Tusiukubali mradi wa Wachina wa Bandari ya Bagamoyo kwa sababu zozote zile. Utakuwa ni mtego utakaotunasa kama nchi

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,597
46,224
Tuna sababu moja kubwa ya kuukata Mradi wa Wachina wa Bandari ya Bagamoyo nayo ni historia mbaya ya China kona mbalimbali za dunia walipotekeleza miradi ya aina hii au walipozikopesha nchi mikopo mikubwa ya miondombinu. Wamechukua bandari Sri Lanka, Pakistan, Australia na Djibouti kupitia mikataba ambayo haieleweki ni yenye utata sana.

Kama huko wameweza kufanya hivyo sisi hatutaweza kuwadhibiti na kuibakiza bandari ya Bagamoyo kuwa bado mali yetu endapo tukiwakubalia wajenge bandari hapo.

Tusijidanganye, sote tunafahamu jinsi gani mikataba midogo tu ya madini imekuwa changamoto kubwa kwa taifa hili, huu ukizingatia na usiri wa mikataba utakuwa funga kazi, tutauzwa mchana kweupe kama enzi za Mangungo wa Msovero.

Tukubali tu kwamba wao ni wajanja na kutekeleza kwa miradi ya aina hii duniani kumewapa ujanja zaidi. Tusikubali bandari zetu kujengwa na kuendelezwa na wageni kwa sababu yoyote ile. Kama tunafikiri ni muhimu sana na tunatakiwa kuwa na Bandari Bagamoyo tukope pesa tujenge wenyewe, vinginevyo tutaiuza nchi yetu nzuri.
 
Unaifahamu vizuri serikali yako mkuu. Hawana utaratibu wa kuweka mikataba ya uwekezaji hadharani hivyo usitegee kuna siku utauona. Endapo mkataba utaridhiwa watakuja na maneno matamu tu ya kuupamba na kuwaaminisha wananchi kila jambo liko sawa kama ilivyofanyika kwenye mikataba mingine.
Kwani mkataba wake unasemaje??kwani naona maneno mengi, si uwekwe wazi ndio watu waamue?huyu anasema vile, huyu anasema hivi hata hatuelewi, utakataaje/utakubalije kitu ambacho hujijui?!!
 
Unaifahamu vizuri serikali yako mkuu. Hawana utaratibu wa kuweka mikataba ya uwekezaji hadharani hivyo usitegee kuna siku utauona. Endapo mkataba utaridhiwa watakuja na maneno matamu tu ya kuupamba na kuwaaminisha wananchi kila jambo liko sawa kama ilivyofanyika kwenye mikataba mingine.
Hatutaki maneno mengi, tuwekee mkataba hapa tuusome

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani hatuwezi kuendesha movement...#wekenimkatabahadharani.

Kwenye account ya Twitter ya Rais?

Hatuwezi andamana 😳🙄😂😂😂
 
Mother akikubali Kuna njia Tena ya kukataa, wabunge wengi si unaona vichwa vyao ni bendera fuata upepo, Tena wabunge wa CCM hawa akina profesa muongo, watakataa hawa dumila kuwili, sidhani.
 
Salamuni wanangu katika jamvi. Japo hili si jipya na limeishajadiliwa sana, kuna haja ya kushupaa ili kujua sababu zilizosimamisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo ambayo baada ya kifo cha Magufuli sasa inaonekana kupigiwa upatu na wapigaji. Si hili tu, hata mradi wa Nyerere wa kuzalisha umeme kule Rufiji tunaambiwa ni bomu. Kesho tutaambwa na SGR ni bomu ukiachia mbali kununua ndege.

Hata mwili wa Magufuli haujaoza tunaanza kuonyeshwa mambo ya ajabu ajabu. Je kunani? Tuanzie na hili la Bagamoyo. Nani aliidhinisha na kwa nini? Nani aliubatilisha na kwanini? Je, kuna kitu hapa umma unafichwa au ulifichwa? Miradi yote ni mali yetu na si ya watawala. lazima tuambiwe ukweli hata kama mchungu. Naomba kuwasilisha tena kwa heshima baba yenu nyote.
 
Salamuni wanangu katika jamvi. Japo hili si jipya na limeishajadiliwa sana, kuna haja ya kushupaa ili kujua sababu zilizosimamisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo ambayo baada ya kifo cha Magufuli sasa inaonekana kupigiwa upatu na wapigaji. Si hili tu, hata mradi wa Nyerere wa kuzalisha umeme kule Rufiji tunaambiwa ni bomu. Kesho tutaambwa na SGR ni bomu ukiachia mbali kununua ndege.

Hata mwili wa Magufuli haujaoza tunaanza kuonyeshwa mambo ya ajabu ajabu. Je kunani? Tuanzie na hili la Bagamoyo. Nani aliidhinisha na kwa nini? Nani aliubatilisha na kwanini? Je, kuna kitu hapa umma unafichwa au ulifichwa? Miradi yote ni mali yetu na si ya watawala. lazima tuambiwe ukweli hata kama mchungu. Naomba kuwasilisha tena kwa heshima baba yenu nyote.
Kwani ripoti y CAG inasemaje? Hii ndio itakata mizizi yote ya fitina.

Marehemu hata achukue miaka 10 kutooza halitaondoa ukweli kuwa hafufuki tena.
 
Huu mradi uliidhinishwa kipindi cha kikwete mwishoni kabisa alivyoondoka aliiacha mchakato huo ukiendelea. Magufuli alipoingia akaona ulikuwa mradi wa kifedhuli sana kutokana na masharti ya mwekezaji.

Watu walipiga makofi na kushangilia hao hao wakasifia na kusema Magu ni shujaa sasa leo hayupo wanaanza kufukua uozo na madili yao ndio muone jinsi CCM ilivyo ya hatari ndugu zangu.

Tumechezewa vya kutosha ndugu zangu, tumepigwa mno.
 
Salamuni wanangu katika jamvi. Japo hili si jipya na limeishajadiliwa sana, kuna haja ya kushupaa ili kujua sababu zilizosimamisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo ambayo baada ya kifo cha Magufuli sasa inaonekana kupigiwa upatu na wapigaji. Si hili tu, hata mradi wa Nyerere wa kuzalisha umeme kule Rufiji tunaambiwa ni bomu. Kesho tutaambwa na SGR ni bomu ukiachia mbali kununua ndege. Hata mwili wa Magufuli haujaoza tunaanza kuonyeshwa mambo ya ajabu ajabu. Je kunani? Tuanzie na hili la Bagamoyo. Nani aliidhinisha na kwa nini? Nani aliubatilisha na kwanini? Je kuna kitu hapa umma unafichwa au ulifichwa? Miradi yote ni mali yetu na si ya watawala. lazima tuambiwe ukweli hata kama mchungu. Naomba kuwasilisha tena kwa heshima baba yenu nyote.
Ni mwendelezo wa Siasa chafu zikiongozwa na, Dhidi ya Hayati. Hakuna kingine hapo kuhusu mradi wa Bagamoyo unaoonekana bora kuliko SGR,Hydro Rufiji,daraja la Busisi- Kigongo, ununuzi wa ndege na ujenzi wa viwanja vya ndege,meli. Tukutane 2025 tutathmini utekelezaji wa ILANI majibu mtapata siyo mbali.
 
Salamuni wanangu katika jamvi. Japo hili si jipya na limeishajadiliwa sana, kuna haja ya kushupaa ili kujua sababu zilizosimamisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo ambayo baada ya kifo cha Magufuli sasa inaonekana kupigiwa upatu na wapigaji. Si hili tu, hata mradi wa Nyerere wa kuzalisha umeme kule Rufiji tunaambiwa ni bomu. Kesho tutaambwa na SGR ni bomu ukiachia mbali kununua ndege. Hata mwili wa Magufuli haujaoza tunaanza kuonyeshwa mambo ya ajabu ajabu. Je kunani? Tuanzie na hili la Bagamoyo. Nani aliidhinisha na kwa nini? Nani aliubatilisha na kwanini? Je kuna kitu hapa umma unafichwa au ulifichwa? Miradi yote ni mali yetu na si ya watawala. lazima tuambiwe ukweli hata kama mchungu. Naomba kuwasilisha tena kwa heshima baba yenu nyote.
Baada ya mzee magufuli kuondoka,kuna watu watakua wana pressurize mama kuhusu huo mradi.sidhani kama ataweza kusema No.
 
Unaifahamu vizuri serikali yako mkuu. Hawana utaratibu wa kuweka mikataba ya uwekezaji hadharani hivyo usitegee kuna siku utauona. Endapo mkataba utaridhiwa watakuja na maneno matamu tu ya kuupamba na kuwaaminisha wananchi kila jambo liko sawa kama ilivyofanyika kwenye mikataba mingine.
Sasa iyo nguvu unayotumia tukatae huo mkataba basi ielekeze ili tuweze kuuona huo mkataba.

Unakataaje kitu ambacho hukifahamu? Embu jaribu kutafakari na wewe.

Nikukumbushe tu kuwa, hao hao wachina unaowaona na kusema wametaka bandar sijui wapi, ndio waliomsaidia Nyerere kuongoza nchi kwa kipindi chote alichokuwa madarakani.

Kuanzia ndege za jeshi, silaha za kijeshi, mifumo ya utawala n.k
 
Ndio ule Mkataba unaowala Djibout, Zambia na Kenya? Ule mkataba nakumbuka Mwendazake aliwahi kuweka baadhi ya masharti pindi tu ilipoibuliwa na Job bungeni. Moja kati ya Masharti alisema ni kutokuendeleza Bandari yoyote ile katika nchi hii na yeye Mchina ndiye angekuwa anasimamia kila kitu kuanzia Ukurugenzi mpaka kibarua hapo ndani kwa miaka 100 arudishe faida yake.
 
Back
Top Bottom