stop.
Kama Tanzania ni nyumba yetu, then Magufuli ndiye baba mwenye nyumba, ni baba.

Hili la rais Magufuli kuwa baba yetu, nimelizungumza hapa kama ilivyo kwa Nyerere ni baba wa Taifa, rais Magufuli ndie baba Tanzania kwa sasa.

P
 
Yaani zikamatwe zote, mtu anakubali anunue ndege nane, wakati watu wanakosa dawa hospitalini, wakati watu wanakunywa matope badala ya maji, zikamatwe tu tena waongeze kuzikamata zee lina roho mbaya sana.
 
Pambaneni wenyewe si mnasema ndege za magufuli na ccm!
 
Bro tujiulize bila unafiki kwa nini watu sasa hivi wanafurahia matatizo ya taifa!?...lakini pia uzalendo haufundishwi wala kuhimizwa unakuwepo tu moyoni ila unaondoka wenyewe bila hata kuhimzana wala kuambiana kama kuna mambo ambayo siyo rafiki kwake
 
P, hakuna anayefurahia Mali ya mwingine kutiwa matatani! Na uzalendo ni uzalendo tu hauna tafsiri nyingine! Mliopo huko serikalini mnajua pasi na Shaka Nani anadai Nini na tangu lini! Kwanini msilipe hata kidogokidogo? Au mnadhani mzungu ni sawa na wafanyakazi wa umma mnaowakopa na kuwadhulumu malimbikizo yao ya mishahara na bado wakawavumilia? Huu kwako na kwa wengine ni uzalendo kwa kumdhulumu mtumishi! Ona wenzako wa gazeti la mtanzania anavyomwaga gesi kwenye Moto wa petrol! Hamtoki Canada kwa maandishi Yale!
 
Yaani zikamatwe zote, mtu anakubali anunue ndege nane, wakati watu wanakosa dawa hospitalini, wakati watu wanakunywa matope badala ya maji, zikamatwe tu tena waongeze kuzikamata zee lina roho mbaya sana.
Tatizo vipaumbele mambo yanafanywa kwa mzuka wa kisiasa mashirika ya Rwanda na Kenya yanapumulia mashine sisi nao tunaiga.
 
KWA HILI NADHAN WAZIRI AUATUINGIZA CHAKA. KUNA UKWELI ANAOUFICHA
 
Bado maandamano tu kwenye ubalozi hahaaa!!
 
Ehh Mwenyezi Mungu umtangulie mkulima Steyn apate haki yake.[emoji120]🏾
Hakika. Hatutaki tabia za ukagame za kupora mali za wengine. Huyu mkulima si mwendawazimu akurupuke kudai malipo hewa. Alipww haki zake kulinda heshima ya nchi yetu.
 

P,
Call a spade a spade and not a ''Big spoon''.
Hakuna mtu anafurahia kukamatwa kwa ndege. Moral support iliyoko ndani ya mioyo ya Wazalendo wa Kitanzania ni kumalizana na Mkulima STEYN kwa KUMLIPA na kuachana naye...!!
Hii kulalamika, kusingizia kina Lissu siji MABEBERU ni utoto na kukosa hekima...!!!Sheria zitapindishwa hapa Tanzania lakini nje ya Mipaka CCM na Serikali wawe makini sana...!!!
Serikali hiihii ya CCM iliamua KUTAIFISHA MALI ZA STEYN na swala likafika Mahakama Kuu ikaamuliwe Mkulima alipwe 33m USD kwa awamu. Mzee Ruksa,Mkapa na JK wakalipalipa sehemu ya deni. Alipoingia 'homeboy' akasema halipi deni la BEBERU hapa....!!!
Hii biasahara ya kukimbia huku na huko kwenda kupambana na Steyn kwenye Mahakama za watu ni Ubabe na kujidhalilisha kwene Jumuia za Kimataifa...!!!
Ushauri wa bure: Serikali ikae meza moya na Mr. Steyn hoja iwekwe mezani ijulikane anadai bei gani, alishalipwa ngapi na kilichobaki ni ngapi pamoja na riba....!!! Tusidanganyane kuwa ati Steyn ni BEBERU wakti CCM ndio walio mleta Steyn Tanzania kama Mkulima mwekezaji...!!!Ubeberu unatokea wapi?
 
Huondoa credit kwa wapinzani na KUONGEZA CREDIBILITY ya wapinzani, wanajitambulisha kama true voices of reason, sio political comedians
Si kweli. Hoja za kijinga kama hizi ni cheap politics, kumbuka watanzania wana mwamko wa kisiasa zama hizi, wamejua mema na mabaya. Ni vema kujikita kwenye siasa zenye maslahi kwa taifa kuliko kujaribu kushabkia mambo ambayo hayana uwiano wa kisiasa na kuyapoliticise. Kwenye siasa wekeni siasa, kwenye patriotism wekeni hiyo, sio kusimama dhidi ya Tanzania kwa kujifanya mnasimama dhidi ya CCM. Tukiiangusha Tanzania hata siasa hazitakuwa na maana.
 


Tuwe wamoja halafu tufanye nini mkuu? Tutoe hela za watoto Wetu za school fees tumlipe Mkulima ili ndege itoke au tuwe wamoja kwa kupeana matumaini ya uongo uongo kwenye mitandao??πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

Sikiliza ndugu yangu dawa ya deni ni kulipa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…