Mantiki ya ubunge wa viti maalumu kwa wanawake ni ipi? Sera hii ina ukomo?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,621
46,266
Naelewa vizuri sana na nakubaliana na mantiki ya kuchukua wanafunzi wa kike wenye ufaulu chini kidogo ya wale wa kiume kuwapeleka kidato cha sita na vyuo vikuu. Naona hilo ni jambo lenye mashiko.

Linapokuja suala la ubunge wa viti maalumu ndio huwa nashindwa kuelewa mantiki hasa ni nini. Wabunge wengi wanawake wanaopewa ubunge wa viti maalum ni watu wanaojiweza na wanaoweza kugombea ubunge sawa kabisa na wanaume na hata ikibidi kusaidiwa na vyama vyao kisha wapiga kura wenyewe wakaamua wanamtaka nani.

Wabunge wengi wanawake huwa wa viti maalum huwa hata hawajikiti katika mambo yanayowahusu wanawake tu katika maeneo yao bali wanazungumzia mambo yale yale ambayo yanazungumziwa na wabunge wanaume, sasa uwepo wao bungeni unasaidiaje mahususi maslahi ya wanawake wa nchi kwa ujumla?!

Na je serikali ina mpango mkakati wowote wa muda maalum wa kuhakikisha huo usawa unaotafutwa katika bunge unafikiwa na kwamba hiyo sera ya viti maalum kuna wakati itafika ukomo wake au hili ni jambo litaendelea kuwepo tu daima?
 
Naelewa vizuri sana na nakubaliana na mantiki ya kuchukua wanafunzi wa kike wenye ufaulu chini kidogo ya wale wa kiume kuwapeleka kidato cha sita na vyuo vikuu. Naona hilo ni jambo lenye mashiko.

Linapokuja suala la ubunge wa viti maalumu ndio huwa nashindwa kuelewa mantiki hasa ni nini. Wabunge wengi wanawake wanaopewa ubunge wa viti maalum ni watu wanaojiweza na wanaoweza kugombea ubunge sawa kabisa na wanaume na hata ikibidi kusaidiwa na vyama vyao kisha wapiga kura wenyewe wakaamua wanamtaka nani.

Wabunge wengi wanawake huwa wa viti maalum huwa hata hawajikiti katika mambo yanayowahusu wanawake tu katika maeneo yao bali wanazungumzia mambo yale yale ambayo yanazungumziwa na wabunge wanaume, sasa uwepo wao bungeni unasaidiaje mahususi maslahi ya wanawake wa nchi kwa ujumla?!

Na je serikali ina mpango mkakati wowote wa muda maalum wa kuhakikisha huo usawa unaotafutwa katika bunge unafikiwa na kwamba hiyo sera ya viti maalum kuna wakati itafika ukomo wake au hili ni jambo litaendelea kuwepo tu daima?
Katiba ya Kenya nimependa kwenye viti maalimu, Wabunge wa Viti maalumu wanapigiwa kura hakuna huu uhuni kama wa Bongo, wanashindanishwa wanawake wa vyama tofauti, na ni wachache sana, kila count ina Vit maalimu mmoja, na anaweza toka chama chochote kile, Hivyo Kenya nzima wanawake wa Viti maalumu wako 47 pekee na wamepigiwa kura.Sio haoa wanateuliwa vyumbani huko
 
Kwanini Ubunge wa Viti Maalum ni wa wanawake peke yao?

Kama hivi viti maalumu vya ubunge ilikuwa ni kwa ajili ya wanawake peke yake kwa nini visiitwe viti maalumu kwa wanawake?

Kwa nini hakuna viti maalumu vya ubunge kwa ajili ya jinsia zote mbili?
 
Back
Top Bottom