Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,197
- 25,517
Mimi si mtu mzima sana ingawa nami najongea miaka ya kuweza kugombea Urais wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba yetu ya sasa(miaka 40). Hatahivyo, nimekuwa mfuatiliaji mkubwa wa siasa na mambo ya kinchi tangu nikiwa mdogo. Leo, nitalizungumzia Bunge kama Mhimili mmojawapo wa dola. Mingine, wengi mnajua, ni Serikali na Mahakama. Nimeanza kulifuatilia Bunge lililokuwa likiongozwa na Hayati Chief Adam Sapi Mkwawa.
Bunge hili chini ya Hayati Mkwawa lilikuwa la chama kimoja: CCM. Lakini, Wabunge walipambana kwa hoja na kulipuana kwa shahidi mbalimbali. Mbunge alipokuwa akisimama kuchangia hoja au kutoa hoja, kiti cha Spika na Wabunge wenzake walitega sikio vya kutosha kusikia 'madini' ya Mbunge husika. Ilikuwa ni hoja juu ya hoja, vijembe, kebehi na matusi havikuwepo. Kama ni 'upinzani' basi ilikuwa ni kutofautiana kwa mawazo na hoja.
Likafuata Bunge la Spika Pius Msekwa. Lilifanana pakubwa na lile la Chifu Mkwawa ingawa hili lilikuwa na Wabunge kadhaa wa upinzani kama wa CHADEMA na NCCR-Mageuzi. Hatahivyo, hoja kinzani zilitolewa hata na Wabunge wa CCM. Katika Bunge hili, kashfa za kifisadi ziliibuliwa na wapinzani na hata Wabunge wa CCM. Ndipo paliposhamiri hoja nzito za Mzee Mzindakaya na wengineo (mfano kumhusu Waziri Mbilinyi na Waziri Simba).
Likaja Bunge la Hayati Samwel Sitta. Bunge la Viwango na Ubora. Likajionyesha na kujisimamia hivyo. Hoja, kutoka CCM na wapinzani zikawa motomoto na za uhakika. Bunge hili lilimuweka kwenye chati Balozi Slaa, kwa kumtaja mmoja. Baadaye likaja Bunge la Mama Makinda. Ufanano mkubwa wa Mabunge haya ya Hayati Sitta na Mama Makinda ni 'uhuru' wa Wabunge kutoa hoja zao na kutumia tafiti kujenga hoja zao. CCM na wapinzani walifanana katika hilo.
Baadaye, hivipunde, likaja Bunge la Spika Ndugai. Hakika, Bunge hili lilianza vyema katika kufuata nyendo za watangulizi wake. Halafu, mambo yakabadilika. Bunge likawa sehemu ya 'mapambio', 'kejeli', 'vijembe', matumizi makubwa ya maneno ya kuudhi na kutweza na kadhalika. Katika hali hiyo, Wabunge wengi wa upinzani wakajikuta kwenye wakati mgumu wa kukumbana na adhabu za mara kwa mara. Si kwamba wa CCM hawakuwa wakitenda makosa, ila wingi wao na kiti cha Spika viliwabeba.
Bunge la Ndugai limeonyesha taswira la Bunge lijalo. Limeonyesha uzito au urahisi wa Ubunge na kuwafanya maelfu ya watanzania kutamani kuwa Wabunge. Kiukweli, kama ni wa CCM wanaamini kuwa wakiwa Wabunge hali itakuwa ile ile. Wanajiamini na kuona kuwa hakuna haja ya 'hard work' katika Ubunge wao. Kwa wapinzani, wao wanatamani na kuamini kwenda kuendelea kupambana na kiti cha Spika. Hoja zinawekwa kando. Labda yaonekana hoja si ajenda tena ya Bunge lijalo. Mambo yamekuwa rahisi na kila mtanzania anaweza kuwa Mbunge.
Kuna wa kulaumiwa au kupongezwa kwa kufikisha hali hii ya Bunge na Ubunge kwa ujumla?
Bunge hili chini ya Hayati Mkwawa lilikuwa la chama kimoja: CCM. Lakini, Wabunge walipambana kwa hoja na kulipuana kwa shahidi mbalimbali. Mbunge alipokuwa akisimama kuchangia hoja au kutoa hoja, kiti cha Spika na Wabunge wenzake walitega sikio vya kutosha kusikia 'madini' ya Mbunge husika. Ilikuwa ni hoja juu ya hoja, vijembe, kebehi na matusi havikuwepo. Kama ni 'upinzani' basi ilikuwa ni kutofautiana kwa mawazo na hoja.
Likafuata Bunge la Spika Pius Msekwa. Lilifanana pakubwa na lile la Chifu Mkwawa ingawa hili lilikuwa na Wabunge kadhaa wa upinzani kama wa CHADEMA na NCCR-Mageuzi. Hatahivyo, hoja kinzani zilitolewa hata na Wabunge wa CCM. Katika Bunge hili, kashfa za kifisadi ziliibuliwa na wapinzani na hata Wabunge wa CCM. Ndipo paliposhamiri hoja nzito za Mzee Mzindakaya na wengineo (mfano kumhusu Waziri Mbilinyi na Waziri Simba).
Likaja Bunge la Hayati Samwel Sitta. Bunge la Viwango na Ubora. Likajionyesha na kujisimamia hivyo. Hoja, kutoka CCM na wapinzani zikawa motomoto na za uhakika. Bunge hili lilimuweka kwenye chati Balozi Slaa, kwa kumtaja mmoja. Baadaye likaja Bunge la Mama Makinda. Ufanano mkubwa wa Mabunge haya ya Hayati Sitta na Mama Makinda ni 'uhuru' wa Wabunge kutoa hoja zao na kutumia tafiti kujenga hoja zao. CCM na wapinzani walifanana katika hilo.
Baadaye, hivipunde, likaja Bunge la Spika Ndugai. Hakika, Bunge hili lilianza vyema katika kufuata nyendo za watangulizi wake. Halafu, mambo yakabadilika. Bunge likawa sehemu ya 'mapambio', 'kejeli', 'vijembe', matumizi makubwa ya maneno ya kuudhi na kutweza na kadhalika. Katika hali hiyo, Wabunge wengi wa upinzani wakajikuta kwenye wakati mgumu wa kukumbana na adhabu za mara kwa mara. Si kwamba wa CCM hawakuwa wakitenda makosa, ila wingi wao na kiti cha Spika viliwabeba.
Bunge la Ndugai limeonyesha taswira la Bunge lijalo. Limeonyesha uzito au urahisi wa Ubunge na kuwafanya maelfu ya watanzania kutamani kuwa Wabunge. Kiukweli, kama ni wa CCM wanaamini kuwa wakiwa Wabunge hali itakuwa ile ile. Wanajiamini na kuona kuwa hakuna haja ya 'hard work' katika Ubunge wao. Kwa wapinzani, wao wanatamani na kuamini kwenda kuendelea kupambana na kiti cha Spika. Hoja zinawekwa kando. Labda yaonekana hoja si ajenda tena ya Bunge lijalo. Mambo yamekuwa rahisi na kila mtanzania anaweza kuwa Mbunge.
Kuna wa kulaumiwa au kupongezwa kwa kufikisha hali hii ya Bunge na Ubunge kwa ujumla?