Tindikali
JF-Expert Member
- Mar 26, 2010
- 2,129
- 2,914
Na mwanga wa milele umwangazie eee BwanaEhh Mwenyezi Mungu umtangulie mkulima Stern apate haki yake.🙏🏾
Mamilioni ya Watanzania tunamwombea Mkulima!
Ukija na Swiss Air, KLM 80% wanashuka Nairobi, dege linakuja KIA na DAR tupu toka Ulaya!
Ni data gani zinazowaonyesha watalii hatuna kwa sababu hakuna ndege ya kuwaleta???
Mpaka British Airways wakafunga biashara baada ya kuja DAR miaka 50 mfululizo...
leo mnasema mnanunua ndege kuleta watalii... Kutoka wapi, Katavi? Kule mlikosema kuanzia leo nataka kuona ndege inatua Katavi???
Kwani wangesema tunataka kufufua ATC, kuendesha biashara ya ndani na nje, watalii wawepo wasiwepo, tumerekebisha hiki na kile, daftari la mahesabu ya hasara na faida hili hapa, mwenye maoni ya kuponda na kujenga apeleke maandishi kwa mdhibiti mkuu TCAA, kama tunavyopeleka malalamiko EWURA, TCRA, SUMATRA, au akaongee viwanja vya Mwembeyanga saa sita mchana mpaka sauti ikauke, sisi tunajaribu biashara... nani angewaombea mabaya?? nani duniani anaanzisha biashara na uhakika wa mafanikio??
🏾