U-SPIKA: Sitta, Chenge wapigwa panga CCM!

U-SPIKA: Sitta, Chenge wapigwa panga CCM!

Chenge alijiuzulu kutokana na habari zilizoandikwa na vyombo vya habari kuhusiana na ununuzi wa radar, Bunge halikuhusika kwa Chenge kujiuzuli.

You are myopic. Ilianzia Bungeni baada ya Dr. Slaa kufichua ufisadi huo na yeye kujiudhuru. Unaposema Bunge halikuhusika una maana gani?
 
hao wanawake wengine wawili ni smoke screens,ccm wamemuappoint huyu kigagula anna makinda awe ndiyo spika wabunge hili,watch out.
 
Natumaini kila Mtanzania mzalendo ataungana na mimi kumtangaza Mh. Sitta kuwa ni mmoja wa mashujaa wa nchi hii.
Ni spika wa kwanza tangu Tanzania izaliwe kuweza kuruhusu bunge kufanya kazi yake inavyotakiwa.

Ameanzisha harakati za ukombozi kwa watanzania kutoka kwa wakoloni 'wazawa'. Bahati mbaya chama chake hakikumfurahia kwa sababu anaenda kinyume na sera za CHAMA za kutetea MAFISADI na kuwanyonya wanyonge.

Hata kama ameondolewa kwenye uspika lakini atabaki katika kitabu cha historia ya nchi hii itakayoenziwa milele:israel::israel::israel::israel::israel:
 
Tayari maigizo yameanza.yatachukua miaka mitano.sitta tokea lini akawa mtetezi wa taifa.ndiye alizima hoja ya richmond kihuni.nashukuru ccm imemuonyesha kuwa ukiamua kuwa mkweli,kuwa hivyo siku zote.atataabika uzeeni,vuvuzela aliyepinga hadharani sera ya elimu bure,akaomba mdahalo na Slaa PhD.alikuwa akijikosha kwa mafisadi.bali waliopitishwa ccm wote hawafai,na hawana uwezo wa kusimamia bunge hili labda kama mnataka walie hadharani.tumewalaumu wananchi kumpoteza dr.slaa tukasema ni ujinga na njaa.fursa mpya hiyo,spika wa chadema.mpumbavu pekee aweza kumwacha marando kupigia hao wanawake.na itakuwa ishara ya kwanza kama bunge hili ccm wana ujinga uleule wa kupenda chama kuliko taifa.msimamo wangu,kama ccm watamkataa marando,sitalitambua bunge hili na wabunge wataonyesha nao ni mbumbumbu kama wapiga kura wao.CHADEMA tuanze kazi ya kujenga chama.wabunge wetu endeleza mema ya wale waliopita.hongereni nyote.
 
Imekula kwao,wapinzani wakisimamisha mwanaume mmoja,na wakimuunga mkono vizuri atapata hata kura za kundi la Samweli Sitta.
 
CCM nawapa hongera kwa jambo moja tu nalo n la kumcholopoa Chenge, basi.
 
mimi ngeni sana janvini labda hii ndo post yangu ya kwanza.....!lkn hili limeneuma sana na siamini kama inawezekana kutokea.
For [neno baya] [neno baya]hivi nikweli kuna ofisi ya spika imejengwa jimboni kwake...!?sihoji yeye kuendelea kuwa spika lkn suala la kujenga ofisini ya spika jimboni kwake na raisi kufungua...!haiingii kabisa katika tundu lolote la mwili wangu [samahani sana waungwana].
Timekwisha watanzania.serious nafuta machozi kama si kweli naomba aliyesema uongo atububu hii dhambi .sitaki kuamini nasema sitaki kuamini...!tunakokwenda siko kabisa afadhali tulipotoka.
Mwenyezi mungu tusaidie sisi watanzania,saidia tanzania.
Amen.

mkuu hii sio post yako ya kwanza. Chini ya avatar yako ndipo record za post zako zilipo nazo ni nane.
 
SASA KAMA SITTA OUT, ITAKUWAJE KUHUSU LILE JENGO LA SPIKA LILILOZINDULIWA NA KIKWETE MWAKA HUU KULE URAMBO? JE MAKINDA AKIPITA NAYE ATAJENGA LA KWAKE KULE NJOMBE AU ATAKUA ANAKWENDA URAMBO? INA MAANA SERIKALI HAINA MIPANGO YA MUDA MREFU? NAOMBA YALE MAJIMBO YATAKAYOKUWA NA UCHAGUZI THIS WEEKEND WASIFANYE MAKOSA KUICHAGUA CCM.
https://www.jamiiforums.com/attachment.php?attachmentid=16687&d=1289409892[/IMG


wakuu hebu toeni habari kamili kwani hilo jengo la spika urambop mna maana lilishajengwa?
na madhumuni ya kulijenga ilikua nini ofisi ya spika au makazi? nashindwa kujumlisha 0+1 hapa

msaada jamani manake nchi hii kila siku inanishangaza
 
kwa mimi nijuavyo ni kwamba bunge lilipitisha kujengwa kwa ofisi za wabunge kila jimbo(sio ofisi ya spika) na walianza na kujenga kwa ofisi ya sita ,ila kwa kuwa ndio alikuwa spika basi kila mtu anaita ni ofisi ya spika,huu sio ukweli ni upotoshaji mkubwa kabisa.hata takapo maliza ubunge wake hizo ofisi zitatumika kwa mbunge yeyote atakaye chaguliwa.hizo ni ofisi za wabunge na zitajengwa kila jiombo tanzania nzima,tujaribu kufuatialia ukweli sio kuwa washabiki tu wauongo..lol..:a s-baby:

mkuu mallaba (sidhani kama ni isack) si umeona mwenyewe kuwa ofisi za wabunge zilitengewa mil 65 lkn ya sitta ni mil 500? Jengo la sitta halina hadhi ya mbunge bali lina hadhi ya spika.
 
Mungu wetu Mungu wetu kuna nini Tanzania
Nchi yetu inauzwa Mafisadi wana nia
Tuhurumie Mungu wetu mafisadi zao nia
Nchi yetu nchi yetu Mafisadi waiuza

Angalia zao nia Matokeo chakachua
Wenye haki wananyimwa Kura zao Kuibiwa
Kwa kishindo watangaza Aliyeshindwa Kashinda
Nchi yetu nchi yetu Mafisadi waiuza

Nawaombea Mabaya Mafisadi angamiza
Wenye haki wabakie Nchi nzuri wawe nayo
Mafisadi wafutike kwa ajali wamalize
Nchi yetu nchi yetu mafisadi wanauza

Wananchi wamtaka SITA wetu Uspika
Mafisadi chakachua wameweka vibaraka
Wanawake wanafaa kumbe nao mafisadi
Nchi yetu nchi yetu mafisadi wanauza

Tumesha wasoma mbeleni Makindakinda Kumuweka
Wanasema anafaa ni wakati wanawake
Wanawake kitu gani mbona chaguo Fisadi
Nchi yetu nchi yetu mafisadi waiuza

Bora angkuwa KIlango tungesema wameweza
Makindakinda kumuweka Mafisadi kuwalinda
Wanawake gani hawa mkakati twaujua
Nchi yetu nchi yetu mafisadi waiuza

Walipanga awe Chenge wengi wutu tukaguna
Wakaona watuvunge Makindakinda kumuweka
Huyu makindakinda ni wakwao wananchi tukatae
Nchi yetu nchi yetu mafisadi waiuza

Mkumbukeni kinda kinda enzi zile ni naibu
Tofaute yake na SITA hoja nzuri alipinga
Mafisadi kumuweka ni faida yao pia
Nchi yetu nchi yetu mafisadi waiuza

Nitamati nafikia ndugu zangu muwaase
Wawakilishi wasitoe kura zao kwa vibaraka
Bora sana MABERE kuliko kinda kinda wa mafisadi
Nchi yetu nchi yetu Mafisadi waiuza
 
Ngoja tuone baraza la mawaziri litakuwaje, inawezekana JK kamwomba Sitta awe Waziri Mkuu badala ya kuwa Spika.

Never never never u-PM kwa Six kwani Six hatakiwi kabisa kabisa ndani ya CCM, kumbuka maneno ya Vijisenti alivyodai eti Six kuwa ndiye aliyeporomosha chama kwa kuruhusu mijadala fulani kujadiliwa mjengoni (kwa maana nyingine aliruhusu Democrasia ambapo CCM hawaitaki bali kinadharia) ila naamini kuwa Six anaweza kupozwa kama Bilali kuepusha kuutanua mpasuko walionao kwa kumpa ka ulaji mjinga fulani hivi
 
ilikuwa ni ufisadi kupitisha ofisi ya bunge kujengwa jimboni kwa spika aliyeko madarakani kwa wakati huo.

hivi kila baada ya miaka mitano tutajenga ofisi mpya?
Waliposhindwa kumvua uanachama ili wamng'oe,walimtega kwa hiyo ofisi ili naye atumbukie humo ufisadini na achafuke kama wao pia,na ndo maana amirijeshi mkuu wa ufisadi akabariki kama ilivyo ada.Hii imemfanya aonekane ni mbinafsi yaani jamaa kajionesha "his inner part"
 
Sitta amepata alichostahili, unafiki wake umemfikisha hapo alipo, sasa asubiri yafuatayo, (1) kuundiwa kamati ya bunge ya kumchunguza kwa utendaji wake na kumfukuza bungeni mara moja (2) kufunguliwa kwa kesi ya kuvunja sheria kwa mkewe kwa kutoa rushwa wakati wa uchaguzi, alikutwa na simu kibao usiku wa manane eti anasema alikua anakwenda kuona mgonjwa. Sita hata baada ya kuchukua hela za watu chungu mzima katika maandalizi haya na kutegemewa kucheza tofauti na wapinga ufisadi, aliwasaliti wote tena bila taarifa kwa kukubali kuzima hoja ya richmond, na baada ya hapo kuanza kujikomba kwa Lowassa eti yeye alishtushwa sana na kujiuzulu kwa lowasa shit, imekula kwake hatumuhitaji muacha aishie, tunachoomba ni wale wabunge wote wanaotakia heri nchi hii wawatupilie mbali hao wanawake wa CCM, hawawakilishi hata mahitaji ya wanawake wenzao, hatudanganyiki...
 
Hapa naona tunajaribu kuchagua yule mwenye uafadhari katika Ufisadi na kumvisha kilemba cha manyasi apendeze
Hata Chief Adam Sapi hakujenga ofisi ya Bunge Kalenga.
Kwa hiyo Spika President na Troupe zima la CCM wamejipakaza Ufisadi
Hatuna haja ya kujitia hofu ,huyo spika aje tu vijana wetu wapo makini na ni wengi.
Anna makinda au yeote yule kibano cha hoja hakiangalii Makunyazi pajini.
Hiki ndicho kinatakiwa kufanywa... hakuna kuangalia makunyanzi, ni kumkoma nyani tu ndani ya mjengo
 
Hatutaki wanawake mapandikizi, kuna wanawake wenye uwezo naona wawape hao wakina vicky kamata maana ndio viwango vyao kwa vigezo duni
 
Wasubiri kifo chao wana ccm 2015

Hata uchaguzi wa juzi 2010 mlisema mnasubiri kuapishwa kwa Dr. Slaa, labda subiri 2060 ndio CCM inaweza ng'olewa madarakani. CCM ni chama kilichojiwekea mizizi kwa zaidi ya miaka 40 sasa. Ni numu kuking'oa
 
Back
Top Bottom