Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,468
- 113,583
Wanabodi,
Huu ni wito tuu kwa wana jf kuhusu ukosoaji wa Rais wa nchi, Mhe. Dr. John Pombe Joseph Magufuli, ufanyike kwa staha kwa kutanguliza mbele uzalendo, na maslahi ya taifa mbele, ukiwemo utaifa. Kuitanguliza mbele Tanzania kwanza ndipo rais Magufuli afuatie.
Rais Magufuli nae ni binadamu na sio malaika, hivyo, kama binadamu ni haki yake kukosea, kwasababu no one is perfect, the only perfect being is God!, hivyo Magufuli kama Magufuli kuna mahali anakosea au amefanya ndivyo sivyo, tupaseme sio kwa kubeza au kukejeli, bali kufanyike kwa heshima, kwa lugha ya staha na unyenyekevu kwa lengo la kumuonyesha makosa yake, kisha tuweke na ushauri wa the right thing to do, hivyo ukosoaji kwa rais, ufanyike constructively kwa nia njema ya kujenga na sio kubomoa, yaani tufanye "a constructive criticism" in good faith kwaa nia ya kumsaidia rais wetu kuwa rais bora zaidi na kulisaidia taifa kusonga mbele na sio kurudi nyuma kwa sababu kwa mujibu wa katiba yetu, rais hawezi kukosea ndio maana hawezi kushitakiwa.
Rais ana sehemu mbili, rais ni taasisi ya presidential institution hivyo rais kama taasisi hawezi kufanya kosa lolote ni perfect being kila kauli yake ni sheria, inafuatiwa na utekelezaji tuu, lakini hiyo institution inashikiliwa na kuongozwa mtu apmbaye ni binadamu tuu kama sisi anayeitwa John Pombe Joseph Magufuli, huyu ni binadamu wa kawaida kama sisi wengine wote, he is a human anaweza kukosea. Katika kumkosoa rais, tumkosoe kwa heshima in such a way tusije kujikuta tunakosa uzalendo, badala ya kumkosoa, tumamuaibisha na kujikuta tunajiabisha sisi kama taifa.
Nakiri kupandisha uzi huu kutokana na mchango wa mwana jf huyu
Hata ikitokea baba mwenye nyumba au baba nyumbani amekosea jambo fulani, anakosolewa kwa heshima kiutu uzima kwa kutumia lugha ya heshima na staha na sio lugha za dharau, kebehi, machukizo au matukano! .
Hata akidanganya haitwi muongo anaitwa hayuko sahihi sana, au ameshauriwa vibaya kwa sababu rais wa nchi hawezi kudanganya, wala hawezi kusema uongo!.
Hata akichelewa kwenye shughuli haambiwi kachelewa maana mkubwa hachelewi bali anakuwa bado hajawasili kutokana na kutingwa na shughuli muhimu, na asipotokea kabisa ni kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu!.
Simaanishi rais Magufuli yeye ni malaika hivyo hawezi kukosea au kufanya makosa, no!, rais Magufuli naye ni binaadamu tuu kama sisi binaadamu wengine wote, na siku zote sisi binaadamu ni viumbe dhaifu, hivyo rais Magufuli naye ana madhaifu yake ikiwemo kuonekana kama ni mtu wa kupenda kusifiwpa kupindukia, anapoongea kuna wakati anaonekana kama ni msema chochote na katika kufanya maamuzi, kuna wakati anaonekana kama anatenda badhi yap maamuzi kwa haraka na baadhi ya maamuzi yake, kuonekana kama ni maamuzi ya uamuzi wa haraka hivyo kukosa tafakuri ya kina ila kwa vile yeye ndie kiongozi wetu Mkuu, kuna mambo ambayo hatupaswi kuyasema hivyo yalivyo, hata kama ni kweli, hata kama ni kweli sometimes anaweza kusema kitu ambacho sio sahihi, hatupaswi kusema rais ni muongo bali rais hakuwa sahihi sana au alikuwa hajashauriwa vizuri au alikuwa ana joke tuu, au anazungumza kwa utani tuu, yaani rais anatania au rais ameteleza tuu ulimi!.
Mfano rais alipohimiza kufyatua tuu watoto kisa atasomesha bure. Tamko hili lilikwenda kinyume cha uzazi wa mpango, hapa rais kiukweli aliropoka na kuteleza ulimi, lakini haiwezi kusemwa kuwa rais karopoka, bali rais alikuwa anatania tuu watani zake, wazaramo!. Siku alipotamka hivyo, hata mimi nilishitushwa na tamko lile ( Rais Kusitisha Uzazi wa Mpango Kwa"Fyatueni Watoto wa Kutosha",Ni Yake au ni ya Wale Wazee wa..?!.)
Lakini baada ya siku mbili tatu, Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu aliibuka na kulitolea ufafanuzi wa kina tamko lile kuwa lilikuwa sii kweli bali rais alikuwa akiwatania tuu watani zake Wazaramo!.
Mfano kwenye hoja ya udikiteta, ni kweli rais Magufuli ni kama dikiteta fulani hivi, ila ni dikiteta Mzalendo. Hivyo ndivyo alivyo, tangu akiwa Waziri, he is a no nonsense man, hataki ujinga na hawezi kuvumilia uzembe, na sio kwamba anajifanyisha, ila pia, kwa Tanzania hapa tulipofika, seriously tulihitaji sana mtu mwenye sifa, silika na haiba za udikiteta ndio anaweza kuinyoosha hii nchi ilivyopinda kupindukia hadi kufanywa ni shamba la bibi!. Siku nyingi tumekuwa tukmlaumu JK kwa u pole wake hadi kumuita "dhaifu" hivyo tumekuwa tukisali kumuomba Mungu atupe kiongozi imara, shupavu, thabiti, ambaye sio mtu wa mchezo mchezo, na kweli hatimaye Mungu akaisikia sala yetu ametupatia Magufuli ambaye ni dikiteta kweli ila sio dikteta mbaya kama Hitler, huyu ni dikiteta mzuri " a benevolent dictator", hivyo badala ya watu kuulaumu huu udikiteta wa rais Magufuli, tunapashwa kumshukuru Mungu kutupatia Magufuli.
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata!. Atakayeleta Fyoko, Ataisoma Namba!
Watu walipoitwa Vila.za, hatukunyamaza, tulitoa ushauri humu.
Wito kwa Baba Jesca: Watendee Haki Kina Jesca Wote Ili Nao Wapate Bahati Kama Jesca!.
Hata alipozungumzia mishahara ya peponi, pia tulitoa ushauri humu
Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote
Hata majumbani mwetu hasa majumba ya Kiafrika na Kiswahili, baba ambaye ni mkuu na kichwa cha nyumba, kuna mara kibao anakosea hasa sisi mababa wa Kiafrika tunaofuata mila zetu za kiasili za Kiafrika na mambo yetu yalee ya Uafrika wetu, na pia sio malaika hivyo tuna madhaifu mengi tuu ambayo wamama huyajua huyaona, huyavumilia lakini hawayasemi hadharani.
Kuna namna ya ukosoaji wa heshima na staha wenye lengo la kujenga, a constructive criticism ambao hufanywa in good faith na kuna ukoasoaji wa mbaya wa udhalilishaji wenye lengo la kubomoa, kubagaza, kudunisha na kumshusha mtu kwa kumvunjia heshima ambao hufanywa in bad faith, ridiculously au kumdhalilisha, mkosolewa kwa nia ya kumjengea chuki, achukiwe, kumshushia hadhi na heshima ili aonekane ni mtu wa hovyo, etc huu sio ukosoaji mzuri hata kama ni kweli amekosea, yaani japo is the truth but the motive behind is ill motive.
Simaanishi sasa ndio wote kazi yetu iwe ni moja tuu, kumhusu rais wetu, iwe ni kumuimbia tuu nyimbo za sifa na mapambio, no !, tumkosoe rais Magufuli kwa heshima na kwa kutumia lugha ta staha kwa nia njema kabisa kwa lengo la kumrekebisha na kumsaidia na sio kumdhalilisha.
Tanzania ni yetu sote, sio Tanzania ya Magufuli pekee, na japo CCM ndio chama tawala, haimaanishi Tanzania ni ya CCM, Tanzania sio ya CCM pekee, ni Tanzania ya wote, hivyo we all have a role to play and a responsibility of duty of care kujenga nchi yetu kwa kutanguliza uzalendo na kuweka mbele maslahi ya taifa kwa kujenga na sio kuibomoa na kumjenga rais wetu na sio kumbomoa regardless tunampenda, hatupendi, tulimchagua, hatukumchagua, kama wazalendo wa nchi hii ni lazima kuijenga nchi yetu na kumsaidia rais wetu as a responsibility and a duty of care, kama inavyotokea kuwepo kwa mtoto mwenye ulemavu katika familia, hakuna anayependa ulemavu, lakini imetokea, lazima tumpende and we have a duty of care kumsupport, kumsaidia na kupenda kwa dhati, vivyo hivyo ndivyo ilivyo kwa rais Magufuli, ndie rais wetu wa sasa na hivi alivyo ndivyo alivyo, tumkubali, sio lazima tumpende lakini tunawajibu wa kumpa kila aina ya ushirikiano ili aweze kulitawala vyema taifa letu.
Kuna watu katika kumbonda rais Magufuli, kila siku kazi yao wao ni kuponda tuu, hata akifanya mazuri vipi, wao wataponda tuu, kubeza, kukosoa kila kitu na kumbomoa tuu, na katika kuponda huku, sometimes hujikuta wanaponda over and obove na kuliaibisha taifa letu, na wengine humsifia Nyerere, yaani kumtumia wasifu wa Nyerere as a reference, ila kiukweli ukimwangalia rais Magufuli kwa jicho la karibu, yuko kama Nyerere kwa karibu kila kitu
Magufuli Kama Nyerere:Ni Mtu wa Watu, Hapapasi, Hamung'unyi, Ni Kazi Tuu, Ila Pia,Sio Kama Nyerere!.
Katika kujenga nchi the motive iwe ni kujenga kila kitu ikiwemo kujenga watu akiwemo rais anahitaji kuendelea kujengwa na sio kubomolewa tuu.
Japo nafahamu katika kujenga, kuna sehemu inaweza ikakubidi ubomoe kwanza ndipo ujenge, ubomoaji huo hufanyika kwa makini sana ili usibomoe kusiko husika na kila ubomoaji huo ukifanyika hufuatiwa na ujenzi papo kwa papo! .
Nitapenda kuiona jf ya hivyo, wale waashi mahiri wa jf ambao kazi yao ni kubomoa tuu, wapewe jukumu la kujenga pia sio kila siku wao ni kubomoa tuu, mwisho watapewa sifa ya kuitwa wabomoaji tuu ili hali tuna wajenzi imara na mahiri humu tena waliopitia kozi za uanagenzi kwa wale mahiri kabisa.
Wana jf tuwe wakweli kumhusu rais Magufuli toka ndani ya nafsi zetu sio kwa kuvaa miwani yenye kuona upande mmoja tuu wa mabaya tuu, mapungufu tuu na makosa pekee, bali kama kuna mema pia tuyaone, kama kuna mazuri pia tuyaangazie na kuyasema as encouragement kwa rais wetu mpendwa Mhe Dr John Pombe Joseph Magufuli.
Mungu Ibariki Tanzania.
Paskali
Rejea kuhusu ukosoaji. Zifuatazo hapa chini ni baadhi tuu za mada zangu za ukosoaji.
Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria! .
JF Modes, Magufuli ni Rais Wetu, Asiabudiwe, Asiogopwe, Bali Aheshimiwe!.
Katazo la Rais Kusafiri Nje ya Nchi bila Vibali: Je, Halikiuki Haki za Binaadamu?!..
Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote
Rais Magufuli, Waliomchagua Wanajuta!, Wasiomchagua Wanamshangilia!. Akishika Chama, Watakoma
Magufuli, "Kama Unaona Kazi ya Urais ni Ngumu Kwako, Jiuzulu! ".
Je inawezekana huu ndio mwisho wa utumbuaji wa papara na kukurupuka?! Mkuu kutumbuliwa soon!
Huu ni wito tuu kwa wana jf kuhusu ukosoaji wa Rais wa nchi, Mhe. Dr. John Pombe Joseph Magufuli, ufanyike kwa staha kwa kutanguliza mbele uzalendo, na maslahi ya taifa mbele, ukiwemo utaifa. Kuitanguliza mbele Tanzania kwanza ndipo rais Magufuli afuatie.
Rais Magufuli nae ni binadamu na sio malaika, hivyo, kama binadamu ni haki yake kukosea, kwasababu no one is perfect, the only perfect being is God!, hivyo Magufuli kama Magufuli kuna mahali anakosea au amefanya ndivyo sivyo, tupaseme sio kwa kubeza au kukejeli, bali kufanyike kwa heshima, kwa lugha ya staha na unyenyekevu kwa lengo la kumuonyesha makosa yake, kisha tuweke na ushauri wa the right thing to do, hivyo ukosoaji kwa rais, ufanyike constructively kwa nia njema ya kujenga na sio kubomoa, yaani tufanye "a constructive criticism" in good faith kwaa nia ya kumsaidia rais wetu kuwa rais bora zaidi na kulisaidia taifa kusonga mbele na sio kurudi nyuma kwa sababu kwa mujibu wa katiba yetu, rais hawezi kukosea ndio maana hawezi kushitakiwa.
Rais ana sehemu mbili, rais ni taasisi ya presidential institution hivyo rais kama taasisi hawezi kufanya kosa lolote ni perfect being kila kauli yake ni sheria, inafuatiwa na utekelezaji tuu, lakini hiyo institution inashikiliwa na kuongozwa mtu apmbaye ni binadamu tuu kama sisi anayeitwa John Pombe Joseph Magufuli, huyu ni binadamu wa kawaida kama sisi wengine wote, he is a human anaweza kukosea. Katika kumkosoa rais, tumkosoe kwa heshima in such a way tusije kujikuta tunakosa uzalendo, badala ya kumkosoa, tumamuaibisha na kujikuta tunajiabisha sisi kama taifa.
Nakiri kupandisha uzi huu kutokana na mchango wa mwana jf huyu
Rais wa nchi ndio kioo cha taifa, ni kama baba wa familia, anahitaji kuheshimiwa.Mkuu Pasco Mtu anayekupa taarifa ya ambayo haiko sahihi utamuitaje?
Ukaguzi maalumu uliofanywa na ofisi ya CAG katika kipindi cha mwaka wa fedha 2010/11 na 2011/12 umebaini kuwa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, bungeni Novemba 2013 kuwa fedha hizo zilitumika kwa miradi ya ujenzi wa barabara, haikuwa sahihi.
Ufisadi wa kutisha waibuliwa
Hata ikitokea baba mwenye nyumba au baba nyumbani amekosea jambo fulani, anakosolewa kwa heshima kiutu uzima kwa kutumia lugha ya heshima na staha na sio lugha za dharau, kebehi, machukizo au matukano! .
Hata akidanganya haitwi muongo anaitwa hayuko sahihi sana, au ameshauriwa vibaya kwa sababu rais wa nchi hawezi kudanganya, wala hawezi kusema uongo!.
Hata akichelewa kwenye shughuli haambiwi kachelewa maana mkubwa hachelewi bali anakuwa bado hajawasili kutokana na kutingwa na shughuli muhimu, na asipotokea kabisa ni kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu!.
Simaanishi rais Magufuli yeye ni malaika hivyo hawezi kukosea au kufanya makosa, no!, rais Magufuli naye ni binaadamu tuu kama sisi binaadamu wengine wote, na siku zote sisi binaadamu ni viumbe dhaifu, hivyo rais Magufuli naye ana madhaifu yake ikiwemo kuonekana kama ni mtu wa kupenda kusifiwpa kupindukia, anapoongea kuna wakati anaonekana kama ni msema chochote na katika kufanya maamuzi, kuna wakati anaonekana kama anatenda badhi yap maamuzi kwa haraka na baadhi ya maamuzi yake, kuonekana kama ni maamuzi ya uamuzi wa haraka hivyo kukosa tafakuri ya kina ila kwa vile yeye ndie kiongozi wetu Mkuu, kuna mambo ambayo hatupaswi kuyasema hivyo yalivyo, hata kama ni kweli, hata kama ni kweli sometimes anaweza kusema kitu ambacho sio sahihi, hatupaswi kusema rais ni muongo bali rais hakuwa sahihi sana au alikuwa hajashauriwa vizuri au alikuwa ana joke tuu, au anazungumza kwa utani tuu, yaani rais anatania au rais ameteleza tuu ulimi!.
Mfano rais alipohimiza kufyatua tuu watoto kisa atasomesha bure. Tamko hili lilikwenda kinyume cha uzazi wa mpango, hapa rais kiukweli aliropoka na kuteleza ulimi, lakini haiwezi kusemwa kuwa rais karopoka, bali rais alikuwa anatania tuu watani zake, wazaramo!. Siku alipotamka hivyo, hata mimi nilishitushwa na tamko lile ( Rais Kusitisha Uzazi wa Mpango Kwa"Fyatueni Watoto wa Kutosha",Ni Yake au ni ya Wale Wazee wa..?!.)
Lakini baada ya siku mbili tatu, Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu aliibuka na kulitolea ufafanuzi wa kina tamko lile kuwa lilikuwa sii kweli bali rais alikuwa akiwatania tuu watani zake Wazaramo!.
Mfano kwenye hoja ya udikiteta, ni kweli rais Magufuli ni kama dikiteta fulani hivi, ila ni dikiteta Mzalendo. Hivyo ndivyo alivyo, tangu akiwa Waziri, he is a no nonsense man, hataki ujinga na hawezi kuvumilia uzembe, na sio kwamba anajifanyisha, ila pia, kwa Tanzania hapa tulipofika, seriously tulihitaji sana mtu mwenye sifa, silika na haiba za udikiteta ndio anaweza kuinyoosha hii nchi ilivyopinda kupindukia hadi kufanywa ni shamba la bibi!. Siku nyingi tumekuwa tukmlaumu JK kwa u pole wake hadi kumuita "dhaifu" hivyo tumekuwa tukisali kumuomba Mungu atupe kiongozi imara, shupavu, thabiti, ambaye sio mtu wa mchezo mchezo, na kweli hatimaye Mungu akaisikia sala yetu ametupatia Magufuli ambaye ni dikiteta kweli ila sio dikteta mbaya kama Hitler, huyu ni dikiteta mzuri " a benevolent dictator", hivyo badala ya watu kuulaumu huu udikiteta wa rais Magufuli, tunapashwa kumshukuru Mungu kutupatia Magufuli.
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata!. Atakayeleta Fyoko, Ataisoma Namba!
Watu walipoitwa Vila.za, hatukunyamaza, tulitoa ushauri humu.
Wito kwa Baba Jesca: Watendee Haki Kina Jesca Wote Ili Nao Wapate Bahati Kama Jesca!.
Hata alipozungumzia mishahara ya peponi, pia tulitoa ushauri humu
Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote
Hata majumbani mwetu hasa majumba ya Kiafrika na Kiswahili, baba ambaye ni mkuu na kichwa cha nyumba, kuna mara kibao anakosea hasa sisi mababa wa Kiafrika tunaofuata mila zetu za kiasili za Kiafrika na mambo yetu yalee ya Uafrika wetu, na pia sio malaika hivyo tuna madhaifu mengi tuu ambayo wamama huyajua huyaona, huyavumilia lakini hawayasemi hadharani.
Kuna namna ya ukosoaji wa heshima na staha wenye lengo la kujenga, a constructive criticism ambao hufanywa in good faith na kuna ukoasoaji wa mbaya wa udhalilishaji wenye lengo la kubomoa, kubagaza, kudunisha na kumshusha mtu kwa kumvunjia heshima ambao hufanywa in bad faith, ridiculously au kumdhalilisha, mkosolewa kwa nia ya kumjengea chuki, achukiwe, kumshushia hadhi na heshima ili aonekane ni mtu wa hovyo, etc huu sio ukosoaji mzuri hata kama ni kweli amekosea, yaani japo is the truth but the motive behind is ill motive.
Simaanishi sasa ndio wote kazi yetu iwe ni moja tuu, kumhusu rais wetu, iwe ni kumuimbia tuu nyimbo za sifa na mapambio, no !, tumkosoe rais Magufuli kwa heshima na kwa kutumia lugha ta staha kwa nia njema kabisa kwa lengo la kumrekebisha na kumsaidia na sio kumdhalilisha.
Tanzania ni yetu sote, sio Tanzania ya Magufuli pekee, na japo CCM ndio chama tawala, haimaanishi Tanzania ni ya CCM, Tanzania sio ya CCM pekee, ni Tanzania ya wote, hivyo we all have a role to play and a responsibility of duty of care kujenga nchi yetu kwa kutanguliza uzalendo na kuweka mbele maslahi ya taifa kwa kujenga na sio kuibomoa na kumjenga rais wetu na sio kumbomoa regardless tunampenda, hatupendi, tulimchagua, hatukumchagua, kama wazalendo wa nchi hii ni lazima kuijenga nchi yetu na kumsaidia rais wetu as a responsibility and a duty of care, kama inavyotokea kuwepo kwa mtoto mwenye ulemavu katika familia, hakuna anayependa ulemavu, lakini imetokea, lazima tumpende and we have a duty of care kumsupport, kumsaidia na kupenda kwa dhati, vivyo hivyo ndivyo ilivyo kwa rais Magufuli, ndie rais wetu wa sasa na hivi alivyo ndivyo alivyo, tumkubali, sio lazima tumpende lakini tunawajibu wa kumpa kila aina ya ushirikiano ili aweze kulitawala vyema taifa letu.
Kuna watu katika kumbonda rais Magufuli, kila siku kazi yao wao ni kuponda tuu, hata akifanya mazuri vipi, wao wataponda tuu, kubeza, kukosoa kila kitu na kumbomoa tuu, na katika kuponda huku, sometimes hujikuta wanaponda over and obove na kuliaibisha taifa letu, na wengine humsifia Nyerere, yaani kumtumia wasifu wa Nyerere as a reference, ila kiukweli ukimwangalia rais Magufuli kwa jicho la karibu, yuko kama Nyerere kwa karibu kila kitu
Magufuli Kama Nyerere:Ni Mtu wa Watu, Hapapasi, Hamung'unyi, Ni Kazi Tuu, Ila Pia,Sio Kama Nyerere!.
Katika kujenga nchi the motive iwe ni kujenga kila kitu ikiwemo kujenga watu akiwemo rais anahitaji kuendelea kujengwa na sio kubomolewa tuu.
Japo nafahamu katika kujenga, kuna sehemu inaweza ikakubidi ubomoe kwanza ndipo ujenge, ubomoaji huo hufanyika kwa makini sana ili usibomoe kusiko husika na kila ubomoaji huo ukifanyika hufuatiwa na ujenzi papo kwa papo! .
Nitapenda kuiona jf ya hivyo, wale waashi mahiri wa jf ambao kazi yao ni kubomoa tuu, wapewe jukumu la kujenga pia sio kila siku wao ni kubomoa tuu, mwisho watapewa sifa ya kuitwa wabomoaji tuu ili hali tuna wajenzi imara na mahiri humu tena waliopitia kozi za uanagenzi kwa wale mahiri kabisa.
Wana jf tuwe wakweli kumhusu rais Magufuli toka ndani ya nafsi zetu sio kwa kuvaa miwani yenye kuona upande mmoja tuu wa mabaya tuu, mapungufu tuu na makosa pekee, bali kama kuna mema pia tuyaone, kama kuna mazuri pia tuyaangazie na kuyasema as encouragement kwa rais wetu mpendwa Mhe Dr John Pombe Joseph Magufuli.
Mungu Ibariki Tanzania.
Paskali
Rejea kuhusu ukosoaji. Zifuatazo hapa chini ni baadhi tuu za mada zangu za ukosoaji.
Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria! .
JF Modes, Magufuli ni Rais Wetu, Asiabudiwe, Asiogopwe, Bali Aheshimiwe!.
Katazo la Rais Kusafiri Nje ya Nchi bila Vibali: Je, Halikiuki Haki za Binaadamu?!..
Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote
Rais Magufuli, Waliomchagua Wanajuta!, Wasiomchagua Wanamshangilia!. Akishika Chama, Watakoma
Magufuli, "Kama Unaona Kazi ya Urais ni Ngumu Kwako, Jiuzulu! ".
Je inawezekana huu ndio mwisho wa utumbuaji wa papara na kukurupuka?! Mkuu kutumbuliwa soon!